strong ruler
JF-Expert Member
- Nov 2, 2013
- 4,921
- 3,306
Uzi wa kinafki huu
Unafiki utaisha lini?
Uzi wa kinafki huu
Vipi bwana sukari ashamaliza kuigawa ile ya Mbagala,maana chai hainyweki huku kwetu
Kwani Lowassa ni Mmasai????????ameandika kinafiki...ajabu umemurudia mwenyewe
Ama hakika Lowassa ana damu ya kupendwa. From Urais hadi ULAIGWANAN safi sana. HAPA KAZI TU!
Leo nimejionea jinsi mheshimiwa Lowassa akikomaa kujiuza katika vyombo vya habari.
Ni jambo jema kwa mwanasiasa yeyote kuiga style hii.
Kabla ya uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani 2015, mheshimiwa Lowassa aliteka vyombo vya habari kwa asilimia kubwa sana kuliko wagombea wote na nilijua ndie Rais ajae.
Kumbe ilikua ni hadaa ya kuteka vyombo vya habari.
Lakini baada ya Rais Magufuli kuapishwa na kupiga kazi ya kutukuka kwa muda mfupi, jamaa alipotea gafla.
Sasa amehamia kwenye mambo ya kimila angalau kupata Kiki kiaina.
Kweli Magufuli noma!
Namshauli pia asiache zile harambee za makanisani kwani zina tija kwake, ataendelea kuwepo miongoni mwa jamii kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa 2020.
Nashauri jamii imtie moyo kwa kumualika kwenye kila harambee, Ni mwenzetu jamani.
Namalizia kwa kusema yaliyopita si ndwele, tugange yajayo, Rais ni Magufuli aungwe mkono kwa afya ya taifa letu.
Kukubali makosa ni uungwana. Siyo Lowasa kawa Laigwanani ila kamsimika Laigwanani wa Africa Mashariki.
Nadhani ungeanza kwanza kuwalaumu ITV kwani nimeitoa huko huko na nakuomba Saa tano ( 5 ) usikose kuangalia marudio ya TAARIFA ya Habari ya ITV kisha utarudi kunihukumu kama nimepatia au nimekosea lakini kwa sasa kwangu huna HOJA na unanifanya NIKUDHARAU tu.
Laigwanani wa Dunia hiyoooooo !Hata hujafuatilia undani wa tukio la leo Edward Lowasa ashakuwa Lwaiganani wa EA na leo alikuwa anamsimika Laigwanani wa Tz
Mbona hicho cheo alipewa zamani sana mara tu baada ya kufukuzwa kazi ya uwaziri mkuu kwa mujubu wa Mzee Makamba. Alipewa cheo hicho kama faraja kwa yaliyomkuta. Sasa leo nikisikia tena kapewa hikihiki cheo nashangaa sana.Ama hakika Mwenyezi Mungu hamtupi mja wake.
Baada ya kuusaka kwa nguvu zote na udi na uvumba aliyekuwa Mgombea wa Urais kwa tiketi ya UKAWA na Waziri Mkuu ALIYEJIUZURU Edward Ngoyai Lowassa hatimaye leo amepata Cheo kikubwa cha KIKABILA ambapo sasa amekuwa ni LAIGWANAN wa Maasai wote Afrika ya Mashariki na hata wale Wamaasai waliopo ng'ambo / Ulaya / Majuu.
Pongezi zako sana Mzee Lowassa na angalau sasa utajikita zaidi katika kuwapa MAENDELEO Wamaasai wote. Waliokubeza kuwa huna Cheo chochote sasa aibu imewakuta na laiti wangejua kuwa Cheo cha LAIGWANAN ni Kikubwa nadhani wangeacha KUKUBEZA ila Sisi tunaojua hicho cheo tunasema safi sana na pambana.
Nawasilisha.