Steven mushi mushi
JF-Expert Member
- Jul 25, 2016
- 533
- 739
Faru ni miongoni mwa wanyama ambao ni BIG FIVE kwa Africa, wengine ni chui, simba, mbogo na tembo. Kuna takribani aina tano za faru duniani na Africa tuna aina mbili za faru ambazo ni WHITE RHINO na BLACK RHINO na aina nyingine tatu silizobaki zinapatikana barani Asia, na kwa Tanzania sisi tuna aina moja tu ya faru ambayo ni Black rhino ingawa pia kuna white rhino wanaopatikana mkomazi ambayo ni introduced species waliochukuliwa kutoka South Africa.
Faru pia ni wanyama ambao wapo hatarini kutoweka duniani kutokana na kuwindwa sana na majangili kutokana na pembe zao ambazo zina thamani kubwa barani Asia na pembe hizi hutumika kutengenezea dagger pamoja na dawa maarufu ambayo hutumiwa na akina Baba kuleta heshima nyumbani (VIAGRA) ambayo ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume na wanaamini hivyo kutokana na huyu mnyama FARU kutumia mda mwingi wakati wa kujamiana ambapo anaweza kukaa mgongoni kwa jike kwa zaidi ya dakika 40.
Kutokana na kuwa na nguvu za kujamiana kwa mda mrefu watu wakafikiri kuwa nguvu zake zinatoka katika pembe kitu ambacho kimethibitishwa na wanasayansi kwamba si kweli kuwa pembe zake ndizo zimamsaidia kustahimili mda mrefu wakati wa kujamiana. Kwa kawaida faru ni wanyama ambayo huishi maisha ya mmoja mmoja (Solitary ) na dume na jike hukutana tu katika msimu wao wa ujamianaji ambapo kipindi hicho hutafutana kwa njia ya harufu ambayo hutolewa na jike pale anapokuwa anamuhitaji dume.
Anabeba ujauzito wake kwa kipindi cha miezi 18 na huwa anazaa mtoto mmoja ( Mapacha huwa ni nadra). Faru pia ni miongoni mwa wanyama wakubwa wanaopatikana nchi kavu ambapo anaweza kufikia hadi uzito wa 2000-2300KG kwa white rhino na 800-1500KG kwa black rhino.
Na tofauti kati ya Black rhino na White rhino ni kuwa ana mdomo mweusi uliochongoka ambao unamwezesha kula majani ya juu katika matawi ya mti (Browser) na white rhino yeye anakuwa na mdomo mpana mweupe kwa ndani ambao unamwezesha kula nyasi(Grazers), tofauti nyingine ni kwamba White rhino akiwa na mtoto huwa anatabia ya kumtanguliza mtoto mbele Kama wafanyavyo wamama wa kizungu ambao humbeba mtoto kwa mbele na kwa upande wa Black rhino yeye huwa mtoto anakaa nyuma ya mama kama wafanyavyo wamama wa kiafrica ambao huwabeba watoto wao mgongoni.
Na tofauti nyingine ni kwamba White Rhino ni mkubwa kuliko Black rhino. Na rhino huishi kwa kipindi cha miaka 30-50 na wanapendelea maeneo tambarare na yenye fichaka na kila mmoja huwa anamiliki eneo lake la himaya ambapo hutumia mkojo kuweka mipaka katika maeneo yao yaani hawa tunawaita territorial (Wanyama ambao humiliki maeneo ya himaya). Na kwa hapa Tanzania sehemu nzuri ya kuwaona hawa FARU ni NGORONGORO CRATER.