Marekani haipaswi kukaa kimya juu ya video ya siri kuhusu kampuni ya Pfizer

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,018
1,042
VCG41661788251.jpg



Hivi karibuni, video ya siri inayomwonyesha Jordon Trishton Walker, aliyeelezwa kuwa Mkurugenzi wa wa Pfizer anayeshughulikia Utafiti na Maendeleo, Operesheni za Mkakati na Mipango ya Kisayansi ya mRNA, akisema jinsi kampuni hiyo inavyotafiti kubadili virusi vya Corona ili kuongeza faida ya chanjo za mRNA katika siku za baadaye, ilisambaa katika mitandao ya kijamii.

Katika video hiyo, Bw. Walker anasikika akimwambia mwanahabari wa Project Veritas kuhusu mpango wa kampuni ya Pfizer wa chanjo ya COVID-19, huku akikubali kuwa watu hawatafurahia habari hiyo kama ikitangazwa.

Takwimu zilizotolewa na kampuni ya Pfizer zinaonyesha kuwa, zaidi ya chanjo bilioni 4.3 za BioNTech za COVID-19 zilisafirishwa katika nchi 181 duniani mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka jana.

Takwimu kutoka Shirika la Afya Duniani zinaonyesha kuwa, zaidi ya watu milioni 6 wamefariki kutokana na virusi hivyo. Inasikitisha kuona kuwa, pamoja na idadi hii kubwa ya vifo, na watu wanaendelea kuambukizwa COVID-19, lakini mkuu wa kampuni kubwa kama Pfizer anadiriki kusema kuwa wana mpango wa kutafiti njia za kubadili virusi vya Corona ili kampuni yake iendelee kufaidia? Mkurugenzi huyo pia anadaiwa kudai kuwa, virusi vya Corona vitakuwa kama ng’ombe wa maziwa kwa kampuni ya Pfizer kwa muda ujao.

Kutokana na video hiyo, watu wamejiuliza maswali mengi sana. Je, Pfizer inatumia janga la COVID-19 kujipatia faida na inafanya hivyo kwa siri? Je, utafiti huo umefanyika kwa kiasi gani, una hatari gani kwa binadamu? Haya ni baadhi tu ya maswali ambayo watu wanajiuliza, lakini cha kushangaza, vyombo vingi vya habari vya nchi za Magharibi na Marekani vimekaa kimywa kuhusu video hiyo iliyovuja. Jambo hili ni la kustaajabisha ukizingatia kuwa uwanja wa maoni ya umma ya Wamarekani unajulikana kwa unyumbufu wake!

Ni kweli kwamba uhakika wa video hiyo bado haujathibitishwa, labda ndio sababu wahusika wamekaa kimya. Lakini hata hivyo, kwa jambo kubwa kama hilo, haipaswi kwa Mamlaka ya Chakula na Dawa ya Marekani, watunga sera na vyombo vya habari kufanya uchunguzi zaidi na kutoa maelezo kwa umma?

Hatua hii inafanya watu kuwa na maswali mengine, kwa mfano, je, kama video kama hiyo ingekuwa imevuja kutoka China, jamii ya kimataifa ingebaki kimya bila ya kuizungumzia?

Ni wazi kama video ya siri kama hiyo ingesambaa nchini China, maofisa wa ngazi husika pamoja na serikali zingefanya uchunguzi wa kina, na kampuni ama mamlaka husika zingetakiwa kutoa maelezo kikamilifu, na hatua za kinidhamu pia zingechukuliwa dhidi ya wahusika.

Mtaalamu mmoja wa China ambaye hakutaka jina lake litajwe ameweka wazi kuwa, vyombo vya habari vya Magharibi vinajali zaidi maslahi kuliko ukweli. Na hili limethibitika kutokana na video hiyo, ambapo pamoja na kuwa imevuja kwenye mitandao ya kijamii na kuonekana na wahusika, lakini hakuna aliye tayari kulizungumzia suala hilo.

Tunaweza kusema kuwa, kampuni kubwa za dawa za nchini Marekani pamoja na vyombo vya habari vikubwa vinajikuta vinashindwa kuchukua hatua yoyote kutokana na maslahi yao.

Kimya hiki kufuatia video hiyo kinaonyesha wazi unafiki wa vyombo vya habari vya Marekani!
 
Hiyo Nchi na watu wake Nihatari sana
Unatakiwa Kuwa na Shida ya Akili Kuishabikia US
 
Back
Top Bottom