Mfano Uwanja wa Uhuru usipojaa Simba Day, tumeshaandaa cha Kuwajibu ambao Watatucheka na Kutucharura kwa Misifa yetu ya Kijinga?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
57,115
110,509
Yaani Timu iliyobeba Ubingwa na kufika Fainali ya CAFCC katika Siku yao ya Wananchi pamoja na baadae Kuruhusu Fungulia Ng'ang'a ( Mbwa ) Uwanja wa Mkapa haukujaa na hata kule Shamba la Bibi ( Uhuru Stadium ) haukujaa.

Halafu leo anatokea Pimbi Mmoja ( tena ametumika sana Kutuumiza Simba SC ) kwa Matokeo na anajua kabisa kuwa kwa miaka ( misimu ) Miwili mfululizo Klabu ya Simba SC haijawa Bingwa anatuaminisha kuwa Simba Day ya tarehe 6 August, 2023 kws Mkapa patafurika hadi Pomoni na Wengine watamwagwa / watatupwa Uwanja wa Uhuru ambako kutaweka Screen Kubwa ili washuhudie Tamasha na Mechi Usiku huku Mbu wakali wa Miti ya Kambi ya Jeshi ya Twalipo wakiwauma na Kuwavimbisha Pua na Midomo.

Timu mpaka sasa Haina Kipa namba moja halafu mnataka Watu wajae na Kujipa Moyo kuwa hata na ule Uwanja wa Uhuru utajaa na mnaomba mpewe.

Mkiambiwa hamna Akili mnanuna.
 
Huu ndo ushindi wa Simba, kelele nyingii mno saiv ligi likianza wanapotea na kutoa lawama kedekede.
 
Back
Top Bottom