Mtoa mada umeongelea hili swala vzr sana, pongezi.
Nakubaliana na wewe kua hao mabinti wa vyuo kinachowasumbua ni utoto wa kutokujitambua baadae watakua wapi, makundi yenye vishawishi vya ajabu (coz mnakutana na tabia mbali mbali, sasa binti akiwa kichwa panzi, ndio anaendeshwa)
Wkt wakiwa pale wanachojua wao wanasoma wakimaliza watapata kazi maisha yatazidi kua mazuri,
Lkn kwa kua bado ni binti kila mwanaume anamtolea macho hvy hujiona hakuna kama yeye duniani na kuamua kuwapanga.
Matukio ni mengi sana kiukweli ila yote hua sababu ni hizo hapo juu,
So mnaweza kuwavumilia au mnaweza kuwaacha wamalize ujana mje muwaoe wakiwa makazini au wakiwa wanasota maisha nyumbani.
WordMain problem is that wengi ndio wanatoka advance secondary so wagen kwenye maisha ya kujitawala akili bado mbichi thn ww una invest kwenye akili mbichi.
Ukafa na kufufuka.... TyeheNilifanyiwa mazingaombwe na demu wa chuo hadi nikafa
ugomvi na nani tena?Tooba
Mbona waninunulia ugomvi![]()
hesabu kama unawajuanikuhesabie
Na my boougomvi na nani tena?
Kaazi kweli kweli.Nyie endeleeni na hao wana vyuo sisi wengine tuna deal na mama lishe, house girls, na watu wa kada hizo. Huko tutakuja na monopoly power
Wadau nawasalimu,
Nimeshawishika kuuliza hili swali baada ya mfululizo wa matukio mfano wa lile la SAUT ambalo si la kwanza kutokea katika vyuo vyetu lingine lilitokea chuo fulani hapa dar kati ya 2011-2012 ambapo binti alimwitia mwizi mpenzi wake wa siku nyingi ambapo alipigwa vibaya hadi marafiki wa binti walipoanza kupaza sauti kwa uchungu wakiiiambia ile mob iliyokua ikimpiga yule jamaa kuwa jamani huyo sio mwizi bali ni mpenzi wake
Wakaacha kumpiga akakimbizwa hospital na akafa upon arrival
Mob ile ilishikwa na hasira sana baada ya kuelezwa ukweli hasa zilipokuja taarifa jamaa kafa.Binti alishauriwa ahame chuo kwa usalama wake
Lakini cha kushtua zaidi huyu jamaa alikua ndio mfadhili mkuu wa huyu binti chumbani kwa binti kulichafuka kwa thamani na appliances mbali mbali kwa hisani ya huyu jamaa, hata hivyo msaada wa hali na mali aliokua akiutoa kwa binti huyo ndio uliotumika kumuhonga kijana mwingine wa chuo na siku ya tukio marehemu alikua amewafuma hotelini wakifundishana hesabu na ndipo akaamua kuwahi chuoni chumbani kwa binti kwenda kusomba mali zake alizomnunulia binti ikiwemo laptop, printer ndogo, music system tv set na vingine vingi, wakati akiendelea na zoezi la kuingiza vitu hivyo kwenye gari binti akafika na kumuitia mwizi.
Milolongo ya visa vya mabinti wa chuo kuwatendea unyama wafadhili wao ni vingi mno Ingawa sio vyote vinaishia kwenye kifo.Duce pia kati ya 2009-2010 kulitokea kisa cha namna hii ambapo kijana alifariki kwa kujichoma/kuchomwa kisu kwa utapeli wa mapenzi uliofanywa na binti wa chuo hicho hasa baada ya jamaa kupiga gharama za mnara wa matumizi aliokwisha kuujenga tangu binti akiwa first year.
2006 nikiwa bado sijaoa nilikwenda kumtembelea msichana wangu hostel kwake alipanga nje ya chuo hostel zilizotambuliwa rasmi na chuo, alipanga vyumba viwili self contained na ndani palijaa kila kitu friji ndogo chumbani kubwa sebuleni, dining table, sofa set ya nguvu kitanda cha kifahari na vingine vingi.Nilikua nakosa nguvu ya kumuuliza hivyo vitu alivitoa wapi wakati ni mwanafunzi na hana kazi hadi siku moja nilipopata majibu ya swali Hilo
Nilikua ndio nimemaliza chuo hivyo Sina kazi Nilikua naenda kushinda hapo nakula hapo na hata kulala hapo
Usiku wa manane tukiwa tumelala na binti baada ya kutoka kuangalia dunia kigeu geu live makumbusho, mfadhili mkuu wa huyu binti akafika na gari nje na kuja kugonga dirishani akimwasha binti amfungulie mlango nikamuuliza binti ni nani akajibu hata yeye hujui.Hakufungua mlango na jamaa nje akaanza kufoka kwamba nilijua tu una bwana mwingine na maneno mengi
Watu wakatoka na landlord akamuomba binti afungue mlango binti akafungua
Bila watu kuwepo tungeweza kuuana na yule jamaa.Jamaa alilia kwa uchungu akisema anasubiri pakuche alete canter abebe vitu vyake binti hakua remorseful at all na ikawa ndio mwisho wao kwa tabia ile nami nikabaki nae kama pambo tu mwisho nikaoa msichana mwingine na yeye pia ameolewa na jamaa mmoja Tegeta Nyuki na ametulia kabisa.
Sasa ni nini hasa kinawafanya mabinti wanapokua chuo wawe na mawenge kiasi cha kukosa utu?
Je sio wao labda ni umri?
Na kwa hali hii Je tunawashauri vipi wanaume wenzetu wanaowekeza kimapenzi kwa wasichana wa vyuo? Maana tumeona wazi kundi Hilo halina utulivu kwenye mapenzi, Ingawa sio wote lakini iwapo tukisema tuweke katika % inaweza kuvuka 50%
Kwa muktadha wa matatizo yaliyojitokeza kwa ujumla wake Je ipo haja ya kuwashauri wanaume wenzetu ambao bado hawajaoa na wanatafuta kuaandaa wenza wa maisha kuachana kabisa na kundi hilo la mabinti wa vyuo na badala yake waweke nguvu zao kutafuta mabinti waliokwisha kufika kazini? Ambao wameshafanya fujo zote na sasa wametulia na wanahitaji familia?
Karibuni kwa mjadawanaojiuza mkuu
Watu wanaoa hata wanaojiuza
hakuna kitu kama hicho.. Nastahili kuwa mmiliki pekee kwakoNa my boo![]()
We nawe!Nilifanyiwa mazingaombwe na demu wa chuo hadi nikafa
ndo manakeWe nawe!
Kwa hiyo unaandika ujumbe huo ukiwa umefufuka?