Kobe Motor yatoa zawadi kwa wateja wake

MZALENDO TZ

Member
Feb 14, 2012
9
124
View attachment Photo 01.JPG



Na Mwandishi Wetu

Kampuni ya kuuza magari yaliyotumika kutoka Japan ya Kobe Motor,imetoa zawadi mbali mbali kwa wateja wake ikiwa ni sehemu ya kuimarisha uhusiano na wateja pamoja na kusherehekea mafanikio yake.

Ikiwa ni moja kati ya makampuni makubwa ya Kijapan yanayoongoza kwa kuuza magari kwa ajili ya matumizi binafsi na ya kibiashara sehemu mbali mbali duniani,Kobe Motor tayari imeshauza magari zaidi ya 150,000 hapa Tanzania.

Akiongea wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na kampuni hiyo kwa wateja wake, mkuu wa kitengo cha masoko Ken Aoki alisema mafanikio ambayo kampuni hiyo imeyapata ni kutokana na wateja wake waaminifu.

“Leo tunajivunia kampuni yetu kutokana na ukubwa wake pamoja na uwezo wa kuwafikia maelfu ya wateja hapa Tanzania na sehemu nyingine duniani. Mafanikio haya tunayojivunia yamepatina kutokana na wateja hawa ambao leo tumejumuika pamoja kusherehekea mafanikio,” alisema mkuu huyo wa masoko.

Katika hafla hiyo ya chakula cha jioni, iliyoambatana na burudani mbali mbali,ilichezeshwa droo ambapo wateja wa Kobe Motor walijishindia zawadi mbali mbali kama simu za mkononi,tablet, komputa mpakato (lap top).

Mmoja wa wateja wa kampuni hiyo aliyejitambulisha kama Dallas Mulamba alisema amekuwa akikafanya biashara na Kobe Motor kwa miaka zaidi ya mitano na kwamba huduma bora za kampuni hiyo zimemsaidia kukuza biashara yake.

“Biashara ya kuagiza magari ina changamoto zake kwa kuwa unaagiza kwa kuona picha tu. Wakati mwingine picha hudanganya na makampuni yasiyo na uaminifu hutuma picha nzuri lkn gari likifika hali inakuwa tofauti. Lkn nikiagiza na Kobe Motor huwa sina shaka maana unachokiona kwenye picha ndicho utakachokipokea,” alieleza

Katika hatua nyingine hiyo ilitangaza kuwa imeanzisha huduma ya kuuza magari kwa mfumo wa mteja kutoa asilimia 35 ya thamani ya gari na kiasi kilichobaki anaweza kulipa kwa kipindi cha mwaka mmoja hadi miwili. Lengo la mpango huo ni kuwawezesha wateja wenye mahitaji ya magari lakini hawana fedha za kulipa mara moja kuweza kupata magari ya ndoto zao.

Mwisho…..
 
Back
Top Bottom