Masaa 24 biashara Kariakoo, hali ya usalama mitaani wanakotoka wateja inaruhusu?

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
13,718
14,152
Mitaa yetu ina giza nene totoro na vibaka wengi sana, na wakati mwingine hakuna umeme kabisa.

Ni jambo jema sana biashara kariakoo masaa 24, itasaidia kuchechemua uchumi wa watu, familia, jiji na taifa kwa ujumla. Usalama Kariakoo umeimarishwa kwa kufunga taa, kamera na kuwa na walinzi wa watu na mali zao wakiwa Kariakoo. Hata hivyo kuweka usala Kariakoo tu peke yake bila kufanya hivyohivyo na kwenye mitaa wanakoishi wananchi (wanunuzi/wateja) ni kuhatarisha usalama wao na mali wazilizozinunua usiku wa manane Kariakoo. Wataporwa watakapokuwa wanarudi nazo majumbani kwao kwenye mitaa yenye giza na isiyokuwa na kamera wala ulinzi wowote.

Tuache kukopi na kupesti matukio kutoka nchi za watu bila kuchota na kupesti mazingira ya matukio hayo huko mlikoyakopi.

Tujiandae kuona watu wakiporwa na kuumizwa wakati wakitoka Kariakoo saa 9 usiku kurudi majumbani kwao.
 
Mitaa yetu ina giza nene totoro na vibaka wengi sana, na wakati mwingine hakuna umeme kabisa.

Ni jambo jema sana biashara kariakoo masaa 24, itasaidia kuchechemua uchumi wa watu, familia, jiji na taifa kwa ujumla. Usalama Kariakoo umeimarishwa kwa kufunga taa, kamera na kuwa na walinzi wa watu na mali zao wakiwa Kariakoo. Hata hivyo kuweka usala Kariakoo tu peke yake bila kufanya hivyohivyo na kwenye mitaa wanakoishi wananchi (wanunuzi/wateja) ni kuhatarisha usalama wao na mali wazilizozinunua usiku wa manane Kariakoo. Wataporwa watakapokuwa wanarudi nazo majumbani kwao kwenye mitaa yenye giza na isiyokuwa na kamera wala ulinzi wowote.

Tuache kukopi na kupesti matukio kutoka nchi za watu bila kuchota na kupesti mazingira ya matukio hayo huko mlikoyakopi.

Tujiandae kuona watu wakiporwa na kuumizwa wakati wakitoka Kariakoo saa 9 usiku kurudi majumbani kwao.
Hata sasa kuna watu wanatoka usiku mkubwa kwenda masokoni kununua bidhaa,,,,machinjioni n.k.....
kwa hiyo faida ni nyingi kuliko hasara.....hatuwezi kuacha kufanya kazi kwa kuogopa wahalifu...dawa ni kupambana nao.
 
Kuna muda viongozi sijui huwa wanafikiria nini, mfano kuna miji wamebadili mifumo ya maji, wakaweka mabomba mapya kwenye sources bila kuzingatia size, kilichotokea kule kwenye source maji yanakuja na presha kubwa hivyo kupasua mabomba ya huku mitaani ambayo yamekaa muda mrefu.

Kitu hikohiko kinatokea hapa, tutegemee wizi, ukabaji kuongezeka maeneo jirani na kkoo sabab usalama wa dar siku hizi umeshuka. Watu wameripoti humu ule wizi wa kupigwa mapanga kurudi.
 
Soko la Mbagala Zakhem mbona wanakesha? Mimi nakaa mbagala na naenda hapo sokoni saa 4,5 usiku soko limefurika , inategemea na mazingira unayoishi,dar saa 5 usiku mtaani watu kibao
 
Watanunua wafungashaji mizigo kwenda mikoani hususani wenye magari
Labda hivyo, lakini hata hao watayaweka maisha yao na mali zao mashakani. Barabara zetu hazina kamera Wala askari usiku. Wacha tujaribu tuone, maana sisi huwa tunafanyakazi baada ya tatizo kutoka (reactive) hasa baada ya kupoteza maisha ya wenzetu wengi.
 
Hata sasa kuna watu wanatoka usiku mkubwa kwenda masokoni kununua bidhaa,,,,machinjioni n.k.....
kwa hiyo faida ni nyingi kuliko hasara.....hatuwezi kuacha kufanya kazi kwa kuogopa wahalifu...dawa ni kupambana nao.
Nani atapora nyama wewe!! be serious.
 
Mitaa yetu ina giza nene totoro na vibaka wengi sana, na wakati mwingine hakuna umeme kabisa.

Ni jambo jema sana biashara kariakoo masaa 24, itasaidia kuchechemua uchumi wa watu, familia, jiji na taifa kwa ujumla. Usalama Kariakoo umeimarishwa kwa kufunga taa, kamera na kuwa na walinzi wa watu na mali zao wakiwa Kariakoo. Hata hivyo kuweka usala Kariakoo tu peke yake bila kufanya hivyohivyo na kwenye mitaa wanakoishi wananchi (wanunuzi/wateja) ni kuhatarisha usalama wao na mali wazilizozinunua usiku wa manane Kariakoo. Wataporwa watakapokuwa wanarudi nazo majumbani kwao kwenye mitaa yenye giza na isiyokuwa na kamera wala ulinzi wowote.

Tuache kukopi na kupesti matukio kutoka nchi za watu bila kuchota na kupesti mazingira ya matukio hayo huko mlikoyakopi.

Tujiandae kuona watu wakiporwa na kuumizwa wakati wakitoka Kariakoo saa 9 usiku kurudi majumbani kwao.
Wanasema cctv zipatazo 24 zitagarimu milion 500 .
 
Wezi tutakuwa nao wakati wa kununua kisha tutaondoka nao kurudi mitaani kwetu, patashika itakuwa huko njiani.
Kuna muda viongozi sijui huwa wanafikiria nini, mfano kuna miji wamebadili mifumo ya maji, wakaweka mabomba mapya kwenye sources bila kuzingatia size, kilichotokea kule kwenye source maji yanakuja na presha kubwa hivyo kupasua mabomba ya huku mitaani ambayo yamekaa muda mrefu.

Kitu hikohiko kinatokea hapa, tutegemee wizi, ukabaji kuongezeka maeneo jirani na kkoo sabab usalama wa dar siku hizi umeshuka. Watu wameripoti humu ule wizi wa kupigwa mapanga kurudi.
tu
 
Mitaa yetu ina giza nene totoro na vibaka wengi sana, na wakati mwingine hakuna umeme kabisa.

Ni jambo jema sana biashara kariakoo masaa 24, itasaidia kuchechemua uchumi wa watu, familia, jiji na taifa kwa ujumla. Usalama Kariakoo umeimarishwa kwa kufunga taa, kamera na kuwa na walinzi wa watu na mali zao wakiwa Kariakoo. Hata hivyo kuweka usala Kariakoo tu peke yake bila kufanya hivyohivyo na kwenye mitaa wanakoishi wananchi (wanunuzi/wateja) ni kuhatarisha usalama wao na mali wazilizozinunua usiku wa manane Kariakoo. Wataporwa watakapokuwa wanarudi nazo majumbani kwao kwenye mitaa yenye giza na isiyokuwa na kamera wala ulinzi wowote.

Tuache kukopi na kupesti matukio kutoka nchi za watu bila kuchota na kupesti mazingira ya matukio hayo huko mlikoyakopi.

Tujiandae kuona watu wakiporwa na kuumizwa wakati wakitoka Kariakoo saa 9 usiku kurudi majumbani kwao.
Kariakoo kuna maduka mengi tu yanafungwa hadi saa 7-8 usiku hasa wakati huu wa mfungo wa Ramadhani. Watu walitoka Tarawehe wanakwenda Shopping.

Kuna mitaa yake kama Mkunguni, Eneo toka Big Bon hadi Lumumba na Tandamti kuanzia sikukuu kwenda Lumumba,

Kuna potential yake kukaa masaa 24, sio kwa Mteja wa Tandale ama Mwananyamala bali kwa Wageni na wa kazi wa mjini. Kuna wageni wanalala pale pale kkoo toka Malawi, Zambia, Congo, Comoros etc badala ya kupakana Majasho mchana wanaweza fungasha mizigo yao usiku kwa Amani tu.
 
watz tuko na shida sana, kama unaona usalama mtaani kwako ni mdogo nyakat za usiku, nenda mchana, usiku waachie wengine, kwani umelazimishwa kwenda kkoo usiku wa manane.
 
Kariakoo kuna maduka mengi tu yanafungwa hadi saa 7-8 usiku hasa wakati huu wa mfungo wa Ramadhani. Watu walitoka Tarawehe wanakwenda Shopping.

Kuna mitaa yake kama Mkunguni, Eneo toka Big Bon hadi Lumumba na Tandamti kuanzia sikukuu kwenda Lumumba,

Kuna potential yake kukaa masaa 24, sio kwa Mteja wa Tandale ama Mwananyamala bali kwa Wageni na wa kazi wa mjini. Kuna wageni wanalala pale pale kkoo toka Malawi, Zambia, Congo, Comoros etc badala ya kupakana Majasho mchana wanaweza fungasha mizigo yao usiku kwa Amani tu.
nakazia, hao wa tandala na nyamala waende mchana wakapakane majasho huko.
 
Soko la Mbagala Zakhem mbona wanakesha? Mimi nakaa mbagala na naenda hapo sokoni saa 4,5 usiku soko limefurika , inategemea na mazingira unayoishi,dar saa 5 usiku mtaani watu kibao
Zakem si wanauza nyanyachungu na dagaa mchele tu, kibaka nani atakupora fugu la bamia? Saa tano usiku ni muda wa kawaida dar lakini sio saa 9 usiku. Hebu ajaribu kwenda kisha urudi kwenu mtaa wa mnyamani na TV Yako moya uone kitakachokupata.
 
Mitaa yetu ina giza nene totoro na vibaka wengi sana, na wakati mwingine hakuna umeme kabisa.

Ni jambo jema sana biashara kariakoo masaa 24, itasaidia kuchechemua uchumi wa watu, familia, jiji na taifa kwa ujumla. Usalama Kariakoo umeimarishwa kwa kufunga taa, kamera na kuwa na walinzi wa watu na mali zao wakiwa Kariakoo. Hata hivyo kuweka usala Kariakoo tu peke yake bila kufanya hivyohivyo na kwenye mitaa wanakoishi wananchi (wanunuzi/wateja) ni kuhatarisha usalama wao na mali wazilizozinunua usiku wa manane Kariakoo. Wataporwa watakapokuwa wanarudi nazo majumbani kwao kwenye mitaa yenye giza na isiyokuwa na kamera wala ulinzi wowote.

Tuache kukopi na kupesti matukio kutoka nchi za watu bila kuchota na kupesti mazingira ya matukio hayo huko mlikoyakopi.

Tujiandae kuona watu wakiporwa na kuumizwa wakati wakitoka Kariakoo saa 9 usiku kurudi majumbani kwao.
Politics as usual
 
Back
Top Bottom