Kupasua Chungu na kufunga kwaajili ya kesi ya Ugaidi ya Mbowe kuna madhara kwa wasiotenda haki na vizazi vyao?

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
539
3,507
Kuna Jambo linasambaa kwa Kasi Sana kwamba wenzetu huko Kaskazini wanapasua vyungu pale wanapoona Jambo limekaa kinyume Cha haki ili miungu yao iangaike na wale walioshiriki aidha kuua, kuiba, kudhulumu au kumnyanyasa mtu mwingine.

Kwa wasimavyo Chungu uangaika na kizazi na hakichagui kabila Wala umri. Kwa mnaofuatilia kuna kipindi tuliona matangazo kwenye groups kuhusu kusudio la kupasua Chungu huko Moshi nadhani Tundulisu alipopigwa Risasi na serikali baada ya kusikia lile tangazo walielekeza wahusika wakamatwe na njia zifanyike kisipasuliwe.

Means wapo baadhi ya watu wanaamini kina madhara na kinaua. Swali langu, kwa kuwa Taarifa zinadai safari hii Kuna vyungu vimepasuliwa huko Moshi kwa ajili ya wale wanawatesa watuhumiwa na Ugaidi, je tunaamini kinaweza kuleta madhara?

Lakini kwa upande w pili ,wapo watu wameamua kufunga na kumwomba Mungu awaadhibu wanaohusika na uovu huu. Je tunaamini maombi yao hayatapokelewa? Je yakipokelewa Nani ataadhibiwa na Nani hatoadhibiwa?

Kama tunaamini Chungu na Kufunga Ni njia sahihi yakuangaika na wanaotesa wanadamu wenzao kwa kujitwalia mamlaka, kuna haja gani yakuangaika kumbembeleza kiongozi wa kisiasa au mtumishi wa Umma atende haki wakati tayari mitego yakumshughulikia asipotenda haki ipo? Na kwanini wanaopindisha haki wanatafuta laana kwa vizazi vyao?
 
Chadema mnahangaika sana!
Mlipofurahia Sabaya kufungwa kimizengwe sasa ni zamu ya mwenyekiti Mbowe.
Acheni mahakama ifanye kazi yake.
 
Chadema mnahangaika sana!
Mlipofurahia Sabaya kufungwa kimizengwe sasa ni zamu ya mwenyekiti Mbowe.
Acheni mahakama ifanye kazi yake.
Sabaya kafungwa kimizengwe ? Anatuhuma hadi za kutaka kumbaka msanii maarufu hotelini kwake achana na kesi za sasa, hio tu ilitosha kumtupa jela miaka 30.

Kwa nini magufuli alijiwekea kinga za kutoshitakiwa akitoka madarani kama hakuwa akitenda maovu.

Magu mwenyewe alikuwa na wasiwasi kuwa wayltu wangeweza mchenjia baada ya kutoka madarakani lakini mungu kamuokoa na jela akamwita milele.
 
Haya manbo ni magumu na sitaki kuamini Sana Kama Yana nguvu kwa wenye kusimamia haki, ila naamini tunapoteza maisha ya Viongozi wengi Sana miaka ya hivi karibuni kwa sababu ya mambo wanayofanya wabafamilia kwenye ulimwengu wa Roho

Wapo watu wanalia na Mungu na wapo wanaolia na mizimu. Duniani ni mara chache sana Viongozi waandamizi kufariki toka zamani Hadi Sasa, lakini siku hizi kwa Tanzania speed nikubwa Sana na kusahau kumekuwa kukubwa Sana kwa wanaochukua ofisi.

Viongozi wanaingia ofisini wakiwa na hofu ya Mungu lakini wanapokalia viti wanaingiwa na roho wakupenda viti kuliko kumtukuza Mungu, kwanini tuwe na Viongozi wakatili kwa Kasi hii inayoendelea Sasa? Kwanini watu wanaoumiza wenzao ndio wanateuliwa na kuchaguliwa kuwa Viongozi? Kwanini Hawa Viongozi wa kisiasa wanapokosea hakuna kiongozi wa dini anayekemea? Upofu unatoka wapi?

Lazima tukubali tumejiingiza kwenye mapambano ya mizimu na mazimwi na kila anayetaka nafasi lazima ajiunganishe na mizimu. Tusione Jambo la kawaida watoto wakafanya matendo yaleyale waliyotenda baba zao, tusishangae Viongozi kufa au watoa maamuzi kufa Bali tujiulize tulikosea wapi? Nini tufanye?
Ukiona mada Kama hizi zinaanza kujadiliwa maana yake watu wameanza kutafuta kila njia kupambana na wabaya wao na kwakuwa wanatamaduni zao basi wanatumia tamaduni zao kujilinda.

Naamini kila Kona ya nchi watu wanaangaika kwenye miungu kutafuta namna yakuwaondoa Duniani wale waliohusika kwa namna moja kuwaadhibu wapendwa wao.......mizimu nayo inafanikiwa kushughulika na nafsi za Viongozi wetu kwa sababu na zenyewe zimeunganishwa na mizimu. Mtu anateuliwa utasikia ameenda Tanga, ofisini anaingiza hirizi, anaabudu miungu watu Kama Hawa ofisi zao haziwezi kukosa laaana na kafara ni ibada zao.

Viongozi wa Dini mnanafasi kubwa Sana yakuokoa nafsi za Viongozi lakini pia kuponya nafsi zinazotaka kuanza kurejea kwenye miungu ikiwemo kupasua hivyo vyungu vinavyosema.

TUOMBE UPATANISHO NA MUNGU SIYO MIUNGU
 
Sabaya kafungwa kimizengwe ? Anatuhuma hadi za kutaka kumbaka msanii maarufu hotelini kwake achana na kesi za sasa, hio tu ilitosha kumtupa jela miaka 30.
Kwa nini magufuli alijiwekea kinga za kutoshitakiwa akitoka madarani kama hakuwa akitenda maovu.
Magu mwenyewe alikuwa na wasiwasi kuwa wayltu wangeweza mchenjia baada ya kutoka madarakani lakini mungu kamuokoa na jela akamwita milele.
 
Aisee chungu kinafanya kazi kwa asilimia mia moja. Ushauri kwa wahusika wote wanaojua ukweli juu ya shauri la Mbowe watafakari na wachukue hatua haraka sana
 
Kuna watu wanafunga novena kwa wote walioshiriki katika kesi ya mbowe isivyo haki.
Hakuna novela wala alovera mhalifu ni mhalifu mpaka pale mahakama itakapotoa hukumu Kama ana hatia au Hana hatia, nyie vunjeni vyungu matofali fungeni novela kunyweni alovera
 
Ni kweli chungu kinanuizwa tu kwamba kama Mboe anaonewa na wenzie basi kama chungu kinavyopaduka vipande na kuwa udongo vivyo hivyo kila mtesi wao na moyo wake ukapasukepaduke na kuwa udogo.

Halafu chungu hakiui wale watesi wakuu tu lakini hadi vizazi vyao vya kwanza hadi vya nne.

Jamani hebu tuhimizane kutendeana haki Mwenyezi Mungu anapendezwa na matendo ya haki anachukizwa na Uzalimu.
 
Tayari kuna mashahidi wa uwongo wana msiba,huku wengine wakiugua/kuuguza kwa siri.
Tutasikia mengi kadri muda unavyosonga.
Wapigweee🔥🔥🔥
 
Tayari kuna mashahidi wa uwongo wana msiba,huku wengine wakiugua/kuuguza kwa siri.
Tutasikia mengi kadri muda unavyosonga.
Wapigweee🔥🔥🔥
Doh kama ni kweli itakuwa ni hatari. Alafu vifo huwa vinatokea katika mazingira ambayo ni ya kawaida sana na unaweza ukasema ni natural causes kumbe chain ndio imeanza kutembea, na mkija kushtuka inakuwa too late..!
 
Hakuna novela wala alovera mhalifu ni mhalifu mpaka pale mahakama itakapotoa hukumu Kama ana hatia au Hana hatia, nyie vunjeni vyungu matofali fungeni novela kunyweni alovera
emoji23.png
emoji1787.png

Aisee chungu kinafanya kazi kwa asilimia mia moja. Ushauri kwa wahusika wote wanaojua ukweli juu ya shauri la Mbowe watafakari na wachukue hatua haraka sana
Alipokufa JPM waliwakamata watu waliokunywa bia na kufurahi leo wanarudia kosa lile lile Kama mbowe ni mkosefu muwe na amani hakuna baya litakalotokea Ila Kama mnamfix kisa kuendelea kukaa madarakani aminini Giza laja mpaka mtu wa mwisho ataguswa.
 
Alipokufa JPM waliwakamata watu waliokunywa bia na kufurahi leo wanarudia kosa lile lile Kama mbowe ni mkosefu muwe na amani hakuna baya litakalotokea Ila Kama mnamfix kisa kuendelea kukaa madarakani aminini Giza laja mpaka mtu wa mwisho ataguswa.
Blah blah blah
 
Ubaya wa chungu kama ni kweli anahusika yeye itarudi upande wake inanze kutafuna uko uko
 
Sabaya kafungwa kimizengwe ? Anatuhuma hadi za kutaka kumbaka msanii maarufu hotelini kwake achana na kesi za sasa, hio tu ilitosha kumtupa jela miaka 30.
Kwa nini magufuli alijiwekea kinga za kutoshitakiwa akitoka madarani kama hakuwa akitenda maovu.
Magu mwenyewe alikuwa na wasiwasi kuwa wayltu wangeweza mchenjia baada ya kutoka madarakani lakini mungu kamuokoa na jela akamwita milele.

Tuletee proof na sio story za vijiweni magufuli alijiekea kinga coz kuna watu aliowatumbua walitaka kummaliza. Na wamefanikiwa na baada ya hapo wakataka waue image yake
 
Haya manbo ni magumu na sitaki kuamini Sana Kama Yana nguvu kwa wenye kusimamia haki, ila naamini tunapoteza maisha ya Viongozi wengi Sana miaka ya hivi karibuni kwa sababu ya mambo wanayofanya wabafamilia kwenye ulimwengu wa Roho

Wapo watu wanalia na Mungu na wapo wanaolia na mizimu. Duniani ni mara chache sana Viongozi waandamizi kufariki toka zamani Hadi Sasa, lakini siku hizi kwa Tanzania speed nikubwa Sana na kusahau kumekuwa kukubwa Sana kwa wanaochukua ofisi.

Viongozi wanaingia ofisini wakiwa na hofu ya Mungu lakini wanapokalia viti wanaingiwa na roho wakupenda viti kuliko kumtukuza Mungu, kwanini tuwe na Viongozi wakatili kwa Kasi hii inayoendelea Sasa? Kwanini watu wanaoumiza wenzao ndio wanateuliwa na kuchaguliwa kuwa Viongozi? Kwanini Hawa Viongozi wa kisiasa wanapokosea hakuna kiongozi wa dini anayekemea? Upofu unatoka wapi?

Lazima tukubali tumejiingiza kwenye mapambano ya mizimu na mazimwi na kila anayetaka nafasi lazima ajiunganishe na mizimu. Tusione Jambo la kawaida watoto wakafanya matendo yaleyale waliyotenda baba zao, tusishangae Viongozi kufa au watoa maamuzi kufa Bali tujiulize tulikosea wapi? Nini tufanye?
Ukiona mada Kama hizi zinaanza kujadiliwa maana yake watu wameanza kutafuta kila njia kupambana na wabaya wao na kwakuwa wanatamaduni zao basi wanatumia tamaduni zao kujilinda.

Naamini kila Kona ya nchi watu wanaangaika kwenye miungu kutafuta namna yakuwaondoa Duniani wale waliohusika kwa namna moja kuwaadhibu wapendwa wao.......mizimu nayo inafanikiwa kushughulika na nafsi za Viongozi wetu kwa sababu na zenyewe zimeunganishwa na mizimu. Mtu anateuliwa utasikia ameenda Tanga, ofisini anaingiza hirizi, anaabudu miungu watu Kama Hawa ofisi zao haziwezi kukosa laaana na kafara ni ibada zao.

Viongozi wa Dini mnanafasi kubwa Sana yakuokoa nafsi za Viongozi lakini pia kuponya nafsi zinazotaka kuanza kurejea kwenye miungu ikiwemo kupasua hivyo vyungu vinavyosema.

TUOMBE UPATANISHO NA MUNGU SIYO MIUNGU
Ndio lile neno kwenye biblia sijui ni kitabu gani ,anasema " napatiliza wana maovu ya baba zao kizazi hadi cha nne,
 
Back
Top Bottom