Mikasa aliyopata rafiki ya mama yangu

fimboyaukwaju

JF-Expert Member
Aug 3, 2020
3,569
4,632
SEHEMU YA KWANZA: URAFIKI WA DHATI.

Ni kwenye ile wilaya niliyoiongelea kwenye ile stori yangu ya jinsi nilivyokutana na singo maza wa kiarabu.
Ni miaka mingi imepita, wakati huo nilikuwa kidato cha kwanza.

Marehemu mama yangu alikuwa na rafiki yake, mama mmoja ambae alikuwa mpambanaji sana kwenye maisha.

Huyo mama alikuwa akifanya biashara ya kupika na kuuza chakula, na alikuwa maarufu sana kwa kupika kuku na alikuwa akitembeza kwenye mabaa. Pia alikuwa na banda ambalo kila siku mida ya mchana na jioni alikuwa akiuza vyakula.

Alikuwa na mumewe ambae alikuwa akifanya kazi kwa muhindi mmoja, usiku akilinda na mchana akifanya kazi mbalimbali hapo kwa huyo muhindi ambae alikuwa na biashara ya duka kubwa na malori ya kukodisha, malori ya tani 7 na tani 10.

Alibahatika kupata watoto 2 mmoja wa kike ambae nimwite Bankorwa japo sio jina lake, na wa kiume nimwite Sagala,nalo sio jina lake.

Huyu mama alikuwa ni rafiki mkubwa sana wa mama yangu. Mama akipata wageni humwita huyo mama Bankorwa kuja nyumbani kumsaidia kupika. Kutokana na urafiki huo nami pia nikawa ni rafiki wa huyo mama na wanae wakawa ni wadogo zangu, Sagala alikuwa akisoma la saba na Bankorwa alikuwa la tano.

Nikitoka shule nilikuwa naenda kwa huyo mama namkuta akifanya kazi za maandalizi ya upishi nami nikawa nasaidia kazi, kama mtoto wa hapo nyumbani. Yule mama alinizoea sana na mara kadhaa alikuwa akinituma kwa mama, na mama pia mara kwa mara alikuwa akinituma kwa huyo mama. Mara kadhaa mama alikuwa ananipa pesa kumpelekea huyo mama.

Nilikuwa nikifurahia sana maisha hayo maana yule mama alikuwa akinipa finyango ya nyama ya kuku na ilikuwa tamu mno hata sijui alikuwa anapikaje, na alikuwa anapata oda ya kuku mara kwa mara.

Katika mazingira ya ajabu, huyu mama alianza kupata mikasa ya ajabu, ambayo ndio msingi wa stori hii. Hii ni stori ya kweli kabisa. Naiandika nipendavyo mimi, ukiisoma sawa na usipoisoma pia sawa, ukitaka kutoa mapovu we toa, mie sitahangaika na mtoa mapovu.

Itaendelea baadae kidogo.
 
SEHEMU YA KWANZA: URAFIKI WA DHATI.

Ni kwenye ile wilaya niliyoiongelea kwenye ile stori yangu ya jinsi nilivyokutana na singo maza wa kiarabu.
Ni miaka mingi imepita, wakati huo nilikuwa kidato cha kwanza.

Marehemu mama yangu alikuwa na rafiki yake, mama mmoja ambae alikuwa mpambanaji sana kwenye maisha.

Huyo mama alikuwa akifanya biashara ya kupika na kuuza chakula, na alikuwa maarufu sana kwa kupika kuku na alikuwa akitembeza kwenye mabaa. Pia alikuwa na banda ambalo kila siku mida ya mchana na jioni alikuwa akiuza vyakula.

Alikuwa na mumewe ambae alikuwa akifanya kazi kwa muhindi mmoja, usiku akilinda na mchana akifanya kazi mbalimbali hapo kwa huyo muhindi ambae alikuwa na biashara ya duka kubwa na malori ya kukodisha, malori ya tani 7 na tani 10.

Alibahatika kupata watoto 2 mmoja wa kike ambae nimwite Bankorwa japo sio jina lake, na wa kiume nimwite Sagala,nalo sio jina lake.

Huyu mama alikuwa ni rafiki mkubwa sana wa mama yangu. Mama akipata wageni humwita huyo mama Bankorwa kuja nyumbani kumsaidia kupika. Kutokana na urafiki huo nami pia nikawa ni rafiki wa huyo mama na wanae wakawa ni wadogo zangu, Sagala alikuwa akisoma la saba na Bankorwa alikuwa la tano.

Nikitoka shule nilikuwa naenda kwa huyo mama namkuta akifanya kazi za maandalizi ya upishi nami nikawa nasaidia kazi, kama mtoto wa hapo nyumbani. Yule mama alinizoea sana na mara kadhaa alikuwa akinituma kwa mama, na mama pia mara kwa mara alikuwa akinituma kwa huyo mama. Mara kadhaa mama alikuwa ananipa pesa kumpelekea huyo mama.

Nilikuwa nikifurahia sana maisha hayo maana yule mama alikuwa akinipa finyango ya nyama ya kuku na ilikuwa tamu mno hata sijui alikuwa anapikaje, na alikuwa anapata oda ya kuku mara kwa mara.

Katika mazingira ya ajabu, huyu mama alianza kupata mikasa ya ajabu, ambayo ndio msingi wa stori hii. Hii ni stori ya kweli kabisa. Naiandika nipendavyo mimi, ukiisoma sawa na usipoisoma pia sawa, ukitaka kutoa mapovu we toa, mie sitahangaika na mtoa mapovu.

Itaendelea baadae kidogo.
Hatutatoa mapovu ila bando linaisha kwa kusubiria story!
 
SEHEMU YA PILI:KUPOTEA KWA MUMEWE NA WATOTO.
Maisha ya huyo mama na familia yake yalikuwa ni ya wastani tu,walikuwa wamepanga nyumba moja,iliyojengwa kwa matope ila imepigwa bati vizuri na imepakwa chokaa.
Yule mume wa huyo mama alikuwa mkimya mno,na hata akikutana nami barabarani au pale kwake huniuliza kama kwetu hawajambo namjibu ndio basi kimyaaa.
Ghafla siku moja,yule mama akaja kwetu na kwenda chemba kuongea na mama.
Baada ya dakika 20 nikaitwa,nikawa naulizwa iwapo najua kama bankorwa huwa na wanaume,nikajibu sijui kabisa.
Mama akaniambia bankorwa kafukuzwa shule maana kakutwa na mimba.Nilishangaa sana,maana mie nilikuwa naongea nae sana na hata siku moja sijawahi kuona dalili zote za wanaume,lakini sagala akasema yeye aliwahi kumuona mdogo wake na mwanaume mmoja ni dereva.
Mama akanituma nijamtafute bankorwa na nimlete nyumbani.Nikamtafuta na nilimpata kwao kalala nikampeleka hadi kwetu ambako mama na rafiki yake walikuwa wanamsubiri.
Wakamhoji kuhusu mimba,na bankorwa wala hakuwasimbua alimtaja mwanaume mwenye hiyo mimba,ni dereva anayefanya kazi kwa yule muhindi ambae na baba yake anafanya kazi.

Nikatumwa kumwita baba yake bankorwa,nikaja nae hapo kwetu,akapewa hizo taarifa na alijibu yeye hana la kufanya.
Basi mama na rafiki yake wakalivalia njuga hilo suala.Mama akaamua bankorwa akae na sisi hapo nyumbani mpaka jambo hili litakapo pata ufumbuzi.

Baba yetu alipokuja akapewa hiyo stori akakubaliana na mama kuwa bankorwa akae kwetu na yeye atamwita huyo mwanaume anayedaiwa kumpa mimba bankorwa.
Yule bwana akaitwa siku moja jioni hapo nyumbani na moja kwa moja alikubali kuwa ndio anahusika na hiyo mimba na yuko tayari kumuoa bankorwa.
Ikapangwa harusi ndogo tu na bankorwa akaolewa na akaenda kuishi na mumewe.
Bankorwa alipojifungua mtoto wa kiume,alirudi kwa mama yake ambako alikaa miezi 3 na akarudi kwa mumewe.Ghafla siku moja wakati mumewe akiwa safari bankorwa alifariki.
Aliugua ghafla mama na rafiki yake walimpeleka hospitali ya wilaya ambako alikufa kesho yake.Ulikuwa msiba mkubwa sana na mama aliubeba huo msiba akisaidiana na wanawake wengine.Ikabidi huyo rafiki ya mama amchukue huyo mtoto kumlea yaani mjukuu wake,hali hii ilimfanya rafiki ya mama kupunguza kazi za upishi ili kumlea mjukuu,yule baba wa mtoto alijitahidi sana kupeleka matumizi na mama pia alitoa msaada mkubwa sana.
Baada ya mwezi mmoja,nikamwona rafiki yake na mama anakuja mbimbio hapo nyumbani na akamwambia mama kuwa wale wahindi matajiri wa mumewe wamakwenda kwake kumuuliza mumewe maana hawamwoni kazini siku 2.
Akawajibu hata yeye hajamuona na alitoka hapo kama kawaida tu akiaga anaenda kazini.
Basi mama na rafiki yake na mimi tukaenda polisi kutoa taarifa,wale wahindi pia waliitwa kutoa statement yao na wakasema hakuna kosa lolote alolofanya na hawajui kimempata nini.Hivyo ndivyo alivyopotea baba bankorwa ambae hakuonekana tena hadi leo hii.
Mama bankorwa akawa na huzuni kubwa sana na hata biashara ikawa anashindwa kufanya,akawa anadaiwa kodi ya nyumba,mama yangu akawa analipa.

Sagala akawa anasoma huku anaendesha biashara ya mama yake kidogokidogo.
Ulipofika mtihani wa darasa la sana,sagala akafaulu na kwenda sekondari moja,iliyopo mkoani.
Mama akachukua jukumu la kumuandalia sagala kila kitu na ndie alimpeleka shuleni akitumia landrova ya baba.

Baada ya mwezi mmoja mama yangu akaitwa kwa mkuu wa wilaya,tukaenda nae mimi,tulipofika tukaulizwa tuna taarifa zozote za sagala,mama akasema hana ila yeye ndio alimpeleka shule na akaacha mawasiliano yake hapo shuleni,ndipo akaambiwa sagala hajulikani aliko,kwani kuna jumamosi wanafunzi waliruhusiwa kwenda mjini kutembea toka siku hiyo hajarudi tena
Tulishtuka sana sana,dereva wa mkuu wa wilaya akatumwa kumleta mama yake sagala,ambae alipofika akapewa hizo taarifa,akabaki kulia.Basi tukarudi nyumbani huyo mama akaishiwa nguvu kabisa,kapoteza binti yake,mume hajulikani alipo na sasa mwanae pia hajulikani alipo.Serikali ikatangaza kupotea kwa sagala kwenye gazeti ili aliyemuona atoe taarifa.Ila alikuwa hajafanya kosa lolote shuleni na alikuwa ni kijana mwema,mpaka leo hii sagala hakuonekana tena.

Mama bankorwa aliishiwa nguvu ikawa anazimia kila mara,mume wa bankorwa akamchukua mwanae iki kumpa fursa mama bankorwa kupata utulivu

Baba na mama yangu wakamchukua mama bankorwa akae kwetu mpaka atakapokaa sawa.
Baada ya mwezi mama akaniambia nimsindikize kitongoji fulani kipo kama kilometa 2 kutoka hiyo wilaya tuliyokuwa tunaishi.Akakutana na mwenyekiti wa kijiji na akanunua nyumba moja ya mzee mmoja wa kitusi ambae aliamua kuhama,ni nyumba ya vyumba 3 na ua uliozungushiwa minyaa na shamba la ekari moja.Taratibu zote zikafanywa,mama akalipa pesa,hati ya mauziano ikaandikwa na mama akakabidhiwa nyumba.
Tukarudi nyumbani na mama akamuarifu rafiki yake kuwa wamemnunulia nyumba na wiki ijayo watampeleka kwake.

Siku ya siku,mimi,mama,baba na warafiki wa mama tukampeleka mama bankorwa kwenye nyumba yake ambayo aliishi huko.Mama yangu na baba walihama waka relocate nami niporudi baada ya kumaliza masomo nilienda kumtafuta yule mama ambae alikuwa kazeeka sana,tukaongea na tukafurahi sana.
Hayo ndio mikasa aliyopitia huyo mama ambae baadae nilipata taarifa alifariki na hiyo nyumba alimrithisha mjukuu wake ambae yu hai hadi leo.MWISHO
 
Ingekuwa USA,mama yako angekuwa suspect number one
Sio kwa wema huo
Kikukacho kinguoni mwako
Panya hupuliza huku akikuuma
 
Back
Top Bottom