Paul Makonda Afanyiwa Maombi Na Mtume Boniface Mwamposa.Atahadharisha Walaghai wanaotumia Neno La Mungu Kuwarubuni Watu.

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
23,327
17,190
Ndugu zangu Watanzania,

Mkuu wa Mkoa Wa Arusha Mwamba Mwenyewe Mheshimiwa Paul Christian Makonda Kijana Jasiri kusini Mwa jangwa la Sahara .Amefanyiwa Maombi Na Mtumishi wa Mungu Mtume Boniface Mwamposa wa Kanisa la Inuka Uangaze.

Ambapo Mwamba huyo na jabali La siasa hapa Nchini na ambaye amekuwa Kipenzi cha watanzania na ambaye Nyota yake imeendelea kuwaka Muda wote ,ametoa tahadhari na kuwatahadharisha Watanzania kujiepusha kabisa na watu wanaotumia Neno la Mungu na mavazi ya viongozi wa Dini katika kuwarubuni wananchi na kujipatia ukwasi na utajiri.

Amesema wapo watu wanajiita viongozi wa Dini wanaukwasi mkubwa kupitia Dini,ambapo ukichunguza vizuri unaona hawahubiri na kumhubiri Yesu kristo,bali wanafanya kulitumia tu jina na neno la Mungu kujitajirisha na hawa utawajuwa kwa matendo yao.

Mwamba Mwenyewe Paul Makonda Ambaye siku zote amekuwa akimtumainia Mungu na kuwaheshimu sana viongozi wa Dini zote na wa Madhehebu yote, Amemmiminia sifa na pongezi Mtumishi wa Mungu Mtume Boniface Mwamposa Kuwa ni Mtumishi wa Mungu wa kweli na ambaye amekuwa akilihubiri neno la Mungu wakati wote Mwanzo mpaka mwisho wa mahubiri yake.

Na kwamba watu wote ni mashuhuda wa kazi njema na nzuri inayofanywa na Mtume huyo kwa watu . Mwamba Mwenyewe Paul Makonda anaendelea kujinyenyekeza na kujiweka mikononi Mwa Mungu Mwenyewe kiimani ,kwa kutambua kuwa huyo ndiye Mlinzi wake na ambaye anaendelea kumlinda ,kumtetea na kumpigania dhidi ya maadui zake wenye chuki binafsi na wivu tu
Screenshot_20240921-073429_1.jpg


Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Back
Top Bottom