Nitamshangaa sana Nape kama hatachukua hatua za haraka kwenye hili

Ili wawe wamefanya kosa ni lazima kwanza ithibitike takwimu zao ni za uongo.
Pili, NBS ni taasisi ya takwimu ya serikali, siamini wala sidhani (pamoja na upuuzi mwingi wa serikali) kuwa kila takwimu rasmi ni lazima zitoke NBS.
Kuna uhuru wa kufanya utafiti na kutoa matokeo kwa njia ya takwimu, jambo ambalo hata gazeti linaweza kufanya.
 
Sheria namba 9 ya Takwimu ya mwaka 2015 ambayo katika kifungu cha 37(3) kimeainisha makosa na adhabu kuwa ni pamoja na vyombo vya habari kuleta takwimu za upotoshaji.

Nachojiuluza ni je, taarifa ya kiutafiti ya gazeti la JamboLeo kuhusu kukubaliki kwa Raisi Magufuli hakuhusiana na sheria hii?

Kama inahusika,gazeti hili litasalimika?

Kama nakumbuka sawaswa, adhabu yake huwa ni kifungo kisichopungua miezi 6 jela au faini isiyopungua shilingi milioni moja.

Gazeti limefanya kazi yake, lakini je,litasalimika?

Swali muhimu kuliko yote hapa ni je,gazeti hili limepata ruhusu ya National Bureau of Statistics(NBS) kabla ya kuchapisha habari hii?
Unamfahamu Juma Pinto ?
 
Ili wawe wamefanya kosa ni lazima kwanza ithibitike takwimu zao ni za uongo.
Pili, NBS ni taasisi ya takwimu ya serikali, siamini wala sidhani (pamoja na upuuzi mwingi wa serikali) kuwa kila takwimu rasmi ni lazima zitoke NBS.
Kuna uhuru wa kufanya utafiti na kutoa matokeo kwa njia ya takwimu, jambo ambalo hata gazeti linaweza kufanya.
Ndio maana uzi huu umeletwa ili wasomi mchangie .
 
Kama research inaonesha kuwa imani kwa Rais imepungua ni wajibu wa polls hizo kutoka ili Rais ajue watu wangapi wanamuunga mkono na wangapi wanaona priorities alizonazo hazijawagusa. Tuache vyombo viripoti as long as kuna scientific research imefanyika au kuna facts zingine zimehusika. Mi kumpenda Magufuli isiwe kigezo cha yule asiempenda kutosema,let them speak their minds and let him do the best on what he does.
 
Sheria namba 9 ya Takwimu ya mwaka 2015 ambayo katika kifungu cha 37(3) kimeainisha makosa na adhabu kuwa ni pamoja na vyombo vya habari kuleta takwimu za upotoshaji.

Nachojiuluza ni je, taarifa ya kiutafiti ya gazeti la JamboLeo kuhusu kukubaliki kwa Raisi Magufuli hakuhusiana na sheria hii?

Nafahamu si kila tafiti zinabanwa na hii sheria kwa mfano zile za wanafunzi wa vyuo vikuu, n.k

Lakini je,tafiti hizi zinazohusu vyombo vya habari ziko huru kiasi hiki?

Kama nakumbuka sawaswa, adhabu yake huwa ni kifungo kisichopungua miezi 6 jela au faini isiyopungua shilingi milioni moja.

Gazeti limefanya kazi yake, lakini je,litasalimika?

Swali muhimu kuliko yote hapa ni je,gazeti hili limepata ruhusu ya National Bureau of Statistics(NBS) kabla ya kuchapisha habari hii?
Kipima joto cha Itv takwimu zao zinatoka NBS?
 
Kipima joto cha Itv takwimu zao zinatoka NBS?
Sheria huwa zipo ila wakati mwingine huwa inategemea nani kaguswa.

Inawezekana kweli JamboLeo wakawa hawana kosa kwa mujibu wa hii sheria kama ilivyo kwa ITV, lakini huu unaweza kuwa ni mwanzo wa sheria hii kufanyiwa marekebisho maana mambo haya sijui kama yatavumiliwa kwa sasa.
 
Sheria huwa zipo ila wakati mwingine huwa inategemea nani kaguswa.

Inawezekana kweli JamboLeo wakawa hawana kosa kwa mujibu wa hii sheria lakini huu unaweza kuwa ni mwanzo wa sheria hii kufanyiwa marekebisho maana mambo haya sijui kama yatavumiliwa kwa sasa.
Nadhani NBS inahusika sana na tafiti ambazo tayar zimefanywa mfano sensa,uchaguzi nk
 
Kama hawana imani na rais inabidi JPM ajiuzulu uchaguzi ufanyike .
Nafikiri lowasa atashinda.
 
juzi nilileta uzi hapa nikawaambia kuwa kuna jamii fulani wa chama fulani wanaamini jpm atapinduliwa kabla ya 2020 na mapinduzi hayo wao wanaamini yatatokea soon. gazeti kama hili ni la hao hao watu wa jamii hiyo wa chama hicho
We naye Nina mashaka na akili zako
 
Back
Top Bottom