Pre GE2025 Kama madai ya uchaguzi huru na wa haki hayatekelezeki, tunafanya uchaguzi wa nini?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Elias Msuya

Member
Dec 23, 2011
15
37
Simbachawene...jpg

Hatimaye Serikali imekiri kwamba madai ya kuwa na uchaguzi ulio huru na wa haki hayawezekani kutokana na muda uliopo kufikia tarehe ya uchaguzi yaani Oktoba 25, 2025.

Mbali na wadau wengine, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimekuwa na madai ya kuwepo kwa mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi maarufu No Reforms, No Election' ili kuwa na uchaguzi ulio huru na wa haki.

Chama hicho kimeapa kuwa hakutakuwa na uchaguzi mwaka huu kama mabadiliko hayo hayatafanyika.

Akizungumza na waandishi wa habari Aprili 17, 2025 jijini Dodoma kuhusu mafanikio ya Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita, Waziri wa wizara hiyo, George Simbachawene alisema madai ya chama hicho kutaka katiba mpya kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu, hayatekelezeki kwa kipindi kilichobaki kuelekea Oktoba mwaka huu.

“Lakini msingi na jambo la maana hapa ni je, mawazo yao hayo yanatekelezeka kwa kipindi hiki na kama yanatekelezeka yana gharama kiasi gani kwa kuangalia muda, kuwashirikisha wananchi ili kuwapatia haki ya kuwashirikisha kwa sababu jambo linalogusa katiba haliwezi kuwa ajenda ya kikundi cha watu, haliwezi kuwa ajenda ya CCM peke yake au ajenda ya chama fulani peke yake ni lazima liwe ajenda ya Watanzania wote.

“Je, katika kipindi hiki ambacho katiba yetu inasema uchaguzi ni Oktoba tunaweza tukayafanya hayo yote ya kuwashirikisha wananchi wote kwa sababu ule mchakato wa katiba mpya ile ya wakati ule tulichukua mwaka mzima sasa tunaweza tukafanya hayo? Ni dhahiri mtu anapodai kitu ambacho hakiwezekani unajiuliza dhamira yake ni nini?” amesema Simbachawene.

>>>>>>>Msikilize Waziri Simbachawene hapa

Ni madai ya muda mrefu

Chadema imekuwa kufanyika kwa mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi ikiwa pamoja na kufanya marekebisho ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Katika maboresho hayo wanataka iundwe Tume Huru ya uchaguzi tofauti na hii ya sasa (INEC) ambayo viongozi wake akiwamo Mwenyekiti na makamu wake wanateuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM na ndiye mgombea wa chama hicho.

Hata uteuzi wa makashina wa tume hiyo pamoja na upatikanaji wa wafanyakazi wa tume hiyo wote ni watumishi wa umma wanaofanya kazi chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano ambaye ni mwenyekiti wa CCM. Hali hiyo hiyo haiifanyi tume hiyo kuwa huru.

Soma pia:
Uchaguzi ukiwa huru na wa haki

Madai haya yamekuwepo kwa zaidi ya miaka 30 tangu mfumo wa vyama vingi uliporejeshwa nchini mwaka 1992 na uchaguzi mkuu wa kwanza kufanyika mwaka 1995. Kumekuwa na madai ya kuwa na Tume huru ya uchaguzi, lakini yanapigwa danadana tu.

Kimsingi kulipaswa kuwa na mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ili kuweka uwanja sawa wa uchaguzi kwa vyama vyote kwa kuondoa nguvu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano kuingilia mfumo wa uchaguzi. Hilo CCM wamekuwa wakilikwepa miaka yote.

Ni Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete aliyeanzisha mchakato wa mabadiliko ya Katiba mwaka 2012 uliotarajiwa kutoa majibu ya muda mrefu ya kupatikana uwanja sawa katika uchaguzi, pamoja na mengine.

Lakini mchakato ule haukufika mwisho, kwani mwaka 2014 baada ya Bunge Maalum la Katiba kutoa Katiba inayopendekezwa kwa ajili ya kupigiwa kura, mambo ndio yaliishia pale.

Baada ya Rais wa awamu ya tano, Hayati John Magufuli kuingia madarakani, alifutilia mbali mchakato huo, akijikita zaidi kwenye miradi ya maendeleo. Lakini baada ya kifo chake, Rais Samia Suluhu Hassan, alirejesha matumaini ya utawala wa kidemokrasia kwa kuanza kufanya mikutano ya maridhiano na makundi mbalimbali vikiwamo vyama vya siasa, huku sera yake ya 4R (Reconciliation, Resilience, Reform and Rebuild).

Mbali na kikosi kazi alichokiunda kupitia Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Chadema pia walifanya mazungumzo na timu ya CCM kusaka maridhiano. Hata hivyo, mazungumzo hayo yalikwama, huku Chadema wakidai kuwa CCM walikataa mapendekezo mengi waliyopeleka.

Badala yake Serikali ilipeleka muswada wa Sheria za uchaguzi ikiwamo Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya 2023, Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (2023) na Sheria ya Vyama vya Siasa (2023), ambazo zilipitishwa.

Sheria hizo zimekuwa zikilalamikiwa kutojibu maswali ya kupatikana mfumo huru wa uchaguzi, kwani ili kupata mfumo huru wa uchaguzi ni lazima kwanza kufanya mabadiliko ya Katiba. CCM haikukubaliana tena hoja hiyo.

Leo, Waziri Simbachawene anaposema madai ya Chadema hayatekelezeki, maana yake ni kwamba: kwanza anakubaliana na hoja zao lakini tatizo muda wa kuzifanyia kazi hautoshi. Pili, huenda anamaanisha kuwa uchaguzi ujao ujao hautakuwa huru wala wa haki, ila inabidi upelekwe hivyo hivyo kwa kuwa muda hautoshi?

Kwa maana nyingine, kauli hii inaashiria kuwa Serikali inajua wazi kwamba uchaguzi hautakuwa huru wala wa haki, lakini inabidi upelekwe hivyo hivyo ilimradi CCM ishinde, kisha mambo mengine yaendelee.

Kama ni muda, Rais Samia alikuwanao wa kutosha kufanya mabadiliko tangu alipoingia madarakani Machi 2021. Isitoshe, hata kama angetaka kufanya hayo mabadiliko mwaka huu 2025 yangefanyika tu, suala ni nia.

Kutofanyika kwa mabadiliko hayo ni makusudi kwa lengo la kuilinda CCM. Ni mwendelezo wa danadana za Serikali kwa madai ya kupatikana kwa mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano yatakayoleta mfumo huru wa uchaguzi pamoja na mengine.

Leo Simbachawene atasema hivi, uchaguzi utafanyika, kesho atakuja mwingine atasema lake, ilimradi mfumo wa uchaguzi unazidi kuchakachuliwa kila unapowadia uchaguzi.

Soma pia Wanaopinga mabadiliko wanavyosema
 
Hayo madai ya tume huru na uchaguzi free and fair wameyakalia Kwa zaidi ya miaka 30 Kwa nia Ovu tu. sasa wana tofauti gani na uhaini wa Tundu Lisu?
Kama haki hawataki, ya nini kuendelea kukaa madarakani maana kutoa haki imekuwa kizungumkuti
 
Uchaguzi Tanzania ni kuhalalisha uchafu wa CCM

Basi yatumike maamuzi ya kikao Cha Dodoma za kumchagua Rais na Makamo
Waendelee na kuwaidhinisha wabunge Dodoma
Waende halmashauri kwa Madiwani
Wamaliziane waachane na kutudanganya Watanzania!!
 
Makosa ya Pilato
 

Attachments

  • TUJIFUNZE MAKOSA SITA ALIYOYAFANYA PILATO WAKATI WA HUKUMU YA YESU- Mhashamu Lazarus Vitalis M...mp4
    44 MB
  • TUJIFUNZE MAKOSA SITA ALIYOYAFANYA PILATO WAKATI WA HUKUMU YA YESU- Mhashamu Lazarus Vitalis M...mp4
    44 MB
Uchaguzi Tanzania ni kuhalalisha uchafu wa CCM

Basi yatumike maamuzi ya kikao Cha Dodoma za kumchagua Rais na Makamo
Waendelee na kuwaidhinisha wabunge Dodoma
Waende halmashauri kwa Madiwani
Wamaliziane waachane na kutudanganya Watanzania!!
Wajichagueee juu kwa juu....wasipoteze pesa na kuua raia kisa uchaguzi
 
Wajinga watakwenda kuwachagua viongozi wajinga wa ccm wanao hubiri Amani lakini wachukia Haki hadharani.
 
hata sisi wananchi hatuna haraka, wamuongezee RAIS mwaka mmoja ili reform ifanyike then twende kwenye uchaguzi ili watu waende kwenye uchaguzi na confidence ya uchaguzi huru na wa haki.

Hiyo tayari kengere ya tahadhari wameisikia, sasa wasisubiri matokeo mabaya ya chaguzi zisizo za haki, maana raia wakichoka wanaweza kumwaga damu.
Wote kama Watanzania tunahitaji chaguzi huru na haki ili tuweze kupata viongozi walio bora na si Bora viongozi.
 
Chaajabu CCM wanajitapa wana uungwaji mkono mkubwa huku wanaogopa uchaguzi huru na wa haki 😂😂
 
Hatimaye Serikali imekiri kwamba madai ya kuwa na uchaguzi ulio huru na wa haki hayawezekani kutokana na muda uliopo kufikia tarehe ya uchaguzi yaani Oktoba 25, 2025.
Huyu ni kondakta wa daladala aliyedondokewa na nafasi ya uwaziri. Hivyo haelewi chochote.

Kila akisimama jukwaani haaamini kama ndiye yeye alikuwa akikusanya nauli kwenye daladala
 
Back
Top Bottom