Nini kimeikumba timu ya Simba baada ya mechi ya Dodoma Jiji kuahirishwa?

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
7,683
12,707
Huu uzi nautoa kama tahadhari ili kama kuna sehemu ya kusafisha ifanyike haraka. Sitaenda kumnyooshea mtu kidole wala kumlaumu mtu bali ninachotegemea ni wahusika kuangalia mambo kwa jicho la tatu.

Baada ya gemu ya Dodoma Jiji kuahirishwa, Simba ililazimika kukaa siku kadhaa zaidi ya timu nyingine bila kucheza na hili gepu likaiwezesha Yanga kurudi kileleni na kukaa mpaka sasa. Game ya Simba iliyofuata ilikuwa ni dhidi ya Namungo.

Ukiweza kaangalie tena ile game na performance ya mchezaji mmoja mmoja, sijawahi kuona wachezaji wa Simba wote kwa pamoja, mmoja mmoja, wakiwa na game mbaya msimu huu kama game ile. Watu wanalaumu kiwango cha Ngoma kwa game ya jana dhidi ya Azam ila kwenye game ya Namungo alikuwa hovyo kupita maelezo. Asilimia kubwa ya mipira yake ilipotea katika ile game. Hiki hapa chini ndiyo nilichosema wakati game ya Namungo inaendelea.

Hii mechi imewakataa Ngoma na Janshalewa. Wakiendelea na hii game, Simba itapata shida.
Kwenye game ya Azam ndiyo kabisa, niliona muendelezo wa poor performance ya Ngoma kama ilivyokuwa dhidi ya Namungo na pasi yake mbovu ndiyo ilizaa goli la kwanza la Azam.

Kiujumla, performance ya mchezaji mmoja mmoja kwenye mechi na Azam ilikuwa bora kidogo zaidi ya ilivyokuwa mechi na Namungo, ukiacha labda Ngoma na Kibu ambaye touch zake hazikuwa nzuri, ila kilichokuwa hovyo kupita maelezo ni uchezaji wa timu nzima kwa pamoja.

Yaani beki ilikuwa inakatika kupita maelezo, watu hawarudi nyuma kukaba, pumzi ilikata, eneo la kati na pembeni lilikuwa na mapengo, ungeweza kudhani Simba ilikuwa inacheza na wachezaji 8 uwanjani. Fadlu naye akajisahau "kumaliza mchezo" baada ya kupata goli la pili. Msimu huu hii ni mara ya kwanza hafanyi sub wakati ndiyo mechi ya kwanza ya Simba msimu mzima ambayo timu ilionekana kukata moto. Hii inafikirisha sana.

Swali langu, nini kimeitokea timu ya Simba baada ya kuahirishwa ile mechi dhidi ya Dodoma Jiji? Mbona kama kuna kitu kimedrop ghafla.
 
Baadhi ya mashabiki wa simba siku moja tutawavalisha jezi ili mkacheze kwa niaba ya wachezaji wenu, halafu tuone mtakachokifanya. Maana kila siku nyinyi ni malalamiko tu. Yaani timu isitoe sare, au kufungwa!
Kama hauna cha kuchangia, unaruhusiwa kukaa kimya. Umeona kuna malalamiko hapo?
 
Kuwa mwanamichezo mkuu
Ligi ni marathon
Huwezi kuwa Bora msimu mzima
Kuna game au kipindi timu itaamka vibaya
Yanga alianza msimu vibaya
Ilikuwa ngumu kujitafuta wakati ligi inaendelea
Simba vs Azam, Simba walifanya vyema lakini kumbuka Azam na Simba Zina uzani sawa
Msimu Jana Azam alikuwa wa pili na Simba akawa 3 ndo tiketi ya kwenda huko shirikisho UMISETA
 
Kuwa mwanamichezo mkuu
Ligi ni marathon
Huwezi kuwa Bora msimu mzima
Kuna game au kipindi timu itaamka vibaya
Yanga alianza msimu vibaya
Ilikuwa ngumu kujitafuta wakati ligi inaendelea
Simba vs Azam, Simba walifanya vyema lakini kumbuka Azam na Simba Zina uzani sawa
Msimu Jana Azam alikuwa wa pili na Simba akawa 3 ndo tiketi ya kwenda huko shirikisho UMISETA
Yanga ilianza ligi baada ya kutoka kuchukua Toyota Cup kwa kumkanda Kaizwr Chiefs ambapo mlitamba sana ila baada ya kushtukia hamna anayewazingatia mkanyamaza. Mlianza ligi baada ya toka kucheza na timu ya Ujerumani. Mlianza kwa matarajio makubwa mliyowajaza wachezaji na mashabiki wenu na siyo kwa sababu ya kushuka ghafla kwa kiwango cha wachezaji. Kama sikosei, Yanga imekuja kupoteza gemu zake katikati ya msimu.
 
Huu ni uzi wa ngapi umeanzisha huku ukiwa na maudhui yale yale! Hivi si hata mashabiki wenzako watakuwa wanakushangaa Comrade! Relax, ok?
Sasa sijui haamini kuwa Dodoma Jiji walipata ajali na gari kudumbukia mtono au alitaka wachezee wakiwa na vidonda?

Azam alimfunga Yanga na Yanga tuliona ni sehemu ya mchezo, wao wametoa draw Bado analalamika

Hawa watu ni mbumbumbu
 
Huu ni uzi wa ngapi umeanzisha huku ukiwa na maudhui yale yale! Hivi si hata mashabiki wenzako watakuwa wanakushangaa Comrade! Relax, ok?
Nionyeshe uzi wangu mwingine wenye maudhui kama haya ya uzi huu. Tena nakupa challenge, niletee uzi wa mtu yoyote au content popote pale utakapoikuta mtandaoni wenye maudhui kama ya uzi huu nakurushia 50K sasa hivi.
 
Baadhi ya mashabiki wa simba siku moja tutawavalisha jezi ili mkacheze kwa niaba ya wachezaji wenu, halafu tuone mtakachokifanya. Maana kila siku nyinyi ni malalamiko tu. Yaani timu isitoe sare, au kufungwa!

Wewe unashabikia team gani?
 
Yanga ilianza ligi baada ya kutoka kuchukua Toyota Cup kwa kumkanda Kaizwr Chiefs ambapo mlitamba sana ila baada ya kushtukia hamna anayewazingatia mkanyamaza. Mlianza ligi baada ya toka kucheza na timu ya Ujerumani. Mlianza kwa matarajio makubwa mliyowajaza wachezaji na mashabiki wenu na siyo kwa sababu ya kushuka ghafla kwa kiwango cha wachezaji. Kama sikosei, Yanga imekuja kupoteza gemu zake katikati ya msimu.
Wakati Yanga anashinda Kwa taabu
Wachezaji wanaoneka hawana fitness
Wachezaji walicheza kawaida tu
Huwezi kushinda kila mechi
Azam alimfunga Yanga na Yanga tukachukulia ni sehemu ya mchezo, Simba ame draw mbumbumbu wanalalama
 
Wakati Yanga anashinda Kwa taabu
Wachezaji wanaoneka hawana fitness
Wachezaji walicheza kawaida tu
Huwezi kushinda kila mechi
Azam alimfunga Yanga na Yanga tukachukulia ni sehemu ya mchezo, Simba ame draw mbumbumbu wanalalama
Mlichukulia kawaida? Nini kilimuondoa Gamondi?
 
Sasa sijui haamini kuwa Dodoma Jiji walipata ajali na gari kudumbukia mtono au alitaka wachezee wakiwa na vidonda?

Azam alimfunga Yanga na Yanga tuliona ni sehemu ya mchezo, wao wametoa draw Bado analalamika

Hawa watu ni mbumbumbu
Mnasoma kitu na mnatafsiri mnavyotaka nyie hata kama ni tofauti na kile kilichoandikwa.
 
Mnasoma kitu na mnatafsiri mnavyotaka nyie hata kama ni tofauti na kile kilichoandikwa.
We una maana gani?
Huamini kwamba Dodoma Jiji walipata ajali?
Mechi ilihairishwa maksudi ili Simba ipoteane?
Wachezaji wanahujumu timu?
Ngoma hafai? Kumbuka mechi alizofanya vyema
Coach Fadlu hafai?
 
We una maana gani?
Huamini kwamba Dodoma Jiji walipata ajali?
Mechi ilihairishwa maksudi ili Simba ipoteane?
Wachezaji wanahujumu timu?
Ngoma hafai? Kumbuka mechi alizofanya vyema
Coach Fadlu hafai?
Asiyejua maana haambiwi maana
 
Asiyejua maana haambiwi maana
Kuwa mwanamichezo
Sio kila kupotezwa mchezo uhusishe na uswahili
Liverpool kafungwa
Man City kapigwa 5
Madrid kapigwa 5
Bayern Munich kapoteza mechi Kibao
Inter Kapoteza mechi Kibao
Ikifungwa Simba mnafunguwa nyuzi za kulamlamika na kutafuta wa kumpa jumba bovu
 
Kuwa mwanamichezo
Sio kila kupotezwa mchezo uhusishe na uswahili
Liverpool kafungwa
Man City kapigwa 5
Madrid kapigwa 5
Bayern Munich kapoteza mechi Kibao
Inter Kapoteza mechi Kibao
Ikifungwa Simba mnafunguwa nyuzi za kulamlamika na kutafuta wa kumpa jumba bovu
Nimekwambiaje, asiyejua maana haambiwi maana! Wanaohitaji kujua kilichoandikwa katika mada yangu watakipata na watakifanyia kazi kama wataona kuna la kufanyia kazi, wewe usiyejua maana unaweza kumute wala sio kesi.
 
Huu uzi nautoa kama tahadhari ili kama kuna sehemu ya kusafisha ifanyike haraka. Sitaenda kumnyooshea mtu kidole wala kumlaumu mtu bali ninachotegemea ni wahusika kuangalia mambo kwa jicho la tatu.

Baada ya gemu ya Dodoma Jiji kuahirishwa, Simba ililazimika kukaa siku kadhaa zaidi ya timu nyingine bila kucheza na hili gepu likaiwezesha Yanga kurudi kileleni na kukaa mpaka sasa. Game ya Simba iliyofuata ilikuwa ni dhidi ya Namungo.

Ukiweza kaangalie tena ile game na performance ya mchezaji mmoja mmoja, sijawahi kuona wachezaji wa Simba wote kwa pamoja, mmoja mmoja, wakiwa na game mbaya msimu huu kama game ile. Watu wanalaumu kiwango cha Ngoma kwa game ya jana dhidi ya Azam ila kwenye game ya Namungo alikuwa hovyo kupita maelezo. Asilimia kubwa ya mipira yake ilipotea katika ile game. Hiki hapa chini ndiyo nilichosema wakati game ya Namungo inaendelea.


Kwenye game ya Azam ndiyo kabisa, niliona muendelezo wa poor performance ya Ngoma kama ilivyokuwa dhidi ya Namungo na pasi yake mbovu ndiyo ilizaa goli la kwanza la Azam.

Kiujumla, performance ya mchezaji mmoja mmoja kwenye mechi na Azam ilikuwa bora kidogo zaidi ya ilivyokuwa mechi na Namungo, ukiacha labda Ngoma na Kibu ambaye touch zake hazikuwa nzuri, ila kilichokuwa hovyo kupita maelezo ni uchezaji wa timu nzima kwa pamoja.

Yaani beki ilikuwa inakatika kupita maelezo, watu hawarudi nyuma kukaba, pumzi ilikata, eneo la kati na pembeni lilikuwa na mapengo, ungeweza kudhani Simba ilikuwa inacheza na wachezaji 8 uwanjani. Fadlu naye akajisahau "kumaliza mchezo" baada ya kupata goli la pili. Msimu huu hii ni mara ya kwanza hafanyi sub wakati ndiyo mechi ya kwanza ya Simba msimu mzima ambayo timu ilionekana kukata moto. Hii inafikirisha sana.

Swali langu, nini kimeitokea timu ya Simba baada ya kuahirishwa ile mechi dhidi ya Dodoma Jiji? Mbona kama kuna kitu kimedrop ghafla.
Hamna chochote litimu libovu toka 2021.
Limejaza wachezaji mazamwamwa tu
 
Back
Top Bottom