Msaada: Urithi kwa watoto wa bi mdogo

Anonymus

Member
Sep 2, 2014
12
50
Habari wana JF, ni matumaini yangu wote mko sawa, nadhani hii ni mara ya kwanza kupost hapa ubaoni ninaombeni msaada maana nimeshindwa hata kulala yaani.

Labda nielezee hivi, sisi ni wakristo, mzee alioa na kuzaa watoto 3 na bi mkubwa, huyu mama walichuma mali nyingi sana (nyumba, magari, viwanja na maduka kadhaa) na kwakweli maisha yalikuwa fresh.

Alipofariki bi mkubwa mzee akaoa tena ndipo kuzaa hawa wa3 wengine, ila kwa bahati mbaya mambo yalianza kuporomoka na vitu vingi sana vikauzwa kiasi kwamba alipoingia bi mdogo vilinunuliwa viwanja vipya viwili tuu lakini vingi vilivyokuwepo enzi za bi mkubwa viliuzwa. Zikiwemo nyumba na magari yaliuzwa pia.

Sasa ikatokea bi mdogo naye akafariki, ukapita mwaka naye mzee akafariki, na taratibu za usimamizi wa mirathi zikafanyika na kuchaguliwa kaka mkubwa kusimamia. Makubaliano ilikuwa tutaendelea kuishi pamoja kama familia ukizingatia asilimia kubwa walikuwa ni wanafunzi hivyo hatukutaka mambo ya kugawana.

Tumeishi hivyo toka hapo na sasa wote tuko mtaani baada ya kumaliza masomo.

Ishu inakuja kwa baadhi yetu maisha yamekuwa magumu, watoto wa bi mdogo wanaraise na kutaka mali zigawanywe.

Sasa swali langu ni jee, mgawanyo huo unakuwaje? Je mali zilizochumwa kipindi cha bi mkubwa zinabaki kwa watoto wa bi mkubwa au mali zote zinagawanywa sawa bila kuzingatia zilichumwa lini?

Sio mwandishi mzuri sana japo nimejitahidi kueleza, kama sijaeleweka pahala nitajibu kwa comments.

Ninatanguliza shukrani zangu kwenu
 
Pole kwa kukosa usingiz mkuu.. iko hiv ingekua wazaz hawajafark wote mali ingegawanya kwa ratio ya iz mama flan alzkuta hiz n za huyu waliotafuta nae lkn kwa sasa mmebaki wote n matokeo ya mzee kwaio mali ztagawanywa kwa usawa mfano kama kuna nyumba 4 ile kubwa itabak mikonon mwa familia ya mama mkubwa kama ndio chimbuko lenu au pakukutania kpnd cha skukuu na mambo mengne sababu baada ya mama mkubwa kufark mzee alileta mama mdogo apo apo nyumban kama angeenda kumjengea pengne iyo isngekua shda sana kwaio familia zote mbil znahak na nyumba kubwa.. ila izo mali na vtu vngne mtagawana vile mtakavyoona inafaa katika kuviendeleza au kuvsimamia ila point n kwamba wote mnahaki sawa.
NB. Il n funzo kwetu pia tuliobak dunian tunakuja kuwapa shda sana watoto wetu kwa kuzaa nje ya ndoa ama kua na familia zaid ya moja
 
Vijana mngepambana mtafute vyenu usiku huu ungekua umelala mustarehe wala huwazi mali ya mtu..🤣

Anyway, mimi naona hao madogo wamezaliwa wamekuta mali ni za baba yao wala hakuna alichuma akiwa na nani wapi na lini.. hizo ndio tamaduni zetu za Africa, otherwise labda kungekuwa na talaka baina ya mzee wako na mama yako kugawana mali ila hilo halikutokea..

So obviously hizo mali zote mama wa kwanza alimuachia baba zoteee ni zake na watoto waliozaliwa walimkuta baba yao na mali regardless alizipata akiwa na nani..

Kwa maana hio hao watoto wa mama wa pili wana haki zote za hizo mali kama wewe vile ulivyokua nazo..

Cha mwisho hizo mali kama hamkuzitafuta nyie na hamna maarifa ya kuziendeleza basi hakika hazitochukua time mtabaki tena mikono mitupu kama mlivyo hapo sasa ivi😂

NDIO MAANA JUU HAPO NIMESEMA ILITAKIWA UWE UMELALA MIDA HII AMBAYO HUNA USINGIZI KAMA UNGEKUA NA MZIGO WAKO MWENYEWE UMEPAMBANA
 
Pole kwa kukosa usingiz mkuu.. iko hiv ingekua wazaz hawajafark wote mali ingegawanya kwa ratio ya iz mama flan alzkuta hiz n za huyu waliotafuta nae lkn kwa sasa mmebaki wote n matokeo ya mzee kwaio mali ztagawanywa kwa usawa mfano kama kuna nyumba 4 ile kubwa itabak mikonon mwa familia ya mama mkubwa kama ndio chimbuko lenu au pakukutania kpnd cha skukuu na mambo mengne sababu baada ya mama mkubwa kufark mzee alileta mama mdogo apo apo nyumban kama angeenda kumjengea pengne iyo isngekua shda sana kwaio familia zote mbil znahak na nyumba kubwa.. ila izo mali na vtu vngne mtagawana vile mtakavyoona inafaa katika kuviendeleza au kuvsimamia ila point n kwamba wote mnahaki sawa.
NB. Il n funzo kwetu pia tuliobak dunian tunakuja kuwapa shda sana watoto wetu kwa kuzaa nje ya ndoa ama kua na familia zaid ya moja
Kwa situation hii mzee hakua na namna zaidi ya kuoa tena sababu mke alifariki..

ishu ni kwa vijana hawa ndugu ambao wanaotaka kugawana mbao kwa kisingizio maisha ni magumu bila kua na A wala B ya hizo mali..
 
Naomba nianze kuuliza swali, ila samahani kama ntakukwaza, Je wewe ni msimamizi wa mirathi? Ndugu wa mume au mke ? Au mtoto wa mama mmoja wapo?
Jf,saa 9 watu tupo 😀
 
Pole kwa kukosa usingiz mkuu.. iko hiv ingekua wazaz hawajafark wote mali ingegawanya kwa ratio ya iz mama flan alzkuta hiz n za huyu waliotafuta nae lkn kwa sasa mmebaki wote n matokeo ya mzee kwaio mali ztagawanywa kwa usawa mfano kama kuna nyumba 4 ile kubwa itabak mikonon mwa familia ya mama mkubwa kama ndio chimbuko lenu au pakukutania kpnd cha skukuu na mambo mengne sababu baada ya mama mkubwa kufark mzee alileta mama mdogo apo apo nyumban kama angeenda kumjengea pengne iyo isngekua shda sana kwaio familia zote mbil znahak na nyumba kubwa.. ila izo mali na vtu vngne mtagawana vile mtakavyoona inafaa katika kuviendeleza au kuvsimamia ila point n kwamba wote mnahaki sawa.
NB. Il n funzo kwetu pia tuliobak dunian tunakuja kuwapa shda sana watoto wetu kwa kuzaa nje ya ndoa ama kua na familia zaid ya moja
Shukrani kwa majibu mazuri
 
Vijana mngepambana mtafute vyenu usiku huu ungekua umelala mustarehe wala huwazi mali ya mtu..

Anyway, mimi naona hao madogo wamezaliwa wamekuta mali ni za baba yao wala hakuna alichuma akiwa na nani wapi na lini.. hizo ndio tamaduni zetu za Africa, otherwise labda kungekuwa na talaka baina ya mzee wako na mama yako kugawana mali ila hilo halikutokea..

So obviously hizo mali zote mama wa kwanza alimuachia baba zoteee ni zake na watoto waliozaliwa walimkuta baba yao na mali regardless alizipata akiwa na nani..

Kwa maana hio hao watoto wa mama wa pili wana haki zote za hizo mali kama wewe vile ulivyokua nazo..

Cha mwisho hizo mali kama hamkuzitafuta nyie na hamna maarifa ya kuziendeleza basi hakika hazitochukua time mtabaki tena mikono mitupu kama mlivyo hapo sasa ivi

NDIO MAANA JUU HAPO NIMESEMA ILITAKIWA UWE UMELALA MIDA HII AMBAYO HUNA USINGIZI KAMA UNGEKUA NA MZIGO WAKO MWENYEWE UMEPAMBANA
Yaani ndugu yangu umasikini ni mbaya sana, maana ni miaka 10 toka mzee afariki ndio yanakuja kuibuka haya sasa tena kwa ugomvi mkubwa wa kuumizana kabisa, mtoto wa bi mdogo kamvaa mtoto wa bi mkubwa baada ya mabishano kuhusu mali... yaani ndio maana nikajikuta hadi usingizi nakosa kwani nimepatwa na mstuko mkubwa na stress juu!
 
Kwa situation hii mzee hakua na namna zaidi ya kuoa tena sababu mke alifariki..

ishu ni kwa vijana hawa ndugu ambao wanaotaka kugawana mbao kwa kisingizio maisha ni magumu bila kua na A wala B ya hizo mali..
Kweli kabisa
 
Naomba nianze kuuliza swali, ila samahani kama ntakukwaza, Je wewe ni msimamizi wa mirathi? Ndugu wa mume au mke ? Au mtoto wa mama mmoja wapo?
Jf,saa 9 watu tupo
Mimi sio msimamizi bali ni moja ya watoto wa bi mkubwa ambao hatutaki mali zigawanywe.
 
Yaani ndugu yangu umasikini ni mbaya sana, maana ni miaka 10 toka mzee afariki ndio yanakuja kuibuka haya sasa tena kwa ugomvi mkubwa wa kuumizana kabisa, mtoto wa bi mdogo kamvaa mtoto wa bi mkubwa baada ya mabishano kuhusu mali... yaani ndio maana nikajikuta hadi usingizi nakosa kwani nimepatwa na mstuko mkubwa na stress juu!
Wapigeni tafu hao wadogo zenu,hata wwe ungechapwa na shida lazima ungerejea kwenye mali ya Urithi kama kimbilio na muwokozi wa maisha.yako! Alafu mwisho wa siku usijali sana,maana mirathi ni ibaada!!
 
Wapigeni tafu hao wadogo zenu,hata wwe ungechapwa na shida lazima ungerejea kwenye mali ya Urithi kama kimbilio na muwokozi wa maisha.yako! Alafu mwisho wa siku usijali sana,maana mirathi ni ibaada!!
Wanasapotiwa pesa ya kula, pa kulala papo (hiyo nyumba husika) wenyewe wanachotaka ni kupewa kila kitu na kula bata kwa minajili ya mali za urithi
 
Pole kwa kukosa usingiz mkuu.. iko hiv ingekua wazaz hawajafark wote mali ingegawanya kwa ratio ya iz mama flan alzkuta hiz n za huyu waliotafuta nae lkn kwa sasa mmebaki wote n matokeo ya mzee kwaio mali ztagawanywa kwa usawa mfano kama kuna nyumba 4 ile kubwa itabak mikonon mwa familia ya mama mkubwa kama ndio chimbuko lenu au pakukutania kpnd cha skukuu na mambo mengne sababu baada ya mama mkubwa kufark mzee alileta mama mdogo apo apo nyumban kama angeenda kumjengea pengne iyo isngekua shda sana kwaio familia zote mbil znahak na nyumba kubwa.. ila izo mali na vtu vngne mtagawana vile mtakavyoona inafaa katika kuviendeleza au kuvsimamia ila point n kwamba wote mnahaki sawa.
NB. Il n funzo kwetu pia tuliobak dunian tunakuja kuwapa shda sana watoto wetu kwa kuzaa nje ya ndoa ama kua na familia zaid ya moja
Mkuu laki huyiu haja Sema Mzee wake alizaa nje ya ndoa
 
Mimi sio msimamizi bali ni moja ya watoto wa bi mkubwa ambao hatutaki mali zigawanywe.
Lazima mali zigawanywe ili kila mtoto apate haki yake, kwani mkuu wewe kabila gani ? Kwaki kwenye ukoo wenu hakuna wazee waki mila wa zee wa ukoo .
 
Wewe kinachokunyima usingizi ni uchoyo tu na ubinafsi.

Hao ni ndugu zako kabisa nyau wewe. Si mmechangia baba nyie hata ubini wenu si ni mmoja? Ukute hapo hata mama yako yaani bi mkubwa alikuwa mama wa nyumbani na mali zote alichuma baba. Yaani kuna watu mna akili ngumu sana aisee. Unakosa usingizi kabisa eti, kisa tu roho inakuuma kugawana mali na ndugu zako. Umasikini kitu kibaya sana.

Watu wanaungana we jamaa nyie mnataka kubomoana

Hapo ni eiza mbaki na mali muishi katika umoja na upendo au mali iuzwe mgawane sawa kwa sawa kwa upendo
 
Back
Top Bottom