Kumbe kuna sayari tunaweza kuishi kwa muda mrefu kuliko dunia

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Apr 28, 2020
710
1,426
Kumbe Dunia sio Sayari ambayo watu tutaweza kuishi kwa Muda Mrefu sana!!!

Dini Yetu _20250317_213858_0000.png


Utafiti mpya unaonyesha Dunia sio lazima iwe Sayari Bora katika ulimwengu wa Maisha ya binadamu hivyo watafiti wamegundua baadhi ya sayari 24 ambazo ni "zinazoweza kuheshimika", zinazotoa hali zinazofaa zaidi kwa maisha kuliko Dunia.

⭐ baadhi ya Sayari hizo zina Nyota nzuri zenye Mwanga kuliko jua ambalo linatupa Nishati na Mwanga watafiti walisema, utafiti mpya unaonyesha Kuna Ulimwengu mpya mkubwa zaidi wa kukuza maisha Yetu. Ni sayari ambazo zinapata Jua, joto mvua zaidi kuliko Dunia.

Dini Yetu _20250317_213515_0001.png


⚡Utafiti huo ulibainisha sayari 24 za "superhabitable". Zote ziko umbali wa miaka 100 ya mwanga, na kuzifanya kuwa ngumu kuzikaribia na kuziona kwa karibu, lakini utafiti na darubini za siku zijazo unaweza kutupa habari zaidi kuhusu ulimwengu huo.

Sayari moja wapo inaitwa super Earth Kepler -442B ambayo Ina ukubwa takribani mara 1.35 ya Eneo la Dunia, na kuifanya kuwa na ukubwa kuliko Dunia lakini Ina miamba TU.

Dini Yetu _20250317_213515_0002.png


Ni Sayari yenye miamba 1,206 sawa na miaka ya Mwanga kutoka Duniani na inayozunguka eneo linaloweza kukaliwa na nyota yake, ina alama ya 0.836. Dunia iko katika 0.829...!!!

Mwaka mmoja kwenye Kepler-442b ni takriban siku 112 za Dunia (takriban miezi 3.7).

Dini Yetu _20250317_213515_0003.png


Ni sayari nzuri kwa maisha wa binadamu kama tukiamua kwenda kuishi kwani ina ubora kuliko Dunia pia Sayari hiyo ni Sayari ambayo wanadamu wanaweza kuishi kwa Muda Mrefu kuliko Dunia.

#bongotech255 #sayari #superearth #kepler #dunia #planets #fahamu #future #explore #viral
 

Upo Sawa bro?
 
Hata iwe na mazingira bora kiasi gani kwa upande wetu hayo ni mapungufu tu na hatutaweza kumudu vizuri
Umesema hapo ni kubwa kwa 1.35 yaani ukitua hapo unakua unatembea kama umebeba begi la mchele kilo 35!
Jua zaidi nalo naona kama sio advantage, mionzi mionzi mionzi na nina uhakika kwa point hii pekee huko hakuna maisha
 
Yote hii ni katika kujipa moyo kuwa kifo kinakimbilika.... BABU UTAKUFA TU...! na hakuna kitu sayansi itakusaidia USIFE😅😅😅
 
Back
Top Bottom