Msigwa umechemka kumsifia Kikwete

huyu msigwa ni wakupuuzwa tu, mm ndani ya chadema mtu ninayemwamini ni mnyika na mdee baasi! the rest ni wasakatonge.
 
Siyo kweli kwamba jk kwa uhuru WA habari Ana sifa kuliko makomeo? Hilo linahitaji kubishana kweli! Mnashangaa msigwa kusema ukweli!
 
Mtu kaacha kuchunga kondoo wa Bwana kakimbilia siasa, unaanzaje kumuamini mtu wa namna hii?!
 
Amemsifia akasema nini? Tukijua amemsifia nini ndio tunaweza kusema ni sifa asizostahili au la!
we jamaa naona chuki binafsi inakutafuna. jk anastahili sifa aliyopewa na msigwa. nenda tena shule ya propaganda
Kweli watz tubadilike,yani inakua sifa za marehemu akiwa hai mbaya,akifa oooh alikua mzuri,wakati ule mlimsema sana JK leo kamaliza muda wake amegeuka mzur?
 
Makamanda JK hagombei tena urais pambaneni na tingatinga Magufuli.

JK, sasa hivi ana deal na issues za kimataifa kutatua migogoro.

Mnamkubuka JK Ahahhahahahaha!!!
 
Hivi upinzani msimamo wao ni upi? Kuanza kumkumbuka Kikwete mapema hivi ni kujichimbia kaburi.

Msigwa kuanza kumsifia Kikwete bungeni inanipa picha kuwa upinzani unakufa mbele ya Magufuli. Mnashindwa kujenga hoja, mangapi Kikwete mlimsema leo tena mnamkumbuka. Upinzani ovyo kabisa hamna msimamo. Acha CCM watuongoze tu


Ukweli unatabia moja,haufi!

"Mimi nasikitishwa na jambo moja, tumefika hapa kutokana udhaifu wa Rais Kikwete, uzembe wa bunge na wabunge na tumefika hapa kutokana na upuuzi wa CCM, nasema hivi nina ushahidi.” Mnyika (2012)

Ni kweli si dhambi kuanza kumsifia JK lakini kwa jinsi walivyomkataa JK leo wanamkumbuka. Ni unafiki.


mtoa hoja kama unachuki aidha na msigwa binafs ama na wapinzan kaa ujumla ni bora ukae kimya walau utaonekana muungwana kuliko kuthibitisha ujinga wako kwa kuendekeza maslah ya chama badala ya taifa.. alichosema msigwa kwanza hakusema serikal
ya awamu ya nne alisema yafuatayo akihojiwa na mwandish wa ITV asubuh kuzungumzia bajet ya serikal na wala sio bungen nanukuu kipande cha sentens

" nampongeza kikwete kwan aliruhusu uhuru wa vyombo vya habar na uhuru wa mawazo na ushaur kutoka kwa wengine japo alikuwa sio
mtekelezaj " mwisho wa kunukuu sasa hebu nambie huo upinzan unakufaje hapo ama
masigwa amechemkaje hapo... ndo maana nchi inazid kuliwa
na wajanja wakat nyumbu kama ninyi badala ya kuweka mslah ya taifa mnaweka maslah ya chama
ambao
kimeshikwa
na wachache
 
Sasa mbona wengine wanamponda kwa kusaini sheria ya mtandao ambayo wanadai inakandamiza uhuru wao?
Kinachopondwa sio tu kusaini ile sheria ila kusaini bila kurekebisha kwa baadhi ya vipengele ambavyo haviko sawa na baadhi ya maandishi namna yalivyokaa

Mfano: inatamka kifungo kisichopungua miezi 6 au faini isiyopungua mil 2 au vyote kwa pamoja

Hapa ukiangalia kwa makini utagundua inaelezea kiwango cha chini tu cha adhabu bila kuweka ukomo wake yaani ISIYOZIDI AIDHA MIEZI KADHAA AU MILIONI KADHAA.
 
Kinachopondwa sio tu kusaini ile sheria ila kusaini bila kurekebisha kwa baadhi ya vipengele ambavyo haviko sawa na baadhi ya maandishi namna yalivyokaa

Mfano: inatamka kifungo kisichopungua miezi 6 au faini isiyopungua mil 2 au vyote kwa pamoja

Hapa ukiangalia kwa makini utagundua inaelezea kiwango cha chini tu cha adhabu bila kuweka ukomo wake yaani ISIYOZIDI AIDHA MIEZI KADHAA AU MILIONI KADHAA.
Jibu langu lingekuwa na maana sana kwako laiti ungejua kilichoandikwa na huyo ndugu niliyemjibu! Yeye anasema JK ameleta uhuru mpana kwa wanahabari.
 
Thamani ya kitu utaijua ukishakikosa! Thamani ya Afya uliza Mgonjwa, Thamani ya Mzazi Muulize Yatima, thamani ya Urais Muulize Mamvi! Mwacheni Jakaya afanye Mambo yake, issue za kumtaja taja mnasababisha ajing'ate wakati wa msosi huko ughaibuni!
 
Sasa mbona wengine wanamponda kwa kusaini sheria ya mtandao ambayo wanadai inakandamiza uhuru wao?

Sheria ile inapunguza uzalishaji wa Viwanda vya Uongo! Ukisema Uongo au uzushi unashughulikiwa sasa kama wewe sio Mzushi na Muongo iweje uwe na hofu ya kushughulikiwa?
 
Msaada wakuu ivi hili neno CHADEMA linamaana gani maana nime google na kutafuta kwenye ma kamusi lakini sojaona.
 
Akichangia bungeni alitamka bila kuficha awamu hii ya tano inataka kuminya uhuru wa habari wakati awamu ya nne ilikuwa jasiri na kurusha live bunge tunamkumbuka jk kwa kuwa jasiri wa uhuru wa habari.....

Ilibidi nicheke....leo mnamkumbuka tena. Wakati jamaa alikuwa anawasigina mkatoka bungeni kila uchwao. Msigwa uwe na msimamo
Ok, sikusikia aliongea nini. Ila kama kalinganisha kitu kimoja tu cha bunge kuoneshwa live hapo hajakosea.
 
Ukitaka kujua umuhimu wa matako kalia kichwa.

Ukitaka kujua thamani ya ulichonacho,kipoteze.
 
Kweli watz tubadilike,yani inakua sifa za marehemu akiwa hai mbaya,akifa oooh alikua mzuri,wakati ule mlimsema sana JK leo kamaliza muda wake amegeuka mzur?
Kikwete alikuwa kiongozi mbovu kabisa katika historia ya Tanzania. Hilo halina ubishi na ndio msimamo wangu. Lakini pamoja na ubovu wooooote, sio kwamba hakuna areas ambazo unaweza kumsifia! Zipo. Na mtu akimsifia kwenye areas hizo hatakuwa amefanya makosa. Ndio maana nikasema ni muhimu kujua amesifiwa nini?
 
Back
Top Bottom