KERO Hospitali ya Taifa Muhimbili (Mloganzila) Madaktari wanafunzi ni Janga. Watu wanakufa kwa uzembe

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kuna uzembe mkubwa sana kwenye usimamizi wa hawa ma intern huko mahospitalini
Mwaka juzi nilikuwa na mgonjwa amelazwa Hospitali ya Rufaa ya mkoa; Yaani 90% ya matibabu yote anayetegemewa ni Intern

KOSA KUBWA KULIKO YOTE NILILO LIONA NI KUWA, hapakuwa na consistence ya hao ma Intern yaani kila siku mbili anabadilishwa; yaani Kila siku mbili una intern tofauti, fikiria wagonjwa waliopo Hospitali ya Rufaa ni wale waliopo Serious hivyo wanataka mtu wa kufuatilia alichofanya jana kinaendeleaje; pale eti kila siku mbili wana rotate? UTARATIBU WA HOVYO KABISA!

Ukweli niliumia sana kwani ningetaraji hata kama ni Intern akae hata wiki (ajenge uhusiano na mgonjwa) ndio ahamishwe ward nyingine ILI pia ajifunze. Yaani wale Intern wana try and error nyingi sana kama wanatibu Ngombe ila siwalaumu kwa kuwa, wana achiwa kila kitu/hawasaidiwi

Huyo basi anayeitwa Msimamizi alikuwa anapita saa nne asubuhi kwa kama dakika 5; na jioni tena kwa kama Dakika 5.
Mimi sio dactari ILA kwa mtu yeyote aliye elimika, anaweza kuona kabisa kuwa kinachofanyika sio sawa!
Na hao ma intern wanatoka hapo hawajajifunza chochote!
 
Hii hospitali kama serikali na uongozi hautachukua hatua za haraka watanzania wengi wataendelea kufa kwa uzembe wa madaktari wanafunzi ambao hawasimamiwi ipasavyo na wakuu wao kazi.

Nimeshuhudia mgonjwa wangu akiambiwa hana tatizo lolote la nyonga baada ya kumpeleka akiwa amepata ajali na daktari ambaye ni mwanafunzi kusoma vipimo akatuambia mgonjwa aendelee na dawa alizopewa ( tulianzia matibabu hospitali ya wilaya kabla ya kwenda hapo mloganzila)

Tulipata mashaka na tukarudi tena kuomba uchunguzi zaidi ndipo daktari msimamizi wa mwanafunzi huyo alipokuja nadhani alikua kikaoni na baada ya kupitia tena vipimo alibadilika ghafla na kuwa mkali sana na kumfokea yule daktari mwanafunzi kuwa kwanini hajaona tatizo la nyonga kuvunjika? Na ni eneo hatari sana kwa mgonjwa? Japo alikua akimfokea kwa kiingereza ila tuliweza kujuwa kuwa daktari mwanafunzi alizembea katika matobabu ya ndugu yetu.
Nashukuru tumepangiwa tarehe ya operesheni. Ila nimeondoka na maswali mengi kichwani je ni wagonjwa wa ngapi wanaopitia hali kama tuliyopitia sisi?

Naomba serikali na uongozi mzima wa hospitali ya taifa ya Muhimbili (mloganzila) kuchukua hatua za haraka kuokoa maisha ya watanzania.
Upo sahihi kabsa nmewahi kumuuguza faza mdogo pale kwa mwez ....kuna sku wodi moja walikufa karibu wagonjwa wote...dokta kufika asubuh alihamaki balaa....kilichosaidia upande wetu alikuwa ni mtu mzto...
 
Nilipoteza mtoto aliyekua anazaliwa mwaka jana hospital ya ifisi mkoa wa mbeya kwa uzembe wa madaktari wanafunzi. Hili la madaktari kujifunzia kwenye miili ya watu wetu, inakera sana
Si ushitaki, haumfahamu mambulukuku huko mbeya? Mwanasheia anaevizia kesi namna hizo?
 
Nini maana ya neno "mloganzila?". Neno "mloga" ni kinyambulishi cha neno "kuloga" kuwangiwa. Kwahiyo ni hospital ambayo hakuna matumaini!
Mkuu malizia tu na maana ya "Nzila" ni njia kwahyo ni mlogaji anayelogea njian yaani eneo la ulozi kama ulozi mwingine wa njia za panda😭
 
Kuna uzembe mkubwa sana kwenye usimamizi wa hawa ma intern huko mahospitalini
Mwaka juzi nilikuwa na mgonjwa amelazwa Hospitali ya Rufaa ya mkoa; Yaani 90% ya matibabu yote anayetegemewa ni Intern

Ila kosa kubwa kuliko yote nililo liona na ni kuwa, hapakuwa na consistence ya hao ma Intern yaani kila siku anabadilishwa; yaani Kila siku una intern tofauti, fikiria wagonjwa waliopo Hospitali ya Rufaa ni wale waliopo Serious hivyo wanataka mtu wa kufuatilia alichofanya jana kinaendeleaje; pale eti kila siku wana rotate?

Ukweli niliumia sana kwani ningetaraji hata kama ni Intern akae hata wiki (ajenge uhusiano na mgonjwa) ndio ahamishwe ward nyingine ILI pia ajifunze.
Huyo basi anayeitwa Msimamizi alikuwa anapita saa nne asubuhi kwa kama dakika 5; na jioni tena kwa kama Dakika 5.
Mimi sio dactari ILA kwa mtu yeyote aliye elimika, anaweza kuona kabisa kuwa kinachofanyika sio sawa!
Na hao ma intern wanatoka hapo hawajajifunza chochote!
Kwakweli tunaomba wizara ya afya iangalie utaratibu huu tutapoteza wagonjwa wengi kwa magonjwa yanayotibika.
 
Nilikutana nao Muhimbili hao madaktari wanafunzi ni changamoto! Matibabu yaliyohitaji ganzi walinitibu bila ganzi, yale maumivu sitayasahau 😭😭😭
 
baada ya kupitia tena vipimo alibadilika ghafla na kuwa mkali sana na kumfokea yule daktari mwanafunzi kuwa kwanini hajaona tatizo la nyonga kuvunjika?

Haiwezi kamwe kutokea. Kama kosa watajuana wenyewe. We kitu gani hadi afokee mwenzie? Labda kwenye vikao vyao wanaweza,na si mbele ya mgonjwa na muuguzi. Tamathilia ingekuwa nzuri usingepitiliza kituo.
 
Huyo mwanafunzi ndio mzembe kama yeye hajaona tatizo na mgonjwa bado ana maumivu Kwa Nini asiombe ushauri Kwa mwalimu wake
 
Wakubwa wao wako busy sites za dada poa wanatafuta huduma...umkute ofisini hapo kavaa miwani yake kwny computer utajua anafanya kazi ya maana kumbe upupu...kama ni wanawake wapo busy na majungu kusemana...hii nchi Magufuli ndo aliwakomesha watumishi wa uma...kwa sbb alisikiliza kero direct na kutake actions...hapa mpk kijiji kipuputike ndo bi mdashi ataongea...
Ulikutana nao kwenye hizo sites?
 
Back
Top Bottom