Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,304
- 20,170
Ndugu zangu Watanzania,
Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan. Anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika sherehe za maadhimisho ya Miaka 48 ya kuzaliwa kwa CCM. Chama ambacho kimeendelea kubeba matumaini ya mamilioni kwa mamilioni ya watanzania, chama ambacho kimeendelea kuwa kimbilio la watanzania wanyonge na kinachoendelea kugusa Maisha ya watu pamoja na kuleta tabasamu na nuru kwa watu.
Ni Miaka 48 tangia kuanzishwa kwake lakini kinabakia kama chama imara na kiongozi Barani Afrika. kinabakia kuwa chama cha mfano Duniani kwote kwa mfumo wake na hata historia yake.
CCM kimebakia kuwa chama kinachoheshimika na chenye hadhi ya kipekee kabisa barani Afrika na ulimwenguni kwote. si tu kwa historia yake bali kwa kazi kubwa kiliyoifanya ya kulinda heshima ya mwanadamu na utu wa watu wote bila ubaguzi wa aina yoyote ile.
CCM imeendelea kuwa darasa tosha kwa vyama mbalimbali vichanga . Ni CCM pekee ndio chama kilichoendelea kuliweka Taifa letu katika hali ya utulivu,amani ,usalama , mshikamano na umoja wa kitaifa.
Ni CCM pekee ndio imewafanya watanzania tuendelee kuishi kama ndugu na wamoja licha ya kuwa tuna makabila zaidi ya 120 . lakini hatubaguani kwa misingi ya makabila yetu. ndio maana tunaendelea kushirikiana na kusaidiana katika shida na raha. Tunaendelea kuchagua viongozi wetu bila kujali kabila wala rangi wala dini ya mtu . Hii yote ni kazi ya CCM iliyofanywa kwa miaka hiyo yote. kuhakikisha Taifa linaendelea kuwa moja.
Kwa hakika CCM ina kila sababu ya kujivunia miaka 48 ya uwepo wake madarakani. Ambao Umeleta nuru hatta nje ya mipaka yetu. Umeleta heshima mahali palipokuwa na kudharauliwa ,umeleta haki mahali palipokuwa na uonezi na ukandamizaji. CCM Imewapa Sauti na nguvu watu wote ya kupaza sauti zao bila hofu wala wasiwasi ya kuzungumza.
Lakini ni CCM iliyoleta maendeleo makubwa na ya kupigiwa mfano barani Afrika. kuanzia katika Elimu,Afya, miundombinu na mengine mengi sana. Ndio maana CCM inaendelea kuaminika na kuaminiwa na watanzania kuendelea kuliongoza Taifa letu.
Rais Samia anakwenda kuweka rekodi yake ya kukiongoza chama hiki kama mgeni Rasmi akiwa tayari amepitishwa na Mkutano mkuu kuwa mgombea wake wa Urais .Lakini pia ni Rais Samia atakayeweka rekodi ya kuwa Mwenyekiti wa CCM pale ambapo chama hiki kitakuwa kinatimiza Nusu karne hapo Mwaka kesho kutwa tangia kuzaliwa kwake.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan. Anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika sherehe za maadhimisho ya Miaka 48 ya kuzaliwa kwa CCM. Chama ambacho kimeendelea kubeba matumaini ya mamilioni kwa mamilioni ya watanzania, chama ambacho kimeendelea kuwa kimbilio la watanzania wanyonge na kinachoendelea kugusa Maisha ya watu pamoja na kuleta tabasamu na nuru kwa watu.
Ni Miaka 48 tangia kuanzishwa kwake lakini kinabakia kama chama imara na kiongozi Barani Afrika. kinabakia kuwa chama cha mfano Duniani kwote kwa mfumo wake na hata historia yake.
CCM kimebakia kuwa chama kinachoheshimika na chenye hadhi ya kipekee kabisa barani Afrika na ulimwenguni kwote. si tu kwa historia yake bali kwa kazi kubwa kiliyoifanya ya kulinda heshima ya mwanadamu na utu wa watu wote bila ubaguzi wa aina yoyote ile.
CCM imeendelea kuwa darasa tosha kwa vyama mbalimbali vichanga . Ni CCM pekee ndio chama kilichoendelea kuliweka Taifa letu katika hali ya utulivu,amani ,usalama , mshikamano na umoja wa kitaifa.
Ni CCM pekee ndio imewafanya watanzania tuendelee kuishi kama ndugu na wamoja licha ya kuwa tuna makabila zaidi ya 120 . lakini hatubaguani kwa misingi ya makabila yetu. ndio maana tunaendelea kushirikiana na kusaidiana katika shida na raha. Tunaendelea kuchagua viongozi wetu bila kujali kabila wala rangi wala dini ya mtu . Hii yote ni kazi ya CCM iliyofanywa kwa miaka hiyo yote. kuhakikisha Taifa linaendelea kuwa moja.
Kwa hakika CCM ina kila sababu ya kujivunia miaka 48 ya uwepo wake madarakani. Ambao Umeleta nuru hatta nje ya mipaka yetu. Umeleta heshima mahali palipokuwa na kudharauliwa ,umeleta haki mahali palipokuwa na uonezi na ukandamizaji. CCM Imewapa Sauti na nguvu watu wote ya kupaza sauti zao bila hofu wala wasiwasi ya kuzungumza.
Lakini ni CCM iliyoleta maendeleo makubwa na ya kupigiwa mfano barani Afrika. kuanzia katika Elimu,Afya, miundombinu na mengine mengi sana. Ndio maana CCM inaendelea kuaminika na kuaminiwa na watanzania kuendelea kuliongoza Taifa letu.
Rais Samia anakwenda kuweka rekodi yake ya kukiongoza chama hiki kama mgeni Rasmi akiwa tayari amepitishwa na Mkutano mkuu kuwa mgombea wake wa Urais .Lakini pia ni Rais Samia atakayeweka rekodi ya kuwa Mwenyekiti wa CCM pale ambapo chama hiki kitakuwa kinatimiza Nusu karne hapo Mwaka kesho kutwa tangia kuzaliwa kwake.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.