JF Beware: Upinzani si Uadui

Heshima mbele!
Mkuu Kitila asante kwa majibu mazuri, asante kwa watoa hoja wengine. Mimi yangu ni machache tu. Siamini kama kweli tumefika mahali tunasema tumeishiwa kiasi hichi na kusema kuwa hatuna cha kujitete au hata kuweka kitu mezani. Mimi ni Mtanzania na nitakufa na utanzania wangu:

1. Tanzania haiwezi kuendelezwa na wageni:
Tokea uhuru tulijua hili na tukajipanga vizuri kujiendeleza. Heshima yetu ilikuwa ni kupambana na umaskini ujinga na maradhi. Hizi ni sera murua na imara. Sitazungumzia azimio la Arusha, ila nitasema kuwa hatuwezi kuwa na sera bora yenye vipaumbele zaidi ya hivyo. Tatizo letu siku hizi tumekuwa watu wa tofauti sana. Tumeahirisha kufikiria na kuwa wepesi wa kuchukua sera zinazoitwa bora kwa vigezo vya wakubwa zetu. Kwa lugha ya Kitila ni Umalaya wa hali ya juu. Hivi kweli jamani tunaweza kuambiwa shida yetu na watu wengine? Hivi ukiumwa mguu kwa kiatu kukubana, maumivu unayoyasikia anaweza kuyajua mwingine kweli? Hivi tumekuwa fukara wa fikra kiasi hiki? Halafu anajitokeza mkuu wa nchi anasema tatizo letu ni kuwa hatuna wasomi/wataalaum wa kutosha! Mimi ni msomi na mtaalamu katika eneo langu, naomba nisihesabiwe kwenye kundi la wataalamu uchwara aliowataja mkuu wetu.

2. Ni kufilisika kimawazo kuamini kuwa ngome ya jeshi la marekani ni maendeleo kwetu.
Mimi siamini kama watoa hoja walikuwa wanamaanisha au wanatania. Kweli sijui imani hiyo wameitoa wapi. Jamani ngome ya wamerekani ni kwa ajili ya maslahi yao tu, hayatuhusu kiuchumi. Kama tunataka kweli kutengeneza ajira za maana kwa watu wetu, njia iko wazi za kiuchumi siyo hii! Kama tunakubali ngome hiyo iwe kwa sababu nyingine lakini siyo imani kuwa tutapata ajira kwa watu wetu.Hivi hatujifunzi kuwa uwekezaji uchwara ni sababu mojawapo ya sisi kubaki na nakisi ya fedha na kufilisiwa kirasilimali? Tuamke jamani na tujadili mustakabali wa taifa letu.

Ama kweli hoja ya Kitila ya nguzo na maadili ya kitaifa inajidhihirisha kuwa ya lazima. Tazama leo tunatetea ngome ya wamareakani kwetu eti kwa hoja ya ajira! Naomba wengine wasitusikie, maana itakuwa haki yetu kupigwa mawe.

Hivi kutoa mfano wa watanzania wanaofanya kazi ubalozi wa marekani kama mfano si ni kujitukana mwenyewe! Naomba tujenge hoja za lutengeneza ajira za kudumu na zenye staha kwa watu wetu ili tuendelee. Tukimeza kasumba ya kudhani kuwa wazungu wana uwezo zaidi, akili zaidi na kwa hiyo ni watu wazuri zaidi tutaumia. Mimi nasema tujenge uzalendo. Hivi kuna mtu anaweza kujenga hoja ya kukubali upuuzi kama ule wa mtafiti mzungu? Mimi naungana na Kitila, wakati nafanya utafiti wangu nilipata wakati mgumu sana wa kuonyeshwa nyaraka ambazo si za siri. Mpaka nikashtaki mahakamani na kupewa am,ri ya mahakama (Court Order) kuwalazimisha watu wa serikali waniruhusu kuziona nyaraka hizo. Tena hata siyo za siri.

Ukweli ni kwamba maendeleo siyo uchawi na tunaweza bila wazungu.

Heshima mbele!.
 
Son of the Soil:
Usidhani kuwa watu wanaotetea kuiuza nchi kwamba wanatania. Tutajuta sana kuwanyamazia hawa watu, na kujikuta kweli tumeingizwa jangani. Hawa watu wanaodiriki hata kukufuru ,eti Iraq sasa wanayo nafuu kwa ajira wanazozipata, na kwa hiyo na sisi tunastahili ajira hizo hawatanii, pamoja na kwamba utadhani maisha magumu yanayowakabili waIraq lingekuwa fundisho kwetu sote. Nadhani wengi wa hawa wanataka kazi za ukarimani.

nilikuwa Uingereza wakati mmoja miaka ya themanini wakati Namibia wanakaribia Uhuru wao. Nilitokea kukutana na wanafunzi kadhaa waliotoka Namibia, na kujitambulisha kwao nikitarajia kwamba watafurahi kukutana na ndugu yao ambaye kwao ndio maskani makuu ya SWAPO yalipokuwepo. Nilisikitika sana nilipoambiwa kwamba Tanzania tuna kihelehele cha nini kuwapelekea vurugu nchini mwao. Wao walikuwa wameridhika kabisa na maisha chini ya utawala wa Kaburu.

Kwa hiyo haya tunayoyaona na kuyasoma humu hayanishangazi sana. Kuna baadhi yetu hatuoni zaidi ya matumbo yetu.
 
Nilikuwa nimepumzika lakini naona kuna haja ya kujibu hoja zako:
1. Mwaka 2004, Ahmed Khalfan Ghailani alikamatwa Pakistan. Ghailan alikuwa anashukiwa kuhusika katika mabomu yaliyolipuliwa Dar es Salaam na Nairobi na kiongozi katika Al Qaeda.

Heshima mbele mkuu, Al Qaeda walipopiga mabomu Kenya na Dar, kulikuwa na base ya US? au? Kama hazikuwepo hizo base, inakwambia nini kuhusu mission ya Osama? Ni kwamba yeye hupiga anywhere kwenye interest ya US, bila ya kujali base ipo au haipo!

2.
Ni ukweli Kwa kuweka base unaingia katika ulingo wa mapambano ya kivita na si ya kidiplomasia. Angalia waSaudi wanavyohangaishwa na watu wanaopinga kuwepo kwa askari wa kimarekani pale.

Osama, ni rafiki mkubwa wa watwala wa Saudia, na ni hao hao wanaompa misaada ya kuweza kuishi mpaka leo, wanaowasumbua huko Saudia sio Al Qaeda, isipokuwa ni wananchi waliochoshwa na utawala wa kifalme, na walikuwa wakiwasumbua hata kabla base ya US haijawekwa kule, na hata siku moja hawajawahi kudai base iondoke wanachodai ni mabadiliko ya katiba na utawala, kama umesoma historia ya Osama, ni kwamba at one time utawala wa huko ulimkamata na kusihia kumfukuza nchi na kumtoa uraia huku wakimruhusu ahamie Sudan, enzi hizo base ya US haikuwepo huko Saudia mkuu!


3.
Sisi tuna uwezo wa kupambana nao, au tutategemea kuwa mmarekani atatulinda kwenye hili?

Mkuu wangu uwezo tunao tena mkubwa sana, ndio maana tulimng'oa Amin mpaka Kampala na kumfukuza nchi yake mwenyewe, usalama wetu unaaaminiwa sana duniani, at onetime tulikuwa very close na Mossad, kwa efficiency katika usalama, hatuhitaji msaaada wa mtu yoyote kujilinda!


4. .
Huko Okinawa vitendo vya kubaka vya baadhi ya askari wa Marekani(askari 3 waliwahi kumbaka binti wa miaka 12, n.k)vimeongeza kelele za wanachi dhidi ya Base hiyo. Askari wa marekani wanalindwa na sheria ya SOFA inayomzuia prosecutor wa kijapan kumkamata askari wa kimarekani hadi kesi hiyo ifike mahakamani. Huko ni Japan, na hawana imani na vyombo vya sheria vya huko, sembuse kwetu! Si watadai immunity kama ile ambayo ipo Iraq. Mtoto wako akibakwa, wewe ulie tuu!

Hivi mkuu, Mzee Maumba alipokuwa akibaka watoto hapa bongo alikuwa ametokea kwenye base ipi ya US? Yaaani unataka kusema watoto wanaobakwa hapa bongo kila siku huwa wanabakwa na wananchi kutoka base ya US? Kwa hiyo Nguza na watoto wake nao walitoka base ya US? Hayo ya imunity ni makubaliano kati ya nchi na nchi, askari wa ki-Jap wakikamatwa kule Us nao hawataguswa pia, hayo ya Iraq sidhani kama ni kweli maana tunajua kuwa ni majuzi tu askari wa US wamefungwa jela kwa ku-rape Iraq, na wengine sasa hivi wanasubiri kesi zao, lakini kubaka sio lazima kuwe na base ya Us, yaani wananchi walioko kwenye jela zetu kwa kubaka wote wametoka base za US? Kuhusu imunity Japan kama haitaki inaweza kuvunja huo mkataba anytime, kama vile walivyo-pull majeshi yao kule Iraq! Hakuna anyewazuia, lakini tatizo la ubakaji halisababishwi na base ya US tu!

5.
Hali yetu ya umaskini itatupelekea pale panapotokea maonevu, tuvikubali vile visenti tutakavyotupiwa. Angalia matajiri wetu mkweche wanavyotamba na vidola vyao, itakuwa hao wanaotoka zinakotengenezwa?

Ukiwa masikini ukatulia na umasikini wako, hutaguswa na mtu yoyote, lakini ukihitaji msaada wa tajiri, huna njia ila kumtumikia tajiri upate mradi wako, ipi bora vijana wetu kuzamia huko majuu kufanyishwa kazi kama punda kwa ujira mdogo, huku wakinyanyaswa kama mbwa kwa kutokuwa na papers, au kuwakubalia wenye nguvu waje hapa hapa bongo na kutupa ajira?

3.
Wafilipino walikataa kuongeza lease ya Base za Subic na Clark kutokana na wamarekani kukataa kusema kama wanahifadhi silaha za nuklia kwenye base hizo au laa! Je sisi tutakuwa na ubavu wa kuuliza hilo? Na je wakiamua kuihamishia Gutanamo hapa ili wawafungie waafrika waliowakamata, tutaweza kuwakatalia?

Hiyo itategemea na masharti tutakayowapa wakati tukisaini mkataba, lakini tukishakubali tu ni lazima tuheshimu mkataba, ingawa you might have a point, lakini ni very weak maana mkataba ni mkataba kwa hiyo ni lazima kuwa makini kabla ya kuusaini!

4.
Biashara yeyote ina gharama zake. Hauwezi ukaanzisha na kukuza biashara ya Casino bila kukubali kuwa biashara za umalaya, kusafisha fedha n.k nazo zitaongezekeza. Angalia Jollys na Nevada! Mmoja anamsaidia mwenzie. Vile vile, base hizi ambazo zinakuwa na idadi kubwa ya vijana wa kiume ambao hawajaoa zinavutia biashara za umalaya. Wana kitu kinaitwa Rest and recreation, unadhani wataenda wapi? Mombasa?

Mkuu wangu, Margott ilikuwepo kabla mimi na wewe hatujazaliwa na wala hakuna base, umalaya ni lazima uwepo mkuu wangu katika jamii cha muhimu ni kuutumia kwa faida ya taifa kwa kutoza kodi wale wote wanaohusika nao, na kuja kwa base kutaongeza tu value ya hiyo biashara muhimu kwa jamii, maana nchi zote duniani ndvyo zinavyofanya mkuu, halafu pia ni part ya Constitution Rights za wananchi kwenye Bill of rights yaani the right kujamihiana through the right of their speeech bila ya kuingiliwa na serikali, sasa dawa ni kuwatoza kodi ama sivyo watafanya kwa magendo taifa litakosa kodi!

5.
Tunampigia kelele Karamagi kuwa ametuingiza mkenge katika mradi wa Buzwagi na yeye akituambia kuwa alifanya hivyo ili mteja asitutoke, hatumuelewi!

Karamagi, anatuhumiwa kwa ufisadi, it has nothing to do na kukumbatia wawekezaji, ndio maana alisema ataenda mahakamani lakini so far hajaenda maana he is guilty of something, mkataba wa Buzwagi hata wazungu wenyewe wawekezaji wameushitukia mkuu kuwa ni mkenge afadhali hata ungekuwa kanyabyoya tungeeelewa!

6.
Tunajenga mahoteli Serengeti ati tukiogopa kuwa tusipowaruhusu hao wawekezaji uchwara watakimbilia kungine, bila kujali athari katika mazingira ya mbuga hizo hizo tunazozitegemea kuvutia watalii!

Haya ya utalii ndio kabisaa hatuyajui, ni lazima tuwaachie wanayoyaweza yaani wazungu, sasa hivi wanajenga na kutangaza sana huko kwao, guess what wanamiminika kama njugu na ndio kitengo pekee kinachotuokoa as a nation as far as kodi is concerned, ama sivyo tungekulana nyama wenyewe kwa wenyewe, kwa hiyo what ever tunachofanya huko kwenye sekta ya utalii it is working, majuzi rais alipokuwa NY, nilispend muda mwingi sana na katibu mkuu wa utalii na Professor Maghembe, waziri wake kwa kweli niliyoyaona ni wazungu matajiri wa dunia wakililia kuja kuwekeza bongo kwenye hiyo sekta, na wewe unajua huyo mama katibu alivyo na kichwa kizima, huko sasa kwenye utalii mambo ni waaa!

6.
Tunawatetea wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu bila kuangalia athari ya mercury wanayoitumia katika mazingira yetu!Tunaendekezeka mashamba ya prawn bila kuangalia athari yake katika mikoko yetu. Tunaendekeza machimbo ya makaa ya mawe na matumizi yake katika kuzalisha nishati bila kuzungumzia athari yake katika miti yetu (angalia mto Kiwira) na mazingira. Leo hii tunachangamkia base kwa ajili ya kazi za kukata nyasi na dada zetu kuwa mahousegirl? Unadhani kazi gai ya maana utaipata kwenye hizo base wewe mtoo wa kidengereko
?

Great point, lakini the ishu hapa ni elimu duni among wananchi wetu, wakulaumiwa sio kuja kwa base mkuu ila ni sisi wenyewe wananchi na serikali yetu kwa kutohimiza elimu!

6.
Mheshimiwa sijakuelewa unataka kusema nini kuhusu Kuba na sisi. Labda tuzungumzie maadili kati ya Dar es salaam na Mombasa ambako kila kukicha meli za kivita za Kimarekani zimekuwa zikienda kwa ajili ya Rest and Recreation? Wewe niambie, ni wapi ambapo maadili yameporoka zaidi?

Maadili mkuu ya kweli hatujawahi kuwa nayo, maana tungekuwa nayo yangeweza kutusaidia sasa hivi kama yanvyowasaidia wa-china, Cuba wenzetu huwaweka jela wanaouliza ukweli kuhusu siasa yao ya mabavu, mara ya mwisho Castro alipokuja hapa bongo alimwambia wazi Mwalimu kuwa hapa hapakuwa na ujamaa ila hadithi tu, mkuu wangu mwaka 1986 nilikuwa china, kwenye mji wa Shangai yaani ule ndio ulikuwa ujamaa wa kweli mji mzima ilikuwa unaona wananchi wanaendesha baiskeli tu, ukiona Benzi basi ni ya Diplomat ndio maana wenzetu mpaka leo hawan shida ya kusonga mebele maana tofauti kati ya wananchi kwenye jamii financially, sio kubwa sana kama hapa kwetu, siasa ya ujamaa ya Mwalimu ilipaswa ktuweka wote sawa sasa kina Bakhressa na Mengi walitokea wapi? si utajiri wao ulikuwepo hata Mwalimu bado akiwa kwenye power? Ndio maana mkuu ninasema kuwa maadili hatujawahi kuwa nayo hata siku moja, sasa tusiyatafute eti kwa sababu base inataka kuja!

7.
Tujifunze kusema kuwa wakati mwingine the price is not woth paying. Kupenda kwetu dezo kutatupeleka kubaya. Badala ya hivi virahisi rahisi, tujenge uchumi uliokuwa sustainable kwa kuzingatia uwezo wetu wenyewe na si kuwategemea hawa jamaa! Kama wengine walivyosema, hakuna John anayejali yatakayomsibu malaya wake baada ya kutimiza haja yake!

Huo uwezo hatuna, tulijenga nyumba kwenye hewa sasa wanakuja wenye akili wanaojaribu kutusaidia tujenge nyumba kwenye mwamba, mengine yatakuwa mazuri mengine yatakuwa machungu, lakini in the end ni wajibu wetu kutumia akili zetu ili tunufaike na wanayotuleletea, kuja kwa base ni safi sana kwa ajili ya kuendeleza ajira za wananchi, na pia kujifunza mazuri mengi ya US na kuwaachia mabaya yao, umasikini wetu ndio tatizo tatizo sio sisi as wananchi au maadili yetu, kwa hiyo tumtumikie tajiri tupate mradi mkuu, ili yaishe tu!

Ahsante Bro!
 
Heshima mbele mkuu, Al Qaeda walipopiga mabomu Kenya na Dar, kulikuwa na base ya US? au? Kama hazikuwepo hizo base, inakwambia nini kuhusu mission ya Osama? Ni kwamba yeye hupiga anywhere kwenye interest ya US, bila ya kujali base ipo au haipo!

Osama alianza kama financier wa Mujahideen katika mapambano yao na warusi huko Afghanistan. Baada ya haya mapambano alirudi Saudi Arabia ambako alianzisha mtandao wa kuwafasaidia wale waliopigana Afghanistan. Mwaka 1990, Iraq ilipoishambulia Kuwait, utawala wa Saudi Arabia uliruhusu ujengaji wa BASE nchini mwake. Kitendo hiki kilimuudhi Osama hadi kikapelekea kufukuzwa kwake mwaka 1991 kwa kile kilichoitwa vitendo dhidi ya utawala. Akahamia Khartoum ambako akaongoza mashumbulizi dhidi ya wamarekani huko Somalia ambako walikuwa katika harakati ya kuanzisha BASE!
Mwaka 1994 aliondoka Khartoum kuelekea Afghanistan ambako alihifadhiwa kama mgeni wa Taliban hadi hapo walipoangushwa na wamarekani. Kikundi (au mkusanyiko wa vikundi) anachokiongoza cha Al Qaeda kimetangaza vita dhidi ya wamarekani na maswahiba wake hadi watakapoondoa majeshi yao katika nchi zote za kiislamu. Kwa mtazamo wao hizi ni nchi zenye idadi kubwa ya waislamu ( hii haina maana kuwa waislamu wote ni Al Qaeda au idadi kubwa yao ni Al Qaeda). Wanaamini kuwa ni wajibu wa kila muislamu kupigana na wamarekani na wayahudi popote pale alipo. Novemba 2003 wakalipua bomu ubalozi mdogo wa uingereza Istanbul, Uturuki na kuua watu 27, Mwaka 2004 wakalipua bomu Madrid, mwaka 2005 London. Wameishashambulia ubalozi mdogo wamarekani mjini Jiddah, Saudi Arabia n.k. Wamelipua Hoteli Mombasa na kujaribu kuangusha ndege ya Kiisraeli. Hawa mabwana wanatafuta pale palipo na ulaini wa kumuumiza marekani, iwe kwenye ubalozi au la. Kituo cha kijeshi bila shaka kitakuwa na mvuto kwa sababu ya idadi ya wamarekani watakaokuwa pale. (kwa kuruhusu kituo cha kijeshi tutajiingiza katika mapambano ya kivita na si ya kidiplomasia)Kama nilivyosema awali, kutokana na idadi kubwa ya waislamu nchini mwetu utamuongezea urahisi wa kujipenyeza ingawa si wengi watakaokuwa wanamuunga mkono. Yule kijana niliyemtaja, ni mzaliwa wa unguja. Ukweli wa hili, utawafanya wamarekani kuwa waangalifu mara dufu na kuondoa mvuto wa kibiashara wa kituo hicho kwa watanzania. Angalia hali ya ulinzi inavyokuwa tunapotembelewa na mkubwa kutoka huko? Nasikia Clinton alipotutembelea kama waziri hata maji hakuruhusiwa kunywa. Sasa leo unategemea watakuruhusu uwauzie madafu askari wao?


2.

Osama, ni rafiki mkubwa wa watawala wa Saudia, na ni hao hao wanaompa misaada ya kuweza kuishi mpaka leo, wanaowasumbua huko Saudia sio Al Qaeda, isipokuwa ni wananchi waliochoshwa na utawala wa kifalme, na walikuwa wakiwasumbua hata kabla base ya US haijawekwa kule, na hata siku moja hawajawahi kudai base iondoke wanachodai ni mabadiliko ya katiba na utawala, kama umesoma historia ya Osama, ni kwamba at one time utawala wa huko ulimkamata na kusihia kumfukuza nchi na kumtoa uraia huku wakimruhusu ahamie Sudan, enzi hizo base ya US haikuwepo huko Saudia mkuu!

Hii nadhani nimeijibu hapo juu.

3.

Mkuu wangu uwezo tunao tena mkubwa sana, ndio maana tulimng'oa Amin mpaka Kampala na kumfukuza nchi yake mwenyewe, usalama wetu unaaaminiwa sana duniani, at onetime tulikuwa very close na Mossad, kwa efficiency katika usalama, hatuhitaji msaaada wa mtu yoyote kujilinda!

Kwa vile mimi si mtaalamu wa usalama siwezi kukubishia kwenye hili. wasiwasi wangu tuu ni pale ninapoona watu wanaingiza na kutoa bidhaa jinsi watakavyo kupitia njia za panya, bandari bubu na hata bandari halali. Magogo, menu ya faru, madini kama Tanzanite vyote vinatoka kirahisi na madawa ya kulevya na bidhaa fake zinaingizwa. Au wanaachiwa kwa vile hatuoni athari yake? Wasiwasi unazidi pale ninaposoma kila kukicha kuhusu pasi zetu kuuzwa kama njugu!

4. .

Hivi mkuu, Mzee Maumba alipokuwa akibaka watoto hapa bongo alikuwa ametokea kwenye base ipi ya US? Yaaani unataka kusema watoto wanaobakwa hapa bongo kila siku huwa wanabakwa na wananchi kutoka base ya US? Kwa hiyo Nguza na watoto wake nao walitoka base ya US? Hayo ya imunity ni makubaliano kati ya nchi na nchi, askari wa ki-Jap wakikamatwa kule Us nao hawataguswa pia, hayo ya Iraq sidhani kama ni kweli maana tunajua kuwa ni majuzi tu askari wa US wamefungwa jela kwa ku-rape Iraq, na wengine sasa hivi wanasubiri kesi zao, lakini kubaka sio lazima kuwe na base ya Us, yaani wananchi walioko kwenye jela zetu kwa kubaka wote wametoka base za US? Kuhusu imunity Japan kama haitaki inaweza kuvunja huo mkataba anytime, kama vile walivyo-pull majeshi yao kule Iraq! Hakuna anyewazuia, lakini tatizo la ubakaji halisababishwi na base ya US tu!

Hapa unanikosea tena. Ni askari wangapi wakimarekani walioshitakiwa katika mahakama ya ki-iraq? Hata wale security contractors ambao wote wanakubali waliwaua wa-iraq bila hatia hawajashitakiwa. Sijasema kuwa ubakaji na mambo kama hayo yataletwa na wamarekani. biashara ya ukahaba ilianza zamani. hiyo margot unayoizungumzia, wateja wake wakuu walikuwa ni mabaharia wageni. Wakina mimi na wewe tuliishia Kisutu na mtaa wa Morogoro ambako vinjywaji kama gongo na uuzaji wa bangi ulikuwa nje nje. Ninachosema ukileta wenye nazo na walio tayari kulipa vizuri(kwa macho yetu) unaongeza mvuto wa hii biashara. Na kiburi cha mwenye nazo ndicho kinachochangia kwa kiasi kikubwa kwenye hivyo vitendo vya ubakaji, kuanzia wakina Maumba na kuendelea. Wengi wa hawa utumia uwezo wao wa kifedha au nafasi yao katika jamii kuwarubuni wale wasionacho. Tuliopita JKT zama zile tunajua vitendo walivyokuwa wakitendewa mabinti haswa wale wa kujitolea, kwenye kambi hizo na wale wa kutoka vijiji vya jirani. Ulizia sehemu yeyote yenye kambi ya kijeshi na uulizie vitendo vya wanajeshi wake! Sasa shilingi 50,na mikate ya siagi ya zama zile ilikuwa ikiwachengua watu itakuwa hawa watakaokuja na mibenjamin! ingekuwa rahisi hivyo kufunja mkataba wa base, wamarekani wasingekuwepo Gutanamo hadi leo!

5.

Ukiwa masikini ukatulia na umasikini wako, hutaguswa na mtu yoyote, lakini ukihitaji msaada wa tajiri, huna njia ila kumtumikia tajiri upate mradi wako, ipi bora vijana wetu kuzamia huko majuu kufanyishwa kazi kama punda kwa ujira mdogo, huku wakinyanyaswa kama mbwa kwa kutokuwa na papers, au kuwakubalia wenye nguvu waje hapa hapa bongo na kutupa ajira?

Hivi ni bora zaidi kufanyishwa kazi kama punda na kulipwa ujira mdogo , katika mazingira ambayo ni hatari kwa uhai wako na BILA kinga yeyote ya kisheria ili mradi uko kwenu? Hiyo migogoro ya kila siku tunayoisikia si kutoka kwa wale waliojariwa na hao wenye nguvu?3.


Hiyo itategemea na masharti tutakayowapa wakati tukisaini mkataba, lakini tukishakubali tu ni lazima tuheshimu mkataba, ingawa you might have a point, lakini ni very weak maana mkataba ni mkataba kwa hiyo ni lazima kuwa makini kabla ya kuusaini!

Mheshimiwa Rais alipozungumzia haja ya kupatiwa wataalamu wa mikataba kutoka Norway wengi mlimshangaa. Ukweli ni kwamba uwezo wetu wa kunegotiate mikataba ya kimataifa bado uko chini. Hao mawakili wetu wa AG Chambers hawana exposure kwenye masuala kama haya. Huu ni ukweli uliopo. tunahitaji capacity building ya nguvu katika nyanja hii.

4.

Mkuu wangu, Margott ilikuwepo kabla mimi na wewe hatujazaliwa na wala hakuna base, umalaya ni lazima uwepo mkuu wangu katika jamii cha muhimu ni kuutumia kwa faida ya taifa kwa kutoza kodi wale wote wanaohusika nao, na kuja kwa base kutaongeza tu value ya hiyo biashara muhimu kwa jamii, maana nchi zote duniani ndvyo zinavyofanya mkuu, halafu pia ni part ya Constitution Rights za wananchi kwenye Bill of rights yaani the right kujamihiana through the right of their speeech bila ya kuingiliwa na serikali, sasa dawa ni kuwatoza kodi ama sivyo watafanya kwa magendo taifa litakosa kodi!

Bill of Rights? Tanzania? Tudai tuu kodi bila kuwahakikishia usalama wao na mazingira yanayofaa kufanyia biashara yao? bila kuangalia umri na uwezo wa hao makahaba kufanya hii biashara? Si haututakii mema? Pedophiles wote wa ulaya watahamia kwetu! Au kwa vile tunao home grown pedophiles hii nayo ni poa!! Ili mradi watuletee hayo mafaranga?

5.

Karamagi, anatuhumiwa kwa ufisadi, it has nothing to do na kukumbatia wawekezaji, ndio maana alisema ataenda mahakamani lakini so far hajaenda maana he is guilty of something, mkataba wa Buzwagi hata wazungu wenyewe wawekezaji wameushitukia mkuu kuwa ni mkenge afadhali hata ungekuwa kanyabyoya tungeeelewa!

Karamagi alifanya kile unachoadvocate. Aliona kuna hatari ya kumpoteza mwekezaji akajitahidi kwa kdri ya uwezo wake asipotee. Wewe ndiye unayemuita fisadi yeye anaona alifanya uzalendo.
6.

Haya ya utalii ndio kabisaa hatuyajui, ni lazima tuwaachie wanayoyaweza yaani wazungu, sasa hivi wanajenga na kutangaza sana huko kwao, guess what wanamiminika kama njugu na ndio kitengo pekee kinachotuokoa as a nation as far as kodi is concerned, ama sivyo tungekulana nyama wenyewe kwa wenyewe, kwa hiyo what ever tunachofanya huko kwenye sekta ya utalii it is working, majuzi rais alipokuwa NY, nilispend muda mwingi sana na katibu mkuu wa utalii na Professor Maghembe, waziri wake kwa kweli niliyoyaona ni wazungu matajiri wa dunia wakililia kuja kuwekeza bongo kwenye hiyo sekta, na wewe unajua huyo mama katibu alivyo na kichwa kizima, huko sasa kwenye utalii mambo ni waaa!

Soma posting yangu kwenye Hoja Nzito yenye kichwa Mazingira 1. Najua wakuu huwa hamtembelei huko. Kwa kifupi hoteli inayojengwa Bilia, serengeti inamilikiwa na kampuni kutoka Dubai iitwayo Albawardy ambayo inamiliki vile vile Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski. Watalamu wanasema ujenzi wa hizi hoteli, barabara na viwanja vya ndege vitaathiri migratory patterns za wanyama ambazo ni kivutio kikubwa kwenye mbuga hizo. Tunataka kushindana na wakenya badala ya kujifunza kutoka Botswana ambao wanafanya responsible conservation kuhakikisha kuwa vizazi vingi vitaendelea kufaidi utajiri huo. Kwenye mbuga za Kenya watalii wameishalalamikia hali ya kujikuta landrover kumi zimemzunguka tembo mmoja! Tunamchinja bata wetu anaetutagia mayai kwa ajili ya quick returns. Hawa wakezaji tunaowakumbatia si wale wanaowinda kwa SMG na wanaowanyang'anya watanzania halisi( wahadzabe-wewe na mimi ni wakuja tuu) sehemu ya makazi yao!

6. ?

Great point, lakini the ishu hapa ni elimu duni among wananchi wetu, wakulaumiwa sio kuja kwa base mkuu ila ni sisi wenyewe wananchi na serikali yetu kwa kutohimiza elimu!

6.

Maadili mkuu ya kweli hatujawahi kuwa nayo, maana tungekuwa nayo yangeweza kutusaidia sasa hivi kama yanvyowasaidia wa-china, Cuba wenzetu huwaweka jela wanaouliza ukweli kuhusu siasa yao ya mabavu, mara ya mwisho Castro alipokuja hapa bongo alimwambia wazi Mwalimu kuwa hapa hapakuwa na ujamaa ila hadithi tu, mkuu wangu mwaka 1986 nilikuwa china, kwenye mji wa Shangai yaani ule ndio ulikuwa ujamaa wa kweli mji mzima ilikuwa unaona wananchi wanaendesha baiskeli tu, ukiona Benzi basi ni ya Diplomat ndio maana wenzetu mpaka leo hawan shida ya kusonga mebele maana tofauti kati ya wananchi kwenye jamii financially, sio kubwa sana kama hapa kwetu, siasa ya ujamaa ya Mwalimu ilipaswa ktuweka wote sawa sasa kina Bakhressa na Mengi walitokea wapi? si utajiri wao ulikuwepo hata Mwalimu bado akiwa kwenye power? Ndio maana mkuu ninasema kuwa maadili hatujawahi kuwa nayo hata siku moja, sasa tusiyatafute eti kwa sababu base inataka kuja!

Hapa siingii kwa vile naona unapersonal issues na Mwalimu.

7.

Huo uwezo hatuna, tulijenga nyumba kwenye hewa sasa wanakuja wenye akili wanaojaribu kutusaidia tujenge nyumba kwenye mwamba, mengine yatakuwa mazuri mengine yatakuwa machungu, lakini in the end ni wajibu wetu kutumia akili zetu ili tunufaike na wanayotuleletea, kuja kwa base ni safi sana kwa ajili ya kuendeleza ajira za wananchi, na pia kujifunza mazuri mengi ya US na kuwaachia mabaya yao, umasikini wetu ndio tatizo tatizo sio sisi as wananchi au maadili yetu, kwa hiyo tumtumikie tajiri tupate mradi mkuu, ili yaishe tu!

Ahsante Bro!

Mazuri yapi tutajifunza kutoka kwenye base ya wamarekani?

Shukurani, Mkuu.
Lakini natumaini haya yote tunayoyajadili ni speculations tuu.
 
Samahani, Clinton alitutembelea kama RAIS na si waziri. na osama aliunda mtandao wa KUWASAIDIA waliopigana Afghanistan.
 
Samahani, Clinton alitutembelea kama RAIS na si waziri. na osama aliunda mtandao wa KUWASAIDIA waliopigana Afghanistan.

Hiyo ya Rais Clinton ipo obvious ni makosa tu ya kiuhandishi, sidhani kama ilihitaji ulichofanya!!!!. Nani asiyejua kama Clinton alikuwa Rais na si waziri???. Watu bwana......
 
Jumamosi iliyopita hapa JF palikuwepo na mjadala uliohusu Kikwete kuwauzia waMarekani sehemu ya kuweka kambi ya kijeshi kwa jeshi la waAmerica.

Tuliambiwa Rais wetu atafunga safari ya kwenda huko hivi karibuni kuonana na wahusika ili jambo hilo lijadiliwe na pengine likubalike.

Hii ni taarifa nzito sana isiyohitaji utani, na hata kama ni katika nyanja za upinzani wa kisiasa, jambo kama hili ni zito mno; na hasa linapohusishwa na ofisi kuu ya kitaifa kama hiyo ya Rais wa nchi.

Mtu mzima ukiwa ni mwenye akili timamu ukiamua kukaa mbele ya kompyuta na kupanga uongo kama huo na kuusambaza kwenye kadamnasi ya watu, kwa sababu tu za kipinzani za kisiasa; (mtaniwia radhi nikisema kuwa) utakuwa una mawazo ya kihaini kwa nchi yako.

Jumapili tunaambiwa Rais Kikwete anakwenda huko kwa shughuli za kibiashara (Sullivan.......), jambo ambalo lipo mbali kabisa na hiyo mipango iliyosemwa katika mjadala ule.

Maombi yangu ni kwamba tusiupeleke mbali sana huu upinzani wa kisiasa tukafikia hata mahali pa kuuana au kulisaliti taifa letu.

Ninazielewa mbinu chafu zinazotumika katika siasa, lakini kila mara tuwe waangalifu kuhakikisha kuwa tunaweka usalama wa taifa letu katika janga.



wahenga walisema tangu zamani
 
Back
Top Bottom