Hivi Tanzania hatuna taasisi inayochunguza ubora wa huduma zinazotolewa kwenye hii mighahawa hapa nchini?

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,811
15,404
Siku hizi ukiingia kwenye mitandao ya kijamii utakutana na manung'uniko mengi kutoka kwa watu hususan sisi wazawa wenye rangi nyeusi yakituhumu ubaguzi katika kutoa huduma kwa wateja wenye ngozi nyeusi kwenye hii mighahawa ya kitalii.

Ukisoma maoni kutoka kwenye malalamiko ya mtoa hoja unakuja kugundua kwamba tatizo ni kubwa sana na baadhi ya mighahawa inayotajwa ni iliyopo maeneo ya Masaki Jijini Dar es salaam.

Sasa swali langu ni hili. Hivi hapa nchini hatuna taasisi ambayo inachunguza ubora unaotolewa kwa wateja si kwa hii mighahawa pekee bali pia na maeneo mengine?

Hizi tuhuma za ubaguzi kwenye mighahawa siyo ngeni na siamini kama serikali haizisikii lakini zimekuwa sikiishia kwenye mitandao ya kijamii bila kupatiwa suluhu.

Kama taasisi hiyo haipo kisheria kwa nini Bunge kwa busara zake isiunde chombo kitakachosimamia ubora wa huduma kwa wateja siyo kwenye sekta binafsi pekee bali pia kwenye taasisi za serikali ili kuboresha huduma kwa wateja bila ubaguzi.

Taasisi hiyo inatakiwa iwe inatuma wateja bandia na warekodi kila kitu ili kuwe na ushahidi iwapo kutakuwa na huduma mbaya na kuwachukulia wahusika hatua.

Naamini chombo hicho kitasaidia kuondoa malalamiko yanayotolewa kila siku kuhusu ubaguzi kwenye hii mighahawa inayotajwa kila siku.
 
Inauba sada kubaduliwa katika inchi yago mwenyewe

Mamlaba iagalie hii hali
 
Sasa swali langu ni hili. Hivi hapa nchini hatuna taasisi ambayo inachunguza ubora unaotolewa kwa wateja si kwa hii mighahawa pekee bali pia na maeneo mengine?

Hizi tuhuma za ubaguzi kwenye mighahawa siyo ngeni na siamini kama serikali haizisikii lakini zimekuwa sikiishia kwenye mitandao ya kijamii bila kupatiwa suluhu.
Hii nchi tumeshawekwa kwenye matabaka, kuna migahawa ukienda huna kitambi au suti au ukashuka kwenye IST watahudumiwa waliofika saa 9 wewe wa saa 7 unapitwa kama meza tupu
 
Nini kimetokea ? tuelimishe hali ya ubaguzi uliokutana nao. Mbona wahudum wa mighahawa hiyo wana heshima, wanakaribisha vizuri tu, yaan hela yako halafu ubaguliwe?

Siku moja moja najichanganya sehem hizo, mfano hizo za masaki nimeenda enda ingawa sio sana, na bei zao za ajabu ila sijawahi kutana na huduma mbovu au ubaguzi.

Na hizo sehemu ulizotaja wazungu wamejaa kweli, na waafrica wengi wanakuwemo kabisa.

Note: labda vidada vingi vinavyohudumu mule ni vidangaji vipo pale kwa ajili ya kuwadaka wazungu, so ukiona hali yoyote ambayo hujapenda ujuwe hakina time na wewe mawazo yako kwa huyo jirani yako mzungu so lazima kiangaike nae kuliko wewe. Kama umekutana na hili uko sahihi.
Navionaga vihudumu hasa vya kike vikiangaika na wazungu, vinasahau vimejichubua wazungu hawana time na mikolongo yao.

Huduma mbovu ziko kwenye hii mighahawa ya uswahilini, yaani unafika unaagiza chakula muhudumu hata hajali, haji kwa wakati, haombi samahani anapokosea, na usafi sio kiviile ni vurugu tupu huko changanyikeni.
 
Kwa upande wa huduma huwa sipati shida sehemu yoyote huwa natumia njia hii;

Nikifika sehemu husika na kuona huduma ni fake naangalia situation ilivyokaa kama naweza kujihudumia, as kwenda counter nalipa na kuomba nipewe sinia langu la ubwabwa au kama ni kinywaji.

It's very simple.
Na ikiwa ndiyo kijiwe chako daily, watakuzoea na ndiyo yanakuwa your life.
 
Ubaguzi wa nini mkuu? acheni kujishuku, personality zenu munaonekanwa hamna kitu ndio tatizo, hata mimi yashanikuta sana, tuache kulia lia kwa mambo madogo madogo.
 
Back
Top Bottom