Nyani Ngabu Mjengoni! Interview: Mapenzi, Utajiri&Mali, Marafiki na Maisha ya ugenini.

Huyu jamaa na mfaham vzr sanaaa ila yy hanijui, kuna siku tulikua kwenye bas nikaona ana log in JF ni mzee wa makamu muhun muhun tuu yaani wale wazee vijana ana mambo ya kisela sanaaa
Hahahaaaa
 
marafiki wa mitaani na kama utapenda kugusia na marafiki wa mitandao pia itakua poa...(ulishawahi kupata marafiki mitandaoni? Ulitumia vigezo gani ili kukubali awe rafiki yako?)

Marafiki wa huku uraiani:

Kusema ukweli mimi niko 'picky' sana na pia niko 'mfikiriaji' sana.

Huwa siruhusu kirahisi watu wanijue kiundani hadi niwe nawaamini.

Na hadi nije nimwamini mtu hunichukua muda mrefu sana.

Kwa msingi huo, marafiki wa karibu nilionao huku uraiani ni wale niliosoma nao kuanzia chekechea mpaka shule ya upili.

Kwa bahati nzuri sana nilibahatika kusoma nao shule moja...kuanzia chekechea, msingi, hadi upili.

Hivyo hao nimejuana nao tokea utotoni. Nimecheza nao, nimepigana nao, nimewinda nao ndege, nimefuga nao njiwa, na mengineyo mengi.

Idadi yao hao haizidi vidole vya kiganja kimoja!

Wa mtandaoni:

Kusema ukweli, mtandaoni sijawahi kupata rafiki wa kweli.

Ambao ninao ni washikaji tu.

Siwajui kivile na wao hawanijui hata robo.

Huku kwenye mitandao huwa nipo makini sana kuliko hata umakini wenyewe.
 
Nyani Ngabu
Kabla ya kufika USA ulikuwa unavuta picha gani kichwani ambayo ulipofika ulikuta ni tofauti kabisa?
Na katika maisha yako ya ugeni ni kitu gani kilikuwa kinakusumbua mwanzoni?
 
Marafiki wa huku uraiani:

Kusema ukweli mimi niko 'picky' sana na pia niko 'mfikiriaji' sana.

Huwa siruhusu kirahisi watu wanijue kiundani hadi niwe nawaamini.

Na hadi nije nimwamini mtu hunichukua muda mrefu sana.

Kwa msingi huo, marafiki wa karibu nilionao huku uraiani ni wale niliosoma nao kuanzia chekechea mpaka shule ya upili.

Kwa bahati nzuri sana nilibahatika kusoma nao shule moja...kuanzia chekechea, msingi, hadi upili.

Hivyo hao nimejuana nao tokea utotoni. Nimecheza nao, nimepigana nao, nimewinda nao ndege, nimefuga nao njiwa, na mengineyo mengi.

Idadi yao hao haizidi vidole vya kiganja kimoja!

Wa mtandaoni:

Kusema ukweli, mtandaoni sijawahi kupata rafiki wa kweli.

Ambao ninao ni washikaji tu.

Siwajui kivile na wao hawanijui hata robo.

Huku kwenye mitandao huwa nipo makini sana kuliko hata umakini wenyewe.
Tungependa kutambua kwanza je, umeoa? Au upo kwenye mahusiano?
 
Hongera sana!
natambua kwamba kwenye marafiki kunakuwa na jinsia mbili yaani ke na Me,
je, ulishawahi kuwa na rafiki wakike ambae baade akageuka na kuwa mpenzi? Je mlidumu kwa muda gani?

Hahahaa.

Kwa kweli sijawahi kuwa na rafiki wa kike ambaye baadaye tulikuja kuwa wapenzi.

Huwa siamini kwamba mwanaume na mwanamke eti wanaweza tu kuwa marafiki kwa maana ya urafiki wa kawaida.

Hilo sidhani kama lipo aisee.
 
Nyani Ngabu kuna tukio lolote ambalo huwezi kulisahau kuhusu marafiki? Unaweza kushea nasi?

Ndiyo.

Nakumbuka wakati bado niko dogo rafiki yangu mmoja na mdogo wake walinichangia bana.

Siku hiyo nilienda kwao kucheza halafu tukaishia kukorofishana nikaanza kupigana na kaka mtu halafu mdogo mtu naye akaingilia.

Licha ya kwamba walikuwa kwao na wao kunichangia, niliwachakaza wote.

Walipoona wamezidiwa wakaenda kumfungulia mbwa wao na kunisakizia.

Ile wanaenda bandani kumfungulia bobbi wao mi tayari nishaacha vumbi nyuma yao.

Enzi nikiwa dogo nilikuwa na mbio sana.
 
I stay ready!

And if you stay ready you ain't gotta get ready.

So let's get right to it....
Empty headed pal!
FB_IMG_1473161259291.jpeg
 
Ndiyo.

Nakumbuka wakati bado niko dogo rafiki yangu mmoja na mdogo wake walinichangia bana.

Siku hiyo nilienda kwao kucheza halafu tukaishia kukorofishana nikaanza kupigana na kaka mtu halafu mdogo mtu naye akaingilia.

Licha ya kwamba walikuwa kwao na wao kunichangia, niliwachakaza wote.

Walipoona wamezidiwa wakaenda kumfungulia mbwa wao na kunisakizia.

Ile wanaenda bandani kumfungulia bobbi wao mi tayari nishaacha vumbi nyuma yao.

Enzi nikiwa dogo nilikuwa na mbio sana.
Hhahaha, Huenda una kipaji cha ubondia,..
Anyway, ni maisha ya namna gani ambayo uliyapitia na haupendi mwanao aje ayapitie?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom