Merz amwalika Netanyahu Ujerumani licha ya hati ya kukamatwa na ICC

Msela Wa Kitaa

JF-Expert Member
Oct 8, 2021
1,340
2,615
Kansela ajaye wa Ujerumani Friedrich MerzPicha: Volker Hartmann/AFP
Wakati hayo yakiripotiwa, Kansela ajaye wa Ujerumani Friedrich Merz amemwalika Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuitembelea Ujerumani.


Merz amesema atatafuta njia ila kuhakikisha kuwa kiongozi huyo wa Israel hatakamatwa kufuatia hati ya kukamatwa iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC.


Merz ameuambia mkutano wa waandishi wa habari, siku moja baada ya chama chake cha kihafidhina kushinda katika uchaguzi wa bunge kwamba, ni fikra isiyo na mantiki kwamba Waziri Mkuu wa Israel hawezi kuitembelea Ujerumani.


Soma pia: Viongozi duniani wampongeza Merz kwa ushindi


Mahakama ya Kimataifa ya ICC yenye makao yake mjini The Hague, Uholanzi ilitoa hati ya kukamatwa kwa Netanyahu, Waziri wake wa zamani wa ulinzi pamoja na maafisa wa Hamas kwa tuhuma za kuhusika na uhalifu wa kivita uliofanyika Gaza.


Nchi zote 27 za Umoja wa Ulaya, ikiwemo Ujerumani, ni wanachama wa ICC, ambayo ni mahakama pekee ya kimataifa inayoshughulikia kesi za uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.


Israel hata hivyo inapinga mamlaka ya mahakama hiyo na imekanusha pia madai ya kuhusika na uhalifu wa kivita.

Source: DW
 
Hakuna taifa la Ulaya au member wa NATO anayeweza kwenda kinyume na Marekani

Mataifa ya Ulaya na NATO wote ni occupied states controlled by U.S

Wanapelekwa pelekwa na Marekani hawawezi kujifanyia maamuzi kwenye masuala ya geopolitics na geoeconomics

 
Hakuna taifa la Ulaya au member wa NATO anayeweza kwenda kinyume na Marekani

Mataifa ya Ulaya na NATO wote ni occupied states controlled by U.S

Wanapelekwa pelekwa na Marekani hawawezi kujifanyia maamuzi kwenye masuala ya geopolitics na geoeconomics

Wanamuogopa Russia maana bila Marekani kuwasaidia kiulinzi hawamuwezi
 
Hakuna taifa la Ulaya au member wa NATO anayeweza kwenda kinyume na Marekani

Mataifa ya Ulaya na NATO wote ni occupied states controlled by U.S

Wanapelekwa pelekwa na Marekani hawawezi kujifanyia maamuzi kwenye masuala ya geopolitics na geoeconomics

Mkuu unadhani NETANYAHU kuna nchi ya ULAYA anaweza kukanyaga na Asikamwatwe !!!

NETANYAHU Mwenyewe awezi kudanganyika Akaenda uko!!! Mnajichanganya seem!!!!

NETANYAHU Kwenda MAREKANI China RUSSIA Nisawa Sababu sio Members wa ICC!!!!??

Sasa ULAYA yote ni MEMBERS iyo ngumu pengine aende kimya kimya Serikali iwe kama Aina habari!!! Lkn sio mwaliko rasmi Anadakwa NETANYAHU !!!!
 
Ikiwa Watafanya ujinga wa kutomkamata Madhara yake Wanachama Wengi Watajitoa ICC

kwaiyo awawezi kumwita NETANYAHU ktk ULAYA !! Japo najua SLOBADAN alikuwa Sio mwenzao!!!

Zaidi SLOBADAN alikuwa Anaungwa mkono na RUSSIA !! Lkn ULAYA kwenye Sheria Wamenyooka HATARI..
 
Ikiwa Watafanya ujinga wa kutomkamata Madhara yake Wanachama Wengi Watajitoa ICC

kwaiyo awawezi kumwita NETANYAHU ktk ULAYA !! Japo najua SLOBADAN alikuwa Sio mwenzao!!!

Zaidi SLOBADAN alikuwa Anaungwa mkono na RUSSIA !! Lkn ULAYA kwenye Sheria Wamenyooka HATARI..
Mkuu uhusiano uliokuwepo kati ya Slobudan na NATO huwezi kuulinganisha na uhusiano uliopo kati ya Netanyahu na NATO

Hakuna nchi ya EU ama NATO wanaoweza kumkamata Netanyah, hizo nchi zinaiheshimu sana USA,

Kumkamata kiongozi wa Israel unakuwa umemkamata kiongozi wa USA
 
Mkuu unadhani NETANYAHU kuna nchi ya ULAYA anaweza kukanyaga na Asikamwatwe !!!

NETANYAHU Mwenyewe awezi kudanganyika Akaenda uko!!! Mnajichanganya seem!!!!

NETANYAHU Kwenda MAREKANI China RUSSIA Nisawa Sababu sio Members wa ICC!!!!??

Sasa ULAYA yote ni MEMBERS iyo ngumu pengine aende kimya kimya Serikali iwe kama Aina habari!!! Lkn sio mwaliko rasmi Anadakwa NETANYAHU !!!!
Hakuna taifa la Ulaya lenye ubavu wa kumkamata Netanyahu
 
Mkuu uhusiano uliokuwepo kati ya Slobudan na NATO huwezi kuulinganisha na uhusiano uliopo kati ya Netanyahu na NATO

Hakuna nchi ya EU ama NATO wanaoweza kumkamata Netanyah, hizo nchi zinaiheshimu sana USA,

Kumkamata kiongozi wa Israel unakuwa umemkamata kiongozi wa USA
Kwani HATI ya ICC ilitolewa nanani sio ULAYA!!!!!
 
Back
Top Bottom