Muhimu: Nilipelekwa huko ikiwa ni siri ya mimi na ndugu yangu ambae alishafariki, sehem tuliyofikia siikumbuki wala sina mawasiliano yoyote ya huko.
Kuna kipindi mwaka 2014 niliamini nina mikosi na nuksi kwa kuonaa maisha yangu yana utata, ndugu yangu wa karibu niliekuwa nikimshirikisha kwenye mambo yangu mengi aliniasa twende kwa mtaalam wa huko kijijini anakoishi.
huko tiba niliyopewa ni kufukizwa majani, nakumbuka nilifunikwa shuka, ghafla vijana kama wanne hivi walinishikilia kwa nguvu, ndani ya shuka kikaingizwa chungu kina mkaa, mtalam akaanza kuweka majani, moshi ulikuwa mzito sana niliijua thamani ya hewa safi, nilifukizwa karibu dakika 20 nilihisi kuzimia, kuna kijana moja milimgata pajani lile kovu haliji kufutika.
Kiufupi maisha yangu sikuona mabadiliko yoyote, maisha yalikuwa yale yale tu, ila ni hapo mbele kuanzia miaka ya 2017 nilivyoanza kuacha kampani za ovyo, kuwa na nidhamu ya pesa, kuchapa kazi, n.k. ndipo nikaja kugundua sikuwa na mikosi bali ni mtindo wa maisha niliyoyaishi ndio yalikuwa tatizo.
Lakini nilikuwa na tatizo la kuamka na mikwaruzo kwa miaka takribani nane, mimi nilishazoea kwa kuona labda najikwaruza kwa kucha, kwa mwezi naweza kuamka mara mbili mara nina miparuo begani, kwenye kifua, hata kwenye uso
Hilo tatizo liliisha kabisa baada ya kufukizwa kule kwa mtaalam na nikawa najiuliza sana kwamba limeisha sababu ya kufukizwa ? kuna chochote kilihusiana na ugonjwa huo kuwa wa kiroho ?
Kuna kipindi mwaka 2014 niliamini nina mikosi na nuksi kwa kuonaa maisha yangu yana utata, ndugu yangu wa karibu niliekuwa nikimshirikisha kwenye mambo yangu mengi aliniasa twende kwa mtaalam wa huko kijijini anakoishi.
huko tiba niliyopewa ni kufukizwa majani, nakumbuka nilifunikwa shuka, ghafla vijana kama wanne hivi walinishikilia kwa nguvu, ndani ya shuka kikaingizwa chungu kina mkaa, mtalam akaanza kuweka majani, moshi ulikuwa mzito sana niliijua thamani ya hewa safi, nilifukizwa karibu dakika 20 nilihisi kuzimia, kuna kijana moja milimgata pajani lile kovu haliji kufutika.
Kiufupi maisha yangu sikuona mabadiliko yoyote, maisha yalikuwa yale yale tu, ila ni hapo mbele kuanzia miaka ya 2017 nilivyoanza kuacha kampani za ovyo, kuwa na nidhamu ya pesa, kuchapa kazi, n.k. ndipo nikaja kugundua sikuwa na mikosi bali ni mtindo wa maisha niliyoyaishi ndio yalikuwa tatizo.
Lakini nilikuwa na tatizo la kuamka na mikwaruzo kwa miaka takribani nane, mimi nilishazoea kwa kuona labda najikwaruza kwa kucha, kwa mwezi naweza kuamka mara mbili mara nina miparuo begani, kwenye kifua, hata kwenye uso
Hilo tatizo liliisha kabisa baada ya kufukizwa kule kwa mtaalam na nikawa najiuliza sana kwamba limeisha sababu ya kufukizwa ? kuna chochote kilihusiana na ugonjwa huo kuwa wa kiroho ?