Pre GE2025 Jeshi la Polisi latoa onyo wanaopanga kufanya vurugu siku ya kesi ya Lissu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Nov 7, 2023
1,114
1,862
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limeonya wananchi kutojitokeza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Aprili 24,2025 wakati Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu akifikishwa mahakamani hapo, likisisitiza atakayejitokeza atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Katazo la Jeshi la Polisi kwa wananchi ni kufuatia wito wa Makamu Mwenyekiti wa Chadema, John Heche kuwataka wanachama wa chama hicho na wananchi kufika kwa wingi Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Aprili 24,2025 wakati Mwenyekiti wao Lissu akifikishwa mahakamani kusikiliza kesi ya uhaini inayomkabili.

Heche ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Mbezi, wilaya ya Ubungo Aprili 16,2025 wakati akihutubia mamia ya wananchi waliofika kumsikiliza, akiwahimiza wananchi hao kufika mahakamani hapo bila kuwa na silaha yeyote wala kufanya fujo bali wabebe vitambaa vyeupe na maji.

Akizungumzia wito huo, leo Aprili 17,2025 jijini Dar es Salaam Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema jeshi hilo limefuatilia mipango ya viongozi wa chama hicho na kubaini siku hiyo kutafanyika vurugu.

Muliro amesema lengo la vurugu hizo ni kushinikiza mamlaka za kisheria kumwachia kiongozi wao ambaye anatuhumiwa.
 
Haya makomandoo wa demokrasia huu ndio muda wenu wa kukinukisha kama mlivyokubaliana na mwenyekiti wenu. Maneno matupu hayavunji mfupa tuonyesheni sasa.
 

Attachments

  • 20250416_180440.jpg
    20250416_180440.jpg
    132.4 KB · Views: 2
Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar Es Salaam, limetoa onyo kwa wafuasi wa Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA, wanaohamasisha kufanya vurugu, siku ya ambayo Mwenyekiti wao Taifa, Tundu Lissu anayotarajiwa kupandishwa Mahakamani Aprili 24, 2025.

Jeshi la Polisi limesema litashughulika na kila mmoja atakayeshiriki kufanya vurugu yeyote katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam.


Lissu ni Dude kubwa sana nchi hii
20250417_132134.jpg
 
Siyo lazima iwe Sasa. Tunajua mitego yenu yote.
Basi kama sio lazima iwe sasa why wasijaribu kutumia soft ways to infiltrate the system since they still have time instead of adopting barbaric political manouvre procedures?

Heche anakwambia bora CDM ife 😂😂 sasa huyu ni visionary leader kweli?
 
Back
Top Bottom