TANZIA Lawrance Mafuru, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango afariki dunia

Nyingi nafasi za kubebwa na Mzee wa Msoga tu. Kipimo halisi n̈I alipokuwa CEO wa NBC na namna alivyofeli vibaya kiuongozi hadi kutolewa na makaburu
Hawa wengi wao elimu zao za magumashi sema tu wanabebwa na ma Godfather wao wengi wao wamesoma hapo IFM, diploma za Banking wakawa chawa wa maMD waliokuwepo enzi hizo na kukabidhiwa vijiti vya u CEO, utaona mtoa CV hajaandika shule na vyuo alivyosoma, wapo wengi kwenye taasisi za kifedha hasa benki.
 
HIi ni post ya taarifa ya kifo, unaposema ukimwi unaua unamaanisha nini? Unless huelewi hata maana ya kitu unachoandika eti? Au wewe hutokufa?
Kwani kuugua UKIMWI ni dhambi sijui kwanini watu mnaogopa kusema marehemu kafa kwa UKIMWI? Raisi Kaunda na Mandela waliwahi kutangaza kuwa watoto wao wamekufa kwa UKIMWI, kusema mtu kafa kwa UKIMWI si dhambi na kifo kipo tu hata ukisema au usiseme kuhusu Ukimwi siku ikifika utaondoka tu. Kuogopa UKIMWi ni kujidanganya ,UKIMWI upo na unampata mtu yeyote.
 
View attachment 3147717
Lawrence Nyasebwa Mafuru, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango amefariki Dunia leo Novemba 9, 2024 katika hospitali ya Apollo nchini India.

Rais Samia Suluhu Hassan ameandika katika Mitandao yake ya Kijamii kuhusu Kifo cha Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango,
View attachment 3147755
"Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Bw. Lawrence Nyasebwa Mafuru, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango kilichotokea leo tarehe 09 Novemba, 2024 katika hospitali ya Apollo nchini India.

Ninatoa pole kwa familia, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Mheshimiwa Prof. Kitila Alexander Mkumbo, watumishi wa Tume ya Mipango, ndugu jamaa na marafiki kufuatia msiba huu.

Bw. Mafuru atakumbukwa kwa utumishi wake uliotukuka, bidii na ubunifu alipotumikia nafasi mbalimbali ndani ya Serikali.

Mwenyezi Mungu aijalie familia yake subra na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu na ailaze roho yake mahali pema."



Wasifu wa Mafuru

Lawrence Mafuru ni mtaalamu mashuhuri wa masuala ya fedha mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika benki, uwekezaji, na sera za serikali. Ni Certified Chartered Banker kutoka Taasisi ya Wataalamu wa Benki ya London na pia ni Certified Financial Markets Dealer aliyeidhinishwa na ACI Financial Markets.

Alianza safari yake mwaka 1998 katika Benki ya Standard Chartered, akijikita katika Ufadhili wa Biashara za Kimataifa. Kwa kipindi cha zaidi ya miongo miwili iliyofuata, alishika nyadhifa mbalimbali za uongozi katika sekta ya fedha nchini Tanzania, ikiwemo kuwa Mkuu wa Hazina katika Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, na Mwenyekiti wa Chama cha Mabenki Tanzania (TBA).

Uzoefu wake unaenda zaidi ya benki za biashara, kwani pia aliwahi kuhudumu kama Msajili wa Hazina katika Wizara ya Fedha. Kama mamlaka inayotambulika katika masuala ya benki na fedha, Bw.

Mafuru huombwa mara kwa mara kuwa mzungumzaji kwenye mijadala ya sekta hiyo. Ana shauku ya kutumia utaalamu wake ili kuleta manufaa kwa wateja na wadau wake.

Kabla ya nafasi yake ya sasa, Bw. Mafuru alichangia pakubwa katika kuunda sera za uchumi za Tanzania. Alihudumu katika Wizara ya Fedha kama Kamishna wa Idara ya Uchambuzi wa Sera na baadaye kama Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Sera za Usimamizi wa Uchumi.

Hadi kifo kinamkuta, Bw. Lawrence Nyasebwa Mafuru alikuwa akihudumu kama Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango.
Rip dude
IMG-20241109-WA0039.jpg
 
Alikuwa jizi,tu, wala simungunyi maneno,huyu na mkapa, ndio waliuza NBC benk kwa bei ya kutupa, Maghu alimtumbua alipokuwa hazina,kizimkazi, akamrudisha,
TZ is better off without him, he used is expertise to plunder and steal!
Muogope Mungu unamuonea kwa hilo binafsi namfahamu Mafuru na makandokando yake ila hilo mtake radhi hata kama hatakusikia ishu yake ni (EKIA) majasusi wamenielewa.
 
R.I.P mtumishi wa umma wa muda mrefu.
May god give him eternal piece.

Shida inakuja ni nani anajukumu la kuboresha huduma zetu za afya, ili viongozi waamini utoaji wa huduma Tanzania huduma inayotolewa hapo ni sawa kwengine kokotę duniani.

Ni ngumu kuelewa kwanini wengine tulikuwa tunapambana Dr Dorothy Gwajima, abaki afya,

Ndani ya muda wake ata angekaa miaka 10 peke yake asingeweza badili tabia za afya. Iła ndani ya muda huo angeweza kuwa catalyst ya watanzania waelevu kupata elimu on what to expect and demand kwenye wizara ya afya. Hasa alipokuwa naibu TAMISEMI.

Ni kwa sababu huko serikalini wao wenyewe (kwenye mamlaka ya teuzi, ya raisi) hawajui sifa na faida za watu sahihi wa kupewa nafasi zenye faida kwa jamii.

Akili za viongozi ni kwenda kufia nje ya nchi, ndio maana hawaoni sababu ya kutumia wataalamu kuiboresha nchi yao.

Katika maamuzi niliyowahi shuhudia Tanzania na kunikera ni siku huyo mama yenu mwenye akili za darasa la nne kumtoa Gwajima ‘afya’ na Jaffo ‘TAMISEMI’ yaani hapo ndipo nilipo jiridisha huyo mama hana nia njema na nchi.
 


Salaleh, kwa hivyo bank haiwezi uza shares au bonds kutafuta capital na kutengeneza financial products za kuuza.

Marehemu ilikuwa ukimsikiliza sehemu zingine akiongelea masuala ya uchumi, unaona hakukuwa na kitu, ni watu ambao waliohitimu kwa second-second na kukuzwa na Jakaya Kikwete.

The nonsense that came from him hakuna private bank ingeweza mpa ukuregenzi mtu kama yule. Akili zao zilikuwa na faida serikalini tu walikojabza vilaza.
 
Back
Top Bottom