Ni Wakati wa Timu za Tanzania Kutafuta Vyanzo Vya Kudumu vya Mapato Yao.

bryan2

JF-Expert Member
Jun 8, 2016
3,323
4,678
Kwa kweli imefika Mahali hizi timu zetu ziwe na vyanzo vyao binafsi vya kudumu vya mapato,haiwezekani timu zinazjiita wa Kimataifa halafu mchezaji anagoma eti Timu imeshindwa kumlipa mshahara wake.

Hizi timu zetu zimekua kama za mtu mmoja sio ajabu kusikia Baada ya mtu flani kujitoa Kwenye timu,timu inakosa pesa za mshahara kwa Wachezaji.

Ukiangalia wenzetu wa Ulaya Timu zinaendeshwa na wanachama wao na wafadhili mbalimbali ila huku kwetu ni Kinyume kabisa,vyanzo vya Mapato vya timu haviko wazi,utasikia kiongozi huyu ametoa millioni 100 za kusaidia timu,mara kiongozi ametoa ametoa pesa yake mfukoni kumsajili mchezaji flani hii iko Kwetu tu,sijawahi kusikia Mtendaji mkuu wa Manchester/Arsenal ametoa pesa zake mfukoni kusajili mchezaji au kusaidia timu timu zinajiendesha kutokana na vyanzo vyao vya wazi kabisa vya mapato kama vile,mauzo ya jezi,vifaa mbalimbali vya michezo,pesa za makampuni mbalimbali,etc

Ifike mahali na hizi timu zetu ziwe wabunifu kwa kubuni vyanzo mbalimbali vya mapato ni aibu sana Mchezaji Kugoma kucheza kisa timu imeshindwa kumlipa mshahara wake,Viongozi wa timu zetu na wanachama tubadilike kwa maendeleo ya vilabu vyetu.

Ni hayo tuu.
 
namna nzuri ilikuwa ni kuwapa watu binafsi wawekeze lakin li serikali likagoma, ulikuwa ni upuuzi wa kiwango cha lami ule.
 
Daa mkuu acha tu Mpira siku hizi Ni Ajira Sasa mtu anakuja na Gunia lake la Pesa akitaka kuwekeza wewe unalipiga teke tena bila sababu za Msingi?

La msingi hawa wawekezaji Wapewe Miongozo kama vile Kujenga Viwanja vya timu,Maduka ya bidhaa za Michezo,,,etc

Nimeshuhudia Mchezo flani hizi Jezi za hizo timu zilikua zikiuzika kama njugu ila Sijawahi kusikia hata siku moja mapato yatokanayo na jezi inaonekana ni kama mchongo wa watu flani tu.

Imeniuma sana kusikia Obrey Chirwa kagoma kusafiri na timu kisa anadai Club yake mshahara wa Miezi 3 Nyuma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…