Mpenzi niliyekutana naye JF, naye alizingua nikashindwa kuja nae US

Prof Janabi wa JF

Senior Member
Jul 7, 2023
119
363
Uzi wangu wa kwanza kuhusu mpenzi wangu kukataa kuja nami US ulipata wachangiaji kadhaa huku baadhi walionesha nia ya kuja na mimi. Basi nikajitosa kwa mmoja, kuja kukutana naye mtoto mashallah, sauti makini, umbo lenyewe kabisa.

Wakati huo nilikuwa na majukumu kibao ila nikapangua ili nikutane na mrembo, kwenye moja na mbili nikaingia Mbezi nakutana na chombo kikali, dakika kadhaa mbele tukawa tumesha-sign up na kila kitu. Mtoto ni Nesi, nikamwambia njoo unitibu moyo wangu, mtoto akakubali.

Nikawa nabeba mtoto tunakaa sehemu kupata moja mbili, ila mtoto sio mtumiaji nikaona namtesa. Nikawa nakaa naye maeno ya kupata kilaji kizuri, pia nikaona namtesa maana alikuwa hapendi kula manyama ya kuchoma au supu nzitonzito.

Baada ya kuzurura wiki kadhaa, nikaona ngoja nipeleke ngoma ipajue home. Kwa wakati huo mimi nilishapajua kwake, mara nyingine nilikuwa namuibukia hata usiku, tunaenda kuzurura.

Kimsingi nilikuwa na mambo mengi, na mtoto anadeka, ikawa nikiwa kimya na yeye anakuwa kimya. Kumbuka nina paper works kibao za kuandaa safari inaweza kupita siku mtu hujala, maana tangu asubuhi unakuta umeingia hapa umechomokea kula umerudi hapa, kuja kustuka hujala unaenda kokote tu kujipooza. Halafu bado nilinawiri tu.

Nikawa namaliza na mizunguko yangu usiku, namfuata mtoto kwake ili tuje kuangalia tunda. Mtoto akaona kama napenda kummenya tu sina mapenzi naye. Akalalama mara kadhaa, nikamwambia mimi sio mtu wa kumenya na kusepa ndio maana nimekuleta kwangu muda wowote unaweza kuja. Akaelewa ila akawa bado anakitu kimemkwama nafsini mwake.

Mara ya mwisho nilikuwa nae home, akaongea vitu vilinikata sana. Aliona na-namtreat kama kahaba, aisee ile ilinikata sana. Nikaona juhudi zangu za kumfanya awe wangu zinafikia ukingoni, mbali nakwamba I do crazy things na mpenzi wangu lakini kujiona kahaba nikaona haina afya. Nataka mwanamke ajione mke, kujiona kama kahaba maana yake hata yeye haoni nafasi yake kwangu.

Basi nikaona nisiharakishe, mbali na kuwa nilikuwa na ari ya kutaka nioe kabla kuja huku nikafuta. Usiku ule sikumuonesha kama sijapendezwa na maneno yake, asubuhi tuliagana vizuri then nikapiga kimya. Maana sikufuata mbususu kwake, nilitaka anielewe tufanye vitu tupange mipango thabiti.

Hapo mtu mwitu nikaishi kibachela hadi nikasepa. Na kweli mtoto alikuwa anajiona kama kahaba kwangu japo simpi mwanamke status hiyo. Hakunitafuta sikumtafuta. Ila siku moja nikamtext tu WhatsApp kwa namba inayoanza na +1, akaona mwamba kashayeya.

Kiufupi ni mtoto mzuri, akikubali nimtag nitamtag, ila nadhani anaweza kubadilisha mindset yake baada ya kusoma uzi huu. But so far bado niko single.

Uzi wangu mmoja wa kuuliza nichukue goma gani, diaspora mmoja au ngoja nimtaje ni ndugu yangu Mahorii amenishauri nirudi nyumbani kuchukua mke badala ya kutaka vitoto vya kitasha. Ndugu yangu Ushauri wako nauzingatia sana, hopefully tutakutana siku moja huku u-diasporani kwa ajili ya kupika vyakula vya kinyumbani kidogo.

Mada ya Mwanzo
- Mpenzi wangu hataki niende naye ughaibuni
 
Hapo kwa shemeji yako unapolala kwenye korido na baiskeli ndo unaita US ?
Kaka una makasiriko makali! Kwenye corridor ni kweli nimelala katika utafutaji maisha, na mwisho ilikuwa 2013. Baada ya hapo nililala sehemu nyingine ngumu ngumu. Nimelala nje, nimelala sakafuni nk. Ila kwa sasa, namshukuru Mungu kwa nilivyo.

Kifupi kulala kordoni imeshakuwa historia, asante kwa kunikumbusha.
 
.
 

Attachments

  • 198351-Hot-Tea-Vapor.gif
    198351-Hot-Tea-Vapor.gif
    1.6 MB · Views: 6

Similar Discussions

Back
Top Bottom