Mheshimu Kila Mtu Ambaye Anafanya Kazi Ya Kumuingizia Kipata Hata Kama Kazi Hiyo Inaonekana Ni Dhalili Machoni Mwako

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Aug 6, 2020
6,497
15,210
Screenshot_20241213_105644_Google.jpg


Hakuna jambo jema kama kufanya kazi ya halali hapa duniani na haijalishi iwe na hadhi gani, bali kikubwa ni halali na inakidhi mahitaji yako hata kwa kiasi fulani

Na kamwe usijisikie mnyonge kwa hiyo kazi ambayo unayo sasa kwani ndio kazi yako,endelea kupambana mpaka pale utakapo fikia katika level nyingine ya maisha

Kumekuwa na kasumba ya baadhi yetu kubeza kazi au shughuli za watu wengine kwakuwa tu tupo katika ofisi fulani fulani ambazo ni mashuhuli,tambua kwamba wote hatuwezi kuwa katika level moja ya maisha,kwahiyo tambua na heshimu kazi na shughuli za watu wengine pia

Nakumbuka wakati naenda kujiunga na masomo ya elimu ya juu,baba yangu alinipa ushauri mzuri sana,alisema Mwanangu huko unakoenda muheshimu kila mtu hata wale wanao fanya usafi vyooni kwani hakika bila wao hamtakuwa na mazingira mazuri ya kuishi

Niliyakumbuka hayo maneno vizuri sana,na kwa hakika nilikuwa nawaheshimu sana na kuwapenda sana,na niliona furaha zao kila mara nilipo wasalimia kwa upendo na tabasamu kubwa,maana imezoeleka mtu akijiona msomi basi kwake yeye watunza bustani na wafanya usafi si chochote kwake

Na huu ndio mtazamo wa wengi wetu,tumejawa na dharau na viburi kwa wale ambao wanafanya kazi ambazo hazina hadhi kubwa,tambua kwamba ewe boss bila mfanya usafi ofisini kwako hiyo ofisi haitakalika

Ewe mwananchi tambua kwamba bila wafanya usafi katika vituo vya mabasi na daladala hizo stand zitakuwa ni majalala,tujenge tabia za kuheshimu kazi za watu kwani hakika zina umuhimu mkubwa sana,ni kwa vile tu tunazichukulia for granted.

Kazi yangu ya hadhi ya chini haibadilishi utu wangu na ubinadamu wangu,bado nabakia binadamu mwenye utashi na utu wangu pia, tuheshimu kazi ya mtu haijalishi ina hadhi ndogo kiasi gani

Ijumaa Mubarak

Ni hayo tu!
 
Kuna watu kazi yetu kulizisha mishangazi lakini jamii inatuchukulia kama vijana wa hovyo...

Sasa mtu kama mimi mnataka nikabeti kweli... Yaani mimi niwe kama Wagumu Tunadumu kila siku kubeti na kushawishiu watu code za elufu tano na million.

Naheshimu kila kazi mkuu ila sio kazi ya kubeti...
Kuna watu wanadharau kazi ya care for shangazi... Sasa huu ujumbe uwafikie kuwa kukaa na mishangazi ni ajira na ni halali....
 
Back
Top Bottom