Nimeiona hii video ya kijana Ali mwenye ulemavu na tatizo la kifafa. Nimesikitika sana alichofanyiwa na wananchi wenzetu wa Zanzibar.
Huyu kijana kwa wanaomjua wanasema amekulia Sinza na ni mlemavu kweli na amekua akiishi kwa kupata vibarua na kuomba msaada wa chakula na hela.
Udhalilishaji aliofanyiwa umeniacha na maumivu makubwa moyoni. Mtu hata kwa kumtazama usoni unaona dhahiri hayuko sawa na asiye na siha njema. Nimesawijika sana.
Wanasema amewaibia lakini hakuna uthibitisho wa hilo. Zaidi unaona ni chuki ya kwa kua ni mtu wa bara na zaidi ukisikiliza clip kwa uzuri kuna mtu anaropoka hawezi kua na msalaba huyo? Hiyo baada ya mmoja kumuuliza bwana Ali kuhusu mtu anaitwa Eric Masawe.
Nimekerekwa sana kwa udhalilishaji huu. Hii chuki ya dini ya mtu inatoka wapi? Asilani siwezi kumchukia mtu kwa dini yake hata kama si wa imani yangu na siafiki mambo juu ya imani yake. Kulikua na haja gani kutaja suala la msalaba?
Mimi kwetu Arumeru baba yangu alikua anakodisha ardhi kwa wazanzibari kiroho safi bila kujali dini zao wala utofauti wa makabila. Lakini, wenzetu hii chuki inatoka wapi?
Bwana Ali ametwezwa sana utu wake. Na huyu ni ndugu muislam vipi kwa asiye muislam? Hivi ndio dini inaelekeza? Kama mnaona kuomba anapata sana basi nanyi muombe muone kama ni jambo la kujivunia.
Wazanzibari mkae mkijua kama ni hasira zenu basi muipelekee CCM na sio wananchi wa kawaida. Huyo ndie adui yenu na adui wa kila mmoja wetu.
Ifike wakati mstaarabike. Dini badala ya kutujenga zinatufanya kuwa mafala na majinga.
Huyu kijana kwa wanaomjua wanasema amekulia Sinza na ni mlemavu kweli na amekua akiishi kwa kupata vibarua na kuomba msaada wa chakula na hela.
Udhalilishaji aliofanyiwa umeniacha na maumivu makubwa moyoni. Mtu hata kwa kumtazama usoni unaona dhahiri hayuko sawa na asiye na siha njema. Nimesawijika sana.
Wanasema amewaibia lakini hakuna uthibitisho wa hilo. Zaidi unaona ni chuki ya kwa kua ni mtu wa bara na zaidi ukisikiliza clip kwa uzuri kuna mtu anaropoka hawezi kua na msalaba huyo? Hiyo baada ya mmoja kumuuliza bwana Ali kuhusu mtu anaitwa Eric Masawe.
Nimekerekwa sana kwa udhalilishaji huu. Hii chuki ya dini ya mtu inatoka wapi? Asilani siwezi kumchukia mtu kwa dini yake hata kama si wa imani yangu na siafiki mambo juu ya imani yake. Kulikua na haja gani kutaja suala la msalaba?
Mimi kwetu Arumeru baba yangu alikua anakodisha ardhi kwa wazanzibari kiroho safi bila kujali dini zao wala utofauti wa makabila. Lakini, wenzetu hii chuki inatoka wapi?
Bwana Ali ametwezwa sana utu wake. Na huyu ni ndugu muislam vipi kwa asiye muislam? Hivi ndio dini inaelekeza? Kama mnaona kuomba anapata sana basi nanyi muombe muone kama ni jambo la kujivunia.
Wazanzibari mkae mkijua kama ni hasira zenu basi muipelekee CCM na sio wananchi wa kawaida. Huyo ndie adui yenu na adui wa kila mmoja wetu.
Ifike wakati mstaarabike. Dini badala ya kutujenga zinatufanya kuwa mafala na majinga.