TANZIA Mwasisi wa Mapinduzi Zanzibar, Mzee Hassan Nassor Moyo afariki dunia

Mwanasiasa mkongwe na mwasisi wa Mapinduzi Zanzibar, Hassan Nassor Moyo amefariki usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake mkoani Tanga
RIP! Naomba kuuliza , kwake ni Tanga, halafu akwa mwasisi wa siasa za Zanzibar, kwa vipi?
 
Hivi ukiwa wakwanza kupost mtu anapata bakshishi yoyote toka Jf...

Wengi Wana haribu hii forum. Nashauri Moderator waongeze ban hasa kwa wale wanao tukanaka.
Mkuu breaking news mara nyingi huja na heading tu na bila hata ya briefing. Baadae hufata maelezo ya kutosheleza. Nafahamu wengi tunakuwa na hamu sana ya kupata taarifa kamili. Nashauri reaction ya kwanza iwe ku google kwa mtaarifiwa.

By the way, may his soul rest in eternal peace. Aamin.

Alipigana sana kuwaweka Wazanzibar pamoja na alifanikiwa mpaka CCM wakamfuta uwanachama despite ya kuwa kwa wakati ule ndiye alikuwa mwanachama mkongwe zaidi kuliko wote na ni mmoja wa waanzilishi wa CCM na mwanzilishi wa Umoja wa Vijana wa ASP. Concept ya UVCCM iliigwa kutokana na idea kutoka kwake. Ni mzee wa mabadiliko. Ndiye aliyemshawishi Maalim na Karume wapatane na kuitisha referendum ya gov ya national unity na akubali matokeo 2010 na kumwachia Dr Shein aongoze serikali ya Umoja wa Kitaifa lakini Shein akaja kubadilika.
 
Back
Top Bottom