Karibuni kwenye Kazi ya ualimu, lakini usiwe na matarajio makubwa

Optimists

JF-Expert Member
Oct 17, 2021
374
1,068
Naongea kutokana na uzoefu kidogo, nineona kwenye interview vijana wakipanga mistari mirefu kupambania ugali wao, wengine wamekaa mtaani zaidi ya miaka 10, na bado wapo wanapambana kwenye usahili,

Utakapo pata nafasi ya kuingia kwenye ajira, Moja Kwa Moja na utakutana na watu uko kazini wakiwa wanawaza kuacha kazi, yaani wewe unapambana uingie utakutana na watu ambao wanataka waondoke, wakiwa na depression na mawazo tele, utakuta watu senior, wenye miaka 10 kazini wakiwa hawana nyumba, stress zikiwa nyingi mnooo, utashangaa kuona watu wakishinda na cadet mpauko, bado utakua uelewi elewi, utakaa miaka mitano bila ya kufanya jambo lolote la maana, hapo ndio utaanza kupata depression.

Nimeona vijana wengi wakisema tukishaingia tutafanya biashara au tutafanya kilimo, niamini Mimi kati ya walimu 10 waliofanya hivyo mmoja tu ndio alifanikiwa, kwasababu biashara au kilimo lazima uwepo wewe utajichanganya ufungue biashara alafu umuache mtu hapo ndio utakua Mwisho wako.

Huwezi Fanya jambo lolote la maendeo bila kukopa, mfano ukiingia na degree utakopesheka million 18, na mshahara utabaki na laki mbili au tatu, sasa inategemea hiyo million 18 umeipeleka wapi, kama umeenda kujenga chumba na sebule basi ndio mwanzo wa kuishi maisha ya kifukara maisha yako yoote. Ukiiweka kwenye biashara na umemuweka mtu basi ndio mwisho wako huo.

Kukosa matumaini ya uliowakuta kazini, na miaka yako mitano uliyofanya kazi bila kumiliki chochote, ndio kitakufanya uanze kuwaza kuacha kazi, kuvumilia mateso tena unajikuta umepangwa vijijini uko, au kigoma, sumbawanga, Rukwa n.k hapo ndio utatamani urudi tu uache kazi urudi mjini.

Ubaya wa hii kazi hakuna marupurupu au pesa za kuiba, alafu unyonge wa walimu wa miaka iliyopita ndio itasababisha Kila mtu akuchukulie poa tu, ukijitambulisha wewe ni mwalimu hakuna heshima Wala recognition ambayo utaipata kwa mtu yoyote yule.

Karibuni kwenye ualimu, lakini kama una ndoto miaka Yako 15 ya ualimu utazidiwa na mtu aliyeko TRA, TPA mwenye miaka miwili kazini.

Believe me, nioneshe mtu mwenye status yoyote Tanzania hii ambaye kasomesha mtoto wake ualimu.

Asante.
 
Pole sana mkuu,

Binafsi huwa naona kama una kazi haina kipato kizuri na haikupi muda wa kufanya vitu vingine au la wewe mwenyewe huwezi. Ni kheri ukae mikoani tena katika wilaya ndogo ndogo ambapo gharama za maisha zipo chini

Fikiria unalipwa laki nne au tano then unang'ang'ania kukaa Dar Es salaam na uishi kwa standard ya wafanyakazi wa, serikali. Lazma utakwama

Mungu awapiganie asee maana kwenye shughuli za kitaifa walimu wakishapewa posho, tshirt na ubwabwa wa kupangia foleni. Huwa mnasahau kabisa kupigania haki zenu
 
Pole sana mkuu,

Binafsi huwa naona kama una kazi haina kipato kizuri na haikupi muda wa kufanya vitu vingine au la wewe mwenyewe huwezi. Ni kheri ukae mikoani tena katika wilaya ndogo ndogo ambapo gharama za maisha zipo chini

Fikiria unalipwa laki nne au tano then unang'ang'ania kukaa Dar Es salaam na uishi kwa standard ya wafanyakazi wa, serikali. Lazma utakwama

Mungu awapiganie asee maana kwenye shughuli za kitaifa walimu wakishapewa posho, tshirt na ubwabwa wa kupangia foleni. Huwa mnasahau kabisa kupigania haki zenu
Sure, lakini Mungu akutuweka duniani kufanya vitu vidogo vidogo, Bora kupambana Mimi nipo humu ndani naowaona hawana matumani kabisa.
 
Naongea kutokana na uzoefu kidogo, nineona kwenye interview vijana wakipanga mistari mirefu kupambania ugali wao, wengine wamekaa mtaani zaidi ya miaka 10, na bado wapo wanapambana kwenye usahili,

Utakapo pata nafasi ya kuingia kwenye ajira, Moja Kwa Moja na utakutana na watu uko kazini wakiwa wanawaza kuacha kazi, yaani wewe unapambana uingie utakutana na watu ambao wanataka waondoke, wakiwa na depression na mawazo tele, utakuta watu senior, wenye miaka 10 kazini wakiwa hawana nyumba, stress zikiwa nyingi mnooo, utashangaa kuona watu wakishinda na cadet mpauko, bado utakua uelewi elewi, utakaa miaka mitano bila ya kufanya jambo lolote la maana, hapo ndio utaanza kupata depression.


Nimeona vijana wengi wakisema tukishaingia tutafanya biashara au tutafanya kilimo, niamini Mimi kati ya walimu 10 waliofanya hivyo mmoja tu ndio alifanikiwa, kwasababu biashara au kilimo lazima uwepo wewe utajichanganya ufungue biashara alafu umuache mtu hapo ndio utakua Mwisho wako.

Huwezi Fanya jambo lolote la maendeo bila kukopa, mfano ukiingia na degree utakopesheka million 18, na mshahara utabaki na laki mbili au tatu, sasa inategemea hiyo million 18 umeipeleka wapi, kama umeenda kujenga chumba na sebule basi ndio mwanzo wa kuishi maisha ya kifukara maisha yako yoote. Ukiiweka kwenye biashara na umemuweka mtu basi ndio mwisho wako huo.

Kukosa matumaini ya uliowakuta kazini, na miaka yako mitano uliyofanya kazi bila kumiliki chochote, ndio kitakufanya uanze kuwaza kuacha kazi, kuvumilia mateso tena unajikuta umepangwa vijijini uko, au kigoma, sumbawanga, Rukwa n.k hapo ndio utatamani urudi tu uache kazi urudi mjini.

Ubaya wa hii kazi hakuna marupurupu au pesa za kuiba, alafu unyonge wa walimu wa miaka iliyopita ndio itasababisha Kila mtu akuchukulie poa tu, ukijitambulisha wewe ni mwalimu hakuna heshima Wala recognition ambayo utaipata kwa mtu yoyote yule.

Karibuni kwenye ualimu, lakini kama una ndoto miaka Yako 15 ya ualimu utazidiwa na mtu aliyeko TRA, TPA mwenye miaka miwili kazini.

Believe me, nioneshe mtu mwenye status yoyote Tanzania hii ambaye kasomesha mtoto wake ualimu.

Asante.
20250131_160335.jpg
 
Back
Top Bottom