nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,860
- 5,801
JUMAPILI, JULAI 22, 2012 09:32 NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM
KAULI iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe kuwa kuna watu 11 wanayumbisha Serikali, ineonakana kuanza kumtesa.
Wiki iliyopita, Waziri Membe alitoa kauli hiyo, wakati akihojiwa katika kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na kituo cha televisen cha ITV cha mjini Dar es Salaam.
Baada ya kauli hiyo, MTANZANIA Jumapili, iliamua kuwatafuta baadhi ya wabunge ili kupata maoni yao, ambao walisema Waziri Membe ama hajui anakichosema au anatafuta maarufu wa kisisasa tu.
Wabunge hao, wameonyesha waziwazi kutoridhishwa kauli ya kiongozi ambaye ameshika nafasi nyeti serikalini.
Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM), alisema kitendo cha Waziri Membe kudai kuna watu 11 wanaiyumbisha Serikali, hakitakiwi kufumbiwa macho kwa kuwa kinagusa mamilioni ya Watanzania.
"Huyu Membe aache maneno, wiki hii alisema kuna watu anawafahamu wanahusika na mauzo ya rada, sasa anakuja na suala jingine la watu 11 wanaoyumbisha nchi, tumweleweje huyo… hajui kama yeye ni kiongozi aliyeshika nafasi nyeti serikalini,
"Kama kweli anawaelewa… kwa nini asiwataje, wananchi wanataabika halafu yeye anakuja na siasa zake…simwelewi, labda ninyi nao mwambieni awataje," alisema Mpina.
Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje (CHADEMA), alisema Membe anatafuta umaarufu wa kisiasa kwa kuwa ana kitu anachokitafuta.
"Huyu tumemzoea, kama unakumbuka hivi karibuni aliibuka na kusema awatambua wahusika wa rushwa juu ya ununuzi rada, lakini cha ajabu hawajahi kuwataja… sasa unafikiri anataka nini,
"Kama kweli hao watu wapo mbona ameshindwa kuwataj, atuletee majina…nadhani huyo amekwisha tambua kuna wenzake wanataka kumwamisha asigombee urais 2015… anapaswa kujitafakari kwanza," alisema Wenje.
Naye Mbunge wa Kinondoni, Idd Azan (CCM), alionyesha kutoridhishwa na kauli ya Waziri Membe na kusema hakumwelewa hata kidogo katika madai yake.
"Mimi nilimwangalia kwenye luninga akizingumza… nilipomsikia nilishindwa kumuelewa kwa sababu alichokuwa akisema hakiendani na madaraka yake.
"Sasa kama kweli anawajua watu hao, kwa nini asiwataje, atutajie ili hata wananchi waendelee kuimamini Serikali yao," alisema Azan.
Katika kipindi hicho, Waziri Membe aligusia mambo mengine, fedha za mkopo, Dola za Marekani milioni 20 zilizowahi kutolewa na Serikali ya Libya, enzi za utawala wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, hayati Kanali Muamar Gaddafi.
Alisema baada ya Serikali ya Libya kuikopesha Tanzania, nchi hizo zilikutana na kukubaliana fedha hizo zikopeshwe kwa kampuni yoyote itakayozihitaji.
"Baadaye Serikali ya Libya na Tanzania kukutana na kukubaliana fedha hizo zikopeshwe kwa kampuni yoyote itakayotaka kukopa izikope na makubaliano haya yako kwenye maandishi.
"Baadaye ikaja kampuni moja ya (Meize), kwa ajili ya kujenga kiwanda cha saruji kule Lindi na wakati wa kampeni tukawaahidi wananchi wa Lindi kwamba kiwanda hicho kitajengwa.
"Wakati tunaahidi hivyo, kumbe Kampuni ya Mohamed Enterprises, ilikuwa inashirikiana na ofisa mmoja wa ubalozi wa Libya ili apate fedha hizo na hapo ukawa ugomvi.
"Pamoja na hayo, mimi nilisimamia ili kuhakikisha kiwanda hicho cha saruji kinajengwa Lindi kama sehemu ya kumbukumbu yangu. Lakini baadaye wananunue wakabadilisha lugha, wakasema nimewapa marafiki zangu, jamani fedha hizi ni makubalino ya nchi mbili na mimi ni ‘share holder'.
"Sasa nakwambia fedha hizi ziko benki ya TIB, nendeni kwa meneja mkamuulize… huu ujinga gani huu unaozungumzwa, kwanza hata hizo Dola milioni 20 hazitoshi kujenga kiwanda bali zinatakiwa Dola milioni 60.
"Sasa nataka niwaambie wananchi wa Lindi, kwamba kiwanda cha simenti kitajengwa Lindi, hivi vituko vinavyotokea nitavigonga vyote … ipo siku nitawaanika wote, lazima watu hao wajue kwamba, ukikaa juu ya nyoka, ipo siku atakugonga tu.
"Hili nawaachia Watanzania waamue, lakini kuna watu 11 wakiwamo waandishi wawili wa habari, nitawatwanga kweupe, nyie suala la urais 2015 subirini tu, nitawaanika peupe bungeni tena kwa majina," alisema Waziri Membe.
Alipoulizwa kama atagombea urais mwaka 2015, alishindwa kuweka wazi msimamo wake kwa kile alichosema kuwa hajaoteshwa juu ya nafasi hiyo.
"Ole wao nioteshwe, ipo siku nitaoteshwa, najua nchi hii ina watu wanaoivuruga na hawataki kuona mafanikio, ukisema unataka kujivua gamba utaona wana uwezo wa kuchonga uongo, hao wanatumia vyombo vya habari kuchonga uongo.
"Kwa mfano, unawakaribisha vijana kama wa Chadema nyumbani kwako, unawapa chakula baadaye wanageuza mambo, we waache tu.
"Siku moja nitawatoa kwenye magazeti kila mmoja dozi yake, nitakuja kuwatandika kila mmoja na kinachoniudhi ni kwamba, hao watu wako ‘smart' wana fedha na wanataka kutawala hata kama hawana madaraka. Ukiona mtu anaanza kudharau wakati hana madaraka, ujue hapo kuna tatizo.
"Kuhusu uchaguzi unaoendelea ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), alisema chama hicho kina nafasi ya kujiimarisha kupitia uchaguzi huo.
Wiki iliyopita, Waziri Membe alitoa kauli hiyo, wakati akihojiwa katika kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na kituo cha televisen cha ITV cha mjini Dar es Salaam.
Baada ya kauli hiyo, MTANZANIA Jumapili, iliamua kuwatafuta baadhi ya wabunge ili kupata maoni yao, ambao walisema Waziri Membe ama hajui anakichosema au anatafuta maarufu wa kisisasa tu.
Wabunge hao, wameonyesha waziwazi kutoridhishwa kauli ya kiongozi ambaye ameshika nafasi nyeti serikalini.
Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM), alisema kitendo cha Waziri Membe kudai kuna watu 11 wanaiyumbisha Serikali, hakitakiwi kufumbiwa macho kwa kuwa kinagusa mamilioni ya Watanzania.
"Huyu Membe aache maneno, wiki hii alisema kuna watu anawafahamu wanahusika na mauzo ya rada, sasa anakuja na suala jingine la watu 11 wanaoyumbisha nchi, tumweleweje huyo… hajui kama yeye ni kiongozi aliyeshika nafasi nyeti serikalini,
"Kama kweli anawaelewa… kwa nini asiwataje, wananchi wanataabika halafu yeye anakuja na siasa zake…simwelewi, labda ninyi nao mwambieni awataje," alisema Mpina.
Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje (CHADEMA), alisema Membe anatafuta umaarufu wa kisiasa kwa kuwa ana kitu anachokitafuta.
"Huyu tumemzoea, kama unakumbuka hivi karibuni aliibuka na kusema awatambua wahusika wa rushwa juu ya ununuzi rada, lakini cha ajabu hawajahi kuwataja… sasa unafikiri anataka nini,
"Kama kweli hao watu wapo mbona ameshindwa kuwataj, atuletee majina…nadhani huyo amekwisha tambua kuna wenzake wanataka kumwamisha asigombee urais 2015… anapaswa kujitafakari kwanza," alisema Wenje.
Naye Mbunge wa Kinondoni, Idd Azan (CCM), alionyesha kutoridhishwa na kauli ya Waziri Membe na kusema hakumwelewa hata kidogo katika madai yake.
"Mimi nilimwangalia kwenye luninga akizingumza… nilipomsikia nilishindwa kumuelewa kwa sababu alichokuwa akisema hakiendani na madaraka yake.
"Sasa kama kweli anawajua watu hao, kwa nini asiwataje, atutajie ili hata wananchi waendelee kuimamini Serikali yao," alisema Azan.
Katika kipindi hicho, Waziri Membe aligusia mambo mengine, fedha za mkopo, Dola za Marekani milioni 20 zilizowahi kutolewa na Serikali ya Libya, enzi za utawala wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, hayati Kanali Muamar Gaddafi.
Alisema baada ya Serikali ya Libya kuikopesha Tanzania, nchi hizo zilikutana na kukubaliana fedha hizo zikopeshwe kwa kampuni yoyote itakayozihitaji.
"Baadaye Serikali ya Libya na Tanzania kukutana na kukubaliana fedha hizo zikopeshwe kwa kampuni yoyote itakayotaka kukopa izikope na makubaliano haya yako kwenye maandishi.
"Baadaye ikaja kampuni moja ya (Meize), kwa ajili ya kujenga kiwanda cha saruji kule Lindi na wakati wa kampeni tukawaahidi wananchi wa Lindi kwamba kiwanda hicho kitajengwa.
"Wakati tunaahidi hivyo, kumbe Kampuni ya Mohamed Enterprises, ilikuwa inashirikiana na ofisa mmoja wa ubalozi wa Libya ili apate fedha hizo na hapo ukawa ugomvi.
"Pamoja na hayo, mimi nilisimamia ili kuhakikisha kiwanda hicho cha saruji kinajengwa Lindi kama sehemu ya kumbukumbu yangu. Lakini baadaye wananunue wakabadilisha lugha, wakasema nimewapa marafiki zangu, jamani fedha hizi ni makubalino ya nchi mbili na mimi ni ‘share holder'.
"Sasa nakwambia fedha hizi ziko benki ya TIB, nendeni kwa meneja mkamuulize… huu ujinga gani huu unaozungumzwa, kwanza hata hizo Dola milioni 20 hazitoshi kujenga kiwanda bali zinatakiwa Dola milioni 60.
"Sasa nataka niwaambie wananchi wa Lindi, kwamba kiwanda cha simenti kitajengwa Lindi, hivi vituko vinavyotokea nitavigonga vyote … ipo siku nitawaanika wote, lazima watu hao wajue kwamba, ukikaa juu ya nyoka, ipo siku atakugonga tu.
"Hili nawaachia Watanzania waamue, lakini kuna watu 11 wakiwamo waandishi wawili wa habari, nitawatwanga kweupe, nyie suala la urais 2015 subirini tu, nitawaanika peupe bungeni tena kwa majina," alisema Waziri Membe.
Alipoulizwa kama atagombea urais mwaka 2015, alishindwa kuweka wazi msimamo wake kwa kile alichosema kuwa hajaoteshwa juu ya nafasi hiyo.
"Ole wao nioteshwe, ipo siku nitaoteshwa, najua nchi hii ina watu wanaoivuruga na hawataki kuona mafanikio, ukisema unataka kujivua gamba utaona wana uwezo wa kuchonga uongo, hao wanatumia vyombo vya habari kuchonga uongo.
"Kwa mfano, unawakaribisha vijana kama wa Chadema nyumbani kwako, unawapa chakula baadaye wanageuza mambo, we waache tu.
"Siku moja nitawatoa kwenye magazeti kila mmoja dozi yake, nitakuja kuwatandika kila mmoja na kinachoniudhi ni kwamba, hao watu wako ‘smart' wana fedha na wanataka kutawala hata kama hawana madaraka. Ukiona mtu anaanza kudharau wakati hana madaraka, ujue hapo kuna tatizo.
"Kuhusu uchaguzi unaoendelea ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), alisema chama hicho kina nafasi ya kujiimarisha kupitia uchaguzi huo.