Msaada: Nyumba ya urithi, nanufaikaje?

Diwani

JF-Expert Member
Oct 25, 2014
2,673
2,715
Huenda sipo peke yangu hivyo labda maada hii inaweza kuwagusa na wengine watakaoamua kujifunza kutoka kwa wanachama wengine.

Mwaka 2017, rasmi nilikabidhiwa urithi wa marehemu baba yangu ambaye alikufa miaka mingi iliyopita, kitu pekee kuhusu nyumba yetu ni kuwa, hakukuwahi kuwa na migogoro mingi kama zilivyokuwa nyumba nyingi huko kwenye maeneo mengine.

Kiufupi si nyumba ya kifahari, ni ya kawaida sana kwa mazingira ya mjini. Kinachonisikitisha ni kuwa mara nyingi imekuwa nyumba ya kufanyiwa ukarabati ilhali hali yenyewe si nzuri kwa upande wangu.

Nimewaza kuuza, ila naona kama si vizuri, nimeweza kurekebisha lakini sijui pa kuanzia, marekebisho ni makubwa na hayaendani kabisa na kipato changu.

Nimeleta kwenu mada hii kuomba msaada wenu wa dhati ambao huenda ukanipa mwangaza wa kufanya maamuzi sahihi.

NB: Nyumba ipo Dar es Salaam.
 
Mkuu, pole kwa kumpoteza mzazi. Ila nampa hongera amekuachia asset.

Dar ipo sehemu gani? Nashauri ungepangisha.

Hii Dar popote pale nyumba inapangishwa.

Jitahidi utafute pesa kidogo, uikarabati upangishe.

Usifikirie kabisa kuuza wala kukopea bank.
 
Mi nawaza tu kama hela ya kukarabati huna, na kama mahali nilipo ni pazuri kwa maana kwamba ukiuza bei iko vema, nashauri uza Kisha kajenge nyumba yako mahali pako, kama utaishi au utapangisha hilo lako... Ila hiyo ya urithi... Utatoa hela ya kukarabati alafu ndugu hawaelewi kama unaingia gharama kuimaintain, wanakuletea maombi ya pesa nk... Ila ikiuzwa akili zitawakaa Sawa kuwa kisima kimekauka... 😁 😁 Utakuwa huru kiasi Fulani... Na pia hata wanao watarithi nyumba yako na si ya babu...!
 
Huenda sipo peke yangu hivyo labda maada hii inaweza kuwagusa na wengine watakaoamua kujifunza kutoka kwa wanachama wengine.

Mwaka 2017, rasmi nilikabidhiwa urithi wa marehemu baba yangu ambaye alikufa miaka mingi iliyopita, kitu pekee kuhusu nyumba yetu ni kuwa, hakukuwahi kuwa na migogoro mingi kama zilivyokuwa nyumba nyingi huko kwenye maeneo mengine.

Kiufupi si nyumba ya kifahari, ni ya kawaida sana kwa mazingira ya mjini. Kinachonisikitisha ni kuwa mara nyingi imekuwa nyumba ya kufanyiwa ukarabati ilhali hali yenyewe si nzuri kwa upande wangu.

Nimewaza kuuza, ila naona kama si vizuri, nimeweza kurekebisha lakini sijui pa kuanzia, marekebisho ni makubwa na hayaendani kabisa na kipato changu.

Nimeleta kwenu mada hii kuomba msaada wenu wa dhati ambao huenda ukanipa mwangaza wa kufanya maamuzi sahihi.

NB: Nyumba ipo Dar es Salaam.
Kaichukulie mkopo bomoa weka fremu au ghorofa kwa matumizi ya biashara na makazi
 
Nyumba ya urithi tena iko mjini. Wewe ndio umekabidhiwa kuirithi, je huna ndugu wengine? Nyumba ya urithi haipaswi kuuzwa ila ni asset inayohitaji ukarabati, maboresho na kuendelezwa....
Tatizo huna pesa kwa ajili hiyo. Kwa vyovyote una mali zako binafsi ambazo hupaswi kuzichanganya na mali ya urithi... Utayumba!.
Chakufanya:
1. Chukua mkopo benki ufanye ukarabati na maboresho kisha ipangishe kwa mtu mmoja mmoja au mashirika. Fanya Guest house maktaba au hata makumbusho ya familia au mji/Kijiji
2. Tafuta muwekezaji mwenye fedha uingie nae ubia, thamani ya nyumba iwe mtaji wako wakati muwekezaji akiingiza kiasi cha pesa mtakazo kubaliana. Mfano uwe na hisa 60/40 au vyovyote mtakavyo kubaliana. Fanyeni biashara ya real estate. Kila lakheri.
 
Nyumba ya urithi tena iko mjini. Wewe ndio umekabidhiwa kuirithi, je huna ndugu wengine? Nyumba ya urithi haipaswi kuuzwa ila ni asset inayohitaji ukarabati, maboresho na kuendelezwa....
Tatizo huna pesa kwa ajili hiyo. Kwa vyovyote una mali zako binafsi ambazo hupaswi kuzichanganya na mali ya urithi... Utayumba!.
Chakufanya:
1. Chukua mkopo benki ufanye ukarabati na maboresho kisha ipangishe kwa mtu mmoja mmoja au mashirika. Fanya Guest house maktaba au hata makumbusho ya familia au mji/Kijiji
2. Tafuta muwekezaji mwenye fedha uingie nae ubia, thamani ya nyumba iwe mtaji wako wakati muwekezaji akiingiza kiasi cha pesa mtakazo kubaliana. Mfano uwe na hisa 60/40 au vyovyote mtakavyo kubaliana. Fanyeni biashara ya real estate. Kila lakheri.
Namba 2 idea nzuri.
 
Back
Top Bottom