Mikopo na sera mbovu za ubinafsishaji ndizo zimetufikisha hapa, Mwaka 2000 exchange rate ilikuwa(1 Usd=Tshs 803.3)

Rabbon

JF-Expert Member
Apr 16, 2022
19,201
29,912
Salaam shalom!!

Tulipopata Uhuru wa Nchi yetu, hatukuwa na wawekezaji wengi wa kuwekeza kwenye migodi, Serikali ilihodhi vitega Uchumi vyote na kusimamia, Hawa wawekezaji wa sasa, nionavyo Si HAKI kuwaita wawekezaji Bali waporaji, na uporaji huo unashirikisha viongozi wetu wa ndani. Tulipopata uhuru, Dola Moja ya kimarekani, ilibadilishwa Kwa Tshs 7 tu!!

Nisikuchoshe, hii hapa ni historia ya Exchange rate tangu Uhuru Hadi hii Leo, chama Cha MAPINDUZI kikiwa madarakani.

1961.
1usd=7 Tshs

1971
1usd= 7.14 Tshs

1981
1usd=8.2 Tshs

1991
1usd=219 Tshs

2001
1 Usd=876.4 Tshs

2005
1 Usd=1,128.9 Tshs

2010
1usd =1,434.7 Tshs

2012
1usd= 1,600Tshs

2015
1usd=2,037.1 Tshs

2020
1usd=2,330.5

2024
1usd= 2,615 Tshs.

Source: Google, average Exchange Rate, University of Pennsylvania.

Awamu ya kwanza ya utawala wa mwalimu Nyerere Kwa miaka yote 24 aliyokaa madarakani, Dalar halikuwahi kubadilishwa Kwa zaidi ya Tshs 10 pekee!! Na wakati huo, Aliendesha Uchumi Kwa KILIMO PEKEE!! Uchumi wetu ulitegemea zaidi KILIMO Cha biashara na chakula, Tuliuza millions ya tons za mazao ya KILIMO na biashara.

Mambo yameanza kuharibika pale tulipoamua kuingiza sera za ubepari Uchwara, Tukaanza kuruhusu waporaji kushika uchumi wetu Kwa mlango wa Uwekezaji. Alipoingia tu Mzee Ruksa, ikapaa Kutoka Sh 10- tsh 200 kubadili Kwa 1 Usd. Kumbe tulitakiwa tuunde na kuwajenga wazawa ndio wapewe mashirika ya umma kujenga Nchi na kubakiza pesa nchini.

Tungetegemea, Uchimbaji wa Madini usaidie kuimarisha pesa yetu na Uchumi, lakini Cha kushangaza, Dhahabu inachimbwa, lakini Serikali inakosa pesa ya kufadhili budget na kulazimisha kukopa nje, sasa hiyo migodi Si ingefungwa tujue Moja? Tusubiri wazaliwe Watanzania ambao watakuwa na uwezo wa kuchimba Dhahabu yetu wenyewe, ituzwe benki kuu baada ya kununuliwa na Serikali Toka Kwa wachimbaji hao. Pesa yetu irudi kuwa yenye nguvu tena kama zamani.

Nchi yetu tunawezaje kusema tuna wawekezaji ambao hawaleti mchango wowote kwenye kuimarisha pesa yetu na Uchumi wetu?

Iweje tuwape wageni Bandari zetu kwamba wakusanye mapato Kwa weledi mkubwa Kisha tukose pesa ya kufinance budget yetu Kwa mwaka Hadi tulazimike kukopa tena?

SOLUTION.

1. Turudi na kukaa kama nchi na kutafakari tena kuhusu sera zetu za kiuchumi, maana uwekezaji haujaleta TIJA yoyote muhimu zaidi ya kutufanya kuwa maskini zaidi, tunahitaji Sera ambazo ni Mixture ya Ujamaa na Ubepari. Na ubepari huo uwe wa kudeal na Wazalendo wa ndani ya nchi ,wafadhiliwe mikopo Ili waendeshe Uchumi wa Nchi yetu.

2. MIKOPO ya nchi yetu isimamishwe. Iundwe Taasisi huru kikatiba, Taasisi hiyo impore Rais mamlaka ya kujihusisha na mikopo ya nchi, Taasisi hiyo ichakate taarifa nyeti na kuona namna Bora ya kujitegemea wenyewe tukishirikisha matajiri wazawa wa nchini, Dhahabu yetu na Raslimali zetu zimilikiwe na wazawa, hao ndio wafadhili budget ya Uchumi wetu.

3. Tukipumzishe chama Cha MAPINDUZI kuongoza nchi, nasisitiza point hii no 3!!

Vyama vya upinzani pia viangaliwe UPYA, maana Sera na maono Yao kiuchumi ni Yale Yale ya kuamini kuwa tunaweza kuleta wawekezaji Toka nje Kisha tukapata faida za kiuchumi kupitia uwekezaji Uchwara tukiweka rehani raslimali zetu Kwa wageni, tunahitaji vyama vya upinzani vyenye sura ya kizalendo na kuwa na Political na Economical INDEPENDENCE!! Vyama vya siasa nchini visizidi VITATU PEKEE!!!

4. Tupate Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote. Nchi yetu tusiwape wageni kiutawala kupitia sera mbovu na RUSHWA Kwa viongozi wetu ilhali Uchumi na Raslimali za nchi zinazidi kuondoka mikononi mwetu.

5. Tuongeze hasira juu ya Wala RUSHWA!! Rais asione haya kusaini death sentence, watu Wala RUSHWA wa level zote na uhujumu Uchumi wanyongwe, wasiogope, ukinyonga Wala RUSHWA watu hawataisha nchini, Bali wataacha vitendo vya RUSHWA.!!

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Karibuni🙏
 
Salaam shalom!!

Tulipopata Uhuru wa Nchi yetu, hatukuwa na wawekezaji wengi wa kuwekeza kwenye migodi, Serikali ilihodhi vitega Uchumi vyote na kusimamia, Hawa wawekezaji wa sasa, nionavyo Si HAKI kuwaita wawekezaji Bali waporaji, na uporaji huo unashirikisha viongozi wetu wa ndani. Tulipopata uhuru, Dola Moja ya kimarekani, ilibadilishwa Kwa Tshs 7 tu!!

Nisikuchoshe, hii hapa ni historia ya Exchange rate tangu Uhuru Hadi hii Leo, chama Cha MAPINDUZI kikiwa madarakani.

1961.
1usd=7 Tshs

1971
1usd= 7.14 Tshs

1981
1usd=8.2 Tshs

1991
1usd=219 Tshs

2001
1 Usd=876.4 Tshs

2005
1 Usd=1,128.9 Tshs

2010
1usd =1,434.7 Tshs

2012
1usd= 1,600Tshs

2015
1usd=2,037.1 Tshs

2020
1usd=2,330.5

2024
1usd= 2,615 Tshs.

Source: Google, average Exchange Rate, University of Pennsylvania.

Awamu ya kwanza ya utawala wa mwalimu Nyerere Kwa miaka yote 24 aliyokaa madarakani, Dalar halikuwahi kubadilishwa Kwa zaidi ya Tshs 10 pekee!! Na wakati huo, Aliendesha Uchumi Kwa KILIMO PEKEE!! Uchumi wetu ulitegemea zaidi KILIMO Cha biashara na chakula, Tuliuza millions ya tons za mazao ya KILIMO na biashara.

Mambo yameanza kuharibika pale tulipoamua kuingiza sera za ubepari Uchwara, Tukaanza kuruhusu waporaji kushika uchumi wetu Kwa mlango wa Uwekezaji.

Tungetegemea, Uchimbaji wa Madini usaidie kuimarisha pesa yetu na Uchumi, lakini Cha kushangaza, Dhahabu inachimbwa, lakini Serikali inakosa pesa ya kufadhili budget na kulazimisha kukopa nje, sasa hiyo migodi Si ingefungwa tujue Moja? Tusubiri wazaliwe Watanzania ambao watakuwa na uwezo wa kuchimba Dhahabu yetu wenyewe, ituzwe benki kuu baada ya kununuliwa na Serikali Toka Kwa wachimbaji hao. Pesa yetu irudi kuwa yenye nguvu tena kama zamani.

Nchi yetu tunawezaje kusema tuna wawekezaji ambao hawaleti mchango wowote kwenye kuimarisha pesa yetu na Uchumi wetu?

Iweje tuwape wageni Bandari zetu kwamba wakusanye mapato Kwa weledi mkubwa Kisha tukose pesa ya kufinance budget yetu Kwa mwaka Hadi tulazimike kukopa tena?

SOLUTION.

1. Turudi na kukaa kama nchi na kutafakari tena kuhusu sera zetu za kiuchumi, maana uwekezaji haujaleta TIJA yoyote muhimu zaidi ya kutufanya kuwa maskini zaidi, tunahitaji Sera ambazo ni Mixture ya Ujamaa na Ubepari. Na u repair huo uwe wa kudeal na Wazalendo wa ndani ya nchi wafadhiliwe mikopo Ili waendeshe Uchumi wa Nchi yetu.

2. MIKOPO ya nchi yetu isimamishwe. Iundwe Taasisi huru kikatiba, Taasisi hiyo impore Rais mamlaka ya kunihusisha na mikopo ya nchi, Taasisi hiyo ichakate taarifa nyeti na kuona namna Bora ya kujitegemea wenyewe tukishirikisha matajiri wazawa wa nchini, Dhahabu yetu na Raslimali zetu zimilikiwe na wazawa, hao ndio wafadhili budget ya Uchumi wetu.

3. Tukipumzishe chama Cha MAPINDUZI kuongoza nchi, nasisitiza point hii no 3!!

Vyama vya upinzani pia viangaliwe UPYA, maana Sera na maono Yao kiuchumi ni Yale Yale ya kuamini kuwa tunaweza kuleta wawekezaji Toka nje Kisha tukapata faida za kiuchumi kupitia uwekezaji Uchwara tukiweka rehani raslimali zetu Kwa wageni, tunahitaji vyama vya upinzani vyenye sura ya kizalendo na kuwa na Political na Economical INDEPENDENCE!!

4. Tupate Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote. Nchi yetu tusiwape wageni kiutawala kupitia sera mbovu na RUSHWA Kwa viongozi wetu ilhali Uchumi na Raslimali za nchi zinazidi kuondoka mikononi mwetu.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Karibuni🙏
SOLUTION NI KUITOA CCM YANI KUKAA MEZANI NAO WALE JAMAA TUKATAE WANAPOLIPELEKA TAIFA TUTAJIFUNZA HIPO SIKU UKIONA DAMU ZINA MWAGIKA
 
SOLUTION NI KUITOA CCM YANI KUKAA MEZANI NAO WALE JAMAA TUKATAE WANAPOLIPELEKA TAIFA TUTAJIFUNZA HIPO SIKU UKIONA DAMU ZINA MWAGIKA
Ni sawa kuitoa CcM madarakani, lakini Hilo pekee halitoshi,

Sera za Uchumi za upinzani Bado nazo ni tegemezi tu, hata michango na pesa za kuendesha chama, wanategemea msaada Toka nje ambako huko hawajawahi kuwa na " free lunch" IPO siku utalipa.

Muhimu tupate Katiba mpya itokanayo na Rasimu aliyosimamia Judge Warioba. KATIBA itoe sera na mwelekeo wa Uchumi wetu ambapo vyama vya siasa vitashurutishwa kutumia dira na uelekeo huo kutengeza na kuboresha Ilani zao za uchaguzi na dira ya maendeleo Kwa chama kitakachoshika Dola kuanzia 2025.

Ubarikiwe!!
 
Ni sawa kuitoa CcM madarakani, lakini Hilo pekee halitoshi,

Sera za Uchumi za upinzani Bado nazo ni tegemezi tu, hata michango na pesa za kuendesha chama, wanategemea msaada Toka nje ambako huko hawajawahi kuwa na " free lunch" IPO siku utalipa.

Muhimu tupate Katiba mpya itokanayo na Rasimu aliyosimamia Judge Warioba. KATIBA itoe sera na mwelekeo wa Uchumi wetu ambapo vyama vya siasa vitashurutishwa kutumia dira na uelekeo huo kutengeza na kuboresha Ilani zao za uchaguzi na dira ya maendeleo Kwa chama kitakachoshika Dola kuanzia 2025.

Ubarikiwe!!
inatosha kujifunzi nchi ambazo zimeshaanza kuona watawala wa bovu na kuwaondoa au unakaaga rumumba pale
 
Kumbe hatukupasa kutafuta waporaji wa raslimali Toka nje,

Tulitakiwa tubinafsishe Kwa wadau wa ndani, Serikali ikawadhamini mikopo,

Pia Serikali ingetafuta dawa ya wezi wa pesa za umma,

Marais wasiogope kusaini watu kunyongwa kama china, na wanyongwe Kweli.
 
ukiifatilia sana hii nchi uatagombana hadi na mkeo
acha ninywe bia mi
Pole ndugu,

Naona umepata ghadhabu baada ya kuujua UKWELI,

Halafu data hizi ukizisaka kuhusu exchange rate ya Tanzania to USD tangu uhuru ni ngumu kuzipata, ni kama zilipigwa block Fulani Ili tusijue UKWELI.

Tutafika tu ndugu yangu.
 
nilikua kwa daladala asubuh namsikia diwan wa sisi emu kata X anaulizwa wapi anaona ameanguka kwenye kata yake na anataka kufanya marekebisho akipewa nafasi,
daaaaa,alitoa list ya shukrani kuanzia mama hadi mkurugenzi wa halmashauri X yule mtangazaji nahisi alitamani kucheka...
eti anasema ndani ya miaka minne wamepambana kugundua mfereji unaoleta maji kwenye makazi ya wananchi kwahyo akipata tena nafasi atapambana kulishughulikia
ina furahisha kwa kweli
 
nilikua kwa daladala asubuh namsikia diwan wa sisi emu kata X anaulizwa wapi anaona ameanguka kwenye kata yake na anataka kufanya marekebisho akipewa nafasi,
daaaaa,alitoa list ya shukrani kuanzia mama hadi mkurugenzi wa halmashauri X yule mtangazaji nahisi alitamani kucheka...
eti anasema ndani ya miaka minne wamepambana kugundua mfereji unaoleta maji kwenye makazi ya wananchi kwahyo akipata tena nafasi atapambana kulishughulikia
ina furahisha kwa kweli
Ndugu,

Time hii, USIOGOPE wenye pesa chafu,

Tuuingie na kugombea nafasi za kisiasa mbalimbali,

Viongozi Hawa, wanapita sababu wenye AKILI wamekaa pembeni na kuachia hao la Saba kuendelea kuongoza.

Nakushauri tia Nia gombea, utashinda, wananchi wamechoshwanna RUSHWA, ukizingatia pia kuwa time hii, wapigakura ni Hawa watoto wa 2000.
 
Back
Top Bottom