Mfahamu vyema mnyama Rhino (Faru)

Faru pia miguu yao ina vidole vitatu vyenye kwato kwa kila mguu. Black rhino yeye anakuwa na nundu juu kidogo ya mabega wakati White rhino yeye hana nundu na staili yao ya ujamianaji ni polygynous( Dume kujamiana na jike zaidi ya mmoja) na majike wa faru wanakuwa na pembe fupi kuliko madume na wana matiti mawili. Na watoto wa faru huishi na mama yao kwa kwa zaidi ya miaka mitatu hadi hapo jike atakapopata tena ujauzito. Maadui wakubwa wa faru ni binadamu ambao huwaua kwa sababu ya pembe zao na Simba ambao huwinda watoto wao kwa ajili ya kitoweo. Ni wanyama ambao hupendelea kula hasahasa wakati wa asubuhi na jioni ambapo hula takribani aina 200 tofauti tofauti za mimea na wana uwezo mzuri wa kuona, kunusa pamoja na kusikia. Kwa upande wa Black rhino yeye hupendelea maeneo yenye vichaka na miti mifupi kwa sababu yeye ni mlaji wa juu katika matawi ya miti wakati White rhino yeye anapendelea maeneo ambayo ni plains kwa sababu yeye ni mlaji wa nyasi. Pia faru ni wanyama wanaowekewa ulinzi wa kutosha kuwakinga dhidi ya majangili na wanalindwa na askari wa wanyama pori (Park rangers ) kwa saa 24,
 
Nimependa hapo kwa mama Faru mweupe kumtanguliza mtoto mbele kama mama wa kizungu and vice versa.
Naona fahari kuwa Mwafrika. Ndio maana Faru weusi wanapatikana kwetu Afrika.

Kaka ...
 
d8b2b7fe6381d1a97c259bb2c696dc8a.jpg
Faru kwa kiingereza anafahamika kama Rhino na kiswahili ni Faru na sio kifaru kama wengi wanavyomwita. Mnyama huyu anapatikana katika order inayojulikana kama PERISSODACTYLA na familia yake ni RHINOCEROTIDAE na jina lake la kisayansi ni DICEROUS BICORNIS kwa black rhino na White rhino jina lake la kisayansi anajulikana kama CERATOTHERIUM SIMUM.

Faru ni miongoni mwa wanyama ambao ni BIG FIVE kwa Africa, wengine ni chui, simba, mbogo na tembo. Kuna takribani aina tano za faru duniani na Africa tuna aina mbili za faru ambazo ni WHITE RHINO na BLACK RHINO na aina nyingine tatu silizobaki zinapatikana barani Asia, na kwa Tanzania sisi tuna aina moja tu ya faru ambayo ni Black rhino ingawa pia kuna white rhino wanaopatikana mkomazi ambayo ni introduced species waliochukuliwa kutoka South Africa.

Faru pia ni wanyama ambao wapo hatarini kutoweka duniani kutokana na kuwindwa sana na majangili kutokana na pembe zao ambazo zina thamani kubwa barani Asia na pembe hizi hutumika kutengenezea dagger pamoja na dawa maarufu ambayo hutumiwa na akina Baba kuleta heshima nyumbani (VIAGRA) ambayo ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume na wanaamini hivyo kutokana na huyu mnyama FARU kutumia mda mwingi wakati wa kujamiana ambapo anaweza kukaa mgongoni kwa jike kwa zaidi ya dakika 40.

Kutokana na kuwa na nguvu za kujamiana kwa mda mrefu watu wakafikiri kuwa nguvu zake zinatoka katika pembe kitu ambacho kimethibitishwa na wanasayansi kwamba si kweli kuwa pembe zake ndizo zimamsaidia kustahimili mda mrefu wakati wa kujamiana. Kwa kawaida faru ni wanyama ambayo huishi maisha ya mmoja mmoja (Solitary ) na dume na jike hukutana tu katika msimu wao wa ujamianaji ambapo kipindi hicho hutafutana kwa njia ya harufu ambayo hutolewa na jike pale anapokuwa anamuhitaji dume.

Anabeba ujauzito wake kwa kipindi cha miezi 18 na huwa anazaa mtoto mmoja ( Mapacha huwa ni nadra). Faru pia ni miongoni mwa wanyama wakubwa wanaopatikana nchi kavu ambapo anaweza kufikia hadi uzito wa 2000-2300KG kwa white rhino na 800-1500KG kwa black rhino.

Na tofauti kati ya Black rhino na White rhino ni kuwa ana mdomo mweusi uliochongoka ambao unamwezesha kula majani ya juu katika matawi ya mti (Browser) na white rhino yeye anakuwa na mdomo mpana mweupe kwa ndani ambao unamwezesha kula nyasi(Grazers), tofauti nyingine ni kwamba White rhino akiwa na mtoto huwa anatabia ya kumtanguliza mtoto mbele Kama wafanyavyo wamama wa kizungu ambao humbeba mtoto kwa mbele na kwa upande wa Black rhino yeye huwa mtoto anakaa nyuma ya mama kama wafanyavyo wamama wa kiafrica ambao huwabeba watoto wao mgongoni.

Na tofauti nyingine ni kwamba White Rhino ni mkubwa kuliko Black rhino. Na rhino huishi kwa kipindi cha miaka 30-50 na wanapendelea maeneo tambarare na yenye fichaka na kila mmoja huwa anamiliki eneo lake la himaya ambapo hutumia mkojo kuweka mipaka katika maeneo yao yaani hawa tunawaita territorial (Wanyama ambao humiliki maeneo ya himaya). Na kwa hapa Tanzania sehemu nzuri ya kuwaona hawa FARU ni NGORONGORO CRATER.
 
Asieee kweli wanatembea kwenye "Fichaka" Mangi ,halafu kweli jangili anaua faru halafu kinachotengenezwa na pembe yake ni kisu ? Kuna sehemu kwenye vichwa vyetu wanadamu hatupo sawa
 
d8b2b7fe6381d1a97c259bb2c696dc8a.jpg
Faru kwa kiingereza anafahamika kama Rhino na kiswahili ni Faru na sio kifaru kama wengi wanavyomwita. Mnyama huyu anapatikana katika order inayojulikana kama PERISSODACTYLA na familia yake ni RHINOCEROTIDAE na jina lake la kisayansi ni DICEROUS BICORNIS kwa black rhino na White rhino jina lake la kisayansi anajulikana kama CERATOTHERIUM SIMUM.

Faru ni miongoni mwa wanyama ambao ni BIG FIVE kwa Africa, wengine ni chui, simba, mbogo na tembo. Kuna takribani aina tano za faru duniani na Africa tuna aina mbili za faru ambazo ni WHITE RHINO na BLACK RHINO na aina nyingine tatu silizobaki zinapatikana barani Asia, na kwa Tanzania sisi tuna aina moja tu ya faru ambayo ni Black rhino ingawa pia kuna white rhino wanaopatikana mkomazi ambayo ni introduced species waliochukuliwa kutoka South Africa.

Faru pia ni wanyama ambao wapo hatarini kutoweka duniani kutokana na kuwindwa sana na majangili kutokana na pembe zao ambazo zina thamani kubwa barani Asia na pembe hizi hutumika kutengenezea dagger pamoja na dawa maarufu ambayo hutumiwa na akina Baba kuleta heshima nyumbani (VIAGRA) ambayo ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume na wanaamini hivyo kutokana na huyu mnyama FARU kutumia mda mwingi wakati wa kujamiana ambapo anaweza kukaa mgongoni kwa jike kwa zaidi ya dakika 40.

Kutokana na kuwa na nguvu za kujamiana kwa mda mrefu watu wakafikiri kuwa nguvu zake zinatoka katika pembe kitu ambacho kimethibitishwa na wanasayansi kwamba si kweli kuwa pembe zake ndizo zimamsaidia kustahimili mda mrefu wakati wa kujamiana. Kwa kawaida faru ni wanyama ambayo huishi maisha ya mmoja mmoja (Solitary ) na dume na jike hukutana tu katika msimu wao wa ujamianaji ambapo kipindi hicho hutafutana kwa njia ya harufu ambayo hutolewa na jike pale anapokuwa anamuhitaji dume.

Anabeba ujauzito wake kwa kipindi cha miezi 18 na huwa anazaa mtoto mmoja ( Mapacha huwa ni nadra). Faru pia ni miongoni mwa wanyama wakubwa wanaopatikana nchi kavu ambapo anaweza kufikia hadi uzito wa 2000-2300KG kwa white rhino na 800-1500KG kwa black rhino.

Na tofauti kati ya Black rhino na White rhino ni kuwa ana mdomo mweusi uliochongoka ambao unamwezesha kula majani ya juu katika matawi ya mti (Browser) na white rhino yeye anakuwa na mdomo mpana mweupe kwa ndani ambao unamwezesha kula nyasi(Grazers), tofauti nyingine ni kwamba White rhino akiwa na mtoto huwa anatabia ya kumtanguliza mtoto mbele Kama wafanyavyo wamama wa kizungu ambao humbeba mtoto kwa mbele na kwa upande wa Black rhino yeye huwa mtoto anakaa nyuma ya mama kama wafanyavyo wamama wa kiafrica ambao huwabeba watoto wao mgongoni.

Na tofauti nyingine ni kwamba White Rhino ni mkubwa kuliko Black rhino. Na rhino huishi kwa kipindi cha miaka 30-50 na wanapendelea maeneo tambarare na yenye fichaka na kila mmoja huwa anamiliki eneo lake la himaya ambapo hutumia mkojo kuweka mipaka katika maeneo yao yaani hawa tunawaita territorial (Wanyama ambao humiliki maeneo ya himaya). Na kwa hapa Tanzania sehemu nzuri ya kuwaona hawa FARU ni NGORONGORO CRATER.
Hivi ni kweli faru ni mnyama peke ambae hatembei na mzazi wake ? (sex pleasure )
 
Hivi ni kweli faru ni mnyama peke ambae hatembei na mzazi wake ? (sex pleasure )
Ndio mkuu hawa huwa pamoja dume na jike katika msimu wao wa ujamianaji na sio kwa faru tu hata chui vilevile dume na jike hawawezi kuwa pamoja nje ya msimu wao wa ujamianaji
 
Asieee kweli wanatembea kwenye "Fichaka" Mangi ,halafu kweli jangili anaua faru halafu kinachotengenezwa na pembe yake ni kisu ? Kuna sehemu kwenye vichwa vyetu wanadamu hatupo sawa
Ndo hivyo mkuu katika nchi za kiarabu hasahasa nchini yemen mwanaume huonekana tajiri na mwenye hadhi pale anapokuwa anamiliki dagger iliyotengenezwa kwa maligafi ya rhino na ndio maana hata mtu akifanikiwa kufikisha pembe ya faru katika ile nchi anaonekana Kama mfalme na anapewa hela za kutosha pamoja na kujichagulia mwenyewe idadi ya vipusa anaotaka. Ila usije ukathubutu kufanya huu mchezo maana ukikamatwa na pembe ya hawa jamaa unapotezwa maana wako wachache mno waliosalia katika bara la Africa na barani Asia kwa hiyo yatupasa wote kuchukua jukumu la kuwalinda kwa ajili ya kizazi kijacho vinginevyo watabaki tu kwenye makabrasha kuwa walikuwepo kama kina dinaso na wengineo ambao tayari walikwisha toweka!!! SAY NO FOR POARCHING
 
Uume wake una ukubwa gani na bao lake moja ni lita ngapi?anarudia tendo kila baada ya muda gani?
 
Back
Top Bottom