Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,983
- 69,624
MY LAST RIDE; SAFARI YANGU YA MWISHO.
Mtunzi; Robert Heriel
+255693322300
Episode 01.
Sikumaanisha kuua! Wala sikuwahi kuwaza kuwa kuna siku nitakuja kuua mtu. Kwa kweli ningefanya dhambi zote, zote! Lakini sio dhambi ya kumwaga damu ya Mtu. Haya sasa nini kimetokea? Nani kaniloga! Mungu wangu!
Nimeua! Nimeua! Dimoso Mimi Nimeua!
*********
Jina langu naitwa Dimoso. Wengi huniita D, ukifika hapa kiwangwa hutonipata kama utaulizia Dimoso, ingawaje ni jina langu lakini wengi hawalifahamu. D ndio jina Maarufu zaidi. Hilo Mpaka mtoto mdogo ungemuuliza angekuleta mahali ninapoishi kama angenikosa kijiweni mahali ninapofanyia Kazi ya bodaboda, yaani udereva pikipiki.
Ni Miaka miwili sasa tangu niingie katika Kazi ya ubodaboda. Baada ya kumaliza Masomo yangu ya elimu ya juu katika Masuala ya tehama kwenye IT "Shahada ya information Technology" katika Chuo cha DIT. Nilikula msoto haswa nikiwa napambana huku na huku Kutafuta Kazi katika fani niliyosomea.
Lakini jitihada zangu ziligonga mrama na mipango kwenda kombo baada ya tumaini la Kupata Kazi kuyeyuka Kabisa.
Nilihisi kukata tamaa. Nuru ya mafanikio ilimezwa na wingu jeusi la kushindwa. Sasa nikaanza kulia na kujilaumu. Machozi yangu yangemwagika chini kwenye Udongo huenda miche iliyopo udongoni ingeweza kustawi. Yalikuwa machozi Mengi Sana. Lakini haikuwa hivyo. Upepo WA mashaka uliyapeperusha machozi yangu na kuyakausha bila kuacha alama. Ni kwamba hakuna aliyeyaona machozi yangu. Wala hakuna aliyejua kuwa ninalia. Hakuna aliyekaribu Wala aliyejali hali niliyokuwa naipitia.
Kilikuwa Kipindi kigumu Sana kwangu.
Maisha ya Dar es salaam yakanishinda sikujua kama nikiondoka Dar niende wapi. Kurudi nyumbani Morogoro isingewezekana. Ningerudi vipi nikiwa katika Hali kama Ile. Hali ya kushindwa, kuchoka na kukata tamaa. Wazazi wangu wangenitazamaje Mimi? Wangejisikiaje! Mimi kwao nilikuwa kama Jemadari wa vita waliyemuamini Sana. Shujaa wa ukombozi wao. Ati Leo nirudi kichwa chini Mikono nyuma. Hapana! Hiyo nilikataa.
Nayakumbuka Maneno yangu ya kishujaa niliyowaahidi yakuwa ninaenda Chuo kikuu Dar, nikimaliza nitawapa maisha Mazuri. Nitawabadilishia hali ngumu ya umaskini waliyonayo.
Nakumbuka siku Ile Mama yangu akiwa ananisindikiza kituo cha Magari, naikumbuka siku Ile vyema. Nikamwambia Mama; Wakati umefika Mama kuyala matunda yako. Kitambo kidogo unafurahia Kazi uliyoifanya Kwa Miaka mingi. Ulinisomesha ili uishi Maisha mazuri. Nakuahidi Mama. Jambo hilo halipo Mbali tangu Leo"
Siku Ile Mama yangu alikuwa anatabasamu Muda wote. Uso wake uliozingirwa pande zote na mikunjo ya lishe Duni ilipingana vilivyo na tabasamu lake. Niliona nuru ya tumaini ikichomoza katika macho yake. Akanikumbatia kisha akanong'ona nyuma ya mgongo wangu Akiwa amenikumbatia. Baba yako atajivunia sana. Natamani angekuwepo.
Hayo yote nayakumbuka.
Chaguo pekee nililokuwa nalo wakati huo lilikuwa kwenda Kiwangwa, huko Bagamoyo ambapo rafiki yangu wa Chuo aliniitia Kazi ya ujenzi, niende kama Saidia Fundi. Nikaenda. Huko ndiko maisha nilipoyaanzia.
*"
Ulikuwa Ujenzi wa kiwanda cha Nondo na bati. Ilikuwa Kazi ngumu Sana lakini sikuwa na budi kuifanya ili kunusuru maisha yangu. Tayari Mimi ni mwanaume. Unafikiri nani mwingine angeweza kunisaidia kama nisipojikaza na kujisaidia mwenyewe.
Wakati wote nilikuwa nikiishi kwa rafiki yangu. Nilikaa kwake karibu mwezi na nusu Mpaka pale Ujenzi wa kile kiwanda uliposimamishwa kwa Amri ya serikali.
Pesa niliyokusanya ilinisaidia kununua mahitaji yangu ya kuanzia maisha kama kitanda na godoro pamoja na vitu vingine vidogovidogo. Nilimuaga rafiki yangu. Kwa sababu alinifanyia uungwana Sana. Nilimshukuru kwa ukarimu na Msaada alionipatia kwa Kipindi chote nilichokuwa kwake. Ingawaje kilikuwa chumba kimoja na sebule lakini kwangu ilikuwa kama nyumba kubwa iliyonipa utulivu.
Sasa nikaanza Maisha ya kujitegemea, nikiwa nimechukua chumba na sebule mtaa wa tatu kama sio WA nne kutoka alipokuwa amepanga Rafiki yangu.
Nilitegemea mgogoro uliopo baina ya wamiliki WA kiwanda na serikali ungeisha mapema lakini miezi miwili iliisha mambo yakiwa hayaeleweki. Pesa ya akiba ilikuwa imeisha, Kodi nyingine ilikuwa IPO karibu.
Kichwa kilianza Kupata Moto. Nifanye Kazi gani hapa Kiwangwa. Bahati mbaya au nzuri niseme rafiki yangu yeye alibahatika Kupata Kazi serikalini mwezi Mmoja uliofuata baada ya kiwanda kufungwa. Hivyo yeye aliondoka na kwenda Wilayani Kiteto, huko Manyara. Yeye ndiye alikuwa mwenyeji wangu pale Kiwangwa. Hata hivyo tayari nilikuwa nimeshaanza kupazoea na kuzoeleka na wenyeji wa Kiwanga.
******"****
Sikubaliani na wanafalsafa wanaosema maisha ni uchaguzi wa Mtu binafsi. Nakataa. Kwa sababu kama maisha yangekuwa ni uchaguzi wa Mtu binafsi Mimi Wala nisingechagua maisha haya niliyokuwa nayo. Maisha ya kukimbizana na matatizo baada ya matatizo. Maisha ya Kulala njaa. Maisha ya kusimangwa na wenye nyumba.
Ingekuwa ni Maisha yangu ni uchaguzi wangu binafsi ningeenda kufunga chemchem ya matatizo na mikosi iliyokuwa inayaandama maisha yangu.
Mbele yangu alikuwepo Mzee wa Makamo, mwenye sura ya mzaha lakini ndevu zake alivyoziweka zilikinzana na sura yake. Aliziweka ndevu kama Mtu mtata hivi. Sijui kama unamjua Adolf Hitler jinsi alivyokuwa anaziweka ndevu zake. Kama unamjua basi ndivyo huyu Mzee wa Makamo alivyoziweka. Lakini tofauti yake na Hitler ni kuwa Mzee huyu alikuwa na sura ya mzaha.
tuliingia katika mkataba wa pikipiki. Kwamba Mimi nitachukua pikipiki na kuitumia kwa miezi kumi na mbili kisha itakuwa yangu. Lakini itanipasa kila siku nimpelekee Mzee huyu shilingi elfu kumi za kitanzania. Bila kurusha hata siku Moja.
Ikitokea nimerusha siku Moja basi mkataba nimeuvunja mwenyewe na pikipiki ataninyang'anya.
Kuhusu matengenezo ya pikipiki vyote nitafanya Mwenyewe.
Sikuwa na namna zaidi ya kukubali ingawaje masharti yalikuwa magumu. Muda ule nilichokuwa nawaza ni namna ya kuweza kuishi kwa Muda ule. Kupata chakula na Kupata pesa ya Kodi ya mahali ninapoishi ambapo ilikuwa imebaki mwezi Mmoja tuu.
Nikachukua bike nikarudi nayo nyumbani. Nikajiweka zangu kitandani, kisha nikashusha pumzi nzito unhuu! Nikajilaza kitandani, Mawazo yakaanza kunipitia. Daah! Leo nimekuwa bodaboda! Sijui nitaifanya Kazi hii kwa Muda gani. Lakini Sina namna. Muhimu nifanye nimiliki hiki chombo. Yatakuwa mafanikio makubwa Sana.
Punde simu ikaita. Alikuwa ni Mama. Nikapokea;
" Hello Mama! Shikamoo"
" Marhaba mwanangu. Unaendeleaje huko"
" Nashukuru Mungu Mama" Nikasema nikiwa nimeiweka Sauti yangu kwa namna nzuri kuonyesha Sina tatizo.
" Naomba unitumie hata elfu mbili nikanunue unga nipike. Mboga nilichuma Shambani. Sina hata pesa mwanangu"
Mama aliongea kwa sauti ya unyonge Jambo ambalo liliamsha hisia zangu za ndani.
" Usijali Mama, nakutumia, pole Sana mama kila kitu kitakaa sawa"
Nikasema kisha simu ikakatika, nahisi salio la mama lilikuwa limeisha.
Sikuwa hata na Akiba ya Mia Mbovu.
Kama ni kupekua kwenye mifuko ya suruali Kazi hiyo niliifanya Jana. Hakuna pembe Wala Kona ambayo sikuipekua siku ya Jana nikiwa natafuta hata Mia mbili ili niweze Kupata pesa ya mandazi.
"Niende kwa nani nikamkope?" Nikawa najiuliza huku nikiwa nakuna kichwa. Nilikuwa nimetingwa haswa. Mama yangu alale njaa na Mimi nipo. Hapana.
Nikatoka, nikaenda kwenye Duka ambalo lilikuwa mtaa wa pili tuu. Nilijaribu kumkopa muuza Duka lakini alinikatalia akaniambia anachoweza kunisaidia ni kunikopesha bidhaa zake kama unga au mafuta. Sasa hata kama akinikopesha unga au mafuta nitayatumaje Morogoro kwa Mama.
Nikaondoka zangu, lakini nikasema si bora ningechukua nikayatumie mwenyewe. Nikarudi tena lakini mara hii muuza Duka alikataa kabisa hata kunipa bidhaa hizo.
Nilikasirika Sana. Njiani nilitembea kama Kipofu. Nilikuwa na msongo wa mawazo.
Katika Hali isiyo ya kawaida nikajikuga nimeanguka chini na gari likiwa limenigonga. Nikapoteza fahamu. Sikujua nini kiliendelea.
********
Nimekuja Kupata fahamu ni masaa mawili baadaye. Nikiwa katika kituo cha afya cha Kiwangwa. Napiga kelele. Mama! Mama! Jamani mama yangu!
Anaingia mwanamke aliyevalia nguo nyeupe, baadaye nilijua NI muuguzi.
"Vipi unaendeleaje Dimoso" Yule muuguzi akanisalimu akiwa ameikumjua sura yake kwa tabasamu lenye kuweza kutibu.
" Nataka kuongea na Mama. Tafadhali naomba simu yangu"
" Dimoso, hukuletwa hapa na simu. Waliokuleta hapa Mmoja wapo alisema anaitwa Bihawa, mwanamke ambaye ni Jirani yako akasema unaitwa Dimoso"
" Okay! Anyway naomba simu yako nimpigie Mama. Tafadhali"
" Usijali Dimoso, nitakupa. Nataka Kwanza nikupe matibabu kisha mengine yataendelea "
" Hapana! Mimi naendelea vizuri! Nipe simu niongee na Mama yangu tafadhali"
Hapo nilikuwa nimeamka kitandani, niliongea Sauti ya ukali Sana huku nikiwa nimetoa macho. Nikatoka kuamka lakini mkononi nilikuwa na Dripu. Iliyonitonesha mahali nilipokuwa nimechomwa.
Mtonesho huo uliita maumivu katika Maeneo mengine ya mwili wangu. Nikaanza kuhisi maumivu kwenye Paja la kulia, nyuma ya mgongo na kwenye bega.
Nikagugumia, aaaahh!
" Tulia Dimoso bado hauendelei vizuri. Lala! Haya jiegemeze hapo kwenye MTO"
Muuguzi akasema Sauti yake ikiwa Mbali na upole.
Nikajiegemeza kwenye ule mto wa kile kitanda. Yule muuguzi akaja karibu akanipa simu. Nikaipokea. Nikabonyeza bonyeza namba, kisha nikaweka sikioni. Ikaita lakini haikuwa inapatikana. Nikajaribu tena ikawa haipatikani.
"Shiit" nikasema huku Uso wangu ukionyesha kukata tamaa.
" Vipi haipatikani" muuguzi akaniuliza huku anitazama kwa macho ya kupima hisia zangu. Nikamtazama bila kusema kitu.
"Itakuwa simu yake imezima chaji. Maskini huenda alisubiri mpaka akachoka" nikasema kwa sauti ndogo. Muuguzi akiwa ananitazama. Kisha akachukua kipima mapigo ya moyo na kipima presha cha kisasa akanipima. Kabla hajamaliza Mlango ukafunguliwa Mimi ndiye niliyegeuka muuguzi hakugeuka alikuwa akiendelea kunipima. Alikuwa ni Bihawa ambaye ni mwanamke Jirani yangu.
Bihawa alikuwa amebeba hotpot pamoja chupa la Maji na machungwa. Akawa amesimama huku akinitazama kwa macho ya huruma. Baada ya muuguzi kumaliza kunipima akaniambia ninaendelea vizuri.
Kisha akaenda kwenye meza iliyokuwa mule kwenye Ile wodi akachukua kifuko ambacho bila Shaka alikuwa amekuja nacho. Akatoa Dawa kadhaa kisha akawa ananipa maelekezo;
" Hii ni antibiotics, utakunywa mbili mara tatu. Kila baada ya saa nane.
Hii ni antipain, Dawa ya kutuliza maumivu. Utakunywa nayo hivyohivyo. Kila ukinywa hii antibiotics unameza na hii. Usipishanishe Muda. Sawa.
Nimesahau, wewe ulisema ni mkewe au ?"
Muuguzi akamgeukia Bihawa, mwanamke aliyevalia baibui ambaye harakaharaka utagundua ni mtu mwenye kuipenda Dini yake.
Swali hilo likanifanya nimuangalie Bihawa, naye Bihawa alikuwa akinitazama kisha akamjibu muuguzi huku akiwa ananitazama;
" Aam aa! Ni majirani tuu. Yeye ni jirani yangu"
" Mbona kigugumizi bidada! Okay. Nashindwa kukuachia maagizo. Huyu anaishi na Nani kwani?"
" Nipe tuu maagizo muuguzi"
" Hapana! Nahitaji kumpa maagizo mtu anayeishi naye. Sio kila Jambo ninaweza kukuambia wewe kumhusu Mgonjwa"
" Nimekuambia niambie Mimi. Nani aliyemleta hapa? Sio Mimi niliyemleta? Nani kamletea chakula hapa? Ni Mimi au hunioni?"
Nilipoona wanataka kugombana ikabidi nizungumze.
" Muuguzi, Mimi pale naishi mwenyewe. Mji huu Mimi ni mgeni. Hivyo Bihawa anaweza tuu kusikia unachotaka kumwambia"
" Oooh! Kumbe! Sasa si angesema hivyo. Sina haja ya kumpa maelekezo kukuhusu. Sheria zangu za Kazi haziruhusu. Kama ni Kula kwa wakati nitasimamia Jambo hilo mwenyewe.."
Muuguzi akamaliza kisha akatoka, Muda huo Bihawa akawa anamsindikiza na macho ya chuki.
Alipotoka na kufunga mlango. Bihawa akaachia bonge la msonyo. Kisha akanigeukia.
" Huyu nesi hamnazo huyu. Atakuwa anakutaka sio Bure."
" Mmh! Sidhani. Nafikiri anafanya Kazi yake"
" D huna ujualo kuhusu Sisi wanawake. Tangu nimeingia hapa nimemwona namna anavyokuangalia na anavyokuongelesha"
" Hapana Bihawa! Ni Mtazamo wako tuu"
" Unamtetea si ndio?"
" Simtetei! Haya tuachane na hayo!"
" Kama anataka Umalaya si akafanye huo Umalaya wake. Mtcheeeewwi!" Akasonya.
Kisha akatoa lile hotpot kwenye kikapu na Sahani akapakua chakula. Akanipa, kisha akaendelea kumenya chungwa Muda wote ananiangalia kwa macho ambayo sasa nilianza kuyaelewa kwa namna nyingine Kabisa.
Baada ya kula chakula, akaniaga lakini nilikumbuka kuhusu simu yangu. Nikamuuliza simu yangu iko wapi. Akaniambia alipofika eneo nilipokuwa nimegongwa kulikuwa na watu wengi. Hakunikuta na simu.
Nikajua simu yangu ilikuwa imeibiwa.
Kesho yake niliruhusiwa, aliyenileta nyumbani alikuwa ni Yule muuguzi aliyekuwa ananiihudumia tangu siku ya Kwanza. Jina lake alikuwa akiitwa Cathy.
Tulipofika nyumbani kwangu nilimkuta Mzee Abeid ambaye ndiye mwenye Ile bodaboda. Moyo wangu ukapiga paah! Cathy aliona Hofu yangu tukiwa tunakaribia. Akaniuliza kulikoni nikamweleza kwa kifupi hali ilivyokuwa.
Tayari tulikuwa tumefika, nikamsalimu Mzee Abeid naye akanipa Pole ingawaje nilijua alichokifuata pale.
Nikamwambia ngoja niingie ndani alafu nataka kwaajili ya mazungumzo.
Akaniambia hajaja pale kuzungumza na Mimi.
Nikaingia ndani nikiwa na Cathy. Tulipofika ndani Cathy akatoa noti mbili za elfu kumikumi akanipa.
" Kampatie hizi huyo Mzee" akasema,
Nikatoka nikiwa nimezibeba zile pesa. Nikamkabidhi Mzee Abeid, nikamuona akijichekesha hovyohovyo kisha tukaagana.
********
Miezi mitatu ilipita nikiwa tayari nimezoea Kazi ya ubodaboda. Cathy ndiye aliyekuwa amenilipia shilingi Laki tatu za kujiunga kwenye kijiwe cha bodaboda.
Kila kijiwe cha bodaboda kilikuwa na Ada ya kujiungia kwa mara ya Kwanza kwa dereva bodaboda mpya. Bila kutoa Ada hiyo usingeruhuziwa kukaa kwenye kijiwe au kituo hicho cha bodaboda.
Mahusiano yangu na Cathy yalizidi kuimarika ingawaje hakuna miongoni mwetu aliyemuelezea Mwenzake hisia zake. Hata hivyo mioyo yetu ilikuwa kama sarafu moja. Nilihisi kumpenda Sana Cathy naye alionyesha hivyo.
Cathy alikuwa mwanamke Mzuri Sana. Msomi mwenye elimu ya Shahada ya uuguzi. Macho yake mazuri yenye huruma yalifanania Kazi yake ya kuhudumia wagonjwa. Sura yake ilikuwa nzuri pengine hiyo ilimfanya watu wengi wamuone kama ananyodo. Umbo lake lililopangika lilivutia Sana hasa alipokuwa Amevaa Sare zake za Kazi.
Nilikuwa najua Cathy anasubiri kwa Hamu nimwambie ninampenda kisha safari yetu ya Mapenzi ianze upya.
Ni miezi mitatu sasa imepita. Sijui nianzie wapi kumueleza ukweli wa Moyo wangu Binti huyu. Kipato changu ni Duni. KAZI yangu ya kufukuzana na upepo. Ubodaboda. Nitampa nini mwanamke msomi mwenye Kazi yenye kipato zaidi yangu. Nikifikiria hali yangu hiyo ilinifanya nifute Kabisa Wazo la kumwambia Cathy ukweli.
Kama haitoshi, tetesi na duru za mtaani nilizokuwa nazipata zilikuwa zinasema matajiri wa Kiwangwa walikuwa wakiingia na kutoka wakipigana vikumbo kulipata penzi la Cathy. Nilikata tamaa Kabisa niliposikia tajiri anayemiliki kile kiwanda cha Nondo na bati nilichokuwa nafanyia Kazi pia anamfuatilia Cathy. Embu fikiria hata wewe, ungethubutu.?
Unaweza kuniambia nijaribu, mwanaume kujaribu na kujiamini. Hata Mimi kuna wakati nafikiri kama wewe. Lakini Sauti nyingine hunong'ona masikioni mwangu ikiniambia akinikataa nitakosa hata ule ukaribu mdogo niliokuwa nao dhidi yake.
Nikifikia hapo naghairi.
Bihawa naye hakuwa nyuma, yeye ndiye alikuwa ananiona karibu kila siku kwani alikuwa ni lazima kila jioni aniletee chakula cha usiku. Nilishindwa kumkatalia na ningeanzaje kumkatalia mwanamke ambaye alinisaidia kwa gharama zake Kunichukua nikiwa sijitambui siku Ile ya ajali Mpaka Hospitalini kisha akawa ananiletea chakula na hata gharama za matibabu yeye ndiye aliyetoa. Ningewezaje? Nakuuliza!
Licha ya kuwa Bihawa alikuwa mwanamke Mzuri mwenye stara lakini Moyo wangu haukuanguka kwake. Sikuwa nahisia naye. Lakini nitamlipa nini kwa haya anayoendelea kunifanyia. Kila anapokuja kwangu nahesabu deni linaongezeka juu yangu kwake.
***********
Jioni Moja nikiwa nimetulia ghetto kwangu nilimkumbuka Mama yangu. Ni miezi kadhaa imepita sijawasiliana naye Hali ya majuto na kujilaumu kwa kutokumjali MMA yangu vikaukumba moyo wangu. Haikuwa kawaida yangu Mimi kukaa Muda wote huo bila kuwasiliana na Mama yangu. Kikawaida ilikuwa kila siku lazima niwasiliane na mama. Lakini tangu nilipopata ajali namba yake haikuwa imepatikana tena.
Uzembe nilioufanya ni kuwa namba niliyokuwa naitumia haikuwa namba iliyosajiliwa kwa majina yangu. Hivyo kuirudisha kwa matumizi hata baada ya siku kuibiwa isingewezekana. Nilikuwa najilaumu Sana kwa Jambo hilo.
Msomi mzima mwenye Shahada ilikuwaje sikutambua umuhimu wa kutumia laini iliyosajiliwa kwa majina yangu mwenyewe.
Nilikuwa nawaza nikijilaumu.
Ninakaakiba ka Laki tatu, ikifika Laki tano nitaenda Morogoro chapu kumwona Mama. Atafurahi Sana. Nitambebea na zawadi ya nguo.
Bado nilikuwa nawaza.
Wakati nafikiri hayo, punde anaingia Bihawa akiwa amebeba chakula. Kama kawaida Yale alikuwa amevaa hijabu.
Jambo Moja ujue ni kuwa wakati wote huo tangu wakati wa ajali Mpaka wakati huu Bihawa alikuwa akifanya mambo hayo kwa usiri Mkubwa majirani bila kujua ingawaje baadhi ya watu walishaanza kuhisi mahusiano yetu.
Alikuwa kaleta Wali Samaki, kama kawaida lazima aje na chungwa.
Tofauti na siku zote mara hii Bihawa aliniomba Jambo;
" D samahani naomba kwenda msalani"
Sikuwa na ubishi nikamruhusu. Akaniacha sebuleni akaingia zake chumbani ambapo huko kuna Choo na bafu.
Nikawa nakula zangu lakini huko nje manyunyu yakaanza, kwani ulikuwa msimu wa Mvua.
Mpaka nakaribia kumaliza chakula Bihawa alikuwa hajatokea.
Huko Nje Mvua ilikuwa imeshachachamaa.
Mara Mlango unagongwa, Nani atakuwa anagonga Mlango usiku huu WA saa tatu kwenda Sana nne. Kikawaida Mimi sinaga wageni zaidi ya Cathy, Bihawa au mwenye nyumba.
Na mwenye desturi ya kuja usiku na Bihawa ambaye nipo naye. Cathy' hajawahi kuja usiku hata siku Moja ila akijaga anaondoka usiku mnene tofauti n Bihawa.
Mwenye nyumba yeye Hanaga hayo mazoea na haishi hapo. Majirani zangu wao hatujawahi kusumbuana usiku.
Nikafika Mlango nikauliza Nani.
Mara nasikia Sauti Cathy, " Ni Mimi mpenzi. Fungua Mvua inaninyeshea"
Moyo unapiga Paaah!
Hofu na kuchanganyikiwa kwa pamoja vilinivamia.
"Fungua D nalowa"
Hapohapo kabla sijafungua nasikia Sauti kwa nyuma ikiniambia ni Nani. Nageuka namkuta Bihawa amevaa kanga tuu kaipitisha kwenye makwapa ametoka kuoga. Amesimama katikati ya mlango unaotenganisha Sebule na chumba.
" Fungua Baby nalowa jamani"
Inanibidi nifungue. Nafungua mlango Cathy anapita upesiupesi akiwa amelowa chapachapa Akiwa kavaa nguo zake za kazini.
Inaendelea;
Nini kitatokea..?
Usikose sehemu ya Pili?
Mapenzi au Kazi?
Je Pesa Itakupa furaha?
Ni upi uchaguzi sahihi katika Mapenzi?
Uhalifu usiokusudia unapotokea nani atawajibika?
Mtunzi Robert Heriel
CEO Taikon Publishers,
CEO Taikon Cleaning Services,
+255693322300
Mtunzi; Robert Heriel
+255693322300
Episode 01.
Sikumaanisha kuua! Wala sikuwahi kuwaza kuwa kuna siku nitakuja kuua mtu. Kwa kweli ningefanya dhambi zote, zote! Lakini sio dhambi ya kumwaga damu ya Mtu. Haya sasa nini kimetokea? Nani kaniloga! Mungu wangu!
Nimeua! Nimeua! Dimoso Mimi Nimeua!
*********
Jina langu naitwa Dimoso. Wengi huniita D, ukifika hapa kiwangwa hutonipata kama utaulizia Dimoso, ingawaje ni jina langu lakini wengi hawalifahamu. D ndio jina Maarufu zaidi. Hilo Mpaka mtoto mdogo ungemuuliza angekuleta mahali ninapoishi kama angenikosa kijiweni mahali ninapofanyia Kazi ya bodaboda, yaani udereva pikipiki.
Ni Miaka miwili sasa tangu niingie katika Kazi ya ubodaboda. Baada ya kumaliza Masomo yangu ya elimu ya juu katika Masuala ya tehama kwenye IT "Shahada ya information Technology" katika Chuo cha DIT. Nilikula msoto haswa nikiwa napambana huku na huku Kutafuta Kazi katika fani niliyosomea.
Lakini jitihada zangu ziligonga mrama na mipango kwenda kombo baada ya tumaini la Kupata Kazi kuyeyuka Kabisa.
Nilihisi kukata tamaa. Nuru ya mafanikio ilimezwa na wingu jeusi la kushindwa. Sasa nikaanza kulia na kujilaumu. Machozi yangu yangemwagika chini kwenye Udongo huenda miche iliyopo udongoni ingeweza kustawi. Yalikuwa machozi Mengi Sana. Lakini haikuwa hivyo. Upepo WA mashaka uliyapeperusha machozi yangu na kuyakausha bila kuacha alama. Ni kwamba hakuna aliyeyaona machozi yangu. Wala hakuna aliyejua kuwa ninalia. Hakuna aliyekaribu Wala aliyejali hali niliyokuwa naipitia.
Kilikuwa Kipindi kigumu Sana kwangu.
Maisha ya Dar es salaam yakanishinda sikujua kama nikiondoka Dar niende wapi. Kurudi nyumbani Morogoro isingewezekana. Ningerudi vipi nikiwa katika Hali kama Ile. Hali ya kushindwa, kuchoka na kukata tamaa. Wazazi wangu wangenitazamaje Mimi? Wangejisikiaje! Mimi kwao nilikuwa kama Jemadari wa vita waliyemuamini Sana. Shujaa wa ukombozi wao. Ati Leo nirudi kichwa chini Mikono nyuma. Hapana! Hiyo nilikataa.
Nayakumbuka Maneno yangu ya kishujaa niliyowaahidi yakuwa ninaenda Chuo kikuu Dar, nikimaliza nitawapa maisha Mazuri. Nitawabadilishia hali ngumu ya umaskini waliyonayo.
Nakumbuka siku Ile Mama yangu akiwa ananisindikiza kituo cha Magari, naikumbuka siku Ile vyema. Nikamwambia Mama; Wakati umefika Mama kuyala matunda yako. Kitambo kidogo unafurahia Kazi uliyoifanya Kwa Miaka mingi. Ulinisomesha ili uishi Maisha mazuri. Nakuahidi Mama. Jambo hilo halipo Mbali tangu Leo"
Siku Ile Mama yangu alikuwa anatabasamu Muda wote. Uso wake uliozingirwa pande zote na mikunjo ya lishe Duni ilipingana vilivyo na tabasamu lake. Niliona nuru ya tumaini ikichomoza katika macho yake. Akanikumbatia kisha akanong'ona nyuma ya mgongo wangu Akiwa amenikumbatia. Baba yako atajivunia sana. Natamani angekuwepo.
Hayo yote nayakumbuka.
Chaguo pekee nililokuwa nalo wakati huo lilikuwa kwenda Kiwangwa, huko Bagamoyo ambapo rafiki yangu wa Chuo aliniitia Kazi ya ujenzi, niende kama Saidia Fundi. Nikaenda. Huko ndiko maisha nilipoyaanzia.
*"
Ulikuwa Ujenzi wa kiwanda cha Nondo na bati. Ilikuwa Kazi ngumu Sana lakini sikuwa na budi kuifanya ili kunusuru maisha yangu. Tayari Mimi ni mwanaume. Unafikiri nani mwingine angeweza kunisaidia kama nisipojikaza na kujisaidia mwenyewe.
Wakati wote nilikuwa nikiishi kwa rafiki yangu. Nilikaa kwake karibu mwezi na nusu Mpaka pale Ujenzi wa kile kiwanda uliposimamishwa kwa Amri ya serikali.
Pesa niliyokusanya ilinisaidia kununua mahitaji yangu ya kuanzia maisha kama kitanda na godoro pamoja na vitu vingine vidogovidogo. Nilimuaga rafiki yangu. Kwa sababu alinifanyia uungwana Sana. Nilimshukuru kwa ukarimu na Msaada alionipatia kwa Kipindi chote nilichokuwa kwake. Ingawaje kilikuwa chumba kimoja na sebule lakini kwangu ilikuwa kama nyumba kubwa iliyonipa utulivu.
Sasa nikaanza Maisha ya kujitegemea, nikiwa nimechukua chumba na sebule mtaa wa tatu kama sio WA nne kutoka alipokuwa amepanga Rafiki yangu.
Nilitegemea mgogoro uliopo baina ya wamiliki WA kiwanda na serikali ungeisha mapema lakini miezi miwili iliisha mambo yakiwa hayaeleweki. Pesa ya akiba ilikuwa imeisha, Kodi nyingine ilikuwa IPO karibu.
Kichwa kilianza Kupata Moto. Nifanye Kazi gani hapa Kiwangwa. Bahati mbaya au nzuri niseme rafiki yangu yeye alibahatika Kupata Kazi serikalini mwezi Mmoja uliofuata baada ya kiwanda kufungwa. Hivyo yeye aliondoka na kwenda Wilayani Kiteto, huko Manyara. Yeye ndiye alikuwa mwenyeji wangu pale Kiwangwa. Hata hivyo tayari nilikuwa nimeshaanza kupazoea na kuzoeleka na wenyeji wa Kiwanga.
******"****
Sikubaliani na wanafalsafa wanaosema maisha ni uchaguzi wa Mtu binafsi. Nakataa. Kwa sababu kama maisha yangekuwa ni uchaguzi wa Mtu binafsi Mimi Wala nisingechagua maisha haya niliyokuwa nayo. Maisha ya kukimbizana na matatizo baada ya matatizo. Maisha ya Kulala njaa. Maisha ya kusimangwa na wenye nyumba.
Ingekuwa ni Maisha yangu ni uchaguzi wangu binafsi ningeenda kufunga chemchem ya matatizo na mikosi iliyokuwa inayaandama maisha yangu.
Mbele yangu alikuwepo Mzee wa Makamo, mwenye sura ya mzaha lakini ndevu zake alivyoziweka zilikinzana na sura yake. Aliziweka ndevu kama Mtu mtata hivi. Sijui kama unamjua Adolf Hitler jinsi alivyokuwa anaziweka ndevu zake. Kama unamjua basi ndivyo huyu Mzee wa Makamo alivyoziweka. Lakini tofauti yake na Hitler ni kuwa Mzee huyu alikuwa na sura ya mzaha.
tuliingia katika mkataba wa pikipiki. Kwamba Mimi nitachukua pikipiki na kuitumia kwa miezi kumi na mbili kisha itakuwa yangu. Lakini itanipasa kila siku nimpelekee Mzee huyu shilingi elfu kumi za kitanzania. Bila kurusha hata siku Moja.
Ikitokea nimerusha siku Moja basi mkataba nimeuvunja mwenyewe na pikipiki ataninyang'anya.
Kuhusu matengenezo ya pikipiki vyote nitafanya Mwenyewe.
Sikuwa na namna zaidi ya kukubali ingawaje masharti yalikuwa magumu. Muda ule nilichokuwa nawaza ni namna ya kuweza kuishi kwa Muda ule. Kupata chakula na Kupata pesa ya Kodi ya mahali ninapoishi ambapo ilikuwa imebaki mwezi Mmoja tuu.
Nikachukua bike nikarudi nayo nyumbani. Nikajiweka zangu kitandani, kisha nikashusha pumzi nzito unhuu! Nikajilaza kitandani, Mawazo yakaanza kunipitia. Daah! Leo nimekuwa bodaboda! Sijui nitaifanya Kazi hii kwa Muda gani. Lakini Sina namna. Muhimu nifanye nimiliki hiki chombo. Yatakuwa mafanikio makubwa Sana.
Punde simu ikaita. Alikuwa ni Mama. Nikapokea;
" Hello Mama! Shikamoo"
" Marhaba mwanangu. Unaendeleaje huko"
" Nashukuru Mungu Mama" Nikasema nikiwa nimeiweka Sauti yangu kwa namna nzuri kuonyesha Sina tatizo.
" Naomba unitumie hata elfu mbili nikanunue unga nipike. Mboga nilichuma Shambani. Sina hata pesa mwanangu"
Mama aliongea kwa sauti ya unyonge Jambo ambalo liliamsha hisia zangu za ndani.
" Usijali Mama, nakutumia, pole Sana mama kila kitu kitakaa sawa"
Nikasema kisha simu ikakatika, nahisi salio la mama lilikuwa limeisha.
Sikuwa hata na Akiba ya Mia Mbovu.
Kama ni kupekua kwenye mifuko ya suruali Kazi hiyo niliifanya Jana. Hakuna pembe Wala Kona ambayo sikuipekua siku ya Jana nikiwa natafuta hata Mia mbili ili niweze Kupata pesa ya mandazi.
"Niende kwa nani nikamkope?" Nikawa najiuliza huku nikiwa nakuna kichwa. Nilikuwa nimetingwa haswa. Mama yangu alale njaa na Mimi nipo. Hapana.
Nikatoka, nikaenda kwenye Duka ambalo lilikuwa mtaa wa pili tuu. Nilijaribu kumkopa muuza Duka lakini alinikatalia akaniambia anachoweza kunisaidia ni kunikopesha bidhaa zake kama unga au mafuta. Sasa hata kama akinikopesha unga au mafuta nitayatumaje Morogoro kwa Mama.
Nikaondoka zangu, lakini nikasema si bora ningechukua nikayatumie mwenyewe. Nikarudi tena lakini mara hii muuza Duka alikataa kabisa hata kunipa bidhaa hizo.
Nilikasirika Sana. Njiani nilitembea kama Kipofu. Nilikuwa na msongo wa mawazo.
Katika Hali isiyo ya kawaida nikajikuga nimeanguka chini na gari likiwa limenigonga. Nikapoteza fahamu. Sikujua nini kiliendelea.
********
Nimekuja Kupata fahamu ni masaa mawili baadaye. Nikiwa katika kituo cha afya cha Kiwangwa. Napiga kelele. Mama! Mama! Jamani mama yangu!
Anaingia mwanamke aliyevalia nguo nyeupe, baadaye nilijua NI muuguzi.
"Vipi unaendeleaje Dimoso" Yule muuguzi akanisalimu akiwa ameikumjua sura yake kwa tabasamu lenye kuweza kutibu.
" Nataka kuongea na Mama. Tafadhali naomba simu yangu"
" Dimoso, hukuletwa hapa na simu. Waliokuleta hapa Mmoja wapo alisema anaitwa Bihawa, mwanamke ambaye ni Jirani yako akasema unaitwa Dimoso"
" Okay! Anyway naomba simu yako nimpigie Mama. Tafadhali"
" Usijali Dimoso, nitakupa. Nataka Kwanza nikupe matibabu kisha mengine yataendelea "
" Hapana! Mimi naendelea vizuri! Nipe simu niongee na Mama yangu tafadhali"
Hapo nilikuwa nimeamka kitandani, niliongea Sauti ya ukali Sana huku nikiwa nimetoa macho. Nikatoka kuamka lakini mkononi nilikuwa na Dripu. Iliyonitonesha mahali nilipokuwa nimechomwa.
Mtonesho huo uliita maumivu katika Maeneo mengine ya mwili wangu. Nikaanza kuhisi maumivu kwenye Paja la kulia, nyuma ya mgongo na kwenye bega.
Nikagugumia, aaaahh!
" Tulia Dimoso bado hauendelei vizuri. Lala! Haya jiegemeze hapo kwenye MTO"
Muuguzi akasema Sauti yake ikiwa Mbali na upole.
Nikajiegemeza kwenye ule mto wa kile kitanda. Yule muuguzi akaja karibu akanipa simu. Nikaipokea. Nikabonyeza bonyeza namba, kisha nikaweka sikioni. Ikaita lakini haikuwa inapatikana. Nikajaribu tena ikawa haipatikani.
"Shiit" nikasema huku Uso wangu ukionyesha kukata tamaa.
" Vipi haipatikani" muuguzi akaniuliza huku anitazama kwa macho ya kupima hisia zangu. Nikamtazama bila kusema kitu.
"Itakuwa simu yake imezima chaji. Maskini huenda alisubiri mpaka akachoka" nikasema kwa sauti ndogo. Muuguzi akiwa ananitazama. Kisha akachukua kipima mapigo ya moyo na kipima presha cha kisasa akanipima. Kabla hajamaliza Mlango ukafunguliwa Mimi ndiye niliyegeuka muuguzi hakugeuka alikuwa akiendelea kunipima. Alikuwa ni Bihawa ambaye ni mwanamke Jirani yangu.
Bihawa alikuwa amebeba hotpot pamoja chupa la Maji na machungwa. Akawa amesimama huku akinitazama kwa macho ya huruma. Baada ya muuguzi kumaliza kunipima akaniambia ninaendelea vizuri.
Kisha akaenda kwenye meza iliyokuwa mule kwenye Ile wodi akachukua kifuko ambacho bila Shaka alikuwa amekuja nacho. Akatoa Dawa kadhaa kisha akawa ananipa maelekezo;
" Hii ni antibiotics, utakunywa mbili mara tatu. Kila baada ya saa nane.
Hii ni antipain, Dawa ya kutuliza maumivu. Utakunywa nayo hivyohivyo. Kila ukinywa hii antibiotics unameza na hii. Usipishanishe Muda. Sawa.
Nimesahau, wewe ulisema ni mkewe au ?"
Muuguzi akamgeukia Bihawa, mwanamke aliyevalia baibui ambaye harakaharaka utagundua ni mtu mwenye kuipenda Dini yake.
Swali hilo likanifanya nimuangalie Bihawa, naye Bihawa alikuwa akinitazama kisha akamjibu muuguzi huku akiwa ananitazama;
" Aam aa! Ni majirani tuu. Yeye ni jirani yangu"
" Mbona kigugumizi bidada! Okay. Nashindwa kukuachia maagizo. Huyu anaishi na Nani kwani?"
" Nipe tuu maagizo muuguzi"
" Hapana! Nahitaji kumpa maagizo mtu anayeishi naye. Sio kila Jambo ninaweza kukuambia wewe kumhusu Mgonjwa"
" Nimekuambia niambie Mimi. Nani aliyemleta hapa? Sio Mimi niliyemleta? Nani kamletea chakula hapa? Ni Mimi au hunioni?"
Nilipoona wanataka kugombana ikabidi nizungumze.
" Muuguzi, Mimi pale naishi mwenyewe. Mji huu Mimi ni mgeni. Hivyo Bihawa anaweza tuu kusikia unachotaka kumwambia"
" Oooh! Kumbe! Sasa si angesema hivyo. Sina haja ya kumpa maelekezo kukuhusu. Sheria zangu za Kazi haziruhusu. Kama ni Kula kwa wakati nitasimamia Jambo hilo mwenyewe.."
Muuguzi akamaliza kisha akatoka, Muda huo Bihawa akawa anamsindikiza na macho ya chuki.
Alipotoka na kufunga mlango. Bihawa akaachia bonge la msonyo. Kisha akanigeukia.
" Huyu nesi hamnazo huyu. Atakuwa anakutaka sio Bure."
" Mmh! Sidhani. Nafikiri anafanya Kazi yake"
" D huna ujualo kuhusu Sisi wanawake. Tangu nimeingia hapa nimemwona namna anavyokuangalia na anavyokuongelesha"
" Hapana Bihawa! Ni Mtazamo wako tuu"
" Unamtetea si ndio?"
" Simtetei! Haya tuachane na hayo!"
" Kama anataka Umalaya si akafanye huo Umalaya wake. Mtcheeeewwi!" Akasonya.
Kisha akatoa lile hotpot kwenye kikapu na Sahani akapakua chakula. Akanipa, kisha akaendelea kumenya chungwa Muda wote ananiangalia kwa macho ambayo sasa nilianza kuyaelewa kwa namna nyingine Kabisa.
Baada ya kula chakula, akaniaga lakini nilikumbuka kuhusu simu yangu. Nikamuuliza simu yangu iko wapi. Akaniambia alipofika eneo nilipokuwa nimegongwa kulikuwa na watu wengi. Hakunikuta na simu.
Nikajua simu yangu ilikuwa imeibiwa.
Kesho yake niliruhusiwa, aliyenileta nyumbani alikuwa ni Yule muuguzi aliyekuwa ananiihudumia tangu siku ya Kwanza. Jina lake alikuwa akiitwa Cathy.
Tulipofika nyumbani kwangu nilimkuta Mzee Abeid ambaye ndiye mwenye Ile bodaboda. Moyo wangu ukapiga paah! Cathy aliona Hofu yangu tukiwa tunakaribia. Akaniuliza kulikoni nikamweleza kwa kifupi hali ilivyokuwa.
Tayari tulikuwa tumefika, nikamsalimu Mzee Abeid naye akanipa Pole ingawaje nilijua alichokifuata pale.
Nikamwambia ngoja niingie ndani alafu nataka kwaajili ya mazungumzo.
Akaniambia hajaja pale kuzungumza na Mimi.
Nikaingia ndani nikiwa na Cathy. Tulipofika ndani Cathy akatoa noti mbili za elfu kumikumi akanipa.
" Kampatie hizi huyo Mzee" akasema,
Nikatoka nikiwa nimezibeba zile pesa. Nikamkabidhi Mzee Abeid, nikamuona akijichekesha hovyohovyo kisha tukaagana.
********
Miezi mitatu ilipita nikiwa tayari nimezoea Kazi ya ubodaboda. Cathy ndiye aliyekuwa amenilipia shilingi Laki tatu za kujiunga kwenye kijiwe cha bodaboda.
Kila kijiwe cha bodaboda kilikuwa na Ada ya kujiungia kwa mara ya Kwanza kwa dereva bodaboda mpya. Bila kutoa Ada hiyo usingeruhuziwa kukaa kwenye kijiwe au kituo hicho cha bodaboda.
Mahusiano yangu na Cathy yalizidi kuimarika ingawaje hakuna miongoni mwetu aliyemuelezea Mwenzake hisia zake. Hata hivyo mioyo yetu ilikuwa kama sarafu moja. Nilihisi kumpenda Sana Cathy naye alionyesha hivyo.
Cathy alikuwa mwanamke Mzuri Sana. Msomi mwenye elimu ya Shahada ya uuguzi. Macho yake mazuri yenye huruma yalifanania Kazi yake ya kuhudumia wagonjwa. Sura yake ilikuwa nzuri pengine hiyo ilimfanya watu wengi wamuone kama ananyodo. Umbo lake lililopangika lilivutia Sana hasa alipokuwa Amevaa Sare zake za Kazi.
Nilikuwa najua Cathy anasubiri kwa Hamu nimwambie ninampenda kisha safari yetu ya Mapenzi ianze upya.
Ni miezi mitatu sasa imepita. Sijui nianzie wapi kumueleza ukweli wa Moyo wangu Binti huyu. Kipato changu ni Duni. KAZI yangu ya kufukuzana na upepo. Ubodaboda. Nitampa nini mwanamke msomi mwenye Kazi yenye kipato zaidi yangu. Nikifikiria hali yangu hiyo ilinifanya nifute Kabisa Wazo la kumwambia Cathy ukweli.
Kama haitoshi, tetesi na duru za mtaani nilizokuwa nazipata zilikuwa zinasema matajiri wa Kiwangwa walikuwa wakiingia na kutoka wakipigana vikumbo kulipata penzi la Cathy. Nilikata tamaa Kabisa niliposikia tajiri anayemiliki kile kiwanda cha Nondo na bati nilichokuwa nafanyia Kazi pia anamfuatilia Cathy. Embu fikiria hata wewe, ungethubutu.?
Unaweza kuniambia nijaribu, mwanaume kujaribu na kujiamini. Hata Mimi kuna wakati nafikiri kama wewe. Lakini Sauti nyingine hunong'ona masikioni mwangu ikiniambia akinikataa nitakosa hata ule ukaribu mdogo niliokuwa nao dhidi yake.
Nikifikia hapo naghairi.
Bihawa naye hakuwa nyuma, yeye ndiye alikuwa ananiona karibu kila siku kwani alikuwa ni lazima kila jioni aniletee chakula cha usiku. Nilishindwa kumkatalia na ningeanzaje kumkatalia mwanamke ambaye alinisaidia kwa gharama zake Kunichukua nikiwa sijitambui siku Ile ya ajali Mpaka Hospitalini kisha akawa ananiletea chakula na hata gharama za matibabu yeye ndiye aliyetoa. Ningewezaje? Nakuuliza!
Licha ya kuwa Bihawa alikuwa mwanamke Mzuri mwenye stara lakini Moyo wangu haukuanguka kwake. Sikuwa nahisia naye. Lakini nitamlipa nini kwa haya anayoendelea kunifanyia. Kila anapokuja kwangu nahesabu deni linaongezeka juu yangu kwake.
***********
Jioni Moja nikiwa nimetulia ghetto kwangu nilimkumbuka Mama yangu. Ni miezi kadhaa imepita sijawasiliana naye Hali ya majuto na kujilaumu kwa kutokumjali MMA yangu vikaukumba moyo wangu. Haikuwa kawaida yangu Mimi kukaa Muda wote huo bila kuwasiliana na Mama yangu. Kikawaida ilikuwa kila siku lazima niwasiliane na mama. Lakini tangu nilipopata ajali namba yake haikuwa imepatikana tena.
Uzembe nilioufanya ni kuwa namba niliyokuwa naitumia haikuwa namba iliyosajiliwa kwa majina yangu. Hivyo kuirudisha kwa matumizi hata baada ya siku kuibiwa isingewezekana. Nilikuwa najilaumu Sana kwa Jambo hilo.
Msomi mzima mwenye Shahada ilikuwaje sikutambua umuhimu wa kutumia laini iliyosajiliwa kwa majina yangu mwenyewe.
Nilikuwa nawaza nikijilaumu.
Ninakaakiba ka Laki tatu, ikifika Laki tano nitaenda Morogoro chapu kumwona Mama. Atafurahi Sana. Nitambebea na zawadi ya nguo.
Bado nilikuwa nawaza.
Wakati nafikiri hayo, punde anaingia Bihawa akiwa amebeba chakula. Kama kawaida Yale alikuwa amevaa hijabu.
Jambo Moja ujue ni kuwa wakati wote huo tangu wakati wa ajali Mpaka wakati huu Bihawa alikuwa akifanya mambo hayo kwa usiri Mkubwa majirani bila kujua ingawaje baadhi ya watu walishaanza kuhisi mahusiano yetu.
Alikuwa kaleta Wali Samaki, kama kawaida lazima aje na chungwa.
Tofauti na siku zote mara hii Bihawa aliniomba Jambo;
" D samahani naomba kwenda msalani"
Sikuwa na ubishi nikamruhusu. Akaniacha sebuleni akaingia zake chumbani ambapo huko kuna Choo na bafu.
Nikawa nakula zangu lakini huko nje manyunyu yakaanza, kwani ulikuwa msimu wa Mvua.
Mpaka nakaribia kumaliza chakula Bihawa alikuwa hajatokea.
Huko Nje Mvua ilikuwa imeshachachamaa.
Mara Mlango unagongwa, Nani atakuwa anagonga Mlango usiku huu WA saa tatu kwenda Sana nne. Kikawaida Mimi sinaga wageni zaidi ya Cathy, Bihawa au mwenye nyumba.
Na mwenye desturi ya kuja usiku na Bihawa ambaye nipo naye. Cathy' hajawahi kuja usiku hata siku Moja ila akijaga anaondoka usiku mnene tofauti n Bihawa.
Mwenye nyumba yeye Hanaga hayo mazoea na haishi hapo. Majirani zangu wao hatujawahi kusumbuana usiku.
Nikafika Mlango nikauliza Nani.
Mara nasikia Sauti Cathy, " Ni Mimi mpenzi. Fungua Mvua inaninyeshea"
Moyo unapiga Paaah!
Hofu na kuchanganyikiwa kwa pamoja vilinivamia.
"Fungua D nalowa"
Hapohapo kabla sijafungua nasikia Sauti kwa nyuma ikiniambia ni Nani. Nageuka namkuta Bihawa amevaa kanga tuu kaipitisha kwenye makwapa ametoka kuoga. Amesimama katikati ya mlango unaotenganisha Sebule na chumba.
" Fungua Baby nalowa jamani"
Inanibidi nifungue. Nafungua mlango Cathy anapita upesiupesi akiwa amelowa chapachapa Akiwa kavaa nguo zake za kazini.
Inaendelea;
Nini kitatokea..?
Usikose sehemu ya Pili?
Mapenzi au Kazi?
Je Pesa Itakupa furaha?
Ni upi uchaguzi sahihi katika Mapenzi?
Uhalifu usiokusudia unapotokea nani atawajibika?
Mtunzi Robert Heriel
CEO Taikon Publishers,
CEO Taikon Cleaning Services,
+255693322300