Mama na Baba wenye nyumba za kupangisha, karibuni tupeane uzoefu na changamoto

DeepPond

JF-Expert Member
Nov 18, 2017
42,265
105,470
Habarini wakuu,
Ni wasaa wetu pia sisi wababa na WA mama wenye nyumba za kupangisha tupate uwanja wetu WA kujadili fursa,uzoefu na changamoto zinazoikabili hii biashara yetu kongwe ya kupangisha.

UZOEFU WANGU ni HUU.
1. CHANZO kikuu Cha migogoro mingi Kwa wapangaji ni umeme,choo na maji. Ukiweza kuwatenganishia hivyo, utajiepushia Vikao vya hovyo Kila mara na wapangaji wako.

2. Wapangaji wengi WA vyumba vya Bei ndogo (visivyo na finishing nzuri), ndo huwa wanasumbua sana kulipia Kodi Kwa wakati.

3. Wapangaji wengi WA vyumba vya Bei kubwa, Huwa Sio washindaji sana WA nyumbani. Hivyo Nyumba Yako haichakai.

4. Wapangaji wengi WA vyumba vya Bei kubwa, ni Mara chache sana ukute wamebandika magazeti ukutani, wanalala na baiskeli/pikpiki, gunia la mkaa au gunia la mahindi.

5. Watumishi wengi WA serikali ni walipaji wazuri WA Kodi Kwa wakati, isipokua TU kwa maaskali polisi na wanajeshi.

6. Ukipata Wapangaji WA kisabato au wale waislamu Safi wenye msimamo mkali, ni wasafi mno WA kutunza mazingira ya nyumba.

7. Wapangaji wengi WA single room, wengi wao hawana MKE/mume.
Kama unapendelea sharti la "lazima uwe mke/mume" , Sio vyema kujenga vyumba vya single room vingi kupangisha.

8. Wapangaji wengi WA single room, wanachakaza sana nyumba, tofauti na wale WA Chumba na sebule au nyumba nzima (Wanajaza sana vitu).

9. Nyumba yeye tiles, Kama unawapangaji wenye pikipiki, wajengee sehem maalum ya kulaza pikipiki zao nje ya vyumba vyao. zinaharibu sana tiles.

10. Ukijenga Nyumba ya wapangaji, jitahidi nje mlangoni pa kuingilia pawe na Baraza lenye paa, mvua na jua vinachakaza sana milango.

11. Kama mpangaji anataka kubadilisha rangi ya Chumba chake, usimruhusu atumie rangi ya mafuta. Inasumbua sana kukarabati pindi atakapohama.
(Atumiwe ya maji au wash&wear)

12. Kuepusha nyumba Yako kutobolewa tobolewa na misumari, wawekee wapangaji wako enga za Nguo na pazia, vyumbani na vyooni.

13. Kuepusha kuchakaza paa lako, wajengee wapangaji sehemu maalum ya kugongea madishi ya ving'amuzi vyao.

14. Kuepusha kutoboa toboa gypsum bodi Yako au madirisha Yako, jitahidi kuwawekea Tvswitch Kwa ajili ya kuvushia waya WA king'amuzi. (Weka na waya WA dish kabisa utokee nje, akifika aunge na kuchomeka TU)

15. Nyumba ya kupangisha ikishajaa sana Wamama wengi (hasa wanaoshinda nyumbani) jiandae kuitwa kusuhisha kesi za Kila mara.

Mengine tueendelee kufunguka ndani ya Uzi......
 
wapangaji wana tabia ya kuchimba mashimo mafupi ya taka, na yakijaa hawazoi, wanaenda kuchimba pengine.

Usipoweka utaratibu mzuri wa taka, eneo lako lote la nje ya nyumba yako lililobaki wazi, litageuka dampo la taka.

Binafsi: nmewachimbia shimo kubwa la taka, na nmepiga marufuku kuchimba shimo lolote eneo labgu,likijaa wachangiahabe pesa walipe Watu waje wazoe taka wakatupe.
 
Ukipata mpangaji mwenye duka eneo jirani na nyumba Yako, kua makini sana, Chumba ulichompangisha kinaweza geuka godauni. (Kitachakaa vibaya mno)

Mf: nilimpangisha mangi mmoja ana duka mbele ya nyumba yangu, alikigeuza Chumba chake godown, siku anaondoka Chumba hakieleweki
 
Jitahd wapangaji wako Wote wafahamike kwa mwenyekiti wa mtaa, inaweza saidia Endapo lolote likitokea.
Mf: nilimpangisha mangi mmoja, akawa anahifadhi vipodozi HARAMU na mirungi Toka nje ya nchi, kwenye Chumba nilichompangisha, siku ananaswa, nilipata usumbufu Sana, shukran kwa m/kiti WA mtaa
 
Hata kama uchumi unabana,

Jitahd nyumba ya wapangaji wako iwe na ceilingbodi,

Utajiepusha na Vikao vya wapangaji wako kusuluhisha kesi za KELELE za miziki na ngono baina ya wapangaji wako.

Aisee, kusuluhisha kesi za KELELE za ngono na wapangaji wako, wengine Watu wazima kuliko Wewe na wana familia zao, inakua haukai vzuri.
 
Sahii kabisa,kukaa na wapangaji Sio vzur, Nyumba yangu ya kwanza niliishi na wapangaji, wife alkua haishi kugombana na wapangaji
Mkuu tunakulaga wote hapo ndani na hawaambiani ndio uzuri, kila mmoja anahisi kaliwa yeye tu na kwa vile unaishi pale na baba yao mwenye nyumba wanahofia siri kumfikia.

Hao ndio wakija wanakuambia baba au mama na majirani wanakuongelea hivi na vile
 
Habarini wakuu,
Ni wasaa wetu pia sisi wababa na WA mama wenye nyumba za kupangisha tupate uwanja wetu WA kujadili fursa,uzoefu na changamoto zinazoikabili hii biashara yetu kongwe ya kupangisha.

UZOEFU WANGU ni HUU.
1. CHANZO kikuu Cha migogoro mingi Kwa wapangaji ni umeme,choo na maji. Ukiweza kuwatenganishia hivyo, utajiepushia Vikao vya hovyo Kila mara na wapangaji wako.

2. Wapangaji wengi WA vyumba vya Bei ndogo (visivyo na finishing nzuri), ndo huwa wanasumbua sana kulipia Kodi Kwa wakati.

3. Wapangaji wengi WA vyumba vya Bei kubwa, Huwa Sio washindaji sana WA nyumbani. Hivyo Nyumba Yako haichakai.

4. Wapangaji wengi WA vyumba vya Bei kubwa, ni Mara chache sana ukute wamebandika magazeti ukutani, wanalala na baiskeli/pikpiki, gunia la mkaa au gunia la mahindi.

5. Watumishi wengi WA serikali ni walipaji wazuri WA Kodi Kwa wakati, isipokua TU kwa maaskali polisi na wanajeshi.

6. Ukipata Wapangaji WA kisabato au wale waislamu Safi wenye msimamo mkali, ni wasafi mno WA kutunza mazingira ya nyumba.

7. Wapangaji wengi WA single room, wengi wao hawana MKE/mume.
Kama unapendelea sharti la "lazima uwe mke/mume" , Sio vyema kujenga vyumba vya single room vingi kupangisha.

8. Wapangaji wengi WA single room, wanachakaza sana nyumba, tofauti na wale WA Chumba na sebule au nyumba nzima (Wanajaza sana vitu).

9. Nyumba yeye tiles, Kama unawapangaji wenye pikipiki, wajengee sehem maalum ya kulaza pikipiki zao nje ya vyumba vyao. zinaharibu sana tiles.

10. Ukijenga Nyumba ya wapangaji, jitahidi nje mlangoni pa kuingilia pawe na Baraza lenye paa, mvua na jua vinachakaza sana milango.

11. Kama mpangaji anataka kubadilisha rangi ya Chumba chake, usimruhusu atumie rangi ya mafuta. Inasumbua sana kukarabati pindi atakapohama.
(Atumiwe ya maji au wash&wear)

12. Kuepusha nyumba Yako kutobolewa tobolewa na misumari, wawekee wapangaji wako enga za Nguo na pazia, vyumbani na vyooni.

13. Kuepusha kuchakaza paa lako, wajengee wapangaji sehemu maalum ya kugongea madishi ya ving'amuzi vyao.

14. Kuepusha kutoboa toboa gypsum bodi Yako au madirisha Yako, jitahidi kuwawekea Tvswitch Kwa ajili ya kuvushia waya WA king'amuzi. (Weka na waya WA dish kabisa utokee nje, akifika aunge na kuchomeka TU)

15. Nyumba ya kupangisha ikishajaa sana Wamama wengi (hasa wanaoshinda nyumbani) jiandae kuitwa kusuhisha kesi za Kila mara.

Mengine tueendelee kufunguka ndani ya Uzi......
I love this, wenye nyumba wangekuwa wanamwenda na ukisasa huu nadhani wapangaji tungekuwa mikono salama hata aibu kuchelewesha Kodi
 
Mkuu tunakulaga wote hapo ndani na hawaambiani ndio uzuri, kila mmoja anahisi kaliwa yeye tu na kwa vile unaishi pale na baba yao mwenye nyumba wanahofia siri kumfikia.

Hao ndio wakija wanakuambia baba au mama na majirani wanakuongelea hivi na vile
Watu mna roho ngumu sana, unakulaje mali ya mwenye mali ilihali unaendelea kuishi kwa mwenye mali papo hapo kila siku?

Ubinadamu ni kazi/The humanity is work.
 
Mkuu tunakulaga wote hapo ndani na hawaambiani ndio uzuri, kila mmoja anahisi kaliwa yeye tu na kwa vile unaishi pale na baba yao mwenye nyumba wanahofia siri kumfikia.

Hao ndio wakija wanakuambia baba au mama na majirani wanakuongelea hivi na vile
Ha ha hs.....wife alkua anagombana na wanawake wenzie. Yaani ukimshinda, analivaa joho la Maza house, NKAONA HUYU ANASUMBUA WAPANGAJI WANGU, NKAENDA KUPANGA NYUMBA YA UJITEGEMEA, Kodi ya uku,nailipa kule, uku nkijitafta kujenga kwangu
 
Back
Top Bottom