Ishi kifukara, uende peponi!

Nsimbi

JF-Expert Member
Sep 27, 2014
1,091
1,202
Ukitaka kwenda peponi baada ya kifo chako, basi, sali, tenda matendo mema na ISHI KIFUKARA! Ndio, namaanisha! Fanya kazi yoyote halali lakini sehemu kubwa ya kipato chako kitumie kutimiza wajibu wako na hakika kusaidia masikini!

Huwezi kutumikia mabwana ( masters) wawili, so they say! Itakupasa uchague moja kati ya Mungu na Mali_ambayo mara nyingi ni a recipe for doom!!
Hakuna ajuae waendao mbinguni, lakini 'tetesi' zinaonesha mbinguni wamejaa masikini_ walioishi kwa wema hapa duniani.. Tuelewane: umasikini pekee sio 'an automatic ticket' ya kuingia mbinguni!! Sisemi hivyo! Bali tujue mali na utajiri vyaweza kuwa njia pana ya kujongea motoni... Nadhani katika hili hata vitabu vimedokeza kiasi..
Mimi naamini watu kama 'masista' na baadhi ya makasisi ndio waliochagua kazi bora zaidi hapa duniani. Wanaishi kifukara na tabia ya kujinyima... Wameacha shughuli zote za kuhangaikia mali na utajiri ili waweze kumtumikia Mungu kikamilifu.. Masista wengi siku hizi ni wasomi wazuri tu! Wangeweza kupata kazi 'nzuri' zenye ujira wa kutosha hata kuwawezesha kuishi kifahari! Lakini kwa vile Mwenyezi amewajalia neema na akili, wameamua kuishi kifukara_ na kutumia karama zao kama udaktari, ualimu n.k kutoa mchango wao katika ustawi wa jamii zao...
Wako pia makasisi na masheik ambao wanaishi maisha ya kimasikini huku wakitumia muda wao mwingi kwa masuala ya dini tu... Nasema wamechagua njia sahihi.. Hawahangaikii mali na utajiri ambavyo mara nyingi huwa ni recipes for doom.
Kuna baadhi ya wachungaji wanahubiria waumini wao kuwa matajiri! Wenyewe pia huishi kifahari na maisha ya kujikweza! Hawana unyenyekevu wala unyoofu inavyowapasa kuwa kama Biblia inavyowataka.. Baadhi yao nia yao si kuwaokoa watu bali kuyatumia makanisa kujipatia pesa kwa njia ya sadaka!! Hawa ni matapeli tu na yatupasa kuwaepuka kama ukoma!
Si dhambi kuwapuuza wachungaji na manabii wa uongo! Ndio wa uongo_ kwani kwa mujibu wa maandiko mitume na manabii wengi waliishi maisha ya unyoofu, ufukara na kujinyenyekeza. Bwana Yesu alisema mtu akitaka kumfuata sharti achukue msalaba wake!! ... Siku hizi baadhi ya wachungaji wanafundisha watu kuikimbia 'misalaba'!! Bwana Yesu alifundisha pia wafuasi wake kujishusha na siku zote alikemea unafiki!
Kuna wimbi kubwa la wachungaji wa uongo siku hizi lakini baadhi ya waumini wamekubali kuburuzwa kama ngo'mbe!! Ilipaswa watumie akili zao kutafakari yote yanayosemwa na wachungaji wao lakini isivyo bahati wao wameamua kuwa wajinga.. wapumbavu? Ishi kwa kiasi..
Mwanadamu anaaswa juu ya tabia ya choyo na ulafi....
Kwa akina dada, mama na bibi jijengeeni tabia ya kutoa.. Acheni kujaza minguo kwenye makabati na 'shangazi kaja'.. Nguo zote ambazo huvai gawa kwa masikini au ndugu na jamaa wasio na uwezo.... Hayo makenzi, mabazee, miviatu na vitenge usione choyo kupeleka kanisani au msikitini.. Ni bora ukagawa nguo zako ungali hai ili usiwape vishawishi ndugu zako kuzipigia mahesabu!
Nanyi akina kaka, baba na babu hizo suti za toka enzi ya Mkapa za nini? Gawa zote pamoja na mashati na suruali zinazokubana! Gawa mwenyewe ungali hali usije wapa changamoto ndugu zako kuzipigia kura suti zako!

Nawe mkulima ukivuna mazao yako, tenga kiasi cha kutosha kutoa sadaka, hususan kuwapa masikini... Kamwe usitoe mahindi mabovu au maharage yaliyooza... Toa mazao bora na baki na kiasi kiasi cha kukusaidia wewe na familia yako!! Wewe si unamuamimi Mungu? Basi usijaze maghala na maghala ya mavyakula kwani waweza kufa wakati wowote!!!
Dini inataka simplicity, modesty and humility sio kupayuka, mbwembwe, utapeli, choyo, ulafi na unafiki!!
Binadamu tumeumbwa na utashi! Huwezi kupata vyote! Chagua kimoja mbingu au dunia! Huwezi kupata vyote... Never!!!
.......
 
Ukitaka kwenda peponi baada ya kifo chako, basi, sali, tenda matendo mema na ISHI KIFUKARA! Ndio, namaanisha! Fanya kazi yoyote halali lakini sehemu kubwa ya kipato chako kitumie kutimiza wajibu wako na hakika kusaidia masikini!

Huwezi kutumikia mabwana ( masters) wawili, so they say! Itakupasa uchague moja kati ya Mungu na Mali_ambayo mara nyingi ni a recipe for doom!!
Hakuna ajuae waendao mbinguni, lakini 'tetesi' zinaonesha mbinguni wamejaa masikini_ walioishi kwa wema hapa duniani.. Tuelewane: umasikini pekee sio 'an automatic ticket' ya kuingia mbinguni!! Sisemi hivyo! Bali tujue mali na utajiri vyaweza kuwa njia pana ya kujongea motoni... Nadhani katika hili hata vitabu vimedokeza kiasi..
Mimi naamini watu kama 'masista' na baadhi ya makasisi ndio waliochagua kazi bora zaidi hapa duniani. Wanaishi kifukara na tabia ya kujinyima... Wameacha shughuli zote za kuhangaikia mali na utajiri ili waweze kumtumikia Mungu kikamilifu.. Masista wengi siku hizi ni wasomi wazuri tu! Wangeweza kupata kazi 'nzuri' zenye ujira wa kutosha hata kuwawezesha kuishi kifahari! Lakini kwa vile Mwenyezi amewajalia neema na akili, wameamua kuishi kifukara_ na kutumia karama zao kama udaktari, ualimu n.k kutoa mchango wao katika ustawi wa jamii zao...
Wako pia makasisi na masheik ambao wanaishi maisha ya kimasikini huku wakitumia muda wao mwingi kwa masuala ya dini tu... Nasema wamechagua njia sahihi.. Hawahangaikii mali na utajiri ambavyo mara nyingi huwa ni recipes for doom.
Kuna baadhi ya wachungaji wanahubiria waumini wao kuwa matajiri! Wenyewe pia huishi kifahari na maisha ya kujikweza! Hawana unyenyekevu wala unyoofu inavyowapasa kuwa kama Biblia inavyowataka.. Baadhi yao nia yao si kuwaokoa watu bali kuyatumia makanisa kujipatia pesa kwa njia ya sadaka!! Hawa ni matapeli tu na yatupasa kuwaepuka kama ukoma!
Si dhambi kuwapuuza wachungaji na manabii wa uongo! Ndio wa uongo_ kwani kwa mujibu wa maandiko mitume na manabii wengi waliishi maisha ya unyoofu, ufukara na kujinyenyekeza. Bwana Yesu alisema mtu akitaka kumfuata sharti achukue msalaba wake!! ... Siku hizi baadhi ya wachungaji wanafundisha watu kuikimbia 'misalaba'!! Bwana Yesu alifundisha pia wafuasi wake kujishusha na siku zote alikemea unafiki!
Kuna wimbi kubwa la wachungaji wa uongo siku hizi lakini baadhi ya waumini wamekubali kuburuzwa kama ngo'mbe!! Ilipaswa watumie akili zao kutafakari yote yanayosemwa na wachungaji wao lakini isivyo bahati wao wameamua kuwa wajinga.. wapumbavu? Ishi kwa kiasi..
Mwanadamu anaaswa juu ya tabia ya choyo na ulafi....
Kwa akina dada, mama na bibi jijengeeni tabia ya kutoa.. Acheni kujaza minguo kwenye makabati na 'shangazi kaja'.. Nguo zote ambazo huvai gawa kwa masikini au ndugu na jamaa wasio na uwezo.... Hayo makenzi, mabazee, miviatu na vitenge usione choyo kupeleka kanisani au msikitini.. Ni bora ukagawa nguo zako ungali hai ili usiwape vishawishi ndugu zako kuzipigia mahesabu!
Nanyi akina kaka, baba na babu hizo suti za toka enzi ya Mkapa za nini? Gawa zote pamoja na mashati na suruali zinazokubana! Gawa mwenyewe ungali hali usije wapa changamoto ndugu zako kuzipigia kura suti zako!

Nawe mkulima ukivuna mazao yako, tenga kiasi cha kutosha kutoa sadaka, hususan kuwapa masikini... Kamwe usitoe mahindi mabovu au maharage yaliyooza... Toa mazao bora na baki na kiasi kiasi cha kukusaidia wewe na familia yako!! Wewe si unamuamimi Mungu? Basi usijaze maghala na maghala ya mavyakula kwani waweza kufa wakati wowote!!!
Dini inataka simplicity, modesty and humility sio kupayuka, mbwembwe, utapeli, choyo, ulafi na unafiki!!
Binadamu tumeumbwa na utashi! Huwezi kupata vyote! Chagua kimoja mbingu au dunia! Huwezi kupata vyote... Never!!!
.......

Ukiishi kitajiri na ukatenda wema, huendi peponi?

Tunaomba pia kufahamu haya maelezo ni kutokana na chanzo gani, au umeyatoa tu kichwani?
 
Tetesi "Mbinguni kumejaa waliokuwa wanaishi kifukara". Nani aliyefika huko na kurudi na taarifa hizo? La maana tu ujue maisha ni mchezo. Walichokuambia wamisionari changanya na akili yako. Jitahidi uishi maisha mazuri na kupiga chino ufukara.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mfalme sulemani aliishi kimalaya malaya na pasipo ufukara ila ndio alibarikiwa. Kahaba yule aliishi misha ya anasa na dhambi nyingi alifanikiwa.

Ishi maisha ya kumpendeza jirani yako
 
Huo ni uongo mkubwa!!... Mungu haitaji maskini wa mali Bali maskini wa roho(wanyenyekevu) Kuna tajiri alimzidi Ibrahimu, Ayubu, Daudi? Hao ni mifano tu katika bibilia, na maandiko yanawataja Kama watu waliompendeza Mungu mpaka akaapa kwa ajili yao, akina Daniel walikuwa na position katika serikal ya Nebukadreaza walimtumikia Mungu kwa uaminifu, Mungu anachotaka umtegemee kwa asilimia zote, Kuna wengine hawawezi kumtumikia Mungu kwa sababu ya wake zao, wazazi wao, Mali walizonazo ndio maana Yesu anasema huwezi tumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja ukiangalia mifano ya hao niliowataja hawakuangalia vitu walivyokuwa navyo kwa mfano Ibrahim Sarah hakuwa na nafasi kwake, ukifika hatua hata mtoto wa pekee hakupoka nafasi ya Mungu ndani ya Moyo wa Ibrahimu mpaka Mungu akaapa kwa ajili yake
 
Ndugu yangu umeandika vizuri sema ujue nini !!kwenda mbinguni ni zawadi wala haina uhusiano na ufukara wala maisha ya kimaskini uliyoyaishi hapana duniani.

Watumishi wote wa Mwenyezi Mungu ambao tunawasoma kwenye vitabu mbali mbali wengi wao walikuwa na mali za kutosha.Mfano wao ni kama Job,Abraham,Isaac,Jacob,David,Solomon nakuendelea.Najua utaniambia kwamba Yesu alikuwa maskini kwa sababu wengi Yesu wamempa tafsiri mbovu ndio maana husema hivyo.Ukitaka kujua kwamba na Yesu alikuwa tajiri lazima ujue kwanza Yesu alikuwa mfalme na bado ni mfalme.Sasa kama alikuwa mfalme ni lini ulisikia mfalme fukara?

Mwisho kabisa kwenda mbinguni limebaki kama fumbo ambalo majibu yake yapo lakini nani anaweza kuyaona hayo majibu? tupo hapa duniani kama sehemu ya kujifunza kwahiyo ni ushindi wako wa hapa duniani ndio utakupa uwezekano wa kuiona mbingu.Hivyo basi fanya kila jambo ambalo ni sahihi siku zote za uhai wako hapa duniani na Mwenyezi Mungu atakufungulia mbingu kama zawadi siku ya kifo chako.Usipende kuishi ufukara maana kuna uwezekano mkubwa ukakufuru

Heaven is real and so does hell.

Tumsifu Yesu Kristo!
 
Ukitaka kwenda peponi baada ya kifo chako, basi, sali, tenda matendo mema na ISHI KIFUKARA! Ndio, namaanisha! Fanya kazi yoyote halali lakini sehemu kubwa ya kipato chako kitumie kutimiza wajibu wako na hakika kusaidia masikini!

Huwezi kutumikia mabwana ( masters) wawili, so they say! Itakupasa uchague moja kati ya Mungu na Mali_ambayo mara nyingi ni a recipe for doom!!
Hakuna ajuae waendao mbinguni, lakini 'tetesi' zinaonesha mbinguni wamejaa masikini_ walioishi kwa wema hapa duniani.. Tuelewane: umasikini pekee sio 'an automatic ticket' ya kuingia mbinguni!! Sisemi hivyo! Bali tujue mali na utajiri vyaweza kuwa njia pana ya kujongea motoni... Nadhani katika hili hata vitabu vimedokeza kiasi..
Mimi naamini watu kama 'masista' na baadhi ya makasisi ndio waliochagua kazi bora zaidi hapa duniani. Wanaishi kifukara na tabia ya kujinyima... Wameacha shughuli zote za kuhangaikia mali na utajiri ili waweze kumtumikia Mungu kikamilifu.. Masista wengi siku hizi ni wasomi wazuri tu! Wangeweza kupata kazi 'nzuri' zenye ujira wa kutosha hata kuwawezesha kuishi kifahari! Lakini kwa vile Mwenyezi amewajalia neema na akili, wameamua kuishi kifukara_ na kutumia karama zao kama udaktari, ualimu n.k kutoa mchango wao katika ustawi wa jamii zao...
Wako pia makasisi na masheik ambao wanaishi maisha ya kimasikini huku wakitumia muda wao mwingi kwa masuala ya dini tu... Nasema wamechagua njia sahihi.. Hawahangaikii mali na utajiri ambavyo mara nyingi huwa ni recipes for doom.
Kuna baadhi ya wachungaji wanahubiria waumini wao kuwa matajiri! Wenyewe pia huishi kifahari na maisha ya kujikweza! Hawana unyenyekevu wala unyoofu inavyowapasa kuwa kama Biblia inavyowataka.. Baadhi yao nia yao si kuwaokoa watu bali kuyatumia makanisa kujipatia pesa kwa njia ya sadaka!! Hawa ni matapeli tu na yatupasa kuwaepuka kama ukoma!
Si dhambi kuwapuuza wachungaji na manabii wa uongo! Ndio wa uongo_ kwani kwa mujibu wa maandiko mitume na manabii wengi waliishi maisha ya unyoofu, ufukara na kujinyenyekeza. Bwana Yesu alisema mtu akitaka kumfuata sharti achukue msalaba wake!! ... Siku hizi baadhi ya wachungaji wanafundisha watu kuikimbia 'misalaba'!! Bwana Yesu alifundisha pia wafuasi wake kujishusha na siku zote alikemea unafiki!
Kuna wimbi kubwa la wachungaji wa uongo siku hizi lakini baadhi ya waumini wamekubali kuburuzwa kama ngo'mbe!! Ilipaswa watumie akili zao kutafakari yote yanayosemwa na wachungaji wao lakini isivyo bahati wao wameamua kuwa wajinga.. wapumbavu? Ishi kwa kiasi..
Mwanadamu anaaswa juu ya tabia ya choyo na ulafi....
Kwa akina dada, mama na bibi jijengeeni tabia ya kutoa.. Acheni kujaza minguo kwenye makabati na 'shangazi kaja'.. Nguo zote ambazo huvai gawa kwa masikini au ndugu na jamaa wasio na uwezo.... Hayo makenzi, mabazee, miviatu na vitenge usione choyo kupeleka kanisani au msikitini.. Ni bora ukagawa nguo zako ungali hai ili usiwape vishawishi ndugu zako kuzipigia mahesabu!
Nanyi akina kaka, baba na babu hizo suti za toka enzi ya Mkapa za nini? Gawa zote pamoja na mashati na suruali zinazokubana! Gawa mwenyewe ungali hali usije wapa changamoto ndugu zako kuzipigia kura suti zako!

Nawe mkulima ukivuna mazao yako, tenga kiasi cha kutosha kutoa sadaka, hususan kuwapa masikini... Kamwe usitoe mahindi mabovu au maharage yaliyooza... Toa mazao bora na baki na kiasi kiasi cha kukusaidia wewe na familia yako!! Wewe si unamuamimi Mungu? Basi usijaze maghala na maghala ya mavyakula kwani waweza kufa wakati wowote!!!
Dini inataka simplicity, modesty and humility sio kupayuka, mbwembwe, utapeli, choyo, ulafi na unafiki!!
Binadamu tumeumbwa na utashi! Huwezi kupata vyote! Chagua kimoja mbingu au dunia! Huwezi kupata vyote... Never!!!
.......
Vyovyote vile unatakiwa kuwa mkarimu kwa binadamu wenzio
Biblia inasema:

1 Yohane 4:20-21​

Mtu akisema kwamba anampenda Mungu, hali anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Maana mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni. Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.

Ila kwamba lazima uwe masikini ndo uende mbinguni, it is a lie
Ayubu alikuwa mwema sana japo alikuwa tajiri sana, na alihesabiwa mcha Mungu
Pia Ibrahimu naye alikuwa hivyo hivyo, na mali nyingi na pia alikuwa mcha Mungu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom