JF Karibuni Tanzania Professionals Network

Naitwa Sanctus Mtsimbe na naomba niungane na wana JF wengine waliojitambulisha kwa majina yao halisi na kutoa mwito wengine wafanye hivyo ili tuweze kuungana na kufanya mambo ya kimmsingi sasa yanayohitaji kufahamiana na kukutana.

Nimekuwa msomaji mkubwa wa JF toka mwaka 2007 na leo nimeona ni vema nami nijitokeze kuandika machache. Napenda kuishukuru na kuipongeza JF na uongozi na wanachama wake kwa kazi kubwa na nzuri manayoifanya katika kuleta changamoto mbalimbali.

Napenda kutoa mualiko rasmi kwa kuwakaribisha wana JF wenye mtazamo na mwelekeo wa kupenda maendeleo ya kweli kujiunga katika Mtandao wa Wanataaluma Tanzania (Tanzania Professionals Network, TPN). TPN ni mtandao unaowaunganiasha wanataaluma wa fani mbalimbali bila kujali nafasi au vyeo vyao ikiwa na madhumuni ya kuwezeshana Wanataaluma na Wananchi kwa ujumla kiuchumi na kifedha.

Kwa kuwa michango mingi ya Wana-JF ni kwa ajili ya maendeleo na ustawi wa Watanzania na Nchi kwa ujumla (Kitu ambacho TPN pia inafanya), karibuni sana tuweze kuungana na kuonana katika mikutano ya mara kwa mara ambayo ina lengo la kuboresha maisha yetu.

Kwa taarifa zaidi, tafadhali tembelea tovuti ya www.tpn.co.tz (Bado tovuti inaboreshwa . . . )

Na kama kuna ufafanuzi wowote unahitajika, tafadhali tuwasiliane kupitia barua pepe president@tpn.co.tz au +255-754-833-985.


Huyu Jamaa asituchanganye, maana naona hana sera, yeye a invite watu kisha anyamaze. Ikiwa usalama wa Taifa wamekosa mbinu za kujua wanaJF wanaolipua mabomu kwa ajili ya kuliokoa taifa lao ni akina nani ni bora atafute mbinu zingine na sio hii ya zama za mawe.

Haiwezekani nijitambulishe kwa jina langu kisha nimwagie upupu Fisadi Rostam au Lowasa kisha waniache. Hiyo TNP ni bora ukailekeza kwa Mafiosadi waliokutuma, sisi tuna professional body zetu kama NBAA au NBMM bado ziantufaa.
 
Kabla sijaendelea mbele Mtsimbe ningependa unifafanulie hiyo sentensi hapo. Maana ulipowakaribisha wana JF hukusema hivo. Hivi unadhani ya kwamba Wana JF wote ni Graduates? Ama tutafall under Honorary maana hata kwa corporate hatuingii.

Nangoja ufafanuzi!

Yaani, hata km Bill Gates angelikuwa Mtanzania, asingeliweza kujiunga na tovuti hiyo. Au kwamba wenye mawazo ya kimaendeleo ni "graduates" tu! FUNNY!!
 
Watanzania ni lazima tujifunze tabia ya "kupeana shavu". Tusiangalie tu jinsi sisi tutakavyonufaishwa na jumuiya bali pia tuangalie jinsi sisi tunavyozinufaisha jumuiya hizo.


I agree. Lakini isiwe ni kufanya mambo kwa kivuli cha 'kupeana shavu'.


Sijaona ubaya wa rais wa TPN kualika watu kujiunga na TPN, kwanini baadhi yetu tuna mawazo hasi kwa kila jambo linalotolewa bila hata kufikiri? Hivi ni lini watz tutajifunza kuwa negative thoughts kills, and will never take you anywhere! Huu ni wito wa hiari kabisa kama unaona kuna jambo halifai kuna njia za kistaarabu za kuuliza na wa kumuuliza amejitokeza na sio kumattach kila mtu, "After all not everything is for everybody", kama huu si uwanja wako kuna pengine pa kukufaa. Mambo mengine yanadhihirisha wazi upeo tulionao katika maisha, kumbuka " Being positive or negative are habits of thoughts,that have a strong influence in life"

Mimi pia sipendi mtu ambaye yuko too negative. Hata hivyo wakati mwingine ni vizuri kujipa muda kuelewa mawazo ya mtu mwenye mtazamo hasi. Jamii inahitaji watu wenye mtizamo hasi hali kadhalika wenye mtizamo chanya, and so is JF.


Mzalendo mwenzangu Zemarcopolo nashukuru sana kwa kututia moyo.

Kitu ambacho ni ningependa kuweka wazi ni kuwa TPN haiko pale kwa manufaa ya watu wachache au kikundi fulani cha watu. Kwa wale walio wanachama wanaweza wakahakikisha hili. Tumeona kutoka ndani ya TPN watu wakianzisha makampuni, Wengine wakipata kazi, wengine wakipata mikopo maalumu nk.

Najua Wanataaluma wengi wamekata tamaa kwa jinsi mambo yanavyokwenda kimaendeleo. Nia yetu wote ni kuangalia ni namna gani Wanataaluma tunaweza kuungana na kutumia fursa zilizopo kujiletea maendeleo makubwa bila kujitumbukiza katika siasa kama TPN na hatimaye kuleta maendeleo ya nchi.


I don't feel that way, sorry!

Hili jina "Tanzania Professionals Network" silipendi. Nina mashaka kuhusu members composition, mf. wangapi wanatoka mikoani? Kuna elements za ELITISM hapa.

Nilifuatilia kujua TPN ni nini na kwa nini mtu ajiunge. Nilichokiona hakifanani na unachokisema. Naamini TPN ilianzishwa kwa malengo mazuri, lakini nawaona ninyi kama bunch of people who joined kila mmoja akiwa na ka-mission kake kichwani. Halafu website yenu imekaa kisanii, I think you are withholding information.

Katika organisations zilizoko hapa Tanzania au nje ya nchi; ninyi tuwafananishe na organisation ipi?






.
 
Sanctus,

Shukrani kwa kuitumia JF kufikisha ujumbe. Kwangu hii inamaanisha unatambua kuwa JF inaweza kutumiwa pia kwa shughuli hiyohiyo ya kuwaunganisha wataalam wetu (nadhani nikiwemo mimi) kwakuwa JF si siasa tu pia tunaweza kuitumia kwa malengo tofauti tofauti.

Aidha, nakushukuru kwa ujasiri wa kufikisha hoja kwa hekima kubwa!

Mzalendo Mwenzangu Robot, nashukuru sana kwa kwa maneno yenye kuleta faraja. Kama nilivyosema awali, tunatambua kwa unyenyekevu mkubwa mchango wa JF katika kuwaruhusu wadau kutoa maoni yao kwa uhuru na uwazi wa hali ya juu. Kwa asili kila binadamu angependa azungumze alicho nacho bila ya kuzuiwa. Hakika hiyo pia ni haki ya kikatiba na hata pia ni haki ya kibinadamu inayotambuliwa na umoja wa Mataifa.

Tunawopengeza pia Waanzilishi na Uongozi wote wa JF (Nadahani Robot, wewe utakuwa mmoja wa Moderators).

Ni kweli JF si kuwa wanaongea siasa tu, nimeona kuna majukwaa mengi ambako kote kuna michango mingi tu na mizuri.

TPN ni mtandao wa hiari, na hata mualiko uliotolewa yeyote anao uhuru wa kuukubali au kuukataa. Ila tunashauri tu kuwa tuunganishe nguvu ili keleta maendeleo ya kweli katika nchi yetu. Tunaamini sana katika usemi wa "Umoja ni Nguvu".

Hatusemi kuwa TPN iko pefect, lakini wote tukishirikiana tunaweza tukaijenga vizuri sana na tukaitumia kuleta maendeleo yetu bila mizengwe, kwa ukweli na uwazi wa hali ya juu.

Napenda tena kukushukuru kwa maneno yako ya kutia moyo.
 
TPN inatofautiana vipi na vyama/asasi nyingine za kitaaluma kama TLS, TAA, ERB, TAMWA, TAWLA, NBAA,CPT, MEWATA, ... Au ndio katika zile jitihada za kila mtu awe na ka-NGO kake?
 
MTZ Mwenzetu umeeleweka,huo ni mwaliko ambao kila mtu ana hiari yake kwa utashi wake kuamua.
Kama hupendi, basi achana nao kuliko kutoa lugha isiyochujwa.Binafsi niliwahi kuwaona wakijieleza TBC1 Kipindi cha asubuhi cha Jambo Afica huyo MSIMBE na akina dada wawili,mmoja kiswahili kilikuwa kinampa shida kweli,anapendelea ngeli


LOL - Asante sana Single D, ni kweli kabisa mambo haya ya hiari huwezi kumalazimisha mtu kwa kuwa kila mtu ana utashi wake. Hata hivyo mkingano wa mawazo ni kitu cha kawaida katika jamii ya watu wenye mawazo na mitazamo tofauti. Kilicho kikubwa ni kuheshimiana na kushindana kwa hoja.

Ni kweli katika TPN tunao Wanataaluma wa kila namna, kuna wengine kuongea hawawezi lakini ni watendaji wazuri. Kuna wengine kuandika vizuri hawawezi lakini wanaweza kuongea n.k.

Nitamfikishia ujumbe huyo dada ambaye kiswahili kilkkuwa kinampa tabu . . . LOL
 
Nitakuja... Ngoja nione huko TPN kuna nini... Ila suala la kutumia majina halisi Mtsimbe sijajua una lengo gani haswa? Unawatakia Wapambanaji mema ama?

Kutumia hizi Alias doesn't mean watu ni waoga, hapana. Ni katika kuhakikisha yale ambayo tunashindwa kufanya tukilinda maslahi yetu na wale tegemezi kwetu yanakuwa wazi!!! Hata kama tunapambana na Wadhalimu kama Wazalendo, we gotta take care of our own! JF mwendo ule ule...

Nikitoka TPN ntawa na mengi!!!

Mzalendo Mzozo wa Mzozo, nilishajisahihisha kuwa ni vema bado watu kutotumia majina halisi. Lakini kwa wale wanaotaka kutoa michango yao kwa uwazi bila woga hilo pia si baya.

Binasi niliamua kujitambulisha kwa jina langu kwa kuwa nimetoa mualiko wa kuja kushirikiana TPN. Ilikuwa ni haki watu wajue kwa uhakika ni nani anayetoa mualiko huo, ili isije ikadhaniwa labda ni kitu cha kupandikiza tu.

Kwa hiyo ndugu yangu tuko pamoja na usiwe na wasiwasi. Nenda huko TPN na nategemea utakuja na mengi ya kuboresha . . .
 
Mtsimbe uko sawa rai yako ni endelevu na naiunga mkono.
Jamani kujumuika ni mwanzo, kuendelea kukaa pamoja ni hatua na kufanya kazi pamoja kama WANA TPN ni mafanikio.
Wamataaluma tumeanza kujumuika na sasa tuendelee kukaa pamoja ili tufanye kazi na hatimaye tufanikiwe.
BIG UP TPN founders, good idea.


Mzalendo Nyauba, karibu sana ndugu yangu. Hakika tukikaa pamoja tutafanikiwa nina uhakika na hilo. Takwimu za Mwaka 2002 zinaonyesha kuwa kuna takribani watu zaidi ya Millioni moja ambao wana elimu ya kuanzia Form IV na kisha kuendelea na mafunzo mengine. Pia inaaonyesha kuna takribani zaidi ya watu Laki Tano waliomaliza vyuo vikuu. Hakika ni mtaji mkubwa sana wa kuleta maendeleo.

Nimebahatika kuwa mjumbe wa Convocation ya Chuo Kikuu cha DSM. Katika Database nimeambiwa kuwa kuna Takribani registered graduates Elfu 40.

Kwa sasa TPN ina active partcipants zaidi ya 1000.
 
I don't feel that way, sorry!

Hili jina "Tanzania Professionals Network" silipendi. Nina mashaka kuhusu members composition, mf. wangapi wanatoka mikoani? Kuna elements za ELITISM hapa.

Nilifuatilia kujua TPN ni nini na kwa nini mtu ajiunge. Nilichokiona hakifanani na unachokisema. Naamini TPN ilianzishwa kwa malengo mazuri, lakini nawaona ninyi kama bunch of people who joined kila mmoja akiwa na ka-mission kake kichwani. Halafu website yenu imekaa kisanii, I think you are withholding information.

Katika organisations zilizoko hapa Tanzania au nje ya nchi; ninyi tuwafananishe na organisation ipi?

Nashukuru kwa hili maana nimetumia zaidi ya saa moja kupitia Website na majina yote kuanzia founding member na Members wengine lakini haijanipa muamko hata chembe. Haijanishawishi nijiunge [Vigezo sio tija].

Sasa sijui kama katika Mtandao kama TPN vita za wanaJF zitakubalika... Lazima watu kama Mizozo na Jmushi watatimuliwa tu...
 
Anonymity is what makes JF strong, loud and effective. It has shaken hills, mountains and craters because of this, its where people dare to talk openly and others find to know things openly. Sir Mtsimbe, I appreciate your role but you better find an alternative for your kind of invitation. JF doesn't fit your invitation, most of who brings sensitive cases would not like to be known in anyway, and we must keep this to keep JF strong and loud. It's very easy for someone smart to compare whatever somebody shares or goes mad in TPN and what anonymous member shares or goes mad in JF, this can easly reveal somebody's anonymous ID in JF, you sensitive JF members, be careful.
 
Kabla sijaendelea mbele Mtsimbe ningependa unifafanulie hiyo sentensi hapo. Maana ulipowakaribisha wana JF hukusema hivo. Hivi unadhani ya kwamba Wana JF wote ni Graduates? Ama tutafall under Honorary maana hata kwa corporate hatuingii.

Nangoja ufafanuzi!


Mzalendo Mwenzangu Mzozo, ukiangalia katika katiba ya TPN imeandika hivi juu ya members, nanukuu:

ARTICLE THREE

3.1 MEMBERSHIP.

Membership of the Organization shall be open to:

3.1.1 Individuals who is of sound mind and attained the age of majority who are interested in furthering the work of the Organization and who will be appointed and approved by the Executive Committee and who have paid for the registration fees and annual subscription laid down from time to time by the Executive Committee. Must be Tanzanian Graduates from Higher Learning Institutions within or outside the country with a POSITIVE ATTITUDE, and;

3.1.2 Any corporate or unincorporated association or body which is interested in furthering the Organization's work and that has been approved by the Executive Committee and has paid for the registration fees and annual subscription (any such body is being called in this constitution "member organization").

3.1.3 Honorary Membership given to other individuals, groups or Corporate which supports the Vision, Mission and Objectives of Tanzania Professionals Network.


Ufafanuzi:

Lengo kubwa la kwanza ni kuwaunganisha Wanataaluma wote tuwe na sauti moja katika mambo ambayo taaluma moja peke yake isingeweza kuyashughulika, huku Agenda kubwa ikiwa "Financial Empowerment and Wealth Creation for Professionals".

Kwa sasa katika nchi yetu tulikuwa na pengo kubwa kwa kuwa vyama vingi vya Kitaaluma vilikuwa vinashughulikia mambo yanayohusu taaluma zao. Sasa kwa kupitia TPN tunaweza kuwa na Agenda ya Pamoja "Cross-Cuttin Issues".

Lakini hii haina maana kuwa wasio graduates hawawezi kuwa wanachama kwa kuwa wote wanaingia kupitia katika 3.13. hapo juu.

Ukiangalia katika katiba ya TPN ambayo inapatikana katika Website ya TPN under Resource Centre (http://www.tpn.co.tz/download.html), tunayomadhumunini ambayo yanawalenga wengi ambao siyo lazima wawe graduates.

Hata hivyo kuwa Graduate peke yake siyo tiketi ya kuwa mwanachama, tiketi yako ni ile commitment yako ya kupenda maendeleo na kuwa na "Positive Attitude"
 
Yaani, hata km Bill Gates angelikuwa Mtanzania, asingeliweza kujiunga na tovuti hiyo. Au kwamba wenye mawazo ya kimaendeleo ni "graduates" tu! FUNNY!!

Mzalendo Tanzania 1, asante kwa angalizo lako. Tafadhali angalia katika jibu la msingi nililomjibu Mzozo wa Mzozo. Pia ukipata nafasi pitia Katiba ya TPN inapatikana http://www.tpn.co.tz/download.html.

Bila shaka ukipitia maelezo niliyotoa utagundua kuwa TPN inathamini mawazo yoye mazuri ya kimaendeleo.

Karibu sana kama utakuwa hujaridhika na jibu ili nitoe ufafanuzi zaidi.

Hata hivyo TPN na Katiba yake sio vitabu vitakatifu. Vinaweza kubadilishwa kufuatana na mahitaji ya wakati. Kama una mawazo mazuri au mbadala, tafdhali tushirikiane kama utapenda hivyo.
 
Mzalendo Mwenzangu Mzozo, ukiangalia katika katiba ya TPN imeandika hivi juu ya members, nanukuu:

ARTICLE THREE

3.1 MEMBERSHIP.

Membership of the Organization shall be open to:

3.1.1 Individuals who is of sound mind and attained the age of majority who are interested in furthering the work of the Organization and who will be appointed and approved by the Executive Committee and who have paid for the registration fees and annual subscription laid down from time to time by the Executive Committee. Must be Tanzanian Graduates from Higher Learning Institutions within or outside the country with a POSITIVE ATTITUDE, and;

3.1.2 Any corporate or unincorporated association or body which is interested in furthering the Organization's work and that has been approved by the Executive Committee and has paid for the registration fees and annual subscription (any such body is being called in this constitution "member organization").

3.1.3 Honorary Membership given to other individuals, groups or Corporate which supports the Vision, Mission and Objectives of Tanzania Professionals Network.


Ufafanuzi:

Lengo kubwa la kwanza ni kuwaunganisha Wanataaluma wote tuwe na sauti moja katika mambo ambayo taaluma moja peke yake isingeweza kuyashughulika, huku Agenda kubwa ikiwa "Financial Empowerment and Wealth Creation for Professionals".

Kwa sasa katika nchi yetu tulikuwa na pengo kubwa kwa kuwa vyama vingi vya Kitaaluma vilikuwa vinashughulikia mambo yanayohusu taaluma zao. Sasa kwa kupitia TPN tunaweza kuwa na Agenda ya Pamoja "Cross-Cuttin Issues".

Lakini hii haina maana kuwa wasio graduates hawawezi kuwa wanachama kwa kuwa wote wanaingia kupitia katika 3.13. hapo juu.

Ukiangalia katika katiba ya TPN ambayo inapatikana katika Website ya TPN under Resource Centre (http://www.tpn.co.tz/download.html), tunayomadhumunini ambayo yanawalenga wengi ambao siyo lazima wawe graduates.

Hata hivyo kuwa Graduate peke yake siyo tiketi ya kuwa mwanachama, tiketi yako ni ile commitment yako ya kupenda maendeleo na kuwa na "Positive Attitude"

Kamanda,

Kama ambavyo nimeandika mapema, ni kwamba nimeingia katika Website ya TPN na i have managed to download the entire site katika mashine yangu hapa ili niweze kupitia yaliyomo kwa ufasaha zaidi. Nimeelewa mengi na nashukuru kwamba naweza ku-qualify kuwa member kwa vigezo vyote ambavyo vimeainishwa na katiba.

Lakini inapokuja suala la kuelewa haswa TPN ni nini mtu akifungua website ya TPN sidhani kama atawaelewa. Website haijakaa katika mlengo wa kufikisha ujumbe ambao mtandao wa TPN unalenga kufikisha katika Jamii ya Tanzania. Kama sio member Website yenu pekee haitaweza tosha kunishauri niwe member.

Katika ule mualiko ambao uliwatumia Wana JF wote ni kwamba kitu kikubwa ambacho ulitakiwa kufanya ni kujaribu kuelezea TPN kwa lugha nyepesi ambayo nadhani hata wale wenye maswali magumu hapa JF wangekuelewa na kupata ufahamu juu ya TPN. Badala yake, kwa upande wangu mimi Post yako ya kwanza ilizua maswali mengi zaidi kuliko majibu na ndio maana kwa kuwa nina muda kidogo nikasema nidownload kila kitu husiana na TPN kisha niwasome na kuwaelewa. Lakini nani mwengine ana muda kama mimi?

Lakini nadhani utetezi uliotoa husiana na kwamba website yenu bado iko katika matengenezo zaidi kuiboresha nadhani yanaweza kukutetea katika hili. Lakini hata kama ipo katika matengenezo inabidi kuangalia ni ujumbe wa aina gani inafikisha.

Jambo la mwisho linalosikitisha zaidi, na hii ni kwa nafsi yangu mimi ni WEBSITE yenyewe ya TPN. Ni ya kisaniii mno. Hivi mmeshindwa ku-design a Proffessional looking website mpaka mkaamua kuja na site kama ile. Layout ya Site, na muonekano wake kwa ujumla umeshindwa potray image ya TPN. Na ndio maana watu wengi nina hakika wameishia kufungua page ya kwanza na kufunga hiyo site!

Ntarudi bado naendelea kupembua.
 
Mzalendo Lazy Dog;

Nashukuru kwa mchango wako.

Napenda kutoa ufafanuzi katika mambo ya kimsingi uliyoyaibua:

I don't feel that way, sorry!

Hili jina "Tanzania Professionals Network" silipendi. Nina mashaka kuhusu members composition, mf. wangapi wanatoka mikoani? Kuna elements za ELITISM hapa.


Kama nilivyosema huko nyuma TPN imeanza last year 29th July 2007, bado ni kipindi kifupi na mipango na changamoto ni nyingi. Mkakati uliopo sasa hivi ni kufungua Chapters Mikoani na nje ya nchi kazi ambayo inaendelea kufanyika. Kwa sasa tayari kuna Chapter Arusha, Tanga na punde Dodoma na Mwanza na tutaendelea mikoa mingine. Pia kuna uratibu unafanyika kuweza kufungua Chapters UK na USA na nchi zingine ambazo Wanataaluma wa Kitanzania wapo. Natoa wito kwa wale wenye nia ya kuunga mkono wa kufungua Chapters zaidi kufanya mawasiliano na TPN ili kulifanikisha hilo.

Nilifuatilia kujua TPN ni nini na kwa nini mtu ajiunge. Nilichokiona hakifanani na unachokisema. Naamini TPN ilianzishwa kwa malengo mazuri, lakini nawaona ninyi kama bunch of people who joined kila mmoja akiwa na ka-mission kake kichwani. Halafu website yenu imekaa kisanii, I think you are withholding information.

Tafadhali rejea katika katiba http://www.tpn.co.tz/download.html. Ni kweli kila mtu anaweza akawa na mission yake ya maisha, lakini lengo la ujumla la TPN limeelezwa. Pia hilo linaweza kuhakikishwa na mambo ambayo TPN imekuwa ikiyafanya mpaka sasa ambayo yako wazi kwa wanachama wote na mengine yanaonekana.

Kuhusu jina, lilipatikana baada ya Waanzilishi kubuni majina mbalimbali na hili kukubalika. Hata hivyo kama nilivyokwisha andika, bado TPN au katiba yake si vitabu vitakatifu. Hoja na Taaluma ndo zinazopewa kipaumbele. Karibu kama una mchango au hoja za kuboresha.

Kuhusu website, kama nilivyosema mwanzo bado inaboreshwa, unayoyaona katika website yapo mengine mengi ya ziada ambayo yanaweza kupatika na nina imani yatapatikana Website ikiboreshwa. Naomba tuvumiliane kwa hilo.

Katika organisations zilizoko hapa Tanzania au nje ya nchi; ninyi tuwafananishe na organisation ipi?

Kwa hili sijakuelewa na naomba ufafanuzi. TPN ni wazo lilitokana na Watanzania Wanataaluma Wenyewe bila kujali nje ya nchi kuna Organization gani tunayoweza kuifananisha na TPN.
 
Niliwahi kusoma hilo Tangazo la TPN, ila nilipoangalia muudo wa network yenyewe sikuridhika nayo. Katika dunia hii ya leo huwezi kuweka professionals wote katika nyumba moja ukatagemea la maana. Hebu kalisha pamoja professional wa hair style, professional wa boxing, professional wa kutibu magonjwa ya pua, professional dancer, professional wa kuendesha matreni, professional wa kutunza hesabu za fedha, professional wa kusanifu mitambo; unadhani wataongea nini.

Nadhani mlikuwa na maana ya professionals wenye digrii lakini pia bado haina maana yoyote; ninaiona hii TPN kama ni NGO fulani.
 
Naitwa Sanctus Mtsimbe na naomba niungane na wana JF wengine waliojitambulisha kwa majina yao halisi na kutoa mwito wengine wafanye hivyo ili tuweze kuungana na kufanya mambo ya kimmsingi sasa yanayohitaji kufahamiana na kukutana.

Nimekuwa msomaji mkubwa wa JF toka mwaka 2007 na leo nimeona ni vema nami nijitokeze kuandika machache. Napenda kuishukuru na kuipongeza JF na uongozi na wanachama wake kwa kazi kubwa na nzuri manayoifanya katika kuleta changamoto mbalimbali.

Napenda kutoa mualiko rasmi kwa kuwakaribisha wana JF wenye mtazamo na mwelekeo wa kupenda maendeleo ya kweli kujiunga katika Mtandao wa Wanataaluma Tanzania (Tanzania Professionals Network, TPN). TPN ni mtandao unaowaunganiasha wanataaluma wa fani mbalimbali bila kujali nafasi au vyeo vyao ikiwa na madhumuni ya kuwezeshana Wanataaluma na Wananchi kwa ujumla kiuchumi na kifedha.

Kwa kuwa michango mingi ya Wana-JF ni kwa ajili ya maendeleo na ustawi wa Watanzania na Nchi kwa ujumla (Kitu ambacho TPN pia inafanya), karibuni sana tuweze kuungana na kuonana katika mikutano ya mara kwa mara ambayo ina lengo la kuboresha maisha yetu.

Kwa taarifa zaidi, tafadhali tembelea tovuti ya www.tpn.co.tz (Bado tovuti inaboreshwa . . . )

Na kama kuna ufafanuzi wowote unahitajika, tafadhali tuwasiliane kupitia barua pepe president@tpn.co.tz au +255-754-833-985.

Wazo zuri, ila bado nina maswali kadhaa.

Kwa hiyo mtu yeyote anaweza kujiunga?

Hizi Missions and Objective zako nyingi na zimetapakaa mno kwa kweli, ni kama vile TPN lacks focus! Ni vigumu kutekeleza mambo yote hayo unayoyasema effectively.

What have you achieved so far?

Who are the stakeholders?
 
TPN inatofautiana vipi na vyama/asasi nyingine za kitaaluma kama TLS, TAA, ERB, TAMWA, TAWLA, NBAA,CPT, MEWATA, ... Au ndio katika zile jitihada za kila mtu awe na ka-NGO kake?

Mzalendo WildCard, TPN inao wanachama kutoka vyama mbalimbali vya kitaaluma, mfano tunao members ambao ni viongozi na wanachama wa LLS, tunao members toka chama cha Auditors, Wahasibu, Engineering Registration Board, Institute of Engineers, Chama cha Madaktari, Chama cha Waalimu, n.k. na hata asasi mbalimbali za kijamii.

Tofauti ni katika malengo na vision. TPN ina malengo makuu ya Financial Empowerment and Wealth Creation.

Najua kuwa tahadhari uliyoitoa hapo juu ya kila mtu kuwa na Ka-NGO kake ni ya kimsingi sana hasa kutokana na wimbi la wengi kumiliki NGO kama taasisi binafsi badala ya kuwa na picha ya kijamii. Napenda tu nikutoe wasiwasi kuwa TPN inaendeshwa kwa misingi ya uwazi na ukweli na kushirikisha wanachama wake na pia kutumia viyake mbalimbali.
 
Mimi nawapenda sana HakiElimu, kweli hawa wamekuwa ni mfano wa kuigwa.

.

Mzalendo Lazydog, ni kweli Hakielimu wanafanya kazi nzuri sana kama Watch Dog katika masuala ya Elimu. Ni matumaini ya TPN ambayo sasa hivi ina umri wa mwaka mmoja tu kuwa muda si mrefu nayo TPN iwe ni asasi ya kuigwa katika suala zima la Financial Empoernment and Wealth Creation. Tusaidiane kimawazo kuboresha.

Napenda kutumia quote yako unayoipenda kuwa "Africa must refuse to be humiliated, exploited, and pushed around. ...We must act, not just say words - Nyerere, 1973". Hivyo let us start ACTING now. If u you have any better idea, please share.
 
Back
Top Bottom