Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
h.sep7.gif
master.gif

BASATA, iwapi taarabu yetu ya asili?
ban.blank.jpg


Juma Kasesa​

amka2.gif
AHLAN wasaalan mpenzi msomaji wangu wa Jamvi la Kulonga. Ni Ijumaa nyingine tunakutana Jamvini katika kujadili na kuchambua haya na yale yaliyojiri na yanayotarajiwa kutokea katika tasnia ya sanaa na burudani.
Leo katika Jamvi letu nataka nigusie kiduchu kuhusu muziki wa taarabu ambayo una asili ya utamaduni wa jamii ya watu wa pwani ya Afrika Mashariki, hapa nikizungumzia miji ya Mombasa, Tanga, Zanzibar, Kisumu na kwingineko.
Kimsingi hoja iliyonisukuma kuandika Jamvi hili ni baada ya kuutazama kwa jicho la pili muziki huo wapi ulikotoka na wapi unaelekea ambako ni ashirio kuwa anguko la utamaduni wa muziki wa pwani ya Afrika Mashariki.
Pengine kabla Jamvi hili halijaingia kwa undani katika kile ambacho kimelisukuma kuzungumzia muziki huu, ni vema msomaji ukafahamu muziki wa taarabu asili ya pwani ya Afrika Mashariki umeimbwa na waasisi wengi lakini kwa uchache naweza kukutajia Bi Kidude, Issa Matona, Mohamedi Kassim, Shakila Saidi, Sabaha Muchacho, Mwanahawa Ally, Juma Ballo na wengineo wengi.
Waasisi hao kwa nyakati tofauti waliweza kutunga na kuimba nyimbo mbalimbali ambazo ziliitangaza pwani ya Afrika Mashariki na kupata umaarufu na nguvu za kiuchumi kutokana watalii wa ndani na wa kimataifa kwenda kutembelea baadhi ya miji na kujifunza masuala mbalimbali na utamaduni wa wakazi wa pwani hiyo.
Jamvi la Kulonga linakujulisha kuwa nyimbo nyingi za wakongwe hao ambao wengine wameshatangulia mbele ya haki, waliweza kutunga na kuimba nyimbo za kupigana vijembe ama kutambiana kulingana na ubora wa makundi yao, lakini wakitumia tafsida katika mashairi na ilikuwa ni kazi ngumu kutambua kijembe hicho kilikuwa kikililenga kundi gani kutokana na uficho wa maneno.
Pengine nikumbushe mwanzoni mwa miaka ya 1990 wakati mwimbaji nyota wa bendi ya Tanzania One Theatre (TOT), Khadija Omary Kopa, alipotunga wimbo wa ‘TX wangu mpenzi', huu ulikuwa ni wimbo ambao kwa wachambuzi wa muziki wa taarabu ulikuwa na maneno mengi ya karaha na kuudhi na laiti Kopa angeamua kuyatumia bila tafsida usingefaa kusikilizwa katika jamii ya watu wastaarabu na waungwana lakini aliamua kumvika johoo la udaktari mtu ambaye alikuwa akimtaja kama mpenziwe akimsifia kwa namna alivyoweza kumtibu maradhi yake.
Lakini si Khadija pekee hata ilipofika katikati ya miaka ya tisini na mwanzoni mwa mwaka 2000, pale ambapo ndipo mapinduzi ya muziki huu yaliibuka yakiasisiwa na makundi hasimu ya taarabu ambayo yalikuwa ni TOT chini ya Kopa huku Muungano ikitamba na hayati Nasma Kidogo, bado kulikuwa staha katika nyimbo zao walizoimba ingawa hali ilikuja kubadilika baadae kutokana mashabiki kuwalazimisha kuimba bila tafsida.
Lakini ikiwa hiyo haitoshi ubora wa mashairi mengi ya wakati huo yalisaidia kuuutangaza muziki huo sambamba na ala zilizokuwa zikitumika katika kutia nakshi muziki huo, ambao kwa Tanzania, ni Zanzibar ndiko ambako bado hadi leo wanapiga kidogo muziki wa taarabu wenye asili ya Pwani yetu ya Afrika Mashariki.
Jamvi la Kulonga ni mmoja ya wadau wakubwa wa muziki wa Taarabu wenye asili ya Pwani, lakini kutokana na mabadiliko ya dunia na kuibuka kwa utandawazi, muziki huo umeonekana kupoteza muelekeo huku Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kama chombo chenye dhamana ya kulinda utamaduni na sanaa ya Mtanzania kikiwa kimekaa kimya huku hali ikizidi kuwa tete.
Nikirudi katika hoja ya msingi iliyonisukuma kuandika Jamvi hili, ni wazi utagundua kuna tofauti kubwa ya muziki huo na huu wa sasa ambao unaitwa ‘Modern Taarabu' kutokana na kasoro nyingi ambazo zimeutawala muziki huo.
Swali ambalo Jamvi hili linajiuliza hivi kweli huu ndiyo muziki wa taarabu wa asili asili yetu? sitaki unipe jibu lakini kimsingi tumepotea njia na bahati mbaya hatuna wa kutoongoza kutokana waliopewa dhamana ya kulinda utamaduni na sanaa hiyo, ambao ni BASATA wamekumbwa na upofu, nani atamuongoza mwenzake?
Jamvi hili siyo kwamba linaikataa Modern Taarab, lakini kwa namna inavyozidi kuchakachuliwa ni wazi jahazi la muziki huo linaelekea mrama, kama si kuzama kabisa kutokana na muziki huo kuanza kumezwa na vionjo vingi vya Kikongo ambavyo vimekuwa vikiingizwa hapa, nikiwa nayazungumzia masebene na kutajana majina katika nyimbo hizo.
Mzee wa Jamvi la Kulonga anajiuliza, hivi kweli sisi tumekuwa watu wa kuiga kila kitu? Kama muziki wa dansi wenye asili ya Tanzania umemezwa na vionjo vya Kikongo tumeshindwa kuulinda sasa na huu wa taarabu nao? Hii ni hatari zaidi ya hatari na sitaki kuamini Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kama kweli ina maofisa utamaduni ambao wameajiriwa kwa ajili ya kusimamia utamaduni na wakipokea mshahara ambao ni jasho la wanyonge huku wakilikalia kimya suala hili.
Kimsingi muziki wa taarabu ambao asili yake ni pwani ya Afrika Mashariki, ni ule pekee ambao mashairi yake yalikuwa na tafsida, lakini ukielimisha jamii kama ilivyo umuhimu wa muziki katika jamii, pia kwa wapenzi na mashabiki waliokuwa wakienda katika kumbi hizo za maonyesho walikuwa wakivaa mavazi ya kujistiri na wakitulia vitini, je, haya yanafanyika sasa?
Hofu ambayo imelizunguka Jamvi hili ni kwamba wanamuziki wa muziki wa taarabu wa sasa wakiambiwa kwenda nje ya nchi kwa ajili ya maonyesho ya muziki ni wazi hawawezi kuwa wawakilishi wazuri wa muziki huo kutokana na kupiga muziki ambao si wa asili ya Tanzania wala Pwani ya Afrika Mashariki.
Kwa mashabiki wenye kujua asili ya muziki huo, ambao waliwahi kutembelea pwani hii watagundua labda hawa ni Wakongo wanaoishi Tanzania, kutokana na kukosa ladha ile iliyozoeleka miaka mingi ya muziki huo.
Kwa leo nalikunja Jamvi lakini ni changamoto mpya kwa Baraza la Sanaa la Taifa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuanza kutathmini mwelekeo wa muziki wa Tanzania kwa ujumla ili kuepuka anguko ambalo linatunyemelea lakini lengo likiwa ni kulinda utamaduni na asili ya muziki wetu.


h.sep3.gif

Tuwasiliane kwa barua pepe: jkasesa@hotmail.com, simu 0715-629298
 
Wanamuziki bongo vueni gamba
ban.busati.jpg


Khadija Kalili​

amka2.gif
IKIWA katika siasa wanasiasa wamefanikia kujivua gamba, kwa nini katika muziki wa dansi nchini bado mambo ni yaleyale?
Licha ya kwamba upo usemi kuwa nyoka hata kama atajivua gamba sumu yake itabaki palepale, hiyo ni kweli, lakini sasa ufike wakati wote kwa pamoja tuungane na kuchangaya mawazo kwamba ili kuunusuru muziki wetu, hasa ule wa dansi ni lazima wanamuziki wa hapa nchini wajivue magamba.
Watajivuaje na kwa nini nasema wajivue? Binafsi nimekuwa katika muziki na ninaupenda muziki tangu nilipokuwa mtoto mdogo, tena nakumbuka wakati ule muziki ulikuwa ukitumika kwa kucheza santuri, ambapo nilipenda sana kuwa pembeni ya baba yangu wakati alipokuwa akipata muda wa kusikiliza ngoma hizo na nyinginezo zile za zamani.
Kama hiyo haitoshi, pia nilikuwa nikikaa naye usiku kama sikosei ilikuwa kuanzia saa nne usiku, ambapo kila mwisho wa juma kulikuwa na kipindi kile kinachokumbukwa na watu wa zamani cha ‘Zilipendwa', ambacho kilikuwa na mkusanyiko wa nyimbo kibao zilizokuwa zikitamba enzi hizo kutoka kwa bendi ya Less Wanyika ya Kenya, Orchersta Lipua lipua, bendi iliyoundwa na jirani zetu Wakongo, Tabora Jazz, Afro Sabini na TP OK Jazz iliyokuwa ikiongozwa na hayati Le Maestro Luanzo Makiadi Franco na nyinginezo nyingi ambazo hata leo zikipigwa kila mtu ataacha shughuli yake na kutoa ushirikiano wa kutikisa japo kichwa.
Katika bendi zote hizo na nchi zake kwa ujumla, ilikuwa ni rahisi na hata sasa itabaki kuwa hivyo kwamba ngoma hizo bado zitadumu na kudumu kwa vizazi vijavyo.
Kwa nini basi nasema hivyo, ni kutokana na bendi zetu zote zilizopo na zinazoanzishwa kuwa hazina ubora wa kusimama na kujitambulisha kuwa wanapiga muziki wa Kitanzania.
Katika hili naomba nieleweke kwa nini nasema hivyo, ni kutokana na bendi zote kukwapua vionjo vya muziki wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), bila kuficha hili ni jambo la kusikitisha sana.
Binafsi nilidhani kwamba labda wasanii wetu kadiri siku zinavyokwenda au mdau mmoja akijitokeza na kuanzisha bendi huenda mambo yatabadilika, lakini wapi, utasikia mambo ni yale yale kana kwamba wameishiwa ubunifu.
Na katika hili, mifano iko mingi hapa katika bendi zetu , tukianza na hizo zenye wanamuziki wengi wa DRC wao huzichukua nyimbo za wasanii kama Ferre Gola, Fally Ipupa na wengineo wanazitafsiri na kutumbuiza katika lugha ya Kiswahili huku wakijigamba wametunga wao, na sisi kwa ujuha wetu tunazishabikia.
Haya tuje katika bendi zetu ambazo zinaitwa za wazawa, nako pia mambo ndiyo yaleyale, afadhali ya jana, wallah wao nao wanakwapua rapu za haohao Wakongo na kuchanganya na vitimbwiri vya hapa na pale, basi ilimradi muziki wa dansi Tanzania umejaa vurugu tupu na kwa mtindo huu safari yetu karibu tutafika ukingoni.
Taswira ya kufika ukingoni iko karibu kwani hivi sasa kila bendi tungo zinafanana, wote wanaimba visa vya mapenzi huku wakishindwa kuwa wabunifu na kutunga nyimbo zenye tungo za kuchoma, kama hali ya kisiasa nchini tulikotoka, tulipo na wapi tunakokwenda.
Hakika natamani wasanii wangeliwaomba wana habari wawaandikie mashairi huku kazi yao ikiwa ni katika kutia muziki kama ilivyo kwenye taarabu, nadhani kwa kutumia tahariri zinazotoka kila kukicha kwenye magazeti wangeweza kutoka na tungo za kudumu maishani.
Pia wasanii wetu wanaonekana kwamba wamesahau kuwa kwa kupitia nyimbo mtu anaweza kupata hadithi ya miaka kadhaa nyuma, kutunza utamaduni na ngoma zetu za asili pia, lakini wao wamekuwa wakidharau utamaduni wa kwao na kuthamini cha mtu, hakika nakihurumia kizazi kijacho cha muziki, sijui watarithi nini katika medani hii.
Nionavyo watabaki wakiwasikiliza magwiji kama hayati Mbaraka Mwinshehe, Marijani Rajabu, Hemed Maneti na wengine lakini hawa wa sasa tayari wako taabani, kazi imewashinda.
Hivi kuna ugumu gani wa kutunga nyimbo za makabila mbalimbali huku nchi ikiwa imejaliwa kuwa na makabila zaidi ya 120 lakini bado tunaona vya kwetu havifai ni bora kuiga miondoko ya jirani!
Tukianza na Nyanda za Juu Kusini kuna ngoma ya Lizombe, Kanda ya Kati utawakuta Wagogo na ngoma yao ya Palinga Chibite, Wanyamwezi na ngoma yao ya Hiari ya Moyo, Sangula Wapogoro, wenyeji wa Morogoro, Baikoko na Mdumange Tanga, Bogobogo inayochezwa na wenyeji wa Mkoa wa Mwanza, Warumba Kigoma bila kuwasahau Waha ambao walienziwa na bendi ya In Afrika kwa kupitia wimbo wa Indege.
Tuje kwa Wazaramo ambao ndio wenyeji wa Jiji la Dar es Salaam bila kusahau ngoma zao kama Gombe Sugu, Mdundiko, Vanga, Mkwaju ngoma na nyinginezo nyingi.
Hiyo ni baadhi ya mikoa michache tu ambayo nimeitaja kuwa wana ngoma nzuri ambazo laiti kama wanamuziki wakijituma ipasavyo tungo zao na kuweka mahadhi ya nyumbani itapendeza na zaidi katika kujitangaza kimataifa.
Lakini kama mambo ya kujidharau yataendelea, tutabaki kubung'aa katika soko la muziki la kimataifa.
Wadau leo na mimi nimeamua kujivua gamba, wala msiniwekee chuki na kusema huyu leo vipi, huu ni wigo wangu wa kuwakosoa hata kama hamtapenda hilo nalitambua, lakini ukweli ndio huu kwamba kama muziki wa Kitanzania utaendelea kuwa wenye virakaviraka vya ramani za nchi kadhaa hatutapanda, tubadilike.
Nasema hivyo kwa sababu hivi sasa muziki wa bendi zote unafanana, hivi ninyi wenyewe hamuoni au labda mnaturudisha enzi zile za DRC, ambapo nakumbuka enzi za Kwasakwasa wote walicheza mtindo huo.
Kwa mtindo huu bendi zetu zitaendelea kutegemea mapato ya mlangoni pekee na si kujiuza kimataifa au vinginevyo, mtaendelea kushikana uchawi kutokana na labda bendi yako kukosa mashabiki wengi, hiyo inatokana na wote mnafanana sasa kwa nini mtu ajikoseshe usingizi wake kwa kwenda kuona mambo aliyoyaona jana?
Binafsi ni bora niende bendi ya waimbaji wakongwe ambao wako kwenye fani kwa miaka zaidi ya 35 sasa lakini hawajachuja nao si wengine bali ni The Kilimanjaro ‘Wana Njenje' , ambako ukifika kama wewe ni mwenyeji wa mkoa fulani utafurahia kucheza ngoma ya kwenu ambayo imepigwa kisasa lakini katika mtindo uleule, hivyo kwa nini wengine washindwe ilhali zana wanazo na katika kila bendi kuna mwenyeji kutoka mkoa huo?
Hapo ndipo ninapojiuliza, nini tatizo kwa bendi zetu kuigana midundo, rapu na wakati mwingine hata unenguaji, licha ya kwamba huwa wanajaribu kutupotezesha kidogo ila wajanja tunajua, wadau jitokezeni ili kuzisaidia bendi zetu zisimame na kurudi katika uhalisia wa Kitanzania.
Hata hivyo, binafsi nachukua fursa hii kuwashauri wasikate tamaa, kwa sababu muziki ni sawa na bidhaa ambayo hutegemea msimu, huenda hali ikageuka kulingana na wakati husika.
Tukumbushane kwamba wanamuziki wa DRC ambao wamekuwa nyota na kufanikiwa ni kutokana na misingi madhubuti waliyowekewa enzi za Rais Mobutu Seseko, kwamba ilikuwa ni sharti wanamuziki kuimba katika lugha ya kwao na kupiga mahadhi ya kwao, si hao wametoka? Kwanini hawakumuiga Mfaransa ambaye ndiye lilikuwa koloni lake?
Watanzania tuamke sasa. walikuja wasanii kutoka Botswana ‘Makhirikhiri Group' wakatuchezesha tukajaa Diamond Jubilee na kucheza ngoma ambayo wala hakuna aliyekuwa akielewa wanaimba nini, zaidi ya kufasiriwa na Rais wa kundi lile, Rumba Rashega, kwamba wanaimba kuhusu kupambana na ukimwi.
Kwa leo naomba nikunje busati langu, huku nikiwatakia wote wikiendi njema.
 
MARIAM PAKA MAPEPE - Alikimbia Five Stars siku chache kabla ya ajali
ban.blank.jpg


Abdallah Menssah​

amka2.gif
KESHOKUTWA Jumapili, mashabiki na wadau mbalimbali wa mipasho, wanatarajiwa kuungana na baadhi ya wasanii wa kundi la Five Stars, katika kisomo cha kuwaombea dua wenzao waliopoteza maisha kwenye ajali iliyotokea Machi 21, Mikumi, mkoani Morogoro.
Kisomo hicho kitakachoanza majira ya saa 5:00 asubuhi na ambacho kitahudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini na serikali, kimepangwa kufanyika kwenye ukumbi wa PTA ulioko katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere (Sabasaba), jijini Dar es Salaam.
Wakati mashabiki, wapenzi pamoja na wadau wa mipasho wakisubiri kujumuika kwenye kisomo hicho, bila shaka wengine wao watakuwa wanakumbuka baadhi ya matukio haya na yale yaliyowahi kujiri muda mfupi kabla ya ajali hiyo iliyoteketeza roho za takriban wasanii 13 wa kundi hilo la Five Stars.
Moja ya matukio hayo ni kama lile la mwimbaji nguli wa kike na mmoja wa waanzilishi wa Five Stars iliyokuwa ikitumia mtindo wa ‘Watoto wa Bongo', Mariam Khamis ‘Paka Mapepe' kuipa kisogo siku chache kabla ya ajali, ambapo alitimkia katika kundi jingine la Tanzania One Theatre (TOT Taarab).
"Unajua, kama bado ningelikuwa sijaihama Five Stars, ni lazima ningekuwamo kwenye ajali ile," anasema Paka Mapepe katika mazungumzo na mwandishi wa makala hii, yaliyofanyika kwenye makao makuu ya TOT Taarab, CCM Mwinjuma, jijini Dar es Salaam juzi.
Paka Mapepe anasema anaamini kuwa lazima angekuwamo kwenye ajali ile kutokana na kwamba, ndani ya Five Stars alikuwa ni kiraka na kati ya waimbaji wanaotegemewa mno, ambapo ilikuwa si rahisi kwake kukosa kuwamo katika ziara kubwa, hasa za mikoani kama ile.
Akizungumzia zaidi namna anavyoumia kutokana na ajali ile ya wasanii wenzake, Paka Mapepe anaeleza kuwa ni msiba mkubwa uliogonga kwa kishindo moyoni mwake kiasi cha kumfanya mara nyingine awe anaweweseka na kuwaota baadhi ya marehemu wasanii waliokuwa wameshibana zaidi.
Aidha, Paka Mapepe anakumbuka alivyoishi vizuri na wasanii wote wa Five Stars hata pale alipoamua kubadili upepo wa kikazi kwa kuhamishia mabegi katika kundi hili aliloko sasa, lililo chini ya Mbunge wa Mbinga Magharibi, Kapteni mstaafu, John Damian Komba.
"Nakumbuka niliingia Five Stars mwishoni mwa mwaka juzi, 2009, ambako nilifikia kurekodi kibao kinachokwenda kwa jina la ‘Ndo Basi Tena', kilichokuja kubeba jina la albamu ya mwisho ya kundi hilo," anasema Paka Mapepe, miongoni mwa waimbaji wa kike wenye sauti ya kuvutia.
Anasema kuwa baada ya kurekodi kibao hicho, mwanzoni mwa mwaka uliopita, 2010, aliingia tena studio na kuipua wimbo unaokwenda kwa jina la ‘Uzushi Wenu Haunitii Doa', uliokuja kuwamo kwenye albamu ya kwanza ya Five Stars, iitwayo ‘Riziki Mwanzo wa Chuki'.
Wakati akiwa Five Stars, Paka Mapepe alikuwa akionekana kupagawisha mashabiki pamoja na wapenzi waliokuwa wakihudhuria maonyesho yao tofauti, kutokana na namna alivyojaliwa kuimba kwa pozi na mbwembwe za hapa na pale huku akiirembesha sauti yake kwa bashasha hizi na zile.
Unapomuuliza maisha yake kimuziki yalipoanzia, Paka Mapepe anakwambia kuwa alianza kuipenda fani hiyo mara tu baada ya kuhitimu elimu yake ya sekondari, kwa kuvutiwa na baadhi ya magwiji wa mipasho kama vile Zuhura Shaaban, Nasma Khamis na Khadija Kopa.
"Wakati huo, kutokana na shetani wa muziki kunipanda kindakindaki kichwani, nilikuwa nikiandika kwenye daftari mashairi ya baadhi ya vibao vyao na kuviimba mara kwa mara kila nilipotulia," anasema Paka Mapepe.
Anakumbuka kuwa kati ya watu waliokigundua mapema kipaji chake cha uimbaji na kuamua kukifanyia kazi kwa nguvu ni baba yake mdogo aliyemtaja kwa jina la Kessy Abdallah, ambaye alimuunganisha kwenye kundi la Segere No. 2, jijini Dar es Salaam ili kujifua zaidi.
Akiwa katika kundi hilo la Segere ambalo baadhi ya vinara wake alikuwa ni Mussa Msuba aliyeko katika kundi la Jahazi Modern hivi sasa, alirekodi kibao kimoja kinachokwenda kwa jina la ‘Mpenzi Wangu' na kabla albamu yake haijatoka, kundi lilisambaratika na kuvunjika kabisa.
Mwaka 2007, uwezo wake wa kimuziki ulizidi kukua na kuonwa na Mussa Mipango, kati ya wacharazaji mahiri wa gitaa la besi hapa nchini, aliyeko TOT Taarab hivi sasa na ambaye alimuunganishia katika kundi la Zanzibar Stars Modern Taarab ‘Watoto wa Pwani'.
"Sikukaa sana hapa Zanzibar Stars kwani mwaka huohuo, 2007, nilitimka na kuhamia East African Melody Taarab, nilikorekodi kibao ‘Paka Mapepe' kilichotokea kutikisa vilivyo kiasi cha mashabiki pamoja na wapenzi kuamua jina hilo liwe langu moja kwa moja," anasema Paka Mapepe.
Mwaka 2008, Paka Mapepe alivutwa tena Zanzibar Stars, ambako alifikia kurekodi kibao ‘Huliwezi Bifu' kabla ya kufuatiwa na vingine kama ‘Raha ya Mapenzi', ‘Narindima Mie' pamoja na ‘Shoga Habari Ndo Hiyo' kinachopatikana kwenye albamu ya kundi hilo iitwayo ‘Mwanamke Mvuto'.
Paka Mapepe ambaye anakiri kuwa ujuzi wake kiuimbaji unatokana zaidi na kutilia mkazo Madrasa ya Shadria, jijini Dar es Salaam, alikosoma na kufikisha juzuu mbili, anawaahidi mambo makubwa mashabiki pamoja na wapenzi wa kundi lake la sasa la TOT Taarab.
Hivi sasa anatamba na kibao kinachokwenda kwa jina la ‘Sidhuriki na Lawama' alichopewa kurekodi mara tu baada ya kuingia TOT Taarab, ambacho mwenyewe anathibitisha kuwa, kimetokea kumsogeza karibu zaidi na mashabiki wengi wa mipasho hapa nchini.
"Kati ya watu ninaowashukuru kwa dhati kutokana na juhudi zao kuwa ndio zilizonifanya kufika hapa ni baba na mama yangu walionipa moyo tangu nilipokuwa naanza kujiingiza katika muziki, vikundi vyote nilivyopitia ikiwamo Melody pamoja na mashabiki kwa ujumla," anasema.
Paka Mapepe ambaye ni mke wa mcharazaji mahiri wa gitaa la besi wa kundi la Dar es Salaam Modern Taarab, Haji Kijungu, ni mama wa familia mwenye mtoto mmoja aitwaye Taliq (5), anayeishi Magomeni Kondoa, jijini Dar es Salaam na mumewe huyo anayedai anampenda sana.
Huyo ndiye Mariam Khamis, maarufu kama ‘Paka Mapepe' aliyelipa kisogo kundi la Five Stars siku chache kabla halijatokewa na ajali iliyoteketeza maisha ya wasanii wake takriban 13 hivi karibuni Mikumi, Morogoro.


h.sep3.gif

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa simu namba 0718 102050, au barua pepe: abmenssah@yahoo.com
 
Wizara ya Viwanda na dhamana ya sheria ya Hakimiliki/Shiriki Tanzania
ban.blank.jpg


Makuburi Ally​

amka2.gif
WADAU wa tasnia ya sanaa hapa nchini kila kuchao wanapiga kelele ya kuibiwa kazi zao kutoka kwa wadau ambao wametega mipangilio yao inayofanikisha kunyonya kazi za wasanii ambao wanaumiza vichwa kusaka namna ya kupiga hatua.
Mara nyingi inaonekana wizi wa kazi hizo unatokana na wasanii wenyewe kutofahamu haki zao kisheria, hali ambayo inadhoofisha maendeleo yao ingawa kuna wenye kufahamu haki na sheria zao lakini bado taratibu husika zinakosa nguvu ama meno katika utekelezaji wake.
Wizara ya Viwanda na Biashara ndiyo chimbuko la Chama cha Hakimiliki na Shiriki Tanzania (COSOTA) ambacho ndicho chenye mwelekeo wa maendeleo ya wasanii hapa Tanzania na nje ya Tanzania.
COSOTA ndiyo msimamizi wa maendeleo ya sanaa ambako imetunga sheria na kanuni mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia wasanii wa tasnia mbalimbali wakiwemo wa muziki, maigizo, filamu, hadithi na masuala mengine yanayohusu sanaa na utamaduni kuhusu haki zao kwa kazi wanazozifanya.
Weledi wa sanaa wenye kufahamu haki zao wanakiri kwamba sheria za hakimiliki na shiriki zina upungufu ambao unatakiwa ufanyiwe kazi ili sheria ziwe na meno yatakayofanikisha kuwadhibiti wezi wa kazi za sanaa hapa nchini na nje ya nchi.
Rulu Arts Promotions ni mojawapo ya asasi iliyojipanga kwa ajili ya kusaka namna ya kuwasaidia wasanii wa Tanzania, kampeni ambazo walizianza tangu Desemba mwaka 2005 wakishirikiana na Best AC wakiwa na lengo la kusaidia kuziba mianya ya kuibiwa kazi zao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Rulu Arts, Ruyembe Mulimba, anasema walianza kufanya utafiti wa kusaka mpangilio wa awali kwa kuanzia na muziki na matatizo yake, utafiti uliofanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Iringa, Ruvuma, Mwanza, Arusha, Morogoro na Zanzibar ambayo walianza Januari 9, mwaka 2006 hadi Januari 26, mwaka 2006.
Mulimba anasema utafiti huo ulifanywa na mchumi A. Millinga, Mwanasheria Yustus Mkinga, na mwalimu wa muziki, Angelo Luhala, na Meneja mradi akiwa yeye, ripoti yake iliwasilishwa katika warsha ya wadau wa sanaa iliyofanyika Mei 13-15 mwaka 2006, Bagamoyo ambayo ilishirikisha wadau 65 na mtaalamu kutoka Chama cha Hakimiliki cha Malawi (COSOMA), M. Munkondia.
Mulimba, anasema matatizo ya ulanguzi, upungufu wa sheria na mianya ya udhibiti ulanguzi pia ulinzi wa kazi za sanaa na hasa muziki ilikuwa ni mambo yaliyojadiliwa katika warsha hiyo ambapo wadau walifikia hatua ya kuainisha mianya hiyo na upungufu wa sheria husika namba saba ya mwaka 1999 ya hakimiliki na shiriki.
Anasema warsha hiyo ilifuatiwa na ya mjini Dodoma iliyofanyika Julai 17 mwaka 2006 ambayo ilishirikisha wabunge 40 wa Kamati ya Ustawi wa Jamii.
Mulimba anasema Mei 22 na 23 mwaka 2007 katika Hoteli ya Lamada washiriki 21 walishiriki warsha iliyondaliwa na na Rulu Arts na Best AC wakiwamo wataalamu wawili, Dk. Aikaeli Jehovaness, ambaye ni mchumi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na G. Gilfillan wa Afrika Kusini, ambaye ni Mkurugenzi wa South African Recording Rights Association (SARRAL).
Anasema Gilfillan alitoa uzoefu wa Afrika Kusini kwa wadau na viongozi katika idara na wizara husika na shughuli za sanaa kutoka BRELA, COSOTA, BASATA, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, Law Reform Commission, TRA na VIBINDO.
Mulimba anasema ilifanikisha washiriki wa semina hiyo kujifunza elimu hiyo mwaka 2008 nchini Afrika ya Kusini ya kupata uzoefu kuhusu uanzishwaji wa vyama vya kukusanya na kugawa mirabaha (Collecting Societies).
Aidha, Mulimba anasema harakati za kusaka namna ya kuwasaidia wasanii iliendelea Februari 11 mwaka jana, mwanasheria Adam Mambi wa Law Reform Commission aliwasilisha mapendekezo ya mabadiliko ya sheria husika na wahusika walipata fursa nyingine ya kutoa maoni yao na hatimaye Mei 11 mwaka jana Rulu Arts na Best AC walikabidhi rasimu ya mapendekezo ya mabadiliko ya sheria Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko ili iwasilishwe bungeni.
Baadhi ya mapendekezo ya mabadiliko ya sheria ya hakimiliki na shiriki ni pamoja na vifungu vya sheria kuwataja kwa mfumo wake na utekelezaji kama Polisi, mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na uingizaji wa bidhaa kupitia bandarini (Customs).
Sheria nyingine ni utunzaji wa mali zinazokamatwa, adhabu kwa wanaokutwa na mali za wasanii, sheria ilikuwa ikitamka kwamba mtuhumiwa akikamatwa na mali ya wizi atatozwa faini chini ya sh mil. tano na badala yake inatakiwa itambulike kama mtuhumiwa akikamatwa na mali ya msanii atozwe faini zaidi ya sh milioni tano.
Sheria nyingine inayotakiwa kufanyiwa marekebisho ni msisitizo wa ukaguzi wa wizi wa kazi za sanaa ufanywe kwa asilimia kubwa na maofisa wa COSOTA ambao pia wanatakiwa wawe na haki ya kusimamia kwa karibu kesi za wasanii mahakamani.
Nyingine ni mwongozo stahili wa pande mbili za mlalamikaji na mlalamikiwa katika usuluhishi baada ya kesi ya pande mbili kukosa suluhu, kuwepo na usimamizi wa sticker ya Hakigram kuelekea suala la ukaguzi.
Mapendekezo mengine ni matumizi ya baadhi ya maneno kama Inspector, mirabaha, Afisa, Mkaguzi, Promota, Producer na msanii vielezwe maana zake kisheria na nyinginezo kama haki ya kununua na kuuza sehemu nyingine kwa gharama kubwa zaidi, sheria ya kuharibu mali iliyokamatwa, ofisi zinazolinda haki za wasanii na ambao walifariki dunia zaidi ya miaka 50 baada ya kifo cha msanii, haijaainishwa kwamba baada ya miaka 50 ni nani mwenye mamlaka ya kazi ya marehemu.
Mulimba anasema mapendekezo hayo yameshapelekwa Ofisi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko kwa ajili ya kuipeleka bungeni ili ipitishwe sheria hiyo ili iweze kuwasaidia wasanii.
Wakati Rulu Arts wakisaka namna ya kulifanikisha suala hilo hivi karibuni, Mchumi Dk. Aikael Jehovaness alichambua masuala muhimu ya kiuchumi katika sekta ya muziki inayotokana na upungufu wa sheria ya hakimiliki na shiriki ya mwaka 1999 na kutokuwepo utekelezaji wa sheria kikamilifu.
Dk. Jehovaness anasema kwa utafiti wake ndani ya mwaka mmoja ambao ni 2007 pekee, pato la taifa linalotokana na sanaa ya muziki hapa Tanzania ni sh bilioni 71, ikiwa ni karibu asilimia 0.5 ya pato la taifa ambazo zinapotea kutokana na upungufu wa sheria za hakimiliki na shiriki.
Dk. Jehovaness aliweka bayana na suala la ulipaji na upokeaji wa mirabaha, waliolipa ni asilimia 12.50 waliopokea ni asilimia 16.33 wakati ambao hawakulipa ni asilimia 87.50, ambao hawakupokea ni asilimia 83.67, masuala ambayo karibu muda wote wadau hawatambui kupotea kwa mapato ya sanaa.
Alichopendekeza Dk. Aikael, kwa wasanii ili kufikia malengo ni kuzingatia mikataba baina yao na kuzingatia umoja ambao utakuwa na sauti moja na utafikisha kilio chao kwa wizara ili kusajili kazi zao COSOTA na kupendekeza wizara kuharakisha suala hilo ili lifanyiwe kazi bungeni.
Msanii Stara Thomas anasema mara nyingi serikali yetu inafanya kazi kwa unyonge sana hata katika masuala ya msingi, kwa sababu mara nyingi wanapiga kelele lakini hawasikilizwi.
Thomas anasema sababu inayowadidimiza zaidi ni kuwachagua wabunge ambao hawawatetei masuaa yao, jambo linalorudisha nyuma maendeleo yao na kuahidi kutowapigia kura.
Mwanamuziki mkongwe, Kassim Mapil, anasema malalamiko ya wasanii yamekuwa ni mengi lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa kwani tangu mwaka 1911 sheria zilianza kufanya kazi lakini hakuna mabadiliko yoyote.
Mapili anasema lakini pamoja na mabadiliko hayo, hata ile ambayo haijafanyiwa marekebisho wasanii wengine hawaifahamu, bado kuna tatizo kubwa ambalo pia linatakiwa kufanyiwa kazi.
Kikubwa anachopigia kelele mzee Mapili ni kulipwa haki wasanii ambao nyimbo zao zinatumika redioni na kwenye televisheni, jambo ambalo anasema wamelipigia kelele bila ya kufanyiwa kazi ya aina yoyote.
Kuhusu suala hilo kufikishwa bungeni, Mwanasheria wa COSOTA, chama ambacho kiko chini ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, Doreen Anthony, anasema taratibu za mabadiliko ya sheria zinatarajia kufanyiwa kazi baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambako mtendaji wa wizara ambaye ni Katibu Mkuu atalikamilisha baada ya kutoka bungeni.
Anthony anatoa lawama kama alizotoa Mapili ambazo zinawahusu wasanii ambao wengi wao hata ofisi za COSOTA hawajawahi kufika wala hawajui kazi zake, hivyo wana kazi kubwa kwa jamii.


h.sep3.gif

Mwandishi wa makala hii anapatikana kupitia simu 0773508779, barua pepe: makuburia@yahoo.com
 
Assosa umetufaa kwa kitabu cha Lingala
ban.blank.jpg


Abdallah Menssah​

amka2.gif
NIAJE wadau wangu wapendwa wa Kijiwe chetu adhimu cha Burudani, kiwajiacho mara moja tu kwa wiki, tena katika siku iliyotukuka kama ya leo, yaani Ijumaa.
Sina shaka nyote mu wazima kabisa muda huu ambapo mmetulia ama wengine mkiwa mnaendelea na mchakamchaka wa kujitafutia riziki ili mradi tu mkirejea nyumbani familia ziwapokee kwa shangwe.
Mwanakijiweni wenu Jumanne iliyopita nilipewa heshima kubwa na ya kipekee kabisa kama mwandishi mahiri wa siku nyingi katika ukanda huu muhimu mno wa habari za burudani hapa nchini.
Peke yangu nilialikwa kushuhudia namna mwanamuziki nguli, Tshimanga Kalala Assosa alivyofaulu kuandaa kitabu cha kuwawezesha Watanzania wote kujifunza bila taabu lugha ya Lingala.
Kitabu chenyewe kinaitwa ‘JIFUNZE LINGALA', ni toleo la 1 lenye kurasa 56 ambako ndani yake kuna picha pamoja na nyimbo za baadhi ya wakongwe wa muziki nchini Kongo (DRC).
Miongoni mwa picha za wakongwe wa Kongo (DRC) waliomo humo pamoja na vibao vyao ni Franco na Tabuley, Orchestra Veve, Fukafuka, Le Kamalee, Jonie Bokeloo na Sam Mangwana.
Kiukweli, ni kitabu kizuri hasa kutokana na lengo la mwandaaji kuwa ni linaloweza kuingia akilini mwa yeyote mwenye kiu ya kujua zaidi kuhusiana na lugha ya Lingala.
Kwa mujibu wake, Assosaa anasema kuwa, amekiandaa kitabu hiki kwa dhumuni la kuwaondolea taabu watangazaji wa Kitanzania wanaocheza nyimbo za Bolingo bila kujua maana yake.
Aidha, Anasema kuwa kadhalika, kitabu hiki ni muhimu kwa wanamuziki wanaoimba vibao vya Lingala katika mtindo wa ‘Kasuku' pamoja na wanaofanya biashara kati ya hapa nchini na Kongo.
Tayari kitabu hiki kikubwa na kinachovutia hata kukitazama tu, kinapatikana kwa wingi mtaani hivi sasa, ambako kwa atakayekihitaji zaidi, anaweza kuwasiliana na Assosaa kwa simu namba 0713 240 735.
Ninachotaka kukisema hapa ni kuwa, kiukweli Assosaa ametusaidia mno sisi ambao tulikuwa tukihitaji msaada wa aina hii, wa kujifunza Lingala ili tuweze kukabiliana na mazingira ya shughuli zetu.
Kwa sababu, si siri tuko wengi ambao wengine shughuli zetu hazihusiani na Ukongoman, lakini tunapata taabu sana pindi unapopigwa wimbo wa Koffi Olomide redioni, kwani huwa tunacheza ala tu bila kujua kinachoimbwa.
Zaidi ya hilo, nampa moyo wa kuendelea na juhudi zake za kutaka kutufanya tuondokane na ukungu huu wa kiza kizito na kigumu cha kutojua hata kile kinachoimbwa na kina Fally Ipupa.
Sina mengi ya kusema zaidi ya kuwaaga wadau wangu wote na kuwaomba kwa msisitizo kuwa tukutane tena wiki ijayo hapahapa Kijiweni.
Wadau wangu wakuu leo ni Mohammed Mtwale, Taliq Haji Kijungu, Mariam Said, Yahaya Rajab ‘Westi', Super D Mnyamwezi, Ahmed Balozi, Dogo Baraka, Bilsan Hemed, Asha Salum pamoja na Ikota Mhamila.
 
Five Stars waishukuru serikali


na Makuburi Ally


amka2.gif
UONGOZI wa kundi la Five Stars Modern Taarab, la jijini Dar es Salaam, umeishukuru serikali kwa kuwa nao bega kwa bega katika maandalizi ya kulisuka upya kundi hilo, lililowapoteza wanamuziki wake 13 katika ajali ya gari iliyotokea Machi 21, mwaka huu Mikumi, Morogoro.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi, Mwenyekiti wa kundi hilo, Hamis Slim, alisema serikali imekuwa karibu yao katika kuhakikisha kundi hilo linarudi katika hali yake kama ilivyokuwa zamani.
Slim alisema kuwa baada ya kufanya kisomo kitakachofanyika Jumapili hii kuwaombea wanamuziki wao waliofariki dunia na majeruhi, kundi hilo litatoa tamko la mwelekeo wake baada ya kumaliza kuomboleza.
"Tumejipanga kulirudisha kundi letu, baada ya pigo kubwa tulilolipata tunashukuru kwamba hadi sasa serikali imekuwa upande wetu ikitupa sapoti ya hali ya juu ili kuhakikisha kundi linarejea upya," alisema Slim.
 
Kimwana wa Twanga kufunguliwa duka


na Khadija Kalili, Zanzibar


amka2.gif
KAMPUNI ya Manywele kwa kushirikiana na The African Stars Entertainment jana wamezindua rasmi shindano la kumsaka Kimwana wa Twanga 2011.
Mratibu wa shindano hilo, Maimatha Jesse, amesema kwamba baada ya kufanya uzinduzi huo fomu za kushiriki zinapatikana ofisi za Manywele Kinondoni Manyanya, ASET na Steers jijini Dar es Salaam na kila bendi ya Twanga itakapofanya maonyesho.
Maimatha alisema mshindi wa shindano hilo ambalo litatambulishwa Mei 6 mwaka huu kwenye ukumbi wa Club Sunciro Sinza, jijini Dar es Salaam, atapata zawadi ya uhakika kwa kufunguliwa duka la vipodozi lenye thamani ya sh milioni tano.
"Tumeamua kutoa zawadi ambayo itamkwamua mshindi, tofauti na ile tuliyokuwa tukiitoa ya gari, ambayo huwaongezea gharama kama za kununua mafuta na kadhalika," alisema Maimatha.
Aliongeza kuwa katika onyesho hilo la kuwatambulisha washiriki, msanii aliyetia fora kwenye tuzo za mwaka huu za Kili Music Award, 20% atatoa burudani pamoja na bendi ya Twanga Pepeta.
 
ZFA haitaki mabadiliko - Wadau


na Mohamed Said Abdullah, Zanzibar


amka2.gif
BAADA ya kumalizika kwa mchakato wa uchukuaji wa fomu za kuwania nafasi ya urais na nafasi mbili za Makamu wa Rais wa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), wadau mbalimbali wametoa maoni yao na kuelezea sababu za kutojitokeza wagombea wapya katika kinyang'anyiro hicho.
Miongoni mwa wadau waliotoa maoni yao ni mwandishi mwandamizi wa kituo cha televisheni cha Channel Ten visiwani Zanzibar, Munir Zakaria, ambaye alisema kuwa hiyo ni ishara ya kuhofia kupoteza fedha na muda wao, kwa vile viongozi wa ZFA wana kila mbinu za kuwawezesha kuendelea kubakia madarakani.
Zakaria ambaye katika uchaguzi uliobatilishwa matokeo alipata kura mbili, alisema ameamua kutoingia katika uchaguzi huo kwa vile ni vigumu kushinda, hasa kwa kuzingatia kuwa wajumbe wa mkutano mkuu wamejengewa dhana kuwa ZFA ni hakimiliki ya viongozi fulani na haiwezi kuongozwa na watu wengine.
Kutokana na hali hiyo, Zakaria ameishauri kamati ya uchaguzi ya ZFA kuwaidhinisha wagombea waliochukua fomu kwa vile hawana wapinzani ili kuokoa fedha zitakazotumika kugharamia uchaguzi huo uliopangwa kufanyika Aprili 30, kisiwani Pemba.
Alisema ni vyema fedha zilizotengwa kugharamia uchaguzi huo, zikatumika kuwapeleka viongozi wote wa ZFA pamoja na wajumbe wa Mkutano Mkuu kwa mzee Ambilikile Mwasapila ili wakape kikombe cha dawa ambacho kinaweza kuwasaidia katika kurejesha imani za wadau wa soka waliokata tamaa kutokana na kuanguka kwa kiwango cha soka na kukosekana kwa hamasa miongoni mwa wanamichezo.
 
Simba waaswa kuwa watulivu


na Juma Kasesa


amka2.gif
MWENYEKITI wa matawi ya Simba Wilaya ya Kinondoni, Martin Kumaliga, amewataka wanachama wa klabu hiyo kuwa watulivu na badala yake waelekeze nguvu katika zoezi la usajili kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara na mashindano ya kimataifa.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Martin ambaye pia ni mlezi wa tawi la Simba, la Ubungo Terminal, ‘Wekundu wa Terminal mwanzo mwisho' alisema wanachama wa klabu hiyo wanapaswa kuwa watulivu na kukubaliana na matokeo ya Simba kupokonywa ubingwa na watani zake wa jadi, Yanga.
Alisema huu si wakati wa kusaka mchawi aliyesababisha timu hiyo kupoteza ubingwa badala yake wanachama wanapaswa kushirikiana na uongozi katika zoezi la usajili linalotarajiwa kuanza hivi karibuni ili kujiimarisha na msimu ujao wa ligi hiyo na mashindano ya kimataifa.
"Tusisake mchawi, kimsingi tumeshapoteza ubingwa, tunapaswa kujitazama pale tulipoangukia ili tunyanyuke na kuanza safari yetu upya," alisema Kumaliga.
Akizungumzia uzinduzi wa tawi la Ubungo Terminal, Kumaliga, alisema wanatarajia kukutana Jumapili kujadili ushiriki wa timu yao katika Ligi Kuu Tanzania Bara iliyomalizika hivi karibuni na mipango ya kuelekea uzinduzi wa tawi hilo ambao wamepanga ufanyike mwisho wa mwezi huu.
Aidha, Kumaliga alisema mipango ya uzinduzi huo inakwenda vyema na tayari wameshapata wanachama 100 kwa ajili ya kusaidiana na uongozi wa Simba.
 
Mikoa yathibitisha ‘Cycling Tour of Tanzania'


na Makuburi Ally


amka2.gif
MIKOA saba imethibitisha kushiriki mbio maalumu za kilomita 800 zitakazojulikana kama ‘Cycling Tour of Tanzania' zitakazopita mikoa tisa hapa nchini kuanzia Julai 17-24, mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Chama cha Baiskeli Tanzania (CHABATA), Lado Haule, alisema mashindano hayo ni makubaliano kati ya chama chake na SPORPUB ya Burkina Faso ambapo mwisho wa kuthibitisha ilikuwa Aprili 10.
Haule alisema mashindano hayo yatachezwa kwa hatua, yatashirikisha timu saba zenye wachezaji 10 kila moja.
Katibu huyo aliitaja mikoa hiyo ni Dodoma, Arusha, Mwanza, Shinyanga, Dar es Salaam, Zanzibar na timu ya taifa.
Haule alisema mashindano hayo yatagharimu sh milioni 150, ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika Tanzania hivyo inahitajika wachezaji kuwa wavumilivu.
Alitaja njia ambazo mbio hizo zitafanyika ni pamoja na Bagamoyo, Dar es Salaam, Mlandizi, Morogoro, Dodoma, Shinyanga, Mwanza, Bunda, Serengeti, Karatu, Arusha, Segera, Chalinze hadi Dar es Salaam.
 
Julio:Tusiwape sifa sana watalewa Send to a friend Thursday, 14 April 2011 20:55

u23%20bendera.jpg
WACHEZAJI wa timu ya taifa ya vijana [U-23] baada ya kukabidhiwa bendera ya taifa mkurugenzi wa baraza la michezo Tanzania Idd Kipingu tayari kwa safari ya mechi yao ya Kimataifa dhidi ya timu ya taifa ya Uganda 'The Cranes' itakayochezwa kesho Jumamosi, Picha na Doris Maliyaga.

Kalunde Jamal
TIMU ya vijana chini ya miaka 23 imeondoka jana kwenda Uganda tayari kwa mchezo wake wa kwanza wa kuasaka kufuzu kwa Michezo ya Afrika 2011Maputo, huku kocha wake Jamhuri Kihwelo akiwataka Watanzania wasiipe kichwa timu hiyo kwa sasa ila wategemee mazuri zaidi.

Julio alisema kuwa wao wanaenda kushindana na Watanzania wategemee mazuri zaidi kutoka katika timu hiyo ila wasiwape sifa sana wachezaji hao wakajiona ndio wenyewe na kuharibu malengo yake.

''Matumaini yangu ni kucheza michuano hiyo mikubwa hapa Afrika na kuweka historia, ila ninachowaomba Watanzania kuendelea kuiunga mkono timu yao, lakini sifa kwa sasa hazitakiwi sana kwa kuwa bado kuna safari ndefu,'' alisema Julio.

Akikabidhi bendera kwa timu hiyo, Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT) Idd Kipingu aliwataka vijana hao kujiamini na kujenga fikra kuwa wanaweza kwa sababu hakuna tofauti katika wachezaji bali ni katika vitendo.

Alisema huu ni wakati wa timu hiyo kuweka malengo ya kufanya vizuri kwa kuwa uwezo wanao tena mkubwa sana kama wote wakiungana kwa pamoja.

''Yale mlioyafanya kwa Cameroon mkayafanya mara tano mkiwa Uganda mimi nimemsifu sana mchezaji Juma Abdi jinsi alivyohamasisha wakati anaenda kupiga penati katika mchezo wao na Cameroon huo ndio uchezaji unaotakiwa,'' alisema Kipingu.

Naye Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) Leodegar Tenga aliwataka vijana hao waendelee kuwatoa kimasomaso Watanzania na waende huko kupambana kabla ya mechi na baada ya mechi.

Kwa upande wake mkuu wa msafara Hafidhi Ally mjumbe wa kamati ya utendaji ya (TFF), aliwataka Watanzania kuwa na matumaini na jeshi lake kwani uwezo wa kufanya hivyo wanao na hali ya kufanya hivyo wanayo hasa baada ya matokeo ya juzi dhidi ya Cameroon ila amewataka watanzania wawaombee dua.

Nahodha wa timu hiyo Shabani Kado alisema kuwa watanzania wategemee maajabu kutoka kwa timu hiyo baada ya kuwatoa wacameroon wameamua kuelekeza macho katika michuano hiyo kwani ushindi ni lazima kwa hali na mali.
 
Comments




0 #4 majabaka 2011-04-15 13:42 kila la heri vijana wetu.
kila mtu awajibike na sio kufikiria fulani ndio atafanya.
KULENI NA KUNYWA KWA KIASI,SHIBE NI MBAYA!
Quote









0 #3 Emmanuel 2011-04-15 11:48 kilalakheri mtuwakilishe vyema huko uganda.
Quote









0 #2 Ruga 2011-04-15 10:24 tupo pamoja
Quote









0 #1 Asante Mungu 2011-04-15 10:01 Kila la kheri ngongoro stars
Quote







Refresh comments list
 
Kaseba, Maugo kupambana Jumamosi

Imeandikwa na Na Evance Ng'ingo; Tarehe: 15th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 22; Jumla ya maoni: 0





BONDIA Japhet Kaseba na Mada Maugo Jumamosi hii wanapambana katika ukumbi wa PTA uliopo viwanja vya Sabasaba, Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Ijumaa katika Ukumbi wa Idara habari, Maelezo, promota wa pambano hilo Yassin Abdallah, alisema maandalizi ya pambano hilo yamekamilika.

Alisema mapambano ya utangulizi itakuwa kati ya Yohana Robert na Said Zungu, Fadhil
Awadh na Bakari Dunda, Joseph Martin na George Dimoso, Hassan Mandula na Uwesu Said.

Aliyataja mapambano mengine kuwa ni Mohamed Matumla atakayezipiga na Sadiki Momba,
Deo Njiku na Issa Sewa na Ubwa Salum na Mussa Sunga.

Aliwahakikishia wapenzi wa mchezo wa ngumi kuwa pambano hilo litafanyika katika mazingira
salama na litafanikiwa.
 
Vijana Stars vitani tena


*Waondoka na matumaini kibao

Na Addolph Bruno

TIMU ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 23 'Vijana Stars', imeondoka jana mchana kwenda Uganda ambapo kesho itacheza na Uganda katika
mechi ya kuwania kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika. Mechi itachezwa kwenye Uwanja wa Mandela (Namboole).

Vijana Stars imeondoka ikiwa na msafara wa wachezaji 21 na viongozi wanane ukiongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA), Hafidhi Ali Tahir pamoja na makocha Jamhuri Kihwelu 'Julio' na msaidizi wake Adolph Rishard.

Akizungumza kabla ya kuwakabidhi bendera Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la taifa (BMT), Kanali Mstaafu Idd Kipingu aliwataka wachezaji wa timu hiyo kucheza kwa bidii kama walivyofanya Jumamosi iliyopita ambayo iliwafunga Cameroon katika mchezo wa marudiano kwa mabao 4-3 kuitupa nje ya michuano ya kusaka tiketi ya kucheza michuano ya Olimpiki mwakani.

Kipingu ambaye aliwasifu wachezaji hao kwa juhudi walizozionesha walipoumana na Cameroon, alisema wanatakiwa kutambua kuwa hawana tofauti na Uganda na timu nyingine yoyote jambo ambalo ni silaha kubwa kwa timu zinazoshinda.

"Hatuna wasiwasi pia na benchi la ufundi linaloongozwa na kocha Julio, hongera sana kocha, lakini nawaombeni mzidishe bidii katika kufanya mamuzi, hiyo ndiyo silaha kubwa wanayoitumia wenzetu ongezeni bidii ni wakati wenu huu.

"Juzi mlipocheza na Cameroon mlionesha kweli mna nia, Watanzania wote tunaamini mtashinda na Uganda ni wenzetu tumewazoea na kama mkiondoka hapa na nia, mtashinda tu kwa sababu lengo ni kuwa bingwa na dawa ya kuwa bingwa ni kucheza na hata hao Nigeria tuliopangwa nao tutawashinda tu," alisema Kipingu.

Naye Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga aliwataka wachezaji hao kujiamini kabla na baada ya mchezo ili kuendeleza mafanikio mazuri ya juzi, baada ya Cameroon na kuongeza kuwa ushindi uliopatikana ni wa kihistoria.

Kwa upande wake, Julio alisema hana wasiwasi na vijana wake kutokana na mazoezi ya kujenga stamina na mengine waliyofanya na kuwaomba Watanzania, kutulia na kuacha kuwasifia kwa sasa mpaka watakapomaliza kazi waliyowatuma.

Akizungumzia mchezo huo wa kesho, nahodha wa timu hiyo, Shaaban Kado alisema hawana wasiwasi nao na kuahidi ushindi kutokana na kwamba wanaelewa wanachokifanya na kuongeza kwamba wameamua kuwafurahisha Watanzania.

Timu hiyo itacheza mechi ya marudiano na wapinzani wao Aprili 30, mwaka huu Jijini Dar es Salaam na ikiwa itashinda mechi hizo itacheza na mshindi kati ya Kenya na Eritrea ambapo fainali zitafanyika Maputo nchini Msumbiji Septemba 3 hadi 18 mwaka huu.
 
1 Maoni:

blank.gif

Anonymous said... Nikweli wachezaji wanatakiwa kucheza kwa bidii ili ushindi upatikane na sio kuingia uwanjani na dharau pamoja na mawazo yakuwa walishaifunga Cameroon kwa hiyo Uganda si chochote.Yoyote yule anayekuja mbele yako unatakiwa kupigana nae kwa nguvu zote bila ya dharau.Hii ni tahadhari natoa kwani wachezaji wa nyumbani walishazoea kutoa visingizio baada ya kufungwa kuwa wenzao waliwakamia sana kwa sababu walishaifunga Cameroon.Wanatakiwa kuingia uwanjani kwa ari kubwa na ikiwezekana washinde kwa ushindi mkubwa tu ili kuonyesha ya kuwa wao ni wazuri kwa kuingia vitani bila ya dharau na kupata ushindi mnono.
April 15, 2011 12:40 PM

Post a Comment
 
BTL yajitoa NSSF Cup


Na Mwandishi Wetu

TIMU za Business Times Limited (BTL) zimejitoa kwenye michuano ya vyombo vya habari ili kulinda heshima ya waandaaji na wadhamini NSSF.BTL ilitakiwa kucheza
kesho kutafuta mshindi wa tatu katika mpira wa miguu na netiboli kwenye viwanja vya Sigara, Dar es Salaam.

Kwa uamuzi huo, timu ya soka ya Uhuru itakuwa mshindi wa tatu na TBC itashika nafasi hiyo katika mchezo wa netiboli.

"Tunaiheshimu taasisi ya NSSF na uongozi wake kwa hiyo tusingependa uhusiano wetu mzuri uharibiwe na mtu au watu wachache wenye maslahi binafsi," alisema Meneja wa timu za BTL, Masoud Sanani.

Alisema Business Times inaamini kuwa NSSF ilianzisha michuano hiyo ikiwa na malengo mazuri na daima itakuwa inaamini hivyo hasa kwa kuelewa busara za Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dkt. Ramadhan Dau.

Lakini, Sanani akasema BTL imefikia hatua ya kuziondoa timu zake kutokana na kitendo cha kudhihirika bila shaka yoyote kuwa timu ya NSSF, ilichezesha wachezaji mamluki katika mechi ya nusu fainali ya soka iliyochezwa Aprili 12.

Kamati ya Mashindano ya michezo hiyo iliipiga faini ya sh. 500,000 NSSF kwa kosa hilo, jambo ambalo BTL imelipinga ikitaka Kanuni ya 5 za mashindano hayo inayohusu Taratibu za Mchezo namba 14 itumike au vyote kwa pamoja kutokana na ukubwa wa kosa.

Kamishna wa mchezo huo, Mohamed Mharizo wa New Habari alieleza kwenye kikao cha Kamati ya Mashindano jinsi ambavyo timu ya NSSF, ilivyofanya ujanja wa kumtoa mchezaji mamluki na kumwingiza mwingine bila kupitia kwa mwamuzi wa akiba.

Wachezaji wote wawili walitumia namba 16 kwa lengo la kutaka kuficha udanganyifu uliofanywa na timu ya NSSF, baada ya kupata fununu kuwa BTL imegundua.
 
Madina kibaruani Kenya Open

Imeandikwa na Na Mwandishi Wetu; Tarehe: 15th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 16; Jumla ya maoni: 0








MCHEZAJI gofu nyota wa timu ya taifa ya wanawake, Madina Iddi, leo anatupa karata yake kwenye michuano ya Wanawake ya Kenya Open.

Michuano hiyo ya viwanja 36 imepangwa kufanyika kwenye viwanja vya Klabu ya Sigona, Nairobi, Kenya.

Akizungumza na HABARILEO Dar es Salaam Ijumaa, Katibu wa Chama cha Gofu cha Wanawake Tanzania (TLGU), Anita Siwale, alisema Madina aliondoka nchini juzi tayari kwa michuano hiyo ya kila mwaka.

"Madina ni mchezaji pekee ambaye atatuwakilisha Kenya Open, tunaamini amefanya
mazoezi ya kutosha na atafanya vizuri kwenye michuano hiyo," alisema.

Siwale alisema awali walitarajia kupeleka angalau wachezaji wawili wa timu ya taifa akiwepo Hawa Wanyeche, lakini nahodha huyo wa timu ya taifa kwa sasa amebanwa na majukumu mengine ya shule.

Akizungumza kutoka Nairobi Ijumaa, Madina ambaye alikuwa mmoja wa wachezaji walioweka historia kwa Tanzania kushika nafasi ya pili kwenye michuano ya Afrika iliyofanyika Abuja, Nigeria mwaka 2010, alisema amefika salama na yupo tayari kwa mpambano.

"Nimefika salama na kupata muda wa mazoezi, natumaini nitakuwa na mashindano mazuri Mungu akinisaidia," alisema.

Siwale aliwashukuru wadau wa gofu Michael Shirima, Beatus Kasegenya na nahodha wa gofu Arusha, Richard Gomes kuitikia wito wa TLGU na kuwezesha Madina kushiriki michuano hiyo.

Alisema ushiriki wake utamsaidia kuendelea kujijenga kimchezo na kujiamini zaidi.
 
Mambo yaiva Tamasha la Pasaka

Imeandikwa na Na Mwandishi Wetu; Tarehe: 15th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 25; Jumla ya maoni: 0








KAMATI ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka imesema maandalizi muhimu kuhusiana na tamasha hilo yamekamilika.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Alex Msama alisema kuwa karibu vitu vyote muhimu
kuhusiana na tamasha lao tayari wamevikamilisha na wanachosubiri ni siku yenyewe.

"Nimesema mara nyingi kwamba tamasha la mwaka huu tunataka liwe bora kuliko mengine,
kwamba haijawahi kutokea. "Wasanii mbalimbali wameanza kuingia nchini kwa ajili ya tamasha hilo, mazoezi yanaendelea kwa wale waimbaji wa hapa nchini, hivyo mambo ni mazuri," alisema
Msama.

Tamasha la Pasaka limepangwa kufanyika Dar es Salaam Aprili 24 mwaka huu ukumbi wa
Diamond Jubilee na siku inayofuata Uwanja wa Jamhuri Dodoma na Aprili 26 Uwanja wa CCM
Kirumba, Mwanza.

Kiingilio katika tamasha hilo kwa Dar es Salaam ni Sh 4,000 kwa viti vya kawaida, viti
maalumu B Sh 10,000 na viti maalumu A Sh 20,000, ambapo kwa mikoani ni Sh 3,000.
 
Samatta atua Mazembe kwa mil.250/-

Imeandikwa na Na Mwandishi Wetu; Tarehe: 15th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 305; Jumla ya maoni: 0








KLABU Simba imekubali kumuuza mshambuliaji mahiri chipukizi Mbwana Samatta kwa klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kwa ada ya uhamisho ya dola za Marekani 150,000 sawa na shilingi za Tanzania milioni 225.

Makubaliano baina ya klabu hizo mbili yalifikiwa Alhamisi usiku jijini Dar es Salaam, baada ya maofisa wa klabu ya Simba na wawakilishi wa TP Mazembe kukutana.

Habari zilizopatikana ndani ya Simba na kuthibitishwa na Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Rage zilieleza kuwa katika kiasi hicho kitakachotolewa na Mazembe Simba, itapata dola za Marekani 100,000 sawa na shilingi milioni 150 za Tanzania, wakati Samatta atapata dola za Marekani 50,000 sawa na milioni 75 kama ada ya uhamisho.

"Simba na Mazembe wamefikia makubaliano ya kiungwana kuhusiana na uhamisho wa Samatta," kilisema chanzo hicho cha habari.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, mkataba baina ya mchezaji huyo na TP Mazembe unatarajiwa kusainiwa wiki ijayo mjini Lubumbashi, baada ya Samatta kumaliza kibarua cha kuichezea timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 23 ‘Vijana Stars' ambayo ipo Uganda na kisha mchezo wa timu ya soka ya Taifa ‘Taifa Stars' na Msumbiji utakaofanyika mwishoni mwa wiki ijayo mjini Maputo, Msumbiji.

Chini ya makubaliano hayo Mazembe itamlipa Samatta dola za Marekani 5,000 sawa na Sh milioni 7.5 kwa mwezi ukiwa ni mshahara kwa kipindi cha mkataba wa miaka mitatu atakayokuwa na klabu hiyo yenye makao makuu mjini Lubumbashi.

Malipo hayo ni mbali ya marupurupu mengine ambayo atapatiwa ambayo yanaweza kufikia kiasi cha shilingi milioni 90 kwa mwaka.

Akizungumza kuhusiana na suala hilo jana, Rage alikiri Simba kumalizana na TP Mazembe na kwamba fedha hizo hakuna timu ambayo ingeweza kuziacha.

"Ni kweli Mazembe wamekuja na kama ulivyosema tumemalizana nao wametupa dola za Marekani 100,000, kisha Samatta mwenyewe wamempa dola za Marekani 50,000.

"Sitaki kusema mshahara atalipwa kiasi gani kwa mwezi, lakini nieleze ni mkubwa kuliko mchezaji mwingine yeyote wa Tanzania anayecheza nje ama anayecheza hapa nchini.

"Tunamtakia kila la heri katika safari yake ya mpira, naamini ni mwanzo mzuri kwa wachezaji wetu, kuelekea katika mafanikio ya kimpira na kimaisha," alisema Rage.

Kusajiliwa kwa Samatta kumekuja wiki mbili tangu Simba ilipotolewa katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika kwa kufungwa jumla ya mabao 6-3 na TP Mazembe.

Mchezo wa kwanza uliofanyika mjini Lubumbashi, DRC, Simba ilifungwa mabao 3-1 na ziliporudiana Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, Simba ilifungwa mabao 3-2, huku bao moja la Simba likifungwa na Samatta ambaye aling'ara kwenye mchezo huo.

Wakati huohuo, kiungo wa Simba, Patrick Ochan naye anatarajiwa kwenda Lubumbashi kufanya majaribio ya kuchezea TP Mazembe.

Kwa mujibu wa Rage ni kuwa wamepokea maombi hayo na hawana tatizo na mchezaji huyo raia wa Uganda kwenda kufanya majaribio kwenye timu hiyo
 
Twiga yafuzu Afrika, Vijana vitani Jumamosi

Imeandikwa na Na Betram Lengama; Tarehe: 15th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 65; Jumla ya maoni: 0








TIMU ya soka ya Taifa ya wanawake ya Tanzania ‘Twiga Stars' imefuzu fainali za michezo ya Afrika baada ya Sudan kujitoa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam Ijumaa, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah alisema Twiga Stars ilikuwa icheze na Sudan Aprili 30 mwaka huu.

Alisema kujitoa kwa timu hiyo kumeipa fursa Twiga Stars kuingia kiurahisi katika fainali hizo, ambapo hii ni mara ya pili kujikuta ikikwepwa na timu iliyopangwa nayo ambapo awali ilikuwa icheze na Kenya ambayo nayo ilijitoa.

Alisema Twiga Stars walikuwa wakiendelea vema na mazoezi kwa ajili ya mchezo huo, ambapo kama Stars ingeshinda ingekata tiketi kushiriki fainali hizo zitakazofanyika nchini Msumbiji kuanzia Septemba 3 hadi 18 mwaka huu.

Wakati huo huo, timu ya soka ya Taifa ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 23 ‘Vijana Stars' Jumamosi hii itashuka uwanjani nchini Uganda kucheza na timu ya vijana ya huko kuwania kufuzu michezo ya Afrika, ambayo Twiga Stars tayari imefuzu.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura aliyepo na timu hiyo nchini Uganda, wachezaji wote wapo kwenye hali nzuri kimchezo.

"U-23 chini ya Kocha Jamhuri Kihwelo ‘Julio' iliwasili na wachezaji 20; Nahodha Shaaban Kado, Juma Abdul, David Luhende, Babu Ally, Shomari Kapombe, Jabir Aziz, Salum Abubakar, Thomas Ulimwengu, Mbwana Samata, Kigi Makasi, Gharib Mussa, Mbwana Bakari, Idrisa Abdulrahim, Innocent Wambura, Khamis Mcha, Amour Suleiman, Himid Mao, Mrisho Ngasa na Salum Telela," alisema Wambura.



Alisema timu hiyo ilitarajia kufanya mazoezi Ijumaa katika uwanja wa Mandela (Namboole) kwa mechi ya leo na Uganda 23 (The Kobs) inayofundishwa na kocha wa zamani wa Kagera 
Sugar, George Ssemogerere.


Wambura alisema mchezo huo utafanyika Uwanja wa Mandela ambao utatumika kwa mara ya kwanza, kwani kwa kipindi cha miezi sita iliyopita haukutumika kutokana na kuwa kwenye ukarabati.

Kocha Julio alisema wachezaji wake wote wako katika hali nzuri kwa ajili ya mechi ya kesho.
"Tuko vizuri, tumekuja kupambana.

Tunajua Uganda ni timu nzuri, lakini tumejipanga kwa ajili ya kupata ushindi ili kujiweka katika mazingira 
mazuri kwa mechi ya marudiano itakayofanyika nyumbani,"alisema Julio.


Kikosi cha Kobs kina baadhi ya wachezaji wanaocheza soka nje ya Uganda kama Emmanuel Okwi (Tanzania) na Moses Oloya (Vietnam).

Wengine ni Benjamin Ochan, Ayoub Kisarita, Godfrey Walusimbi, Owen Kasule, Patrick Edema, Ivan Bukenya, Sadam Mussa, Mike Mutyaba, Isaac Isinde na Diego Kiiza.

 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom