Msaada wa kupata talaka kwa imani ya kiislam kwa mwanamke

Ksi hii lazima iskilizwe na kadhi au sheikh wa bakwata kwa pande mbili na talaka itatolewa ikionekana hamna namna ya kusuluhisha. Kipigo cha kudhuru ni miongoni mwa sababu zinazokubalika kwa mwanamke kuivunja ndoa
 
Alipochukua uamuzi wa kwenda kwao kwa kweli hiyo haikuwa njia ya busara kwake....wakati tabia ya MME wake ya vipigo vya mara kwa mara, alitakiwa taarifa hizi kuzifikisha kwa WASHENGA wa Mme wake....pengine wangeweza kumkanya na Mme kuweza kubadili tabia...

Kama alitoa taarifa kwa Washenga na hatua kutochukuliwa....angeenda kuwaambia watu wa karibu na Mme wake....mfano Makaka ,Wajomba na hata WAZAZI wake kama wapo....na hata WALEZI..

Kama SULUHU ikiwa ngumu (kwa maana Mme hasikii na kuendeleza vipigo) ndio sasa angeenda kwenye MABARAZA ya usuluhishi ya kijamii....mfano kwa mjumbe wa mtaa...mwenyekiti wa mtaa na hata kwa diwani wa kata (ikiwa kama kweli unataka kuinusuru na kubadili tabia ya MWENZAKO.

Ukiona tabia haibadiliki na vipigo vinazidi elekea sasa ofisi za bakwata zilizo jirani yako, elezea masahibu yako (kero yako) na hatua ulizo pitia katika kutafuta suluhu....

Nina amini BAKWATA wata/wangemuita muhusika (Mme wake) na hapo angeulizwa sababu ya vipigo....angekanywa ...na laiti akitamka hakutaki na ndio sababu ya vipigo....ni matumaini Taraka ingeandikwa..

Vinginevyo kama vipigo vinasababishwa na Mme MLEVI ...Mwanamke yuko huru kudai taraka yake(akishindwa kumsamehe)

Hatua alizo chukua Mwanaume za kuoa Mke mwingine na kukomalia kutoa taraka kwa Mke aliye kimbilia kwao yuko sahihi...kwa maana yeye Mme angali anamtambua mkimbizi kama MKE WAKE HALALI WA NDOA....

Namshauri Mwanamama arudi kwa Mme wake watunze na kulea watoto wao..

Akijidanganya nae kuolewa na mtu mwingine...hakika ndoa hiyo itakuwa BATILI (sio halali)

Nakaribisha mawazo/ushauri.
Familia ya mume na mke yote ilichoka tabia za mume wa dada hivyo ilifikia hatua hat dada akipeleka akipeleka shitaka ukwen hakuna anaejishugulisha nae na ilifikia hatua wanasena kbs hii ndoa ilishatuchosha ,mambo ni mengi sana mengine ni ya aibu nashindwa kuyaandika polis na ustaw wa jamii walishafika huko ndio maana dada anataka kuwa huru tuu
 
mr nzega mungu amweke pema peponi, aliwahi kuniambia ukitaka kumfuta mtu kichwani kwako basi usikumbuke mazuri aliyokutendea bali kumbuka mabaya yake tu.
 
Talaka ktk sheria ya dini ya kiislam inatolewa na mwanaume. Na ikiwa mwanaume ana mtendea mabaya mkewe basi mwanamke ana haki ya kudai talaka nayo ipo kisheria. Kabla ya talaka ni kusikilizwa pande mbili ili ipatikane suluhu kupitia kwa wenye hekima zao katika familia mbili. Ikishindikana anaenda kwa qaadhi ambaye kwa sasa Tanzania wapo ofisi zao zipo bakwata. Anasikilizwa na mwanaume huitwa na ikithibitika ni mkweli qaadhi anavunja ndoa hiyo na mwanamke ana kuwa huru. Pia na haki yake kudai talaka hata bila kokosewa kwa kuchoka tu ana haki kuomba kujitoa kwenye ndoa. Na kama mwanaume hajamuulizia wala kumhudumua huduma yeyote muhimu na kamhama mkewe wakati huyo mwanaume anapatikana, ndani ya miezi sita hajatoa huduma kisheria ya dini huyo mwanamke kaachika illa usipokuwa haolewi na kuwa huru mpaka nyaraka za qaadhi azipate ili kusitokee mvurugano baadaye. Illa ni waajib kwa mwanaume kuwahudumia wanae. Na mwanamke hapati haki ya mali ambayo sio ya kibiashara shirikishi kwa sababu yeye ndio anayetaka kuachika na akiacha mwanaume kwa sababu zsizo na dhambi kubwa kama kuzini n.k. ni wajibu wake kumpa fidia mwanamke. Kwa mahakama ya kawaida kutoa talaka ktk uislam haitambuliki na pia walioana kiislam sio mahakamani yaishe yalipo anzia. Kwa ufafanuzi zaidi tafadha nenda bakwata uliizia ofisi ya qaadhi na umwone yeye na sio wengineo.
 
Msidanganyane,bakwata hawavunji ndoa,kuvunja ndoa ni dhima kubwa mbele ya mola,kama mnaujua vizuri uislam,hakuna mwenye uwezo wa kuvunja ndoa zaidi ya nyie wanandoa,
kinachotakiwa huyo dada ajivue kwenye ndoa,kwa kuwa kwenye uislam ndoa ni vazi,sasa kama akiamua kujivua ajivue kwa kununua talaka,kwa kiasi atakachotaka mume wake,hiyo inaitwa mutwaa!
Amlipe mutwaa,apewe talaka yake.
 
Talaka ktk sheria ya dini ya kiislam inatolewa na mwanaume. Na ikiwa mwanaume ana mtendea mabaya mkewe basi mwanamke ana haki ya kudai talaka nayo ipo kisheria. Kabla ya talaka ni kusikilizwa pande mbili ili ipatikane suluhu kupitia kwa wenye hekima zao katika familia mbili. Ikishindikana anaenda kwa qaadhi ambaye kwa sasa Tanzania wapo ofisi zao zipo bakwata. Anasikilizwa na mwanaume huitwa na ikithibitika ni mkweli qaadhi anavunja ndoa hiyo na mwanamke ana kuwa huru. Pia na haki yake kudai talaka hata bila kokosewa kwa kuchoka tu ana haki kuomba kujitoa kwenye ndoa. Na kama mwanaume hajamuulizia wala kumhudumua huduma yeyote muhimu na kamhama mkewe wakati huyo mwanaume anapatikana, ndani ya miezi sita hajatoa huduma kisheria ya dini huyo mwanamke kaachika illa usipokuwa haolewi na kuwa huru mpaka nyaraka za qaadhi azipate ili kusitokee mvurugano baadaye. Illa ni waajib kwa mwanaume kuwahudumia wanae. Na mwanamke hapati haki ya mali ambayo sio ya kibiashara shirikishi kwa sababu yeye ndio anayetaka kuachika na akiacha mwanaume kwa sababu zsizo na dhambi kubwa kama kuzini n.k. ni wajibu wake kumpa fidia mwanamke. Kwa mahakama ya kawaida kutoa talaka ktk uislam haitambuliki na pia walioana kiislam sio mahakamani yaishe yalipo anzia. Kwa ufafanuzi zaidi tafadha nenda bakwata uliizia ofisi ya qaadhi na umwone yeye na sio wengineo.
Hapo nimeelewa vizuri
 
Akienda mahakamani,watavunja,lakini mahakamani walifunga ndoa huko?
Aache ujinga wa kwenda mahakamani,kwani walifungishwa ndoa na hakimu?
Afuate kama nilivuomuelekeza,kwa wasiojua uislam,wafahamu,hakuna muislamu yeyote mwenye akili aliesoma dini akakubali kuvunja ndoa ya mtu,hata awe hakimu,kama anajua dini hakubali kubeba dhima,labda asiejua uislam.
 
Kwaimani ya kiisilamu hana ndoa tena ikumbukwe ndoa ktk uisilamu ni ibada na ina misingi yake anachotafuta hapo ni uhuru wa kufanya mambo yake ya kidunia haya Uhuru huu akautafute mahakama za kidunia lkn ibada ya ndoa imesha batilika

Sent from my MT6572 using JamiiForums mobile app
 
Hapo nimeelewa vizuri
Pole dada.Siku hizi Bakwata kuna kadhi,mwambie aanzie huko,mwanaume ataitwa mara tatu,asipofika,dada yako atapewa talaka na huyo kadhi.habari inakuwa imekwisha.Ila anao uhuru wa kwenda mahakama ya eneo lao kuomba mgawanyo wa mali n.k
 
aende kwa kadhi wa eneo alipo!aandae na mahari ya kumrudishia mume kiasi kilekile alichopewa yeye mwanamke.
la kuongezea makadhi wengi akishaona hivyo anapata chansi ya kuomba amuoe au amkule hayo mawili ategemee mojawapo
Kwa hiyo mwanamke hana thamani kiasi hicho? Amemtumikia miaka saba kamzalia watoto kapata kipigo bado mahari arudishe hee!! Sio haq.
 
Kasha pata hivo kabwana ka kumtuliza , mwache maana na huko tena ataharibu ww ndo utakuwa sosi
 
Back
Top Bottom