Mfanyabiashara hatokueleza wapi anapata faida, kamwe usije kuomba ushauri ukadhani atafunguka 100%

Kila kitu ni gharama ,ukisema siri kila kitu watu wangezijuaje hizo siri na kufanya biashara?

Kuna biashara zinajulikana ,ukifanya ni kujiongeza kidogo tu

Pia biashara unaweza ajiri watu wakakupa code.

Kwa uzoefu wangu watu wenye uwezo wanatumia pesa mingi sana kujifunza biashara mpya
 
Wewe unavonunua Landrover mbovu na kuzimantain na kwenda kuziongeza chassis zinakua za Utalii hua unaeleza pesa unayopiga? Mbona landcruiser ulileta ikachukuliwa tunduma haukusema zaidi ya sadec ushuru umepanda ? Mwalafyale imbombo ngafu
Mwanafyale njoo SA ununue hayo Mazaga zaga ya kutosha yaani niache kuja na vitu vya maana ninunue Land rover mbovu aisee..
 
Sasa unaongezaje mpinzani haliyakuwa anaekuuliza yupo mwanza wewe upo dar hususani humu mitandaoni
Ukiwa mbali utapata general info's na siyo code halisi.

Mfano kama unauza samaki mbeya, na mm nipo dar nikikuuliza kuhusu biashara ya Samaki utaniambia nini zaidi ya bla bla ambazo ni gen info?

Ila nikija mbeya nkataka kujua unavyofanya hiyo biashara, unatoa wapi, unapelekea wapi, kwa nani, ananunuaje kwako n.k lazima utaninyima baadhi ya info hata kama naenda kuifanya hiyo biashara dar.
 
Ukiwa mbali utapata general info's na siyo code halisi.

Mfano kama unauza samaki mbeya, na mm nipo dar nikikuuliza kuhusu biashara ya Samaki utaniambia nini zaidi ya bla bla ambazo ni gen info?

Ila nikija mbeya nkataka kujua unavyofanya hiyo biashara, unatoa wapi, unapelekea wapi, kwa nani, ananunuaje kwako n.k lazima utaninyima baadhi ya info hata kama naenda kuifanya hiyo biashara dar.
Hivi ndio biashara ilivo hatutoi code kabisa , zaidi nakupa issue za juu juu basi utajiona umefahamu kumbe kwenye Asilimia 100 nimekupa 10 Tu hasa jaribu kivyako uone utavichezea hasara ndio utajua pesa ni siri
 
Huu ni ukweli ambao wakurupukaji kwenye biashara hawaujui
Tatizo ni ukiwa na mtaji akili haitulii, unadhani mambo mepesi.

Siri za Biashara ni mali na zinarithishwa.
Kama umetoka kwenye familia ya mkulima ukataka kufanya biashara una option mbili tu:

1. Uingie Front mwenyewe ujifunze kwa makosa.(Hapa uwe na mtaji maana lazima utapoteza pesa)

2. Ukubali kuwa mnyonge, hata kama una mtaji tafuta kazi kwanza inayohusiana na hiyo biashara. Mfano kama ni kuuza mbao kubali kuwa kijana wa muuza mbao, utumwe tumwe hata mwaka mzima au miaka miwili.
 
Hivi ndio biashara ilivo hatutoi code kabisa , zaidi nakupa issue za juu juu basi utajiona umefahamu kumbe kwenye Asilimia 100 nimekupa 10 Tu hasa jaribu kivyako uone utavichezea hasara ndio utajua pesa ni siri
Ni kweli mkuu, ila pia codes hazifanyi kazi sawasawa kwa kila mtu so wakati mwingine kama mtaji unaruhusu kujifunza we zama utajulia huko huko ila uwe na mtaji sababu elimu ya biashara kwa vitendo ni gharama na ada unailipia kwa kupoteza mtaji.
 
Ukiwa mbali utapata general info's na siyo code halisi.

Mfano kama unauza samaki mbeya, na mm nipo dar nikikuuliza kuhusu biashara ya Samaki utaniambia nini zaidi ya bla bla ambazo ni gen info?

Ila nikija mbeya nkataka kujua unavyofanya hiyo biashara, unatoa wapi, unapelekea wapi, kwa nani, ananunuaje kwako n.k lazima utaninyima baadhi ya info hata kama naenda kuifanya hiyo biashara dar
Wabongo ndio tulivyo imagine hata mshahara mtu anaficha wakati viwango vinajulikana
 
Tatizo ni ukiwa na mtaji akili haitulii, unadhani mambo mepesi.

Biashara ni mali na inarithishwa.
Kama umetoka kwenye familia ya mkulima ukataka kufanya biashara una option mbili tu:

1. Uingie Front mwenyewe ujifunze kwa makosa.(Hapa uwe na mtaji maana lazima utapoteza pesa)

2. Ukubali kuwa mnyonge, hata kama una mtaji tafuta kazi kwanza inayohusiana na hiyo biashara. Mfano kama ni kuuza mbao kubali kuwa kijana wa muuza mbao, utumwe tumwe hata mwaka mzima au miaka miwili.
Mimi niache kuwarithisha biashara wanangu wa kuwazaa eti nikupe michongo wewe hiyo haipo tutapiga story but kufungua direct code never ever
 
Wabongo ndio tulivyo imagine hata mshahara mtu anaficha wakati viwango vinajulikana
Mkuu sio wabongo, hata wewe mshahara wako kama unao huwezi uweka hadharani kwa kila mtu hovyo hovyo. Halafu info za biashara ni mali kama mali nyingine mkuu, unampa yule aliyekugusa huitoi tu. Hata wewe nina uhakika upo hivyo. Si kila anayekufata utampa siri za namna unavyotengeneza pesa.
 
Mimi niache kuwarithisha biashara wanangu wa kuwazaa eti nikupe michongo wewe hiyo haipo tutapiga story but kufungia direct code never ever
Ofcourse nakuelewa. Halafu mpaka unaona biashara imesimama imara ujue safari mara nyingi ilikuwa ndefu mno. Wahindi wapo vizuri kwenye kurithishana biashara tofauti na sisi, sisi huwa tunajisahau tukifa na biashara inakufa.
 
Kuna lijamaa nilikuwa nasoma nalo hata matokeo linaficha hii tabia wengi tumerithi kizazi na kizazi haiwezi koma

Kwenye biashara ndio kabisa code zinachimbiwa ukutani
Wala usilaumu kabisa mtu kaandaa mfumo wake wa pesa kwa maumivu wewe uje uokote bure haipo hiyo mfikie hatua mfahamu hili ni mtu kulinda empire yake na wanaonihusu na hapo kuna DM nzinamiminika huko unawacheck tu
 
Mkuu sio wabongo, hata wewe mshahara wako kama unao huwezi uweka hadharani kwa kila mtu hovyo hovyo. Halafu info za biashara ni mali kama mali nyingine mkuu, unampa yule aliyekugusa huitoi tu. Hata wewe nina uhakika upo hivyo. Si kila anayekufata utampa siri za namna unavyotengeneza pesa.
Namimi ni mbongo mkuu nimerithi tabia hiyo japo sio kwa kiwango kikubwa

Kuna watu mpo karibu sana na hawafungui code mfano mke na mume au baba na mtoto
 
Back
Top Bottom