Nilicho jifunza kutoka Rwanda

Sijali

JF-Expert Member
Sep 30, 2010
2,672
1,814
1. Tatizo kubwa la Tanzania ni uongozi mbaya. Huu ni uongozi usiojua nini muhimu kufanya kwanza na lipi liwe namba mbili. Baya zaidi wengine katika viongozi kwa kweli hawajui kabisa nini la kufanya.

2. Ili kuendelea lazima viongozi wengi katika serikali wawe na 'exposure' kuwa wameishi nje au wamefuatilia kwa muda mrefu yanayoendelea nje. Ukitazama Rwanda, viongozi wengi wako hivyo, na zaidi ya hayo, raia wengi wameishi nje na kurejea.

3. Weledi wa lugha nyingine. Hii imewasaidia sana Wanyarwanda. Ukifika Rwanda unaweza kuzungumza lugha yeyote ukafahamiwa, Kiingereza, Kifaransa, Kiswahili.

Hii imeifanya nchi hiyo kuwa rafiki zaidi na wageni wanaomiminika kila siku kutaka kuishi. Hawa wamefanya maisha mjini Kigali yawe 'international' na siyo maisha ya 'kimkoa' kama Dar! Nini la kufanya? Wahimize wananchi wajifunze lugha kuu na wala usizibehue au kuwabehua wanaoweza kuzizungumza! Himiza na toa ruzuku ya kuanzishwa kwa Shule za lugha za jioni kufundisha Kiingereza, Kifaransa, Kichina, kwa bei nafuu. Vijana wengi watumia wakati huo kukaa bwete vigengeni kuzungumza Simba na Yanga tu! Lugha ni ajira.

4. Neno 'dikteta' linatumiwa vibaya Afrika. Mara nyingi katika Afrika dikteta ni kiongozi asiyetaka mchezo, mwenye nidhamu na anayeipenda nchi yake mno, kiasi kwamba wakati mwingine atauwa ili kutimiza nadharia ya maendeleo. Kwa kweli kama Kagame ni dikteta, huo ni udikteta ambao nausapoti. Alipoingia madarakani, miaka 30 tu iliyopita, pato binafsi la Mnyarwanda kwa mwaka lilikuwa dola 350.

Leo pato la Mnyarwanda ni dola 900 likifukuzana na la Tanzania dola 1200 (yategemea source unazozinukuu. Nimenukuu chanzo kinachoipa pato la juu zaidi, ama wengine wanasema ni dola 995).

Rwanda leo ni nchi ya pili rahisi zaidi mtu kufanya biashaa barani Afrika, baada ya Mauritius.
Matumizi ya neno 'dikteta' naona ni mbinu za wale wale watu wetu wasiolitakia bara hili mafanikio. Huwezi kuwasikia wakilalamika juu ya 'udikteta' wa Saudi Arabia, Misri au Bahrain.

Kwa vyovyote vile, hakuna nchi hata moja iliyoendelea kwa Demokrasia. Nchi zote zilizoendelea, ikiwemo Marekani, Uingereza, Japan, Ufaransa zilipitia na kuendelea kwa udikteta. Hapa napenda nifahamishe kuwa kuna tofauti baina ya 'Udikteta' na "ukatili" Ingawaje dikteta mara nyingine hutumia ukatili, hii huwa ni kwa sababu za msingi.

Katili anafanya ukatili bila ya sababu ya maana, na aghalabu hufanya hivyo dhidi ya maslahi yake mwenyewe na ya nchi.

Nchi ningi Afrika hazina 'Madikteta' zina watu makatili. Dikteta huchukizwa na hali waliyomo watu wake, ama katili huchukizwa na watu wake!
 
Viongozi wetu hawajielewi Kama Ni viongozi au laa! wapo wapo tu wanazidiwa akili na mama ntilie.
Kazi kuibia wananchi

Na sisi wananchi tupotupo tu Kama punda tunabebeshwa mamizigo ya tozo zinazoishia mifuko ya hao mabwanyenye.

Kiufupi hili taifa Lina mambo ya ajabu sana.

Unatumia pesa nyingi kusomesha mtu bado unamnyima ajira.

Unatengeneza miradi ya pesa nyingi Cha ajabu unashindwa kuisimamia.
 
Mkuu hakuna binadamu aliyekamilika.. ..

Lakini hembu fikiri mtu unakuwa katili kisa mtu ana millioni 500 benki na ni mfanyabiashara miaka 30 ..unatumia neno fisadi kwa watu unampiga panga millioni 300 unamuachia 200 .. Unasema hajapata kihalali..
Unaumiza raia zako makusudi...
Unaharibu mzunguko wa hela makusudi..

Hutoi ajira makusudi...
Yaani unasema hadharani nawakomesha....
Ngoja niishie hapa...

Hapo Rwanda.. Pamoja na yooote hawezi kuchezea uchumi wa mtu mmoja mmoja eti ngoja nicheze na salio bank..
Wanajitahidi kuvutia wawekezaji kwa sera nzuri ili uchumi uimarike..

Hujiulizi kwa nini ghafla malori bandarini mengi yalibadili plate no kwenda Rwanda? Ni kwasababu walikuwa wanashughulikiwa sio kisheria.. Bali matakwa ya mtu..
Unaambiwa kampuni flani leta salio hili ..
Tumetoka mbali
 
Mkuu hakuna binadamu aliyekamilika.. ..

Lakini hembu fikiri mtu unakuwa katili kisa mtu ana millioni 500 benki na ni mfanyabiashara miaka 30 ..unatumia neno fisadi kwa watu unampiga panga millioni 300 unamuachia 200 .. Unasema hajapata kihalali..
Unaumiza raia zako makusudi...
Unaharibu mzunguko wa hela makusudi..

Hutoi ajira makusudi...
Yaani unasema hadharani nawakomesha....
Ngoja niishie hapa...

Hapo Rwanda.. Pamoja na yooote hawezi kuchezea uchumi wa mtu mmoja mmoja eti ngoja nicheze na salio bank..
Wanajitahidi kuvutia wawekezaji kwa sera nzuri ili uchumi uimarike..

Hujiulizi kwa nini ghafla malori bandarini mengi yalibadili plate no kwenda Rwanda? Ni kwasababu walikuwa wanashughulikiwa sio kisheria.. Bali matakwa ya mtu..
Unaambiwa kampuni flani leta salio hili ..
Tumetoka mbali
Kwahiyo kuna mtu aliporwa pesa zake na zilikuwa legit?
Unavyoongea Uongo huoni aibu?
 
Mkuu hakuna binadamu aliyekamilika.. ..

Lakini hembu fikiri mtu unakuwa katili kisa mtu ana millioni 500 benki na ni mfanyabiashara miaka 30 ..unatumia neno fisadi kwa watu unampiga panga millioni 300 unamuachia 200 .. Unasema hajapata kihalali..
Unaumiza raia zako makusudi...
Unaharibu mzunguko wa hela makusudi..

Hutoi ajira makusudi...
Yaani unasema hadharani nawakomesha....
Ngoja niishie hapa...

Hapo Rwanda.. Pamoja na yooote hawezi kuchezea uchumi wa mtu mmoja mmoja eti ngoja nicheze na salio bank..
Wanajitahidi kuvutia wawekezaji kwa sera nzuri ili uchumi uimarike..

Hujiulizi kwa nini ghafla malori bandarini mengi yalibadili plate no kwenda Rwanda? Ni kwasababu walikuwa wanashughulikiwa sio kisheria.. Bali matakwa ya mtu..
Unaambiwa kampuni flani leta salio hili ..
Tumetoka mbali
Yule alikuwa mshamba Sana!

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
1. Tatizo kubwa la Tanzania ni uongozi mbaya. Huu ni uongozi usiojua nini muhimu kufanya kwanza na lipi liwe namba mbili. Baya zaidi wengine katika viongozi kwa kweli hawajui kabisa nini la kufanya.

2. Ili kuendelea lazima viongozi wengi katika serikali wawe na 'exposure' kuwa wameishi nje au wamefuatilia kwa muda mrefu yanayoendelea nje. Ukitazama Rwanda, viongozi wengi wako hivyo, na zaidi ya hayo, raia wengi wameishi nje na kurejea.

3. Weledi wa lugha nyingine. Hii imewasaidia sana Wanyarwanda. Ukifika Rwanda unaweza kuzungumza lugha yeyote ukafahamiwa, Kiingereza, Kifaransa, Kiswahili.

Hii imeifanya nchi hiyo kuwa rafiki zaidi na wageni wanaomiminika kila siku kutaka kuishi. Hawa wamefanya maisha mjini Kigali yawe 'international' na siyo maisha ya 'kimkoa' kama Dar! Nini la kufanya? Wahimize wananchi wajifunze lugha kuu na wala usizibehue au kuwabehua wanaoweza kuzizungumza! Himiza na toa ruzuku ya kuanzishwa kwa Shule za lugha za jioni kufundisha Kiingereza, Kifaransa, Kichina, kwa bei nafuu. Vijana wengi watumia wakati huo kukaa bwete vigengeni kuzungumza Simba na Yanga tu! Lugha ni ajira.

4. Neno 'dikteta' linatumiwa vibaya Afrika. Mara nyingi katika Afrika dikteta ni kiongozi asiyetaka mchezo, mwenye nidhamu na anayeipenda nchi yake mno, kiasi kwamba wakati mwingine atauwa ili kutimiza nadharia ya maendeleo. Kwa kweli kama Kagame ni dikteta, huo ni udikteta ambao nausapoti. Alipoingia madarakani, miaka 30 tu iliyopita, pato binafsi la Mnyarwanda kwa mwaka lilikuwa dola 350.

Leo pato la Mnyarwanda ni dola 900 likifukuzana na la Tanzania dola 1200 (yategemea source unazozinukuu. Nimenukuu chanzo kinachoipa pato la juu zaidi, ama wengine wanasema ni dola 995).

Rwanda leo ni nchi ya pili rahisi zaidi mtu kufanya biashaa barani Afrika, baada ya Mauritius.
Matumizi ya neno 'dikteta' naona ni mbinu za wale wale watu wetu wasiolitakia bara hili mafanikio. Huwezi kuwasikia wakilalamika juu ya 'udikteta' wa Saudi Arabia, Misri au Bahrain.

Kwa vyovyote vile, hakuna nchi hata moja iliyoendelea kwa Demokrasia. Nchi zote zilizoendelea, ikiwemo Marekani, Uingereza, Japan, Ufaransa zilipitia na kuendelea kwa udikteta. Hapa napenda nifahamishe kuwa kuna tofauti baina ya 'Udikteta' na "ukatili" Ingawaje dikteta mara nyingine hutumia ukatili, hii huwa ni kwa sababu za msingi.

Katili anafanya ukatili bila ya sababu ya maana, na aghalabu hufanya hivyo dhidi ya maslahi yake mwenyewe na ya nchi.

Nchi ningi Afrika hazina 'Madikteta' zina watu makatili. Dikteta huchukizwa na hali waliyomo watu wake, ama katili huchukizwa na watu wake!
Kwa upande wa RWANDA ni LUGHA ZA KINYARWANDA NA KIFARANSA ndio zinazotumika zaidi, lakini LUGHA ZA KISWAHILI NA KIINGEREZA zinatumika KIGALI na maeneo jirani kama GISENYI.

Na kuna maeneo fulani ukifika wanatumia LUGHA YA KINYARWANDA tu, LUGHA nyingine hawafahamu - kwahiyo inabidi uwe na MKALIMANI.
 
Kwa upande wa RWANDA ni LUGHA ZA KINYARWANDA NA KIFARANSA ndio zinazotumika zaidi, lakini LUGHA ZA KISWAHILI NA KIINGEREZA zinatumika KIGALI na maeneo jirani kama GISENYI.

Na kuna maeneo fulani ukifika wanatumia LUGHA YA KINYARWANDA tu, LUGHA nyingine hawafahamu - kwahiyo inabidi uwe na MKALIMANI.
Ndiyo maana OP kasema kuwe na madarsana hata ya jioni ya kujifunza lugha. Mwisho kabisa OP kasema LUGHA NI AJIRA
 
wanasema Rwanda inaiba rasilimali za Congo ndo maana uchumi wake pamoja na nchi inakimbia kimaendeleo,wakati huo Rais Samia anasema Tanzania tuna madini mengi mpaka mengine hatujui yanaitwaje na bado tupo tupo tu yani.
Inasikitisha kwa kweli
 
Viongozi wetu hawajielewi Kama Ni viongozi au laa! wapo wapo tu wanazidiwa akili na mama ntilie.
Kazi kuibia wananchi

Na sisi wananchi tupotupo tu Kama punda tunabebeshwa mamizigo ya tozo zinazoishia mifuko ya hao mabwanyenye.

Kiufupi hili taifa Lina mambo ya ajabu sana.

Unatumia pesa nyingi kusomesha mtu bado unamnyima ajira.

Unatengeneza miradi ya pesa nyingi Cha ajabu unashindwa kuisimamia.
20220914_163901.jpg
 
Mkuu... wewe si unakaa tuu hujui chochote kilichokuwa kinaendelea..

Ulitarajia vyombo vya habari vitangaze hadharani...

Hata fedha za beural de change ilikuwa undercover operation.. Bahati mbaya ikafumuka wazi
Kwa hiyo alichagua matajiri wachache nakuacha wachache?
Wewe binafsi alikupora Bilioni ngapi?
 
Back
Top Bottom