Kati ya DED na DAS nani bosi wa mwingine?

DAS ana comand watu wachache directly lakini ni kama political post. DED anacomand wakuu wote wa idara japo yupo chini ya DAS kimantiki. Watumishi wote watamtii zaidi DED kuliko DAS
 
lakini kwa uhalisia DED ni kila kitu maana ndie mwenye mafungu ya maendeleo, mwenye miradi na pia watu. yaani kama katibu mkuu ndani ya wizara. DAS ni kazi ya ukaraani na umtumishi wa kisiasa. nimewahi kumkatalia mzee wa chama hii post ya DAS maana nilikuwa sina ajiara nikaenda kulia kwa mzee akaniniambia kuna nafasi ya DAS mkoa wa Nyanda za juu kusini baada ya kushaurina na wenye uzoefu wakaniambi kaka acha utumwa mwambie akupe ajira ktk shirika la umma au wizarani siyo huo utumwa. DAS hakipo katika muundo wa utumishi wa umma ni kama katibu tarafa tu.
 
Nimepata mkanganyiko kujua nani bosi wa mwenzake kati ya DAS na. DED naomba kuelemishwa mwenye kujua.

DED na DC wana ukubwa sawa ikiwa DED anaongoza team ya maendeleo ya serikali ya mitaa na DC ana own wananchi na maendeleo yao. Kwa nafasi ya uraisi wa wilaya DC anakuwa little above DED..

DAS ni msaidizi wa DC na mamlaka yake hayavuki kwa DED kwa namna yoyote ile unless anataka taarifa za maendeleo nk

Mara zote tumeona migongano kati ya DED na DC ila hutokuta mgongano kati ya DED na DAS

Kwa uelewa wangu mdogo i might be right... just sharing what i know
 
Mkuu nafikiri unamaanisha DAS. RAS ni Boss wa watumishi wote katika Mkoa including wa mashirika na Taasisi zote za Serikali na za umma.
Yap nilimaanisha DAS kama mtoa mada anavyolinganisha
 
Basi hiyo ni special case mkuu WILAYA MBILI kuwa na HALMASHAURI moja, BARAZA LA MADIWANI moja na MKURUGENZI kwa maana ya DED mmoja. Japokua kwenye pointi ya DAS naona bado tupo pamoja kwa maana ya kwamba DAS ni wa wilaya (wilaya moja, DAS mmoja) kama ambavyo idadi ya wilaya mbili ulizozitaja inavyokwenda sawa na idadi ya maDAS uliyoitaja pia.
Ndiyo DAS ni wa wilaya, mkurugenzi ni wa halmashauri.
 
Asante mkuu kwa maelezo yako.
Nimesoma neno kwa neno post zote toka post ya kwanza ya uzi huu nikitafuta majukumu ya DAS.
Mpaka hapa nimepata majukumu mawili tu. Kuwa DAS 1) ni Mshauri mkuu wa DC 2) Ni mkuu wa watumishi wote wa Wilaya
Ila hilo jukumu la pili limenichanganya...! Atakuwaje mkuu wa watumishi wa wilaya wakati hawawajibiki kwake ?
Kama kuna majukumu mengine naomba kufahamishwa tena kwa maelezo ya kina.
watumishi wa wilaya kwa maana ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya sio kwa upande wa DED.... Watumishi wa serikali kuu tu na sio wa serikali za mitaa
 
Kiprotoco DAS mkubwa na ndio maana anauwezo WA kusimamia maDED zaidi ya mmoja kwa Wilaya zenye Halmashauri zaidi ya moja.
DAS hana huo ukubwa.... DAS ni msaidizi wa majukumu ya DC.... Na ni mkuu wa Afisa Tawala (Wilaya), watumishi wa Ofisi ya mkuu wa wilaya na makatibu tarafa..... Hagusi file la mtumishi wowote wa Halmashauri wala hana mamlaka kwa DED

Mimi ni Afisa Utumishi Wilaya niko kwa DED
 
DAS ni mfanyakazi wa mkuu wa Mkoa.
DC ni mfanyakazi wa mkuu wa Mkoa.
RAS ni mfanyakazi wa mkuu wa mkoa.
DED ni mfanyakazi wa TAMISEMI ambaye yupo chini ya Halmashauri ya wilaya/manispaa/mji (council as a whole).
DED hawezi kuwa chini ya DAS wala DAS kuwa chini ya DED.
DED hawezi hata kuwa chini ya DC, wala RC au RAS. Hawamuhusu kihivyo, bali katika kuwapa ripoti.
DED anaweza kumweka mtu selo kama DC anavyoweza au RC anavyoweza. Haingiliani na DAS,

True and clear... hakuna ubishi... Ni kama Padri na shehe
 
Mmoja ni bosi wa wilaya mwingine ni boss wa halmashauri. Ndani ya wilaya moja panaweza kuwa na Halmashauri mbili lkn ndani ya halmashauri moja hapawez kuwa na wilaya 2. Obvious DAS kuna mahali anaweza kuwa juu ya DED japo kila mtu ana majukumu yake na hakuna anaye report kwa mwenzake
Kimuundo hakuna DAS kuwa juu ya DED.... DC anaweza kujaribu ama kujifanya yuko juu ya DED ila DAS no
 
Kwa dhana ya "Wilaya" dhidi ya "halmashauri," mimi nadhani DAS yuko juu kiitifaki kuliko DED kwa mchanganuo ufuatao:-

DAS ni mtumishi wa wilaya. (Wilaya moja, DAS mmoja).

DED ni mtumishi wa halmashauri (kwenye Wilaya moja kunaweza kuwa na halmashauri zaidi ya moja).

Kwa maana hiyo tunaweza kusema kwamba "Wilaya moja, DAS mmoja".

Na pia tunaweza kusema, "Wilaya moja halmashauri moja au mbili na hivyo DED mmoja au wawili"

Katika mazingira haya simuoni DED akiwa juu ya DAS.
kiitifaki DED anaweza kuwa chini ya DC but not DAS... DC na DED wana almost same rank... Ila DC ni raisi wa Wilaya ndio inammeza DED
 
Swali la msingi hapa ni.. Je kuna haja ya kuwa na DED pamoja na DAS kwa wakati mmoja? au nyadhifa mojawapo ingefutwa tu.
DAS Ni afisa Tawala Wilaya, huyu yupo kwa DC. DED, Ni mkurugenzi wa Halimashauri ya Wilaya.
Ni Mkuu wa alimashuri, wakuu wote wa idara huwajibika kwake.
 
Mfumo wa kuwa na DC, RC, RAS na DAS ulirithiwa kwa wakolonI na lengo la hawa viongozi lilikuwa kusimamia interest za kiongozi mkuu wa koloni enzi hizo au Governor kwenye majimbo husika. Hizi local government ziliundwa mahsusi kutoa nafasi kwa machief kuwasimamia watu wao chini ya usimamizi na miongozo ya DC na team yake.
 
Wadungu naomba nami nichangie mada hii ambayo wengi wanaona kama uhusiano wa DED na DAS ki-protokali unachanganya. Mchango wangu utazingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi.
1. Mkuu wa Wilaya (DC)
Mkuu wa Wilaya anateuliwa na Raisi kwa mujibu wa kifungu cha 13 (2) cha sheria ya Tawala za Mikoa (The Regional Adminstration Act, 1997). Majukumu yake ni pamoja na kuwa mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya. Kwa mantiki hiyo anakuwa muwakilishi wa Raisi katika kusimamia ulinzi, usalama na shughuli za maendeleo kwa ujumla. Akishateuliwa mkuu wa Wilaya anaapishwa na kusimamiwa kiutendaji na mkuu wa Mkoa (kifungu 13 kifungu kidogo cha 3).

2. Katibu Tawala wa Wilaya (DAS)
Kifungu cha 16 (2) cha sheria ya Tawala za Mikoa kinamtambua DAS kama principal adviser (yaani mshauri mkuu) wa DC. Kifungu hiki pia kinasema DAS anateuliwa kwamujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma. Bahati mbaya sina hiyo sheria hapa na nimetafuta mtandaoni sijaweza kuipakua. Ila natoa hoja yangu hapa kwa kuzingatia uteuzi wa Ma-DAS uliofanywa tarehe 5.8.2018 na Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma. Katika tangazo lake kifungu cha 1.2 Waziri alisema, "Leo nimewaita kuzungumza nanyi kuhusu Uteuzi na Uhamisho wa baadhi ya Makatibu Tawala wa Wilaya. Kwa mamlaka niliyokasimiwa kwa mujibu wa Sheria nimefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa Wilaya ili kujaza nafasi wazi kumi nane (18) zilizopo katika wilaya za Kinondoni, Mpwapwa, Dodoma, Iringa, Bukoba, Kigoma, Siha, Mtwara, Newala, Misungwi, Njombe, Kondoa, Manyoni, Kilindi, Chunya, Pangani, Bagamoyo na Handeni".
Hivyo, kwamujibu wa tangazo la Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma ambalo nimenukuu hapa, uteuzi wa DAS upo chini yake kisheria.

3. Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya (DED)
Kwa mujibu wa kifungu cha 22 (2) cha Sheria ya Utumishi wa Serikali za Mitaa ( The Local Government Service Act, 1982), DED anateuliwa na Raisi. Majukumu kiutendaji DED anakuwa Chief Executive wa Halmashauri na anaripoti kwa Katibu Tawala wa Mkoa (RAS).

Hitimisho
Kwangu mimi sioni mkanganyiko wowote wa kisheria kati ya DED na DAS, maana DED anateuliwa na Raisi na DAS anateuliwa na Waziri wa Utumishi wa Umma. Sema DAS anaweza kuonekana katika mazingira flani kuwa boss wa DED pale ambapo anatekeleza kazi anazotumwa na DC. Pia, nimewahi kuona mahala DAS anaudhuria vikao vya Council Management (CMT) ambavyo DED ndio mwenyekiti. DC ni mkuu kiitifiki kwa DED ingawa wote wanateuliwa na Rais, utofauti wao unatokana na majukumu. DC anapolinda amani, usalama na maendeleo ni pamoja na kazi anazofanya DED na wakuu wengine wa vyombo vya Ulinzi na Usalama kwenye ngazi ya Wilaya.
Huu ni uelewa wangu kwa kadri nilivyoelewa sheria husika, kama kuna mahala nimekosea niko tayari kukosoloewa maana mimi si mwanasheria kitaaluma. Asanteni
Mkuu, Umenukuu Kifungu cha 22(2) cha Local Government Service Act No. 10 of 1982 ambacho kinampa mamlaka Mhe Rais kuteua wakurugenzi ambao wapo kwenye Category VI to VII na wakurugenzi hao waliokusudiwa hapa ni wa manispaa na majiji (Municipal Directors na City Directors).

Hebu cheki na Kifungu kidogo cha 3 hapo chini yaani 22(3) utaona kuwa Waziri wa TAMISEMI ndiye mamlaka ya uteuzi wa Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya (DEDs) .

Hata awamu zilizopita, wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya walikuwa wakiteuliwa na Waziri wa TAMISEMI isipokuwa wale wa majiji na manispaa.
 
Back
Top Bottom