Mwenyekiti wa TPSF, Bi. Angelina akizungumzia changamoto ya wafanyabiashara sekta binafsi

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
22,462
25,979

WADAU WA TPSF 'WAICHARUKIA' TRA / WADAI KUKADIRIWA KODI ZA 'UWONGO'/ RUSHWA YATAJWA



View: https://m.youtube.com/watch?v=j869hATU_8U

Biashara ya usafirishaji kwa asilimia 75 tunafanya na nchi za kusini za SADC, asilimia 25 iliyobaki tunafanya na Bururundi, Rwanda hilo serikali iliangalie

Sheria za kodi za EAC kutumika SADC ni kikwazo

Makampuni ya usafirishaji yamesajiliwa nje ya Tanzania kutokana na sheria za kodi za Tanzania kutokuwa rafiki

Tunajivunia $260 za bandarini lakini $6,000 zinakwenda kwa wasafirishaji wa malori ambayo makampuni yake yamesajiliwa nje ya Tanzania, yaani faida $6,000 kwa kila Lori inakwenda nje haibaki Tanzania. Tunapoteza pakubwa.


Madereva wa malori ya makampuni ya kitanzania wanasimamishwa njia nzima kila kituo cha ukaguzi katika barabara za Tanzania kuulizwa nyaraka hivyo hubeba rundo la makabrasha , lakini yale malori ya makampuni ya nje hayasimamishwi.

Tunasema tunataka Kariakoo iwe kitovu cha biashara eneo hili la Afrika ya Mashariki lakini bidhaa zinazouzwa Tanzania ni ghali kuliko bidhaa hiyo hiyo inayouzwa nchi jirani iliyopita bandari ya Dar es Salaam kutokana na kodi


Wafanyabiashara wa Tanzania na nchi jirani wanaona bora kwenda kununua bidhaa nchi jirani kuja kuuza Tanzania kutokana na bei kuwa ndogo nchi jirani wakati ilipita hapa bandarini Dar es Salaam

Hakuna nchi unaweza kununua bidhaa dukani halafu ukitoka unaanza kuulizwa risiti na task force ya idara ya kodi, ni Tanzania tu huwezi kuulizwa risiti Dubai, Zambia n.k Wafanyabiashara wameacha kuja Kariakoo kwa kuogopa kuulizwa risiti kwa kuviziwa.

Idara ya Research ya TRA ijifunze kuweka kodi zinazoipa Tanzania unafuu ili kuvutia wafanyabiashara wa SADC na EAC waje wanunue bidhaa zilizoagizwa nje Kariakoo

TRA watafute mfumo mpya utakaoondoa usumbufu wa kuviziwa kuombwa risiti na kufanyiwa ukaguzi, maana mfumo wa EDF umepitwa na wakati hausomani na mifumo mingine ....


View: https://m.youtube.com/watch?v=nV4eqpD9PE0
 
Yawezekana ni kweli,tatizo lingine lililopo ni uwepo wa madalali wa bidha ambao nao inachangia kuongezeka kwa bei ya bidhaa Kwa mlaji wa mwisho.
 
Serikali imetia pamba masikioni


TOKA MAKTABA
19 April 2024 Paul Makonda alifanya ziara ya kustukiza mpaka wa Namanga na kutoa maagizo mazito, sasa sijui maofisa wa TRA leo wamejua RC Makonda yupo labda likizo hayupo


View: https://m.youtube.com/watch?v=4ZzikxDmkxk
Makonda ametembelea mpaka kimataifa wa Tanzania na Kenya "Namanga" kukagua utendaji wa kazi katika ofisi mpakani hapo inayojumisha ofisi za Mamlaka ya Mapato TRA kujua changamoto zao ili aina ya huduma mpakani wananchi na wageni wawe na furaha ....
 
Yupo wapi mkuu wa mkoa wa Arusha sakata hili la Namanga, lango kuu la biashara Afrika ya Mashariki ? Mgomo wa mawakala wa forodha dhidi ya maofisa wa TRA wanaozuia biashara zinazovuka mpaka wa Tanzania na Kenya

1721931013093.png
 
TOKA MAKTABA
19 April 2024 Paul Makonda alifanya ziara ya kustukiza mpaka wa Namanga na kutoa maagizo mazito, sasa sijui maofisa wa TRA leo wamejua RC Makonda yupo labda likizo hayupo


View: https://m.youtube.com/watch?v=4ZzikxDmkxk
Makonda ametembelea mpaka kimataifa wa Tanzania na Kenya "Namanga" kukagua utendaji wa kazi katika ofisi mpakani hapo inayojumisha ofisi za Mamlaka ya Mapato TRA kujua changamoto zao ili aina ya huduma mpakani wananchi na wageni wawe na furaha ....

Itakuwa sumu ilianzia hapa?
 
Back
Top Bottom