Msela Wa Kitaa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2021
- 1,340
- 2,615
Kansela ajaye wa Ujerumani Friedrich MerzPicha: Volker Hartmann/AFP
Wakati hayo yakiripotiwa, Kansela ajaye wa Ujerumani Friedrich Merz amemwalika Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuitembelea Ujerumani.
Merz amesema atatafuta njia ila kuhakikisha kuwa kiongozi huyo wa Israel hatakamatwa kufuatia hati ya kukamatwa iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC.
Merz ameuambia mkutano wa waandishi wa habari, siku moja baada ya chama chake cha kihafidhina kushinda katika uchaguzi wa bunge kwamba, ni fikra isiyo na mantiki kwamba Waziri Mkuu wa Israel hawezi kuitembelea Ujerumani.
Soma pia: Viongozi duniani wampongeza Merz kwa ushindi
Mahakama ya Kimataifa ya ICC yenye makao yake mjini The Hague, Uholanzi ilitoa hati ya kukamatwa kwa Netanyahu, Waziri wake wa zamani wa ulinzi pamoja na maafisa wa Hamas kwa tuhuma za kuhusika na uhalifu wa kivita uliofanyika Gaza.
Nchi zote 27 za Umoja wa Ulaya, ikiwemo Ujerumani, ni wanachama wa ICC, ambayo ni mahakama pekee ya kimataifa inayoshughulikia kesi za uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.
Israel hata hivyo inapinga mamlaka ya mahakama hiyo na imekanusha pia madai ya kuhusika na uhalifu wa kivita.
Source: DW
Wakati hayo yakiripotiwa, Kansela ajaye wa Ujerumani Friedrich Merz amemwalika Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuitembelea Ujerumani.
Merz amesema atatafuta njia ila kuhakikisha kuwa kiongozi huyo wa Israel hatakamatwa kufuatia hati ya kukamatwa iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC.
Merz ameuambia mkutano wa waandishi wa habari, siku moja baada ya chama chake cha kihafidhina kushinda katika uchaguzi wa bunge kwamba, ni fikra isiyo na mantiki kwamba Waziri Mkuu wa Israel hawezi kuitembelea Ujerumani.
Soma pia: Viongozi duniani wampongeza Merz kwa ushindi
Mahakama ya Kimataifa ya ICC yenye makao yake mjini The Hague, Uholanzi ilitoa hati ya kukamatwa kwa Netanyahu, Waziri wake wa zamani wa ulinzi pamoja na maafisa wa Hamas kwa tuhuma za kuhusika na uhalifu wa kivita uliofanyika Gaza.
Nchi zote 27 za Umoja wa Ulaya, ikiwemo Ujerumani, ni wanachama wa ICC, ambayo ni mahakama pekee ya kimataifa inayoshughulikia kesi za uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.
Israel hata hivyo inapinga mamlaka ya mahakama hiyo na imekanusha pia madai ya kuhusika na uhalifu wa kivita.
Source: DW