Nipo njia panda, nichague mke au mzazi?

Ungeacha akaja na wao wakaja wakaona hali halisi hivi watafanya ndoa yenu ianze migogoro ulichonacho hata kama Ni kidogo hicho hicho mtashare nyinyi ndo mjuavyo mnavoish.
 
Kuhusu kifo usihofie! Kwa ninavyowajua wa tz, hawakusaidii ugonjwa lkn msiba watakupa msaada! Tena utashangaa pesa zinatoka wapi, wanaunda kamati ya mazishi, msosi, kina mama nao dk0 wamevaa madera ya sare wote! Yaani utashangaa masuala huwa fasta fasta
 
Pokea mgonjwa kaka. Kama una ndugu wengine waelewa shirikiana nao ili mpate hiyo nauli na gharama zingine.

Fanya uwezalo kusaidia.

Zaidi kuwa mkweli kwa ndugu na baba yako siku nyingine. Mwanzo kabisa ungemwambia mzee hali yako sio nzuri kifedha huenda haya yasingetokea. Umeshamwambia huna nafasi nyumbani halafu sasa umwambie huna hela atajua fika hutaki.

Shirikisha ndugu.
 
Jambo la msingi mgonjwa asije na jeshi la uhamiaji ili kupunguza gharama, huenda neema yaja kupitia mgonjwa huyo na ukimkataa utakuwa umeifunga. Chukulia chanya kila jambo, simama imara, amini kwamba kuna njia mbadala katika kila jaribu, piga moyo konde ili ubongo ukuonyeshe njia ya kumudu jambo gumu na siyo kukupa woga ambao unatafsirika kirahisi.
Ukimpokea mgonjwa aidha atakufa au atapona na hayo yatasahaulika lakini kidonda cha kumkataa nduguyo hakitapona haraka katika mioyo ya wazazi na ndugu zako. Usiogope kumpokea mgonjwa na kumlisha sembe kwa matole, ogopa kumkataa mgonjwa ili ulinde bajeti ya wali samaki. Mtoto wa kiume hulia ndani ya moyo wake, huna hali ngumu kama unavyojidhania...wenye hali ngumu wapo na bila shaka hujawaona.
 
Kuna vitu vinatokea kama lesson katika maisha.

Suala la ugonjwa hakuna mtu anayepanga, vivyo hivyo suala la kupona.

Zamani walikuwa wanaamini kila mtoto anazaliwa na riziki yake. Yawezekana msemo huu ni kweli kwasababu hakuna anayeweza kubashiri kwamba huyu ndie president ajaye.

Point yangu ni kwamba; ongea na mzee wako nafasi uliyonayo kwa kumwelewesha kuwa, kama mgonjwa wanataka aje, basi ukoo uchange pesa hata kwa kuuza mashamba ili nauli na pesa ya matibabu ipatikane.

Suala la kufa au kutokufa sio kazi yako. Ikitokea amekufa mikononi mwako basi Mungu atakuwa ameamua kukupa somo, na nakuhakikishia hautakosa msaada au namna ya kuhandle hilo jambo. Ila kukataa kwamba asiletwe kisa huna nafasi sio busara na hakuna jamii itakuelewa.
Ushauri kutoka kwa mdau huyu ndo wa kuufuata,,, akuna cha kuongeza. Biashara tuifungie apa,,,,
 
Hapo ndio tunapokosea tunaishi kwa kuogopa kuchukiwa na watu, ukiishi maisha ya namna hiyo kwanza unajidanganya mwenyewe we kama huna uwezo na unajua hautaweza sema na moyo wako kama utaweza saidia. Kelele za miluzi hazimpotezi mbwa full stop.
Kuna theory kuwa binadamu tunapenda kukubalika/kutokuchukiwa muda wote kitu ambacho kiuharisia si kweli kabisa.
 
Unakabiliwa na changamoto kubwa.
Sio wakati wa kuchanganyikiwa, kwa chini na uone namna ya kusolve changamoto.
1. Huna hela kiwango cha kukosa uwezo wa kuishi na mgonjwa?!
2. Kwa nini unahitimisha kuwa mgonjwa lazima afe?! Ni hisia tu au? Ni jambo baya sana watu wanapouguza halafu wakakusikia ukiongea Habari za kwamba juhudi hizo hazina maana kwa kuwa mgonjwa atakufa.
3. Hiyo ticket ya ndege unatuma ama, maana kwa hali ilivyo mgonjwa akifa lawama zote kwako kwa kuchelewa kutuma tiketi.
4. Ni wakati muafaka WA kutomhusisha mkeo kwa mambo yako na familia yako. Kama maamuzi yako Ni kutotaka mgonjwa kuja kwako basi Ni vyema ukawaeleza wanafamilia wenzako kuwa hayo Ni maamuzi yako.
Kila la kheri unapofanya maamuzi;
 
Kuhusu kifo usihofie! Kwa ninavyowajua wa tz, hawakusaidii ugonjwa lkn msiba watakupa msaada! Tena utashangaa pesa zinatoka wapi, wanaunda kamati ya mazishi, msosi, kina mama nao dk0 wamevaa madera ya sare wote! Yaani utashangaa masuala huwa fasta fasta
Comment yako ulivoiwekea manjonjo, nimecheka kwakweli
H h h ,,,,,,
 
Jambo la msingi mgonjwa asije na jeshi la uhamiaji ili kupunguza gharama, huenda neema yaja kupitia mgonjwa huyo na ukimkataa utakuwa umeifunga. Chukulia chanya kila jambo, simama imara, amini kwamba kuna njia mbadala katika kila jaribu, piga moyo konde ili ubongo ukuonyeshe njia ya kumudu jambo gumu na siyo kukupa woga ambao unatafsirika kirahisi.
Ukimpokea mgonjwa aidha atakufa au atapona na hayo yatasahaulika lakini kidonda cha kumkataa nduguyo hakitapona haraka katika mioyo ya wazazi na ndugu zako. Usiogope kumpokea mgonjwa na kumlisha sembe kwa matole, ogopa kumkataa mgonjwa ili ulinde bajeti ya wali samaki. Mtoto wa kiume hulia ndani ya moyo wake, huna hali ngumu kama unavyojidhania...wenye hali ngumu wapo na bila shaka hujawaona.
Hilo nalo neno maana wasije wakaja na lundo la wasidizi.
 
Wakati mwingine ndugu huwa ni kikwazo....Inafika mahali inbd ufanye maamuzi ya busara kwaajili yako na familia yako!

Usiwaridhishe ndugu kwa kujiumiza,,,Usimridhishe mke wako kwa kuiumiza familia yako!

Hvyo simamia pale unapopaamin!
 
1. Naungana na ushauri wa kwanza hapo juu, Kuwa wazi kwa wanafamilia,waeleze hali halisi kiuchumi uliyonayo kwa sasa.
2. Kama tujuavyo kuchangia kwenye maharusi basi wachange kwa ajili ya matibabu na usafiri wa huyo mgonjwa.
3. Nyumba za kiafrica huwa hazijaagi hata jikoni wataweka magodoro walale, kukataa ugeni ni kitu kisichokubalika kwenye jamii zetu.
4. Waeleze kuwa wakae mkao wa kula, kila kitu kitakachotokea na kikahitaji fedha basi ushirikiano wao wa asilimia 100 utahitajika.
 
Rafiki sio kila jambo Nilakuwasikiliza na kuwakubalia wazazi! Na Kama ulivyosema gharama za kusafiri shs Kiroba Acha nayo Kama hivyo!!!
 
Wadau,

Ukoo upo kwenye vikao na maandalizi ya mwisho kabisa ya kumsafirisha baba yangu mkubwa kuja Dar kwa matibabu zaidi baada ya ugonjwa wake kushindikana katika hospital ya mkoa.

Ukoo wamepanga afikie kwangu na mimi ndie nishughulike na masuala ya Muhimbili na hiyo rufaa kwa ujumla, baba amenipigia simu kunijulisha kuhusu mgonjwa kufikia kwangu, hakutaka majadiliano, ni kama amri vile, mzee wangu ni mkoloni hakuna mfano.

Kinachotutisha ni hali ya mgonjwa ilivyo, chances za kupona ni very slim, watotoa taarifa wameniambia kwanza akifika hai Dar basi mungu mkubwa, hivyo nikamgomea mzee kuwa haiwezekani hatuna nafasi.

Mzee akasema tutaona, kwamba anajua ni mke wangu ndio kakataa, sababu anawajua wanawake, hivyo akadai atamsafirisha mgonjwa hivyo hivyo tupende tusipende, akampigia na wife simu akamfokea sana.

Wadau, tunalikataa suala hili kwa sababu wote mnajua hali ilivyo kwa sasa, posho za vikao zimefutwa, mianya yote ya deals imefungwa hapo kazini, naishi kwa mshahara tu ambao nao nilishaukopea hivyo hauji kama ulivyo, sasa kwa hali hii nije nipate msiba hapa which is more likely, maana mgonjwa sasa amevelop kwiki kwiki isiyokatika muda wote.

Gharama za kusafirisha msiba kwenda mkoa wetu kwa coaster ni karibu 4 million, na mimi sina watu kihivyo hapa mjini, haya, bado gharama za hospital, tuseme Mungu ametenda muujiza akafika akalazwa najua gharama zote za hospital wataniachia mimi, maana wanaendelea kufikiria nina hela kama zamani

Wanampigia mke wangu simu na kumtisha kuwa watamtoa kwenye hii ndoa kama mgonjwa akifa, baba kila saa ananipigia simu nitume hiyo nauli ya ndege mgonjwa asafirishwe haraka mimi nakua namchenga.Sasa jambo hili limekua kubwa katika familia na limeleta mzozo mkubwa.

Msaada wenu wa mawazo unahitajika haraka sana.
Dah!mkuu hii imekaa vibaya mpaka nakuhurumia-pole sana.
Ushauri wangu ni huu;

Ingawa jambo hili ni zito lakini hutakiwi kuliogopa,ila kama ulimkatalia mzee straight kwamba wasilete mgonjwa naomba nisimung'unye maneno kwamba hilo lilikuwa ni kosa namba one na hukutakiwa kufanya hivyo.

Pamoja na kwamba Dingi ni "mkoloni"(nimekunukuu),ulitakiwa kumuelewesha kwa nidhamu ya hali ya juu kwamba jukumu hilo ni zito kwako na kwa hiyo unahitaji msaada wa karibu sana wa wanandugu wote na yeye ndiye asimame kidete kuhakikisha anawaorganise wanandugu kuhakikisha kwamba financial issues zinasettle.

Changamoto kama hizi zipo lakini hakuna lisilokuwa na mwisho,muhimu ni kwamba litakapokwisha likuache wewe na familia yako salama.
Huwezi kuamini lakini katika kila jambo gumu(lenye kheri)mungu huwa anatoa ufumbuzi kwa namna anavyojua yeye.Hata kama mgonjwa atafia hapo kwako ufumbuzi wa kumsafirisha utapatikana tu(kwa uwezo wa mungu).

Kama utaamua "kukaza" kwa mzee elewa kwamba jumba bovu litamuangukia mkeo,na mwisho wa siku mtakosa baraka za wazee.
Kaa na shemeji,mueleweshe umuhimu wa kulimaliza jambo hili diplomatically na rudi kwa mzee mtake radhi,mueleweshe kwa upole atakuelewa tu.Usiache mkeo akachukiwa na wazee wako kwa sababu unazoweza kuzizuia,hili liko ndani ya uwezo wako Mkuu.
 
pole sana mkuu. hizi familia za kiafrika ni janga hasa tena usiombe ukaishi dar kwenye nyumba yako. ukoo wote utakuona tajiri. ole wako ujenge nyumba kubwa. Piga magoti muombe mungu akupe wepesi wa hilo jambo. kubali
 
Pole mkuu. Mlete baba yako na umtibu. Shirkisha ndugu zako kwenye kuchangia.Baba ni mtu muhimu sana aise.
 
Mkuu zingatia ushauri wa kwanza,

Wauze hata ngo'mbe nk. na wachangishane, ili kukupiga tafu.

Ni kweli hali ni mbaya sana kwa watumishi kwa sasa, maana wengi walichukua mikopo bank wakitegemea deal mbalimbali kuwapiga tafu lakini sasa hali ngumu sana
Mkuu Ambamba!
Asante kwa busara hiyo, pamoja na kwamba chanzo ni cha msukuma ngojaga Nize.
Ngojaga nize amezungumza kama watu kumi!
Jambo la kuzingatia na kulipa kipaumbele sisi ni Binadamu, hakuna jambo lisilotatuliwa kwa mazungumzo.
Katika maisha kuwa transparent ni jambo muhimu hata Mungu atakusaidia. Sababu usipokuwa transparent utapokea lawama siku zote na watu kukumisquote jambo ambalo si zuri
Mwisho nasema hivi; hakuna mtu amewahi kufiwa akakosa mahali pa kumpeleka maiti haya labda akamla.
Hivyo mgonjwa aletwe na atibiwe akifa Mungu ajua kazi yake na ana sababu ya kufanya hivyo. Isije ikawa kataae magonjwa akawa lawama.
Maswala ya mauguzi iwekwe mezani Sera za ukweli na uwazi pesa zichangwe.
Kuna mwana jukwaa anashauri kutishia kujinyonga!
Watu kama hawa wanatoka wapi Mwenyezi Mungu awarehemu.hii ni ile kukurupuka tu kuandika kitu wajulikane wapo na sio kutoka ushauri wa maana. uko msemo wa kizungu unasema; "wise people speak because they have something to speak, but foolish people speak simply because they want to speak"
 
Back
Top Bottom