Pre GE2025 DSM Mwandishi wa habari, Khalifa Said: Hakuna dalili yoyote inayoashiria kuwa CHADEMA kweli watazuia uchaguzi usifanyike

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwa mujibu wa Khalifa, hakuna dalili yoyote inayoashiria kuwa CHADEMA kweli kuzuia uchaguzi usifanyike, wala hakuna dalili za mageuzi yoyote kufanyika kabla ya uchaguzi.

Ameeleza kuwa njia pekee ambayo kauli mbiu hiyo inaweza kuwa na maana ni ikiwa itachukuliwa kama mzaha.

Khalifa anahoji kuwa kauli mbiu hiyo ni mwanzo mbaya kwa uongozi mpya wa CHADEMA kwa sababu inaweka lengo lisiloweza kufikiwa. Pia, amesema kuwa uongozi huo haueleweki kuhusu ushiriki wake katika uchaguzi ujao.

"Lengo hilo si la uhalisia, na kauli mbiu yenyewe inazua mkanganyiko mkubwa," ameandika.

Ameeleza kuwa ukosefu wa msimamo thabiti unaweza kuathiri jitihada za chama katika kukusanya fedha, kwa kuwa wadau watajiuliza fedha hizo zinahitajika kwa shughuli gani hasa.

"Ili kuhamasisha wanachama, kunahitajika uwazi na uthabiti wa msimamo. Hivi sasa vyote vinakosekana," amesema.

Kwa maoni yake, Khalifa anasema kuwa uongozi mpya wa CHADEMA ulipaswa kuchukua msimamo thabiti mara tu baada ya kuchaguliwa kwa kutangaza kuwa kitashiriki uchaguzi, bila kujali mazingira.

Soma Pia: Tundu Lissu: Kauli ya No Reform No Election hatujasema tunasusia Uchaguzi. Tutaongea na Rais Samia lugha atakayoielewa

Soma Pia: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025


Amedai kuwa kwa kufanya hivyo, chama kingeweza kukusanya fedha kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi na kuhamasisha wanachama kujiandikisha.

Aidha, ameonya kuwa kwa hali ilivyo sasa, CHADEMA haina ushawishi wa kulazimisha mageuzi yoyote kabla ya uchaguzi, na kwa hivyo, kauli mbiu ya "No Reform, No Election" inachanganya zaidi badala ya kusaidia.

Pia, amesema kuwa msimamo huo unahujumu juhudi zozote za kushirikiana na vyama vingine vya upinzani ili kuunda muungano imara wa kushindana na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

"Unawezaje kuwa na mjadala wa kweli wa kuunda umoja wa upinzani dhidi ya CCM, ilhali chama kinachoonekana kuongoza upinzani kina kauli mbiu ya ‘No Reform, No Election’ kama sera yake?" amehoji Khalifa.
🤔🤔 💭
 
Kwa mujibu wa Khalifa, hakuna dalili yoyote inayoashiria kuwa CHADEMA kweli kuzuia uchaguzi usifanyike, wala hakuna dalili za mageuzi yoyote kufanyika kabla ya uchaguzi.

Ameeleza kuwa njia pekee ambayo kauli mbiu hiyo inaweza kuwa na maana ni ikiwa itachukuliwa kama mzaha.

Khalifa anahoji kuwa kauli mbiu hiyo ni mwanzo mbaya kwa uongozi mpya wa CHADEMA kwa sababu inaweka lengo lisiloweza kufikiwa. Pia, amesema kuwa uongozi huo haueleweki kuhusu ushiriki wake katika uchaguzi ujao.

"Lengo hilo si la uhalisia, na kauli mbiu yenyewe inazua mkanganyiko mkubwa," ameandika.

Ameeleza kuwa ukosefu wa msimamo thabiti unaweza kuathiri jitihada za chama katika kukusanya fedha, kwa kuwa wadau watajiuliza fedha hizo zinahitajika kwa shughuli gani hasa.

"Ili kuhamasisha wanachama, kunahitajika uwazi na uthabiti wa msimamo. Hivi sasa vyote vinakosekana," amesema.

Kwa maoni yake, Khalifa anasema kuwa uongozi mpya wa CHADEMA ulipaswa kuchukua msimamo thabiti mara tu baada ya kuchaguliwa kwa kutangaza kuwa kitashiriki uchaguzi, bila kujali mazingira.

Soma Pia: Tundu Lissu: Kauli ya No Reform No Election hatujasema tunasusia Uchaguzi. Tutaongea na Rais Samia lugha atakayoielewa

Soma Pia: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025


Amedai kuwa kwa kufanya hivyo, chama kingeweza kukusanya fedha kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi na kuhamasisha wanachama kujiandikisha.

Aidha, ameonya kuwa kwa hali ilivyo sasa, CHADEMA haina ushawishi wa kulazimisha mageuzi yoyote kabla ya uchaguzi, na kwa hivyo, kauli mbiu ya "No Reform, No Election" inachanganya zaidi badala ya kusaidia.

Pia, amesema kuwa msimamo huo unahujumu juhudi zozote za kushirikiana na vyama vingine vya upinzani ili kuunda muungano imara wa kushindana na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

"Unawezaje kuwa na mjadala wa kweli wa kuunda umoja wa upinzani dhidi ya CCM, ilhali chama kinachoonekana kuongoza upinzani kina kauli mbiu ya ‘No Reform, No Election’ kama sera yake?" amehoji Khalifa.
Tumezoea kila harakati za ukombozi zikianza kuwa na mashiko wanaibuka watu kwa makusudi kufifisha ila wakati huu naamini kabisa wanaenda kufeli No reform No Election ndio habari ya mjini
 
Ni kweli kabisa kwamba hakuna uwezekano wa kuzuia kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu Mwaka huu wa 2025.
Aidha, ni kweli kabisa kwamba Hoja za Watu wa CHADEMA ni za kweli, pia ni za msingi. Hoja zao zina mashiko kuhusiana na Kukosekana kwa Mamlaka zinazoaminika kwa ajili ya kusimamia Uchaguzi ulio huru, wa HAKI na ulio wa Wazi.

Jambo muhimu zaidi la kuzingatiwa ni kwamba: KAMWE CCM HAITAWEZA KUKUBALI KWA HIYARI KUBADILISHA MIFUMO YA UCHAGUZI. NA KAMWE CCM HAITAWEZA KUKUBALI KWA HIYARI KUBADILISHA KATIBA YA NCHI.

KAMWE HAUPO KABISA UWEZEKANO WA KUBADILISHA KATIBA YA NCHI KWA NJIA ZA KIDEMOKRASIA. HAUPO UWEZEKANO!

Kwa bahati mbaya sana, huu ndio Ukweli mchungu Sana kupita kiasi!

Ila kama wakikutana na ACT Wazalendo na kuja na msimamo wa pamoja wa Bara na visiwani lazima Maza atatoka kwenye comfort zone yake. Kama kwa sasa tu ameshaanza kutumia pesa ya kufa mtu kufanya kampeni .... shaking kidogo tu inahitajika maana yuko so desperate.
 
Ila kama wakikutana na ACT Wazalendo na kuja na msimamo wa pamoja wa Bara na visiwani lazima Maza atatoka kwenye comfort zone yake. Kama kwa sasa tu ameshaanza kutumia pesa ya kufa mtu kufanya kampeni .... shaking kidogo tu inahitajika maana yuko so desperate.
Unajidanganya, hata viungane vyama vyote kabisa vya upinzani ili kushinikiza jambo hili bado hawatafanikiwa.
Kumbuka: Ccm ni Chama Cha siasa Cha Itikadi za Ujamaa/Ukomunisti ambako kwa kawaida Majeshi ya Watawala ndiyo ambayo huwa yanahusika na masuala yote kabisa ya kazi na shughuli za Chama. Wale ambao huwa wapo kwenye Vyama hivyo wanaoonekana hadharani kuwa ni Viongozi wa Chama Mara nyingi sana huwa ni Wawakikishi tu wa Majeshi, lakini kazi zote na Operesheni zote kabisa za Chama huwa zinafanywa na Jeshi.
Huu ndio utamaduni wa Wakomunisti popote pale duniani.
 
Unajidanganya, hata viungane vyama vyote kabisa vya upinzani ili kushinikiza jambo hili bado hawatafanikiwa.
Kumbuka: Ccm ni Chama Cha siasa Cha Itikadi za Ujamaa/Ukomunisti ambako kwa kawaida Majeshi ya Watawala ndiyo ambayo huwa yanahusika na masuala yote kabisa ya kazi na shughuli za Chama. Wale ambao huwa wapo kwenye Vyama hivyo wanaoonekana hadharani kuwa ni Viongozi wa Chama Mara nyingi sana huwa ni Wawakikishi tu wa Majeshi, lakini kazi zote na Operesheni zote kabisa za Chama huwa zinafanywa na Jeshi.
Huu ndio utamaduni wa Wakomunisti popote pale duniani.
Sema labda mda bado. Diku ikifika hakuna hsyo ya Ukomunist wa baba yake ukomunist.
 
Back
Top Bottom