Kuhusu mgogoro huu wa CUF, Bunge limekosa busara na weledi

Bunge ni chombo kikubwa katika nchi na ni sehemu ambayo hutumika kanuni na busara katika kuamua mambo yake. Mabunge mengi duniani hutumika kama nyenzo ya kutuliza hali pale inapochafuka hata pale muhimili mmoja unapochafua hali. Tumeshuhuidia busara ikitumika kwa kuielekeza serikali kutekeleza baadhi ya mambo ili tu kuondowa sintofahamu kwenye jamii ama baina ya serikali na wafanyakazi ama serikali na kundi fulani katika jamii.


Hili la mgogoro wa CUF bunge limetumika kufanya ushabiki sana na kukoleza moto. Wanajuwa kuna MGOGORO pale na kesi iko mahakamani hili wanalijuwa. Busara ingetumika kuhusu nafasi ya mgombea wa EALA kutoka CUF basi walau wangeiacha nafasi wazi mpaka mgogoro uamuliwe mahakamani.

Ilichokifanya Bunge letu la JMT kupitia Job ndugai na Kashilila ni kutaka kulidhalilisha Bunge letu mbele ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na tuonekane watanzania kuwa ni mbumbumbu. Hapana.

Tokea Mwanzo dalili zilishaonekana kuwakamia upinzani na kufanya siasa zisizo tija. Tunashindwa kujuwa wakati gani maslahi ya Taifa yatangulizwe mbele na wakati gani tufanye siasa. Ikiwa hapa Bunge linafanya zile siasa za kukomoana kwa wapinzani , wamesahau kuwa vyama hivi vina wanasheria weledi na yumkini suala litafika mahakama ya EAC. Itategemea maamuzi ya kisheria lakini naona tunaweeza kuadhirika kama taifa.

CUF inajulikana ilishamfukuza uanachama Habib Mnyaa tena kwa katiba ya CUF mamlaka hayo yako katika tawi lake huko mkanyageni Pemba. Na wala si CUF Taifa. Ikumbukwe pia kuwa Mnyaa alikuwa mwanaCHAMA WA KAWAIDA TU HAKUWA KIONGOZI AMBAYE TUNGESEMA YUKO KWENYE MGOGORO ULE ULIOPO WA KIUONGOZI. Hivi hili bunge letu hili wanalijuwa?

Kukimbilia kuwatambuwa eti wagombea wote wa CUF bila kusubiri kujuwa hatma ya maamuzi ya Mahakama ni kupoteza rasilimali na muda bure. Ikitokea kesi ya msingi ya mgogoro wa CUF ikaamua vyenginevyo dhidi ya Lipumba na genge lake bunge letu litasemaje kuhusu utoto huu waliofanya wa kukosa busara tena za kawaida?

Hawakumbuki kuwa ni juzi tu Mahakama imemzuiya Msajili kuwapa ruzuku CUF mpaka kesi ya msingi itakapoamuliwa iweje leo bunge lije likoleze mgogoro na kushindwa kutumia busara?

Tunawatakia kila la heri wateuliwa.


Kishada.
Jana ilinipa shida sana kuelewa CCM walikuwa wanatafuta uwakilishi gani!!??
Nilifikiri kilichokuwa kikitafutwa ni uwakilishi wa Tanzania ndani ya bunge la Afrika Mashariki,kwa nilichokiona ilikuwa kukomoana kati ya CCM na upinzania.
Honestry kama wabunge wa CCM wataendelea na upuuzi huu,hakuna hata haja ya kuwa na uwakilishi majimboni,ni upotevu wa pesa za walala hoi!!
Kwa nini tuhangaike na uvyama kwenye uwakilishi wa nchi? Busara,hekima na utaifa vinakosekana mpaka kwa spika wa bunge!!??
Inasikitisha, inatia hasira mpaka inafikia hatua unachukia nchi sababu ya kuwa tunahangaishwa na uvyama mpaka sehemu ambayo ni just kuangalia utaifa na kuweka kando upuuzi wa vyama.
Na itachukua miaka mingi sana kwa nchi yetu kwenda mbele mpaka hapo adui MKUBWA na nambari wani kuja kupotea ambaye ni UJINGA...kwa nilivyoona elimu yetu itaendelea kuwa ya chini ili wajinga tuendelee kuwa wengi na wenye dola yao waendelee kuishikilia. Kwa taifa lenye wananchi wenye uelewa sarakasi ya jana ilitosha kabisa kuwaadabisha watu.
Kwa nini????
 
Angalieni maslahi ya nchi sio maslahi ya seif. Cuf ni chama kizuri sana ila njaa zenu ndio zinaiua

Yaani wewe unachekesha. Kwamba watawala wanaihujumu CUf kupitia lipumba na kupewa sapoti zote . Hili bunge halikuwa na haja ya kujiiingiza kwenye mtego huu. Wengetumia busara tu na kupeleka taarifa EAC kusubiri mahakama kwa hili la CUF pekee tu. Sidhani kama kuna tatizo.

Lakini ......
 
Ndugu yangu Pohamba, kama hakuna kesi ya uanachama wa Habi Mnyaa basi alishakubariana na maamuzi ya chama ya kuvuliwa uanachama, maana kama angalikuwa amepinga basi angeenda mahakamani.

1) Msihamishe Magoli, Mwenzio alileta Taarifa kuwa kuna Kesi kuhusu Uanachama wa Mnyaa ni Jukumu lenu kwanza kufafanua Hilo badala ya kujigeuza ni wauliza Maswali tu!


2) Bunge likishapokea Barua ya Chama husika kuhusu Wagombea Kuna haja gani lianze kujiuliza kuhusu uhalali wa Mwanachama husika wakat huyo Mwanachama Jina lake limeletwa na Chama husika? Kuna Maswali Mengine hayahitaji kuuliza ilitosha kufikiri kwa robo dakika then unapata Jibu!
 
Pitia mada vizuri. Habib mnyaa ameshafukuzwa uanachama tawini kwake sio mwanachama huyo. Kupendekezwa na Lipumba na timu yake hakumfanyi awe mwanachama na tayari pingamizi lilishapelekwa BUNGE likakataa bila kujiridhisha.


Bunge limepokea Barua rasmi ya kumtambulisha Eng. Habib Mohamed Mnyaa kutoka kwa Mwnykt wa CUF Prof Lipumba na Kaimu Katibu Mkuu CUF Mh. Magdalena Sakaya , hivi ungekuwa Wewe ndie Katibu wa Bunge ungelikata Hilo Jina kuwa Sio Mwanachama kwa kutumia vigezo gani?

Assume Wewe ndio Katibu wa Bunge unamuandikia Barua Mwnykt na Katibu wa Chama husika kuwaambia kuwa mlietuletea sio Mwanachama wa Chama chenu!
 
HAYA MAJIBU NA ARGUMENTS ZA HUYU ANAYEJIITA "POHAMBA" INAKUWA KAMA VILE HUWA ANAFIKIRI NA KU-ARGUE KWA KUTUMIA MAT*K* -- a.k.a "MASABURI".
 
Bunge limepokea Barua rasmi ya kumtambulisha Eng. Habib Mohamed Mnyaa kutoka kwa Mwnykt wa CUF Prof Lipumba na Kaimu Katibu Mkuu CUF Mh. Magdalena Sakaya , hivi ungekuwa Wewe ndie Katibu wa Bunge ungelikata Hilo Jina kuwa Sio Mwanachama kwa kutumia vigezo gani?

Assume Wewe ndio Katibu wa Bunge unamuandikia Barua Mwnykt na Katibu wa Chama husika kuwaambia kuwa mlietuletea sio Mwanachama wa Chama chenu!

Mbona unashangza wewe kweli ndie Pohamba au ?

Hivi hujasikia na kufahamu kuwa wagombea wote hao wa Lipumba na sakaya waliwekewa pingamizi ? miongonio mwa hoja za pingamizi ni Mnyaaa kufukuzwa uanachama. BUNGE lingejiridhisha na hili kwanza kwa kuacha nafasi ya CUF wazi kutokana na mgogoro huo wa " Mnyaa" na Mamlaka ya uteuzi wa Mnyaa (Lipumba na Sakaya) na wenzao shauri liko mahakamani. Hujafahamu nini wewe ?

Hata hivyo Mnyaa alishafukuzwa uanachama wake na Tawi lake na pingamizi limepelekwa Bungeni na Mbunge. Sarakasi zikatumika Mnbyaa Kapitishwa bila ya kesi ya msingi kutajwa.

Halafu usiseme uongo ni wapi tuliposema kuwa Mnyaa ana kesi Mahakamani.?
 
Mbona unashangza wewe kweli ndie Pohamba au ?

Hivi hujasikia na kufahamu kuwa wagombea wote hao wa Lipumba na sakaya waliwekewa pingamizi ? miongonio mwa hoja za pingamizi ni Mnyaaa kufukuzwa uanachama. BUNGE lingejiridhisha na hili kwanza kwa kuacha nafasi ya CUF wazi kutokana na mgogoro huo wa " Mnyaa" na Mamlaka ya uteuzi wa Mnyaa (Lipumba na Sakaya) na wenzao shauri liko mahakamani. Hujafahamu nini wewe ?

Hata hivyo Mnyaa alishafukuzwa uanachama wake na Tawi lake na pingamizi limepelekwa Bungeni na Mbunge. Sarakasi zikatumika Mnbyaa Kapitishwa bila ya kesi ya msingi kutajwa.

Halafu usiseme uongo ni wapi tuliposema kuwa Mnyaa ana kesi Mahakamani.?


Una ukosefu wa Shule Wewe!

Ingekuwa rahisi hivyo Basi kila Siku Watu wangekuwa wanapeleka a Mapingamizi Bungeni, hata Mimi ningepeleka Barua ya Pingamizi ili tu Mtu fulani azuiwe.

Tambua Bunge linapokea Barua kutoka kwa yeyote lakin inafanyia kazi Barua rasmi kutoka kwa Mamlaka zinazotambulia KISHERIA

Utaratibu umewekwa wa kupokea Barua za uteuzi kutoka kwa Katibu wa Chama husika hii ikimaanisha Ofisi ya Katibu wa Chama ndio itakuwa na Jukumu la kuthibitisha Uanachama wa Mtu sio Bunge!

Bunge lilipaswa kupokea Zuio kutoka Mahakamni sio Barua toka kwa Mtu au Kikundi cha Watu, Kama Engineer sio Mwanachama sasa ni wakati wa hao waliopeleka Pingamizi Bungeni wapeleke Mahakamani!

Spika angemzuia Mnyaa kwa hoja ipi ikiwa Jina lake limeletwa na Kaimu Katibu wa Chama husika anaetambuliwa na Mamlaka za kisheria!

Jifunzeni Masuala ya kanuni mtaishia kulalamika kila Siku kuonewa! Yaani Waibuke Watu kutoka Vichochoroni na Barua ya kutomtambua Mtu halafu Wewe umzuie!!
 
Una ukosefu wa Shule Wewe!

Ingekuwa rahisi hivyo Basi kila Siku Watu wangekuwa wanapeleka a Mapingamizi Bungeni, hata Mimi ningepeleka Barua ya Pingamizi ili tu Mtu fulani azuiwe.

Tambua Bunge linapokea Barua kutoka kwa yeyote lakin inafanyia kazi Barua rasmi kutoka kwa Mamlaka zinazotambulia KISHERIA

Utaratibu umewekwa wa kupokea Barua za uteuzi kutoka kwa Katibu wa Chama husika hii ikimaanisha Ofisi ya Katibu wa Chama ndio itakuwa na Jukumu la kuthibitisha Uanachama wa Mtu sio Bunge!

Bunge lilipaswa kupokea Zuio kutoka Mahakamni sio Barua toka kwa Mtu au Kikundi cha Watu, Kama Engineer sio Mwanachama sasa ni wakati wa hao waliopeleka Pingamizi Bungeni wapeleke Mahakamani!

Spika angemzuia Mnyaa kwa hoja ipi ikiwa Jina lake limeletwa na Kaimu Katibu wa Chama husika anaetambuliwa na Mamlaka za kisheria!

Jifunzeni Masuala ya kanuni mtaishia kulalamika kila Siku kuonewa! Yaani Waibuke Watu kutoka Vichochoroni na Barua ya kutomtambua Mtu halafu Wewe umzuie!!

Unaendelea kujianika halafu unaamini kuwa wewe nawe ni msomi.

Yaani tatizo ni Bunge kuamuwa kujiweka upande Fulani(LIPUMBA na Serikali) katika mgogoro huu.

Barua za teuzi zimetoka pande zote mbili za CUF Original na CUF Lipumba na Bunge zote imezipokea na kuzikubali. Yanakuja mapingamizi kutoka pande zote mbili (Cuf Original na CUF Lipumba) Lakini unatupa mapingamizi na unachaguwa Upande wa Lipumba na mnyaaa wao. Halafu wanakuja wakina Pohamba wanajifanya wanajuwa kanuni.

kipi ni kipi hapo? Hivi bunge mpaka hatua hii ya mamlaka mbili tofauti za teuzi kwa jina la CUF kupeleka majina ya wagombea tofauti na mapingamizi tofauti huoni kuwa huo ni mgogoro? Hapa ndio nikasema Bunge limekosa Busara hujaelewa ? na ndio maana Bunge lilitaka wasawazishe hilo la mamlaka mbili za teuzi kwanza . Lakini tumeshangaa baadae walikubali na kuegemea upande wao.

Kesi iko mahakamani, Bunge linapoteza rasilimali na muda, wanaacha busara na akina Pohamba wanatoka povu.

Tutafika.
 
Unaendelea kujianika halafu unaamini kuwa wewe nawe ni msomi.

Yaani tatizo ni Bunge kuamuwa kujiweka upande Fulani(LIPUMBA na Serikali) katika mgogoro huu.

Barua za teuzi zimetoka pande zote mbili za CUF Original na CUF Lipumba na Bunge zote imezipokea na kuzikubali. Yanakuja mapingamizi kutoka pande zote mbili (Cuf Original na CUF Lipumba) Lakini unatupa mapingamizi na unachaguwa Upande wa Lipumba na mnyaaa wao. Halafu wanakuja wakina Pohamba wanajifanya wanajuwa kanuni.

kipi ni kipi hapo? Hivi bunge mpaka hatua hii ya mamlaka mbili tofauti za teuzi kwa jina la CUF kupeleka majina ya wagombea tofauti na mapingamizi tofauti huoni kuwa huo ni mgogoro? Hapa ndio nikasema Bunge limekosa Busara hujaelewa ? na ndio maana Bunge lilitaka wasawazishe hilo la mamlaka mbili za teuzi kwanza . Lakini tumeshangaa baadae walikubali na kuegemea upande wao.

Kesi iko mahakamani, Bunge linapoteza rasilimali na muda, wanaacha busara na akina Pohamba wanatoka povu.

Tutafika.


Mapingamizi huwa yanaanzia Mahakamani kwa kuiomba Mahakama izuie Habib Mnyaa asiruhusiwe kupigiwa kura Bungeni sio unakurupuka na ki Barua chako mbio mpaka Bungeni

Jukumu lako ni kutaja kipengele gani cha Sheria angekitumia au kinamtaka Spika Kupokea Barua ya kumzuia Mnyaa na kuifanyia kazi?

Mamlaka ipi ya Kisheria ilimjulisha Spika kuwa Ibrahim Lipumba Ana Kesi Mahakamni kuhusu Uenykt wake hivyo Hana Ruhusa ya kujishughulisha na Mambo ya CUF?
 
Bunge ni chombo kikubwa katika nchi na ni sehemu ambayo hutumika kanuni na busara katika kuamua mambo yake. Mabunge mengi duniani hutumika kama nyenzo ya kutuliza hali pale inapochafuka hata pale muhimili mmoja unapochafua hali. Tumeshuhuidia busara ikitumika kwa kuielekeza serikali kutekeleza baadhi ya mambo ili tu kuondowa sintofahamu kwenye jamii ama baina ya serikali na wafanyakazi ama serikali na kundi fulani katika jamii.


Hili la mgogoro wa CUF bunge limetumika kufanya ushabiki sana na kukoleza moto. Wanajuwa kuna MGOGORO pale na kesi iko mahakamani hili wanalijuwa. Busara ingetumika kuhusu nafasi ya mgombea wa EALA kutoka CUF basi walau wangeiacha nafasi wazi mpaka mgogoro uamuliwe mahakamani.

Ilichokifanya Bunge letu la JMT kupitia Job ndugai na Kashilila ni kutaka kulidhalilisha Bunge letu mbele ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na tuonekane watanzania kuwa ni mbumbumbu. Hapana.

Tokea Mwanzo dalili zilishaonekana kuwakamia upinzani na kufanya siasa zisizo tija. Tunashindwa kujuwa wakati gani maslahi ya Taifa yatangulizwe mbele na wakati gani tufanye siasa. Ikiwa hapa Bunge linafanya zile siasa za kukomoana kwa wapinzani , wamesahau kuwa vyama hivi vina wanasheria weledi na yumkini suala litafika mahakama ya EAC. Itategemea maamuzi ya kisheria lakini naona tunaweeza kuadhirika kama taifa.

CUF inajulikana ilishamfukuza uanachama Habib Mnyaa tena kwa katiba ya CUF mamlaka hayo yako katika tawi lake huko mkanyageni Pemba. Na wala si CUF Taifa. Ikumbukwe pia kuwa Mnyaa alikuwa mwanaCHAMA WA KAWAIDA TU HAKUWA KIONGOZI AMBAYE TUNGESEMA YUKO KWENYE MGOGORO ULE ULIOPO WA KIUONGOZI. Hivi hili bunge letu hili wanalijuwa?

Kukimbilia kuwatambuwa eti wagombea wote wa CUF bila kusubiri kujuwa hatma ya maamuzi ya Mahakama ni kupoteza rasilimali na muda bure. Ikitokea kesi ya msingi ya mgogoro wa CUF ikaamua vyenginevyo dhidi ya Lipumba na genge lake bunge letu litasemaje kuhusu utoto huu waliofanya wa kukosa busara tena za kawaida?

Hawakumbuki kuwa ni juzi tu Mahakama imemzuiya Msajili kuwapa ruzuku CUF mpaka kesi ya msingi itakapoamuliwa iweje leo bunge lije likoleze mgogoro na kushindwa kutumia busara?

Tunawatakia kila la heri wateuliwa.


Kishada.
Nilisikitika sana pale katibu wa bunge ndg Kashilila aliposema kuna CUF A na B niliumia sana. Swali langu ni hili Kashilila kaajiliwa na nani? Maana tangu Kikwete, Sijui kama Mkapa namsikia yeye tu. Unajua amejipa mamlaka makubwa sana, kiasi cha kujiona nae ni mungu mtu! Ila kwa spika sishangai najua ni mihula wake wa mwisho.
 
Mapingamizi huwa yanaanzia Mahakamani kwa kuiomba Mahakama izuie Habib Mnyaa asiruhusiwe kupigiwa kura Bungeni sio unakurupuka na ki Barua chako mbio mpaka Bungeni

Jukumu lako ni kutaja kipengele gani cha Sheria angekitumia au kinamtaka Spika Kupokea Barua ya kumzuia Mnyaa na kuifanyia kazi?

Mamlaka ipi ya Kisheria ilimjulisha Spika kuwa Ibrahim Lipumba Ana Kesi Mahakamni kuhusu Uenykt wake hivyo Hana Ruhusa ya kujishughulisha na Mambo ya CUF?

Tokea mwanzo nimesema BUNGE kwa kawaida hutumia kanuni na Busara kutatua jambo. Inafika wakati wanatengua kanuni kupisha busara ifanye kazi hili hulijuwi ?


Chombo kikubwa kama Bunge leo hii kinapelekewa Mapingamizi na pande mbili kwenye taasisi moja halafu wewe unahitaji kifungu ? hio sio busara.

Busara ni kutaka utatuzi kwanza na kujipa muda. Bunge isijifiche kwenye shamba la njugu. Kile kitendo tu cha kupokea teuzi mbili kwa jina la Taasisi moja ingetosha busara kujulisha kuwa kuna mgogoro. Ikiwa unasubiri uwekewe pingamizi na mahakama hio itakuwa si busara ni amri.

Kaka yangu/ ndugu yangu Pohamba tofautisha neno "Busara", "Kanuni" na "Amri"

Tuendelee kueleweshana kwa hekima.


Bunge letu hapa halikutumia busara na weledi.
 
Ni sawa sawa sophia Simba kua Mbunge wa Afrika mashariki

Si hivyo tu , Lakini eti ajitokeze JK ajiite Mwenyekiti wa CCM ,atambuliwe na barua ya msajili wa vyama, amtumie Makamba senior, awe Kaimu katibu Mkuu wa CCM , awatumie akina Sophia Simba na na yule Balozi wetu wa (Urusi sijui) wawe wajumbe wa Kamati kuu/ Baraza kuu la uongozi halafu wapeleke majina Bungeni kupendekeza wajumbe wa EALA, Spika wa Bunge apokee majina na kuyakubali pia apokee majina yaliyopitishwa na Kamati kuu ya JPM na kinanana. Uchaguzi uendelee na Sophia Simba atangazwe kuiwakilisha CCM vipi hapo ?

Nafikiri nchi ingekuwa imesimama muda huu kwa kuwekwa watu ndani na kupotezwa. Lakini kwa kuwa ni CUF ? kimya na ndio kwanza akina Pohamba wanahitaji kanuni.

Tutafika.
 
Back
Top Bottom