Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 577
- 2,594
Ukuaji wa watoto hupitia hatua nyingi tangu kuzaliwa kwao. Mabadiliko haya huhusisha tabia na namna ambavyo mifumo ya mwili hufanya kazi.
Ukuaji wa watoto huwa haufanani, lakini wengi huanza kuota meno wakiwa na umri wa kati ya miezi 4 hadi 7. Tofauti na jinsi ambavyo wazazi wengi huamini, tendo hili la kiasili huwa siyo chanzo cha kuhara kwa mtoto.
Kwa Mujibu wa Taasisi ya National Library of Medicine ya Marekani, Kuhara ni matokeo ya uwepo wa ugonjwa mwingine au uwepo wa mazingira yasiyo salama yanayo mzunguka mtoto kwa wakati huo, hasa yale yenye uchafu.
Ifahamike kuwa wakati huu watoto huwa na hamu ya kula kila kitu pamoja na kusugua fizi zao maana huwasha, hivyo wanaweza kula uchafu wa aina mbalimbali ambao kwa mantiki nyepesi ndiyo huwafanya waanze kuhara.
Dalili za kawaida za kuota kwa meno ni
Hizi siyo dalili za kawaida, apelekwe hospitalini haraka kwa uchunguzi na matibabu.
Chanzo: National Library of Medicine (NLM)
Ukuaji wa watoto huwa haufanani, lakini wengi huanza kuota meno wakiwa na umri wa kati ya miezi 4 hadi 7. Tofauti na jinsi ambavyo wazazi wengi huamini, tendo hili la kiasili huwa siyo chanzo cha kuhara kwa mtoto.
Kwa Mujibu wa Taasisi ya National Library of Medicine ya Marekani, Kuhara ni matokeo ya uwepo wa ugonjwa mwingine au uwepo wa mazingira yasiyo salama yanayo mzunguka mtoto kwa wakati huo, hasa yale yenye uchafu.
Ifahamike kuwa wakati huu watoto huwa na hamu ya kula kila kitu pamoja na kusugua fizi zao maana huwasha, hivyo wanaweza kula uchafu wa aina mbalimbali ambao kwa mantiki nyepesi ndiyo huwafanya waanze kuhara.
Dalili za kawaida za kuota kwa meno ni
- Kuvimba na kulainika kwa fizi
- Hasira na kulia
- Kuongezeka kidogo kwa joto la mwili (homa ya kawaida)
- Kulazimisha kula kila kitu
- Kikohozi
- Kusugua fizi
- Kuweweseka
- Kung’ata na kuvuta chuchu wakati wa kunyonya
Hizi siyo dalili za kawaida, apelekwe hospitalini haraka kwa uchunguzi na matibabu.
Chanzo: National Library of Medicine (NLM)