Jeshi la Afrika Kusini, halina kazi tena DRC, liondoke tu

MBOKA NA NGAI

JF-Expert Member
Jan 31, 2025
228
437
Msemaji mkuu wa kisiasa wa AFC/M23, Lawrence Kanyuka, ametangaza kwamba, wanajeshi wa Afrika Kusini waliopewa hifadhi katika kambi ya MONUSCO huko Goma, walitakiwa kuwa kwao kwa sasa, kwa sababu haoni wanachokifanya huko. Na aliongezea kuwa, muda ndo sasa, na AFC/M23 wapo tayari kuwapa njia ya kuondoka.

Jeshi la Afrika Kusini liliingia vitani mashariki mwa DRC, mwaka 2023, kupitia SAMIDRC, ushilikiano ulolenga kuiongezea nguvu DRC,kukabiliana na makundi yakigaidi, na mwisho wa siku walijikuta wakipigania upande wa serikali ulioshirikiana na FDLR,kundi la waasi wa serikali ya Rwanda, linalokabiliwa na tuhuma za mauwaji dhidi ya watutsi mwaka 1994. Ushilikiano huo pia ulikuwemo kundi la Wazalendo,jeshi la Burundi na mamluki kutoka nchi za Ulaya.

Januari mwishoni, vita vikali viliacha mji wa Goma mikononi mwa kundi la AFC/M23, wanajeshi 14 wa Afrika Kusini wakipoteza maisha, wengine walijikuta wamezingirwa na kundi hilo la M23, walilazimika kukimbilia kwenye kambi ya MONUSCO na kuomba hifadhi huko,ili wanusuru maisha yao. Wengine waliokuwa nje kidogo ya Mji wa GOMA(Uwanja wa ndege wa Goma, na mji mdogo wa SAKE), wapo chini ya ulinzi wa M23 mpaka sasa katika kambi zao huko.

Msemaji huyo, ametangaza kuwa, wao wapo tayari kuwapatia njia, lakini uongozi wao uligoma kukubali wanajeshi hao kusafilishwa kupitia Rwanda, na kuongeza kwamba, uwanja wa ndege wa Goma hauwezi kutumika kwa sasa, kutokana na kuharibika kwa njia ya ndege kulikotokana na makombola.

Afrika kusini ilituma wanajeshi zaidi ya 2,900, wakiwemo wa SAMIDRC
Bunge la Afrika kusini,limekuwa likihoji kilichowapeleka,kutokana na ripoti zisizoeleweka zilizotolewa na uongozi wa nchi hiyo, na kuomba wanajeshi hao warudishwe haraka iwezekanavyo.
 
Mkuu kwa hiyo hao wanajeshi washikiliwa au nini bado kimewaweka huko? Na vipi hakuna wanajeshi wapya wa SA? Kwa nini warudi kwao badala ya kuunguna na kuendelea kupigana? Na kwa nini serikali SA inakanusha kuwa na wanajeshi walio DR?
 
Mkuu kwa hiyo hao wanajeshi washikiliwa au nini bado kimewaweka huko? Na vipi hakuna wanajeshi wapya wa SA? Kwa nini warudi kwao badala ya kuunguna na kuendelea kupigana? Na kwa nini serikali SA inakanusha kuwa na wanajeshi walio DR?
nianze na swali la mwisho. Kukanusha kwa SA, ni aibu si kingine. Nchi inayosifika kiuwezo idhalilishwe mbele za uso wa dunia!!!! Na hiki ndo kilichochelewesha zile maiti zao. Waligoma kuzipitisha Rwanda, M23 na yenyewe ikawambia hakuna njia nyingine. Wakaomba basi zikipita, wanahabari wasiruhusiwe kupiga picha. Rwanda iliwajibu kwamba huo uwezo haina, kwa sababu katiba inamruhusu hata raia wa kawaida kupata habari anazozitaka.

1. Wanajeshi,sema wameshikwa mateka. Wamechanganyika na zile nchi nyingine mbili zina watu humo. Serikali zao, ndo zenye maamuzi. Lakini kwa vile walienda kama SADC, si rahisi kujitenga, bado wanakufa kiume. Kinachowaweka huko, si kingine. Walizingirwa na aliyekuwa adui(M23), kwa kifupi The hunter became hunted. Walilazimika kunyoosha mikono na kupepeza bendela nyeupe. Na hiyo ni ishara ya kushindwa. Wanajeshi wapya wa A.S wapo. Wapo Burundi na Lubumbashi.
Waliopo Burundi watapita wapi? mipaka yote na njia ya maji vipo mikononi mwa M23. Huko Lumbumbashi, lazima wajipange upya. Si unajua viwanja vya ndege vilivyopo karibu vyote si salama kwa sasa! Na Air support lazima iendane na ground forces. Wanaendelea kupigana na nani, kwa lipi? Burundi ilivyoona mipaka yote inaenda kufungwa, ilikimbilia kuondoa watu wake. Maana wangezingirwa, ingekuwa historia moja mbaya sana. Malawi,rais alishasema jeshi lake lirudi tu. South Africa, nae ndo kama hivyo ana wakati mgumu huko.
 
nianze na swali la mwisho. Kukanusha kwa SA, ni aibu si kingine. Nchi inayosifika kiuwezo idhalilishwe mbele za uso wa dunia!!!! Na hiki ndo kilichochelewesha zile maiti zao. Waligoma kuzipitisha Rwanda, M23 na yenyewe ikawambia hakuna njia nyingine. Wakaomba basi zikipita, wanahabari wasiruhusiwe kupiga picha. Rwanda iliwajibu kwamba huo uwezo haina, kwa sababu katiba inamruhusu hata raia wa kawaida kupata habari anazozitaka.

1. Wanajeshi,sema wameshikwa mateka. Wamechanganyika na zile nchi nyingine mbili zina watu humo. Serikali zao, ndo zenye maamuzi. Lakini kwa vile walienda kama SADC, si rahisi kujitenga, bado wanakufa kiume. Kinachowaweka huko, si kingine. Walizingirwa na aliyekuwa adui(M23), kwa kifupi The hunter became hunted. Walilazimika kunyoosha mikono na kupepeza bendela nyeupe. Na hiyo ni ishara ya kushindwa. Wanajeshi wapya wa A.S wapo. Wapo Burundi na Lubumbashi.
Waliopo Burundi watapita wapi? mipaka yote na njia ya maji vipo mikononi mwa M23. Huko Lumbumbashi, lazima wajipange upya. Si unajua viwanja vya ndege vilivyopo karibu vyote si salama kwa sasa! Na Air support lazima iendane na ground forces. Wanaendelea kupigana na nani, kwa lipi? Burundi ilivyoona mipaka yote inaenda kufungwa, ilikimbilia kuondoa watu wake. Maana wangezingirwa, ingekuwa historia moja mbaya sana. Malawi,rais alishasema jeshi lake lirudi tu. South Africa, nae ndo kama hivyo ana wakati mgumu huko.
Aisee viongozi wa Afrika baadhi yao watakufa midomo wazi na macho kodo.
 
Back
Top Bottom